Keren_Happuch
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 1,874
- 935
Hii imenikumbusha kisa cha afande mmoja pale Kijitonyama Mabatini alikuwa mmasai na mkewe mmasai,jamaa alipiga marufuku mkewe kuvaa kimasai na yeye hakuvaa kimasai hata siku moja ili kujificha.Bahati mbaya siku moja mkewe akawasemesha wamasai wenzake kwa lugha ya kwao na wale jamaa kusikia hivyo kesho yake mmoja wao akaja na mkuki wake akauacha hapo mlangoni,basi afande mmasai kurudi nyumbani anakuta mkuki mlangoni..!! We...!!! Palichimbika hapo na wala hapakutosha mpaka mkuu wa kituo akaja kuamulia kwa kumuweka ndani mgoni.....na mmasai akahamishwa kituo.
ST.PM, ..... yaani mpaka mjini wanaendeleza mila??? Basi hii kiboko....!!!1