Wamarekani na Watanzania

siyo.mzee

New Member
Jul 28, 2008
2
0
MWALIMU J.K.Nyerere alishatuasa kuwa ni vyema kukaa mbali sana na Mmarekani. Katika miaka ya hivi karibuni tumeona juhudi kubwa za kuikurubisha Tanzania kwa Marekani na uongozi ulioko madarakani.

Ninachojiuliza ni, je, hofu za Babu sasa hazina msingi? Hata mwanae Benjamin Mkapa naye aliwaogopa sana jamaa hawa. Vipi awamu ya nne inajipeleka mzobamzoba miguuni mwa jamaa hawa ambao hawatabiriki-leo rafiki, kesho ukimuudhi kama Saddam alivyofanya adui mkubwa na anaishia kukuangamiza!

Hofu ninayo bado mie labda akija madarakani Mjalua Obama tunaweza kuonewa huruma. Lakini hata hili naona kama ndoto maana kuna asiyejua kuwa Marekani inaendeshwa na Wayahudi? Na hakuna Obama analoweza kupinga pindi akiamrishwa na wakubwa wake.

Historia inatuonesha nini Wamarekani walichowafanyia ndugu zao huko Marekani ya Kati na Kusini; kisha Vietnam, Korea na Mashariki ya mbali kwa ujumla; na kwa hivi sasa wanachoendeleza Afghanistan na Iraq.

Hili ni taifa linaloishi kwa kukopa miaka nenda rudi. Na linapotishika kuishiwa kama ilivyo sasa basi linageuka jijambawazi kuu na kuzinyonga nchi za kinyonge ili kukwapua chao na kujipatia tena fedha za kuendesha maisha yao aghali. Wana-Jamii, je, sio muhimu kuzungumza hatima ya Tanzania na urafiki wake wa karibu na Marekani bila kujali tuna ndugu zetu na jamaa zetu na pengine wazazi wetu wanaoishi Marekani?

Nia sio kuvunja uhusiano na Marekani. Bali kujilinda kwa hasira na jazba zisizo na mipaka za jamaa hawa pindi wakiona mambo sivyo kwa upande wetu kulingana na maslahi yao. Na ikiwezekana tushawishi kuwepo kwa uongozi wa Marekani na dunia unaojali maisha ya wote; unaowatetea wanyonge badala ya kuwadidimiza; na ulio tayari kushiriki katika ubia maridhawa wa kibiashara na ulinzi wa mazingira na usalama wa dunia!
 
Suala siyo kukaa nao karibu au nini hawa ni Mapebari just like any capitalist state.Hamna cha Obama tena I would like to say that we should just reduce the high expectations we have of him.Actually the biggest question we should ask ourselves is will he even deliver to the Americans all the promises he has promised them and what is it actually he is going to do for us?
Lets be ourselves and solve our own problems tusimtegemee mtu aje kusolve ours.
 
Suala siyo kukaa nao karibu au nini hawa ni Mapebari just like any capitalist state.Hamna cha Obama tena I would like to say that we should just reduce the high expectations we have of him.Actually the biggest question we should ask ourselves is will he even deliver to the Americans all the promises he has promised them and what is it actually he is going to do for us?
Lets be ourselves and solve our own problems tusimtegemee mtu aje kusolve ours.


Well naungana na wewe. Siku zote tumekuwa mstari wa mbele kuwalaumu watu wengine, lakini hauwa hatutaki kujiangalia. The closer intelligently you get to the Americans, the better you are. Ukiwa Bwegebwege they feel so happy, wanakutumia tani yao halafu wanakutupa.
Lakini sio Marekani tu hata wafanya biashara wa TZ wenye wanafanya hivyo, kwahiyo hii ni roho ya kila mtu mwenye akili, so it is up to sisi wenye kujua nini tunataka kwenye ushirikiano huo.
 
Nchi inahitaji mapinduzi...Mapinduzi ya kwanza ambayo yame bear hata jina la chama ni hayo ya Zanzibar!

Na huo ndio unafiki wa Mwalimu uliomsababisha asiuwawe kama kina Nkrumah na Lumumba...Alikubaliana na ukweli kuwa Sultan atarudi hapo Zenji na unajuwa tena mvutano wa kidini kati ya mwarabu na mzungu especially miaka ya 60 ambapo hata hapa USA makanisa ya kiinjili kama assemblies of God yalikuwa yalipamba moto huku watu kama kina Billy Graham wakiandaa mikutano mikubwa Afrika ambayo waliita CRUSADES!

CRUSADES ni neno lililokuwa likitumika kama vile hawa mujahidina wa waislam ambao pia walifanya mauwaji miaka ya nyuma wakati wa vita ya wakristo na waislam.

Lakini dunia imebadilika...NI LAZIMA BINADAMU WOTE WAISHI KWA UMOJA NA KUHESHIMIANA NA DHULMA IWE MWIKO!

Sasa tunataka mapinduzi mapya...Ya kimaendeleo.
Hivyo kwa mtizamo wangu...Marais wote hao waliopita bado walikuwa wakifanya kazi kwenye mazingira magumu na unafiki wao ndio unaendelea kuwaponya kwa kujidai ni washirika wa west na huku chini chini wakiwa na masoshalisti.

Na sasa hata JK si ni yale yale ya mwalimu wanaendeleza karata?

Sasa naona mwisho umefika wa kuendelea kuitumia karata ya zenji kinafki kwa kigezo cha mapinduzi ya kutomtaka mwarabu na wakati mwarabu mwenyewe yuko hadi chumbani.

Hatuwezi kuendelea kuyalinda mapinduzi yaliyopitwa na wakati...Ni muda wa kufanya mapinduzi ya kuzilinda rsilimali zetu amabazo ziko kama hazina mwenyewe mara baada ya kuingia kwenye globalization na viongozi hao wote watalaumiwa kwa kutowatayarisha wananchi na kuwapa elimu.

Kama kweli wangekuwa wazalendo...Wangehakikisha hata wanapanda dala dala ili watoto waende shule...Ndio uzalendo huo...Na si kujenga tabaka la mamluki wa kikoloni kwa kuendelea kusomeshana na kurithishana madaraka na huku wananchi wenye mali wakifa!

Kuendesha mashangingi ya hali ya juu yenye ghrama za utunzanji ambazo labda ni sawa na gharama za kuanzisha shule ama hospitali!

Utaratibu wa kuwahudumia mawaziri na kuwajazia mibia na minyama ya groceries shoppings kwa gharama za wananchi wasiojiweza hata kwa mlo mmoja!

Kama kweli tunataka kulikomboa Taifa...Basi tuwajengee viongozi mazingira ya kuwatumikia wananchi na si wananchi kuwatumikia viongozi...Serikali kuwatumikia wananchi na si the other way round.

Kama viongozi wanapita huku na huko na kusema sisi ni masikini...Basi waonyeshe na mfano kuwa sisi ni kweli masikini!

Wananchi wakiandamana kwenda kwenye hayo mahekalu yenu nyie viogogo na kuomba chumvi,sabuni,mafuta na chakula mtawaambia nini?

Maana mkibisha si na wao watagoma kulipa kodi?

WALIPE KODI KWA KIPI MNACHOWAFANYIA NA WAKATI NCHI MNAUZA?

TIME FOR CHANGE IS NOW!
 
Hakuna ubaya wowote kuwa karibu na Marekani.

Unajua sera za Marekani towards other countries???

Ni vizuri kujua mambo ambayo wamarekani wanajifanya kuyasema kila siku na mambo ambayo huyatenda kwenye nchi nyingine kabla ya kuwa karibu nao..
 
Siyo. mambo yamebadilika na Nyerere alitawala wakati wa Regan mara ya mwisho. Tanzania imebadilika sasa tunafata capitalist system na sera za ujamaa hazijafanikiwa. Kwa ufupi tunaishi muda tofauti na si vibaya kuwa na uhusiano na Marekani kama matokeo yake ni Watanzania kupata maisha bora. Uhusiano huo umesaidia vitu vingi ambavyo si vya siasa mfano kama kwa sasa kuna Watanzania wengi wanasoma na kufanya kazi huku na kutuma pesa nyumbani. Kwa nchi kubwa kama Marekani Tanzanzania tutafaidika.
 
Unajua sera za Marekani towards other countries???

Ni vizuri kujua mambo ambayo wamarekani wanajifanya kuyasema kila siku na mambo ambayo huyatenda kwenye nchi nyingine kabla ya kuwa karibu nao..

Urafiki wa hawa jamaa ni wa undumilakuwili. Siku zote watapenda wao wanufaike zaidi na urafiki huo kuliko haya huyo 'rafiki yao' na wakija na matakwa yao uwatimizie na ukiyakataa basi unakuwa adui yao. Mfno hai ni Saddam ambaye alikuwa ni kipienzi chao na walimpa silaha na pesa nyingi wakati wa vita iliyodumu zaidi ya miaka mitano kati ya Iraq na Iran, lakini baada ya kuwakatalia matakwa yao basi akawa adui yao mkubwa. Kwa hiyo basi kutokana na mifano hiyo mingi ni lazima tuwe waangalifu mno vinginevyo wataiteka nyara Tanzania na watadumu milele kama ambavyo walivyodumu mpaka sasa Japan, Wajapan wanawafukuza kila siku kwenye ardhi yao, lakini serikali za vibaraka bado zinaachia waendelee kupeta. Huko Iraq nako wanataka kuweka makazi yao milele. Naam dunia imebadilika lakini Wamarekani wa mwaka 47 hawana tofauti yoyote na wale wa 2008 siku zote maslahi ya kwao ndiyo yenye kipaumbele na ni lazima wanufaike wao zaidi kuliko wewe.
 
Hakuna ubaya wa kuwa karibu na wamarekani. Tunachotakiwa ni kuwa na priorities zetu kitaifa na kuhakikisha kuwa ukaribu huo unatusaidia kuzitimiza. Viongozi wa sasa hawana priorities zozote za kitaifa, wanachotaka ni sifa na kupewa pasenti tu.
 
Unajua sera za Marekani towards other countries???

Ni vizuri kujua mambo ambayo wamarekani wanajifanya kuyasema kila siku na mambo ambayo huyatenda kwenye nchi nyingine kabla ya kuwa karibu nao..

Kama sera zao ni mbaya hivyo basi tuache kuwababaikia, tuache kuja kusoma na kulowea Marekani. Tuachane na kila kitu cha Wamarekani. Tusipokee misaada yao. Tufunge ubalozi wetu pale DC na wao wafunge wa kwao pale Dar. Tuvunje mahusiano yote na Marekani .....
 
MWALIMU J.K.Nyerere alishatuasa kuwa ni vyema kukaa mbali sana na Mmarekani. Katika miaka ya hivi karibuni tumeona juhudi kubwa za kuikurubisha Tanzania kwa Marekani na uongozi ulioko madarakani.

Ninachojiuliza ni, je, hofu za Babu sasa hazina msingi? Hata mwanae Benjamin Mkapa naye aliwaogopa sana jamaa hawa. Vipi awamu ya nne inajipeleka mzobamzoba miguuni mwa jamaa hawa ambao hawatabiriki-leo rafiki, kesho ukimuudhi kama Saddam alivyofanya adui mkubwa na anaishia kukuangamiza!

Hofu ninayo bado mie labda akija madarakani Mjalua Obama tunaweza kuonewa huruma. Lakini hata hili naona kama ndoto maana kuna asiyejua kuwa Marekani inaendeshwa na Wayahudi? Na hakuna Obama analoweza kupinga pindi akiamrishwa na wakubwa wake.

Historia inatuonesha nini Wamarekani walichowafanyia ndugu zao huko Marekani ya Kati na Kusini; kisha Vietnam, Korea na Mashariki ya mbali kwa ujumla; na kwa hivi sasa wanachoendeleza Afghanistan na Iraq.

Hili ni taifa linaloishi kwa kukopa miaka nenda rudi. Na linapotishika kuishiwa kama ilivyo sasa basi linageuka jijambawazi kuu na kuzinyonga nchi za kinyonge ili kukwapua chao na kujipatia tena fedha za kuendesha maisha yao aghali. Wana-Jamii, je, sio muhimu kuzungumza hatima ya Tanzania na urafiki wake wa karibu na Marekani bila kujali tuna ndugu zetu na jamaa zetu na pengine wazazi wetu wanaoishi Marekani?

Nia sio kuvunja uhusiano na Marekani. Bali kujilinda kwa hasira na jazba zisizo na mipaka za jamaa hawa pindi wakiona mambo sivyo kwa upande wetu kulingana na maslahi yao. Na ikiwezekana tushawishi kuwepo kwa uongozi wa Marekani na dunia unaojali maisha ya wote; unaowatetea wanyonge badala ya kuwadidimiza; na ulio tayari kushiriki katika ubia maridhawa wa kibiashara na ulinzi wa mazingira na usalama wa dunia!

Madai yako sio kweli.

Uhusiano wa Marekani na Tanzania upo na ni lazima uwepo na utaendela kuwepo.

Tena uhusiano huo upo ule wa moja kwa moja na usio wa moja kwa moja.

Marekani ni taifa kubwa duniani na ni tajiri na lina nguvu kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Pia ni taifa lenye nguvu kijeshi duniani na hakuna taifa lolote duniani lenye kuweza kuizidi Marekani kwa vigezo nilivyotaja hapo juu.

Lakini hapohapo America ni ufalme mpa wa kishetani, ule wa iliokuwa Soviet Union. Wanajifanya watu wazuri wakishirikiana na EU/UN kama serikali inayoangalia ulimwengu.

Hii imewaletea matatizo ya kuchukiwa na watu.

Lakini jiulize tatizo kubwa nini?

Ni power na geo-political repositioning kati yake na China, India, Brazil na Russia.

Sasa sisi kainchi kama Tanzania tukijipendekeza si mbaya kama tutafaidika kwa chochote isipokuwa wale wachache.

Tanzania tunakula nao lakini kwa subsidise maendeleo yao.
 
Hakuna ubaya wa kuwa karibu na wamarekani. Tunachotakiwa ni kuwa na priorities zetu kitaifa na kuhakikisha kuwa ukaribu huo unatusaidia kuzitimiza. Viongozi wa sasa hawana priorities zozote za kitaifa, wanachotaka ni sifa na kupewa pasenti tu.

Hizo priorities zetu za kitaifa zitoke kwa viongozi kama wapi? JK, Makamba, Pinda? Maana kwenye ufisadi wameshaonyesha kwamba hawana priorities zilizoweka mbele maslahi ya Tanzania badala ya Chama Chao cha mafisadi na matumbo yao, je, wataweza kuweka priorities za kitaifa kuhusiana na urafiki na Marekani!!!!? Nchi inayofaidika hapa duniani kwa misaada ya Marekani ni Israel peke yake lakini zilizobaki lazima wao wafaidike zaidi ili kulinda "interest zao" Tukifanya makosa na kuingia kichwa kichwa tutajuta milele. Kuna nchi chungu nzima ambazo zinaweza kuwa marafiki wa Tanzania bila masharti ya ajabu ajabu na pia wana nia ya kweli ya kutusaidia. Urafiki na hawa jamaa ni kuhakikisha hawakuzoei kupita kiasi na ushahidi wa hilo upochungu nzima. Wameshasikia Tanzania kuna uranium belele na pia hawajapa nchi ilikubali kuwapa nafasi ya kuweka kituo chao cha kijeshi Africa watajifanya ni marafiki wa kweli ili kuhakikisha uranium haichukuliwi na Taifa jingine lolote duniani ila wao na kisha kupata sehemu ya kutanua makucha yao Afrika.
 
MWALIMU J.K.Nyerere alishatuasa kuwa ni vyema kukaa mbali sana na Mmarekani. Katika miaka ya hivi karibuni tumeona juhudi kubwa za kuikurubisha Tanzania kwa Marekani na uongozi ulioko madarakani.

Mwalimu was wrong about Socialism and many other things bila shaka he was also wrong about this as well.
 
Mwalimu was wrong about Socialism and many other things bila shaka he was also wrong about this as well.

Na hao waliokuwa right kuhusu ubepari ukiwauliza je Tanzania katika kipindi cha ujamaa na katika kipindi cha ubepari ni kipindi kipi ambacho Watanzania walifaidika zaidi? Jibu tunalijua. Wengi tuliona maendeleo makubwa ya Tanzania wakati wa ujamaa pamoja na kuwa nchi za magharibi zilimpiga vita kubwa Mwalimu ukilinganisha na kipindi cha ubepari pamoja na kuwa na marafiki kama US n.k. waliotumwagia "misaada" ya kutununua. Chini ya Mwalimu uchumi ulikuwa mikononi mwa Watanzania, aliweza kusomesha Watanzania hadi chuo kikuu bila kujali uwezo wao na hao ndiyo leo hii wanatamba katika kona mbali mbali za dunia kutokana na uongozi wa Mwalimu.
Sasa hivi kuna mafisadi tu ambao wanaiuza nchi yetu kila kukicha kwa mikataba isiyo na maslahi yoyote kwa Watanzania. Bado naamini kauli ya Mwalimu kwamba UBEPARI NI UNYAMA!!! Na unyama huo unashamiri sasa ndani ya nchi yetu.
 
Wasiwasi wangu kuhusu viongozi wetu ni kuwa ni weak. Hivyo wanadhani kuwa karibu na Mmarekani itakuwa afadhali wakivurunda hasa huyu mtu anayeitwa Kikwete. Bahati mbaya watanzania tulipiga kura huku tumefumba mambo. Hata hivyo bado muda tunao wa kumtoa huyu weak person kabla hajaharibu sana mambo.
 
Na hao waliokuwa right kuhusu ubepari ukiwauliza je Tanzania katika kipindi cha ujamaa na katika kipindi cha ubepari ni kipindi kipi ambacho Watanzania walifaidika zaidi? Jibu tunalijua. Wengi tuliona maendeleo makubwa ya Tanzania wakati wa ujamaa pamoja na kuwa nchi za magharibi zilimpiga vita kubwa Mwalimu ukilinganisha na kipindi cha ubepari pamoja na kuwa na marafiki kama US n.k. waliotumwagia "misaada" ya kutununua. Chini ya Mwalimu uchumi ulikuwa mikononi mwa Watanzania, aliweza kusomesha Watanzania hadi chuo kikuu bila kujali uwezo wao na hao ndiyo leo hii wanatamba katika kona mbali mbali za dunia kutokana na uongozi wa Mwalimu.
Sasa hivi kuna mafisadi tu ambao wanaiuza nchi yetu kila kukicha kwa mikataba isiyo na maslahi yoyote kwa Watanzania. Bado naamini kauli ya Mwalimu kwamba UBEPARI NI UNYAMA!!! Na unyama huo unashamiri sasa ndani ya nchi yetu.

Lets face it Socialism didnt work, never work and never will work. Wewe unakumbuka maendeleo, mimi nakumbuka foleni zakununua sukari na bidhaa nyingine. Nyerere helped create a monster by making a guinea pig project of our beloved Tanzania. Socialistic brainwashing is what it seems like to me. Please dont tell me you truly bbelieve that times were better then. Its true we do live in difficult times; lakini jiulize whose fault is it?? Hawa mafisadi wote ni Watoto wa Nyerere... So you have to ask yourselves what did Socialism achieve apart from setting us back a few decades.... People talk of Peace in this country kwani hamna capitalistic regimes which are peaceful nations. Let get rid of this Ujamaa hangover of ours and "Mwalimu alisema" habits and truly evaluate what went down. Anyways Mwalimu alisema tuofie wamarekani... so what??? unatiakiwa kuofia kila mtu, kama ume lala that is not the Americans fault. Look at us now..., Socialism has taught us to be obidient flock of sheeps and now truly tumelala... Hadi uganda wameaamka!!!!
 
Hutaki kukubali ukweli kwamba Mwalimu alipigwa vita sana na nchi za Magharibi. Haya huo ubepari umewanufaisha vipi Watanzania? Sera za Rukhsa, Mkapa na JK zote ni za kibepari je zimewanufaisha vipi Watanzania? Nadhani unasikia vilio kila kona ya nchi kuhusiana na rasilimali zetu kuporwa na wageni, je hayo unayaweza kuyaita mafanikio kweli ya sera hizo?

Utakuwa mchoyo wa shukrani kama miaka yote 24 ambayo mwalimu alikuwa madarakani hukuona chochote alichokifanya Mwalimu kilichokuwa na maslahi kwa Tanzannia, Watanzania na Afrika kwa ujumla zaidi ya foleni ya sukari na bidhaa nyingine. Huna maoni yoyote kuhusu uchumi wa Tanzania kuwa mikononi mwa Watanzania? Huna maoni yoyote kuhusu vision ya Mwalimu kwamba ili uchumi wa Tanzania uwe mikononi mwa Tanzania inabidi kupata wataalamu wetu wenyewe badala ya kuwaajiri wazungu hivyo kuamua kujenga chuo kikuu na kuhakikisha kwamba watoto wa Watanzania wote bila kujali uwezo wao kifedha watasomeshwa bure na serikali na matunda yake hadi hii leo yanaonekana siyi tu Tanzania bali duniani kote.

Unasahau pia kwamba kupanda kwa bei ya mafuta duniani mwaka 1973 kuliusambaratisha hata uchumi wa US, pia tulikuwa na ukame mkubwa mwaka 1975 na vita vya nduli ambavyo kama nchi tulitumia mapato yetu mengi ya fedha za kigeni ili kumtoa nduli. Vyote hivi huvioni bali unachokumbuka ni FOLENI ZA SUKARI NA BIDHAA NYINGINE TU!!! Duh! Ama kweli waswahili walisema tenda wema wende zako. Rest in peace Mwalimu. You're the hero to many Tanzanians and we will remember you as the one of the best leader in the World.
 
Unasahau pia kwamba kupanda kwa bei ya mafuta duniani mwaka 1973 kuliusambaratisha hata uchumi wa US, pia tulikuwa na ukame mkubwa mwaka 1975 na vita vya nduli ambavyo kama nchi tulitumia mapato yetu mengi ya fedha za kigeni ili kumtoa nduli. Vyote hivi huvioni bali unachokumbuka ni FOLENI ZA SUKARI NA BIDHAA NYINGINE TU!!! Duh! Ama kweli waswahili walisema tenda wema wende zako. Rest in peace Mwalimu. You're the hero to many Tanzanians and we will remember you as the one of the best leader in the World.[/size][/color]

Bei ya mafuta na vyakula bado mpaka leo inasumbua lakini wenzetu kwa sababu ya technology walionayo wanaweza kufikiria njia mbadala.

Kwa ujumla babu alijitahidi sana, amejenga viwanda, akaanzisha mashirika ya umma, na kila aina ya nguzo ya uchumi vitu vilivyokuja kumalizwa na watu wenye uroho wa utajiri wa harakaharaka.

Uliza leo hii THB, UDA, KAMATA,Tanganyika Packers, Sungura Textile, Mwatex, Mbeya Tex vipo wapi je ni Mwalimu wa kulaumiwa au wapumbavu wachache? maana waliiba bila yeye kujua na siku alipoambiwa atembelee maeneo ya karibu na nyumbani kwake ndio alishangaa kuona mahekalu yanajengwa tena karibu na nyumbani kwake Msasani.

Hivi mnakumbuka TANBOND na mkate wa SIHA bidhaa za Tanzania.
 
Na hao waliokuwa right kuhusu ubepari ukiwauliza je Tanzania katika kipindi cha ujamaa na katika kipindi cha ubepari ni kipindi kipi ambacho Watanzania walifaidika zaidi? Jibu tunalijua. Wengi tuliona maendeleo makubwa ya Tanzania wakati wa ujamaa pamoja na kuwa nchi za magharibi zilimpiga vita kubwa Mwalimu ukilinganisha na kipindi cha ubepari pamoja na kuwa na marafiki kama US n.k. waliotumwagia "misaada" ya kutununua. Chini ya Mwalimu uchumi ulikuwa mikononi mwa Watanzania, aliweza kusomesha Watanzania hadi chuo kikuu bila kujali uwezo wao na hao ndiyo leo hii wanatamba katika kona mbali mbali za dunia kutokana na uongozi wa Mwalimu.
Sasa hivi kuna mafisadi tu ambao wanaiuza nchi yetu kila kukicha kwa mikataba isiyo na maslahi yoyote kwa Watanzania. Bado naamini kauli ya Mwalimu kwamba UBEPARI NI UNYAMA!!! Na unyama huo unashamiri sasa ndani ya nchi yetu.

Bubu, Asante kwa kuwaelimisha watu humu.
Wanaosema Mwalimu alifanyamakosa kwa kufuata siasa ya ujamaa ni 'wavivu wa kufikiri'! Siku zote mie huwaambia bila siasa za Mwalimu Nyerere wengi leo wasingelikuwa huko waliko na wasingelikuwa wanatamba kwenye internet badala yake wangelikuwa vijijini wakichunga mbuzi na ng'ombe! Washukuru elimu ya bure waliyopewa baba, mama, shangazi, wajomba zao n.k. iliyotokana na siasa za Mwalimu Nyerere. Leo hii watu bado tunatembea barabarani bila hofu kwa kuwa bado kuna ile chembe ya 'udugu' uliotokana na siasa za Ujamaa.
 
Back
Top Bottom