Wamarekani na wazungu wasituingilie mambo yetu ya ndani, sisi ni Taifa huru

Status
Not open for further replies.

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
9,147
33,302
Kauli hii Ni maarufu Sana kwa VIONGOZi wa awamu hii ya tano muhula wa pili."Mabeberu wasituingilie katika mambo yetu ya ndani, kwani sisi ni Taifa huru, uchaguzi ulikua huru na wa haki, Kama mtu hajaridhika aende Mahakamani"

Haya maneno yanasemwa Sana na Watawala kutoka CCM ya kizazi hiki.

Ila kwa kumbukumbu zangu na kwa kupitia maandiko mengi niliyosoma Ni kwamba, Wakati wa Utawala wa awamu ya kwanza ya Akina Nyerere Tanzania ilikua mstari wa mbele kuwapinga wakoloni na makaburu na Mabeberu waliokua wakiwatesa Waafrika na wanyonge wengine duniani.

Tanzania ilikua kiongozi wa nchi zilizoitwa nchi tano za mstari wa mbele kupigania ukombozi wa Afrika.

Nchi hizo Ni
Tanzania
Zambia
Angola
Msumbiji
Na
Zimbabwe.
Kinara alikua Ni Tanzania.

Kilichokua kinapiganiwa na Tanzania Ni kupinga uonevu wote dhidi ya Binadamu Kama Ubaguzi wa rangi na na ubaguzi wa Aina yoyote, Ukoloni, uonevu au ukandamizaji wa ndani uliokua ukifanywa na Marais au Watawala madikteta,wakoloni,Mabeberu na Makaburu wa Afrika kusini.

Watawala madikteta walikua Ni
Makaburu wa Kusini waliwabagua wazalendo weusi wa Afrika kusini,
Wakoloni waliwatawala bila ridhaa yao Waafrika na kwingineko,

Mabeberu walikua Ni Kama Mataifa yenye nguvu kuzitawala,kuzikandamiza na kizinyonya nchi changa

Madikteta walikua Ni kama kina Iddi Amini wa Uganda,Bokassa wa Afrika ya Kati,Mobutu seseseko wa Zaire,Kamuzu Banda wa Malawi,Watawala wa Sudani dhidi ya Wasudani Kusini Weusi na wababe wengine.
Hawa Ni baadhi.

Lakini wote Hawa kiboko yao alikua Ni Julius K Nyerere.
Aliwasaidi na kuwaunga mkono kwa Hali na Mali wale wote waliokua wakionewa,wakikandamizwa,kudhulumiwa,kubaguliwa,kuteswa na kila Aina ya manyanayaso hapa duniani.
Nyerere na CCM yake waliwasaidia kwa Hali na Mali.
Alitoa misaada kiserikali na kibinafsi.

Hata Hivyo Watawala wa nchi zote hizo walikua wakimpinga Nyerere kwa kauli zinazofanana na kauli zitolewazo Leo na Watawala wa Sasa kuwa,
"Nyerere asiingilie mambo yao ya ndani,kwani wao ni nchi huru".

Malalamiko ya wananchi wengi wa nchi hizo Ni kwamba walikua wanaonewa sawasawa kabisa na Wafanyiwavyo CHADEMA leo,ndipo Mwalimu na CCM ya wakati huo ikamuuma akajitolea kuwasaidi hai waliokua wanateswa.
Baadhi ya waliosaidiwa Ni,

Yoweri Museven wa Uganda
Raurel Kabila wa Zaire
Sam Nujoma wa Namibia
Wazalendo wa Afrika kusini na Namibia
John Garang wa Sudan
Kanyama Chiume wa Malawi
Na wengine wengi.

Watawala wa nchi KandamiI walimuona Nyerere anaingilia Mambo yao ya Ndani na wao Ni nchi huru.
Walimchukia Nyerere.

Leo hii,miongo mingi imepita na mambo yemekua kinyume, waliokua watetezi wa haki wamekua wakandamizaji,leo hii Wazungu wamekua watetezi wa haki na wakandamizaji leo wanadai wao Ni nchi huru wasiingiliwe katika mambo yao.
Wapinzani wanasulubiwa mchana kweupe,wanabaguliwa,wanateswa,wanafungwa nakila Aina ya uonevu na dhuluma Kama jinsi makaburu na madikteta walivyowafanyia wazalendo katika nchi zao.
Tanzania ilikua kimbilio la wanyonge,Sasa inakimbiwa na wanyonge.
 
Hata kama mnapora haki zetu za kuishi, wahanga sisi unatuitisha nasi kusimama imara kuwataka wasituingilie tu kwa sababu ya jina la kuwa ni mambo ya ndani?

Kwani uzuzu utakuwa ni nini basi?
 
Mm ninachokiona ni kwa sababu hajui maumivu wanayoyapata watanzania kuhusiana na hali ngumu ya maisha,yeye anajiona kiburi sana wakati uwezo wake wa kiuchumi,kimaarifa na kimaamuzi yuko ovyo .Huwezi kuwa na kiburi kwa tajiri wakati unajijua wewe ni maskini na una njaaa.
 
Hiki kinachoendelea Bongo,ni kitu fulani kwa lugha ya kigeni kinaitwa,"state capture'"chama tawala,kimezishika taasisi zote nyeti,Usalama,Hazina,Mahakama,hapa nchi imetekwa,rasilimali za nchi,zinaelekezwa kuhudumia mifuko ya watu binafsi,wakubwa huko juu ni kula tu

Taasisi za kudai haki,vyombo vya habari vyote vinabinywa kuhakikisha havisemi kitu,Wala haviwaambii wananchi kinachoendelea,wakati wakubwa wanakula,huku wanacheki polisi wanavyoenenda,na polisi nao,kwa sababu wanaona wakubwa wanavyokula,nao wanaamua kuwafsnyia unyama Raia,kupora,kubambikia kesi,ila wanaonywa wasivuke mipaka

Ukiona taasisi za haki za binadamu,vyombo vya habari,NGOs,zinafungwa na kupigwa vita,huku wanajeshi wakipewa vyeo,na kuboreshewa maslahi,hiyo ni ishara ya state capture,kuitumia nchi kujibinafsisha

Na baada ya kutenda madhambi sana,Hawa wanasiasa utawaona wakikimbilia kwenye makanisa,misikiti wakijifanya ni wacha Mungu(Kama anavyofanya jiwe),hii yote ni kwa sababu ya nafsi kuwasuta,na baada ya muda,viongozi wa dini wanaanza kuwasifia
 
Hiki kinachoendelea Bongo,ni kitu fulani kwa lugha ya kigeni kinaitwa,"state capture'"chama tawala,kimezishika taasisi zote nyeti,Usalama,Hazina,Mahakama,hapa nchi imetekwa,rasilimali za nchi,zinaelekezwa kuhudumia mifuko ya watu binafsi,wakubwa huko juu ni kula tu,
Taasisi za kudai haki,vyombo vya habari vyote vinabinywa kuhakikisha havisemi kitu,Wala haviwaambii wananchi kinachoendelea,wakati wakubwa wanakula,huku wanacheki polisi wanavyoenenda,na polisi nao,kwa sababu wanaona wakubwa wanavyokula,nao wanaamua kuwafsnyia unyama Raia,kupora,kubambikia kesi,ila wanaonywa wasivuke mipaka,
Ukiona taasisi za haki za binadamu,vyombo vya habari,NGOs,zinafungwa na kupigwa vita,huku wanajeshi wakipewa vyeo,na kuboreshewa maslahi,hiyo ni ishara ya state capture,kuitumia nchi kujibinafsisha,
Na baada ya kutenda madhambi sana,Hawa wanasiasa utawaona wakikimbilia kwenye makanisa,misikiti wakijifanya ni wacha Mungu(Kama anavyofanya jiwe),hii yote ni kwa sababu ya nafsi kuwasuta,na baada ya muda,viongozi wa dini wanaanza kuwasifia
Brother unatumia whiskey? Wine.. or something. Tumia kitu ya bei mbaya bill on me.
Umeandika in short our current state hapa nchini.
Bad news ni kwamba.. wabongo wengi wanaishi mtindo wa bora liende.
They dont care
 
Hata kama mnaua wakosoaji msiingiliwe muachwe tu?!.

Kwa maoni yangu, muingiliwe hata kimwili kudadek zenu
 
Nyerere huyo huyo aliwahi kuulizwa katika moja ya mahojiano yake kwamba atachagua nini Kati ya demokrasia na maendeleo akajibu kuwa yeye anaongoza Taifa lenye watu wenye mahitaji mengi muhimu hivyo atachagua maendeleo.

Hivyo mzee don't be carried away na hizo lugha za hao mabeberu.
 
Mahojiano hayo yalifanyika wapi na tarehe ngapi?
Nyerere huyo huyo aliwahi kuulizwa katika moja ya mahojiano yake kwamba atachagua nini Kati ya demokrasia na maendeleo akajibu kuwa yeye anaongoza Taifa lenye watu wenye mahitaji mengi muhimu hivyo atachagua maendeleo.

Hivyo mzee don't be carried away na hizo lugha za hao mabeberu.
 
Nyerere huyo huyo aliwahi kuulizwa katika moja ya mahojiano yake kwamba atachagua nini Kati ya demokrasia na maendeleo akajibu kuwa yeye anaongoza Taifa lenye watu wenye mahitaji mengi muhimu hivyo atachagua maendeleo.

Hivyo mzee don't be carried away na hizo lugha za hao mabeberu.
Nini maana ya maendeleo?
 
Wanayo haki sababu wao ndio uingia gharama kubwa Sana kuhudumia wakimbizi duniani wanaozalishwa na watawala wa kiafrica
 
Haswaaaa.... Tusisahau pia ni sawa ni nchi huru ila SIO KISIWA...pamoja na uhuru huo lakini dunia haiko hivyo. Kuna uongozi na kanuni za kidunia ndio maana tunasaini MAAZIMIO NA MIKATABA YA kimataifa ikiwemo ya haki za binadamu. Dunia pia ina mfumo wa kiuongozi unalenga dunia si uwanja wa fujo kwani tunaishi kwa kutegemeana. Hivyo misingi ya ndani na ya kidunia ni muhimu ikaheshimiwa.

Hivi leo kungekuwa hakuna uongozi wa Kidunia,kila mtu akajiamulia lwake hali ingekuwaje?
 
Sisi ni sehemu ya dunia hatuwezi kuwa tunauliwa na hayawani kwa kututoa kafara kwa mizimu na dunia ikaa kimya.
Ukizaa mtoto si wa kwako ni wa jamii
 
Hiki kinachoendelea Bongo,ni kitu fulani kwa lugha ya kigeni kinaitwa,"state capture'"chama tawala,kimezishika taasisi zote nyeti,Usalama,Hazina,Mahakama,hapa nchi imetekwa,rasilimali za nchi,zinaelekezwa kuhudumia mifuko ya watu binafsi,wakubwa huko juu ni kula tu,
Taasisi za kudai haki,vyombo vya habari vyote vinabinywa kuhakikisha havisemi kitu,Wala haviwaambii wananchi kinachoendelea,wakati wakubwa wanakula,huku wanacheki polisi wanavyoenenda,na polisi nao,kwa sababu wanaona wakubwa wanavyokula,nao wanaamua kuwafsnyia unyama Raia,kupora,kubambikia kesi,ila wanaonywa wasivuke mipaka,
Ukiona taasisi za haki za binadamu,vyombo vya habari,NGOs,zinafungwa na kupigwa vita,huku wanajeshi wakipewa vyeo,na kuboreshewa maslahi,hiyo ni ishara ya state capture,kuitumia nchi kujibinafsisha,
Na baada ya kutenda madhambi sana,Hawa wanasiasa utawaona wakikimbilia kwenye makanisa,misikiti wakijifanya ni wacha Mungu(Kama anavyofanya jiwe),hii yote ni kwa sababu ya nafsi kuwasuta,na baada ya muda,viongozi wa dini wanaanza kuwasifia

Ulichoandika ni kweli tupu. Tatizo tulilonalo hapa nchini kwetu ni kwamba watu wetu hawana ujasiri, ni waoga!! Mambo kama haya hayawezi kutendeka kwa majirani zetu hapo kaskazini. Sisi ni mafundi kwa kupiga porojo lakini sio watu wa vitendo na hiyo inaweza kuelezeka kwa jinsi tulivyopata uhuru wetu toka kwa waingereza bila kumwaga damu!. Nchi zilizopigania uhuru wao na kumwaga damu upuuzi wa " STATE CAPTURE" kama wa JIWE usingevumiliwa!!

Jiwe anawadanganya wananchi kwa kujenga miradi mikubwa yenye kutumia mabilioni ya shillings kuwa ndio maendeleo lakini sidhani kwa hali ilivyo sasa Tanzania inaweza kupata maendeleo ya kweli. Maendeleo ya kweli yanahusisha watu walio na umoja kitu ambacho nchi haina wakati huu, hivyo ni jambo la muhimu nchi kujenga umoja kwanza na umoja huo ndio unakuwa daraja la nchi kuwa na Amani ambayo itaipeleka nchi kuwa na maendeleo!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom