Wamachinga waondolewe kando ya barabara kuepusha magonjwa ya milipuko na ajali za barabarani

Mars 12

JF-Expert Member
Feb 25, 2021
221
349
Labda itakua vigumu kueleweka lakini nimeonelea ni bora nikatoa ushauri kwa manispaa na halmashauri zetu kuwaondoa mama lishe, Wamachinga na vibanda vya kuuza kadi na kusajili simu vilivyoko mabarabarani. Sababu kuu ni kuwa utakuta wanauza chakula, matunda n.k kwenye vumbi na zinaponyesha mvua ndio kabisa.

Hali hii itatuletea kipindupindu (cholera), homa ya matumbo(Typhoid) n.k. sitoshe watembea kwa miguu inatubidi tutembee mabarabarani maana kwenye maeneo ya kupita watu (pedestrian pavements) wamejaa machinga na kutandaza bidhaa zao. Hili linasababisha watu hasa WANAFUNZI kugongwa na bajaji, bodaboda, daladala na hatari magari.

Tusiingize siasa kwenye suala hili. Wamachinga kama zilivyo nchi zingine nyingi wanawekewa maeneo makubwa saizi ya eneo lote la mfano Kibaha. Wanavyofanya wenzetu Afrika na nchi zingine hili eneo linakuwa makhsusi kwa ajili ya machinga. Kila aina ya bidhaa na vyakula na mpaka spea za magari unazikuta huko. Yaani unatoka kwenda huko unapata unachokitaka mpaka yanauzwa magari yaliyotumika. Miji inakuwa misafi inapendeza, wananchi wapo salama na machinga pia wanafanya biashara.

Niliwahi kuitembelea nchi ya Tunisia ikawauliza wenyeji hivi hapa Tunis hakuna machinga? Wakanijibu wapo ila tutakupeleka. Kwa kweli ilibidi nistaajabu kwani hilo eneo ni kubwa na unapata unachokitaka. Huduma zote zipo. Naomba wizara zinazohusika zitume wataalam wao nje wakaone wenzetu wanavyojipanga. HAKUNA SIASA KWENYE HILI. Maana tatizo letu Watanzania ni kulalamika tu, Tubadilike pamoja na umasikini wetu. Isitoshe inasikitisha kuwaona baadhi ya kina mama wanauza zambarau hivi najiuliza huyu anaungua juani kutwa nzima anapata nini kuendesha maisha yake?

Ni bora akaenda kulima kijijini. Kwahiyo hata watembea kwa miguu nao wana haki.

#Salaam za Jamhuri Ya Muungano waTanzania# Kaziiendelee
 
Habari .

Inasikitisha sana ukifuatilia page na post mbalimbali za Chadema wanavyotukanwa kwenye comments na wachangiaji.

Kuna group linaitwa Chadema in blood kule facebook yani kila wanachopost ni kutukanwa tu na watu, huko instagram ndiyo balaa kabisa, njoo Jamii forum hali ni hiyo hiyo!

Nimeangalia comments za kwenye hotuba ya Mbowe aliyoitoa akisema vibaya utawala wa hayati Magufuli, kwa kweli ni huzuni raia walivyomtukana Mbowe. Swali la kujiuliza Chadema imefikaje huku?

Enzi za Dr Slaa ulikuwa unavaa gwanda la Chadema kwa maringo yote ,leo tuvae kwa aibu ya kujifichaficha?

Je, Tundu Lisu ameharibu image ya chama baada ya kuanza kutetea mabeberu?

Je, ni Mbowe ameharibu image ya chama baada ya kuwa anaangushwa na konyagi anasingizia amepigwa na wasiojulikana?, au ule uongo
wake wa kuibia familia inapompeleka mahakamani anasingizia amefungiwa akaunti zake na serikali?

Kiukweli inahitajika tathimini ya haraka sana kuikoa na kuirudisha Chadema kwa wananchi ili waiamini tena kama zamani.
 
Mmejifunga kibwebwe kutumaliza! Hii ni kwa sababu hamtoi Suluhu (ooh sorry in Jesse John voice) hamtoi mbadala mtakaotupeleka.

Mimi najaribu kutoa mbadala!

Njia moja wapo ya kupunguza kadhia ni watu wafanye biashara kwa kutumia vichanja nadhifu na kwa muda wa siku ambao hauna msongamano wa magari na iwe ni siku tatu kwa wiki. Siku moja iwe ni ya muda mrefu na mbili ni muda ule usiona msongamnao. SIDO, na karakana binafsi zipewe kazi ya kutengeza vichanja nadhifu (ama neno lifananalo na hilo) na vichanja hivyo viwe vya kuhamishika kwa urahisi (viwe na mgurudumu) na hakuna kupanga bidhaa chini!

Mnaeweza kuongezea kuboresha hoja hii. Mfano kuhakikisha feeder roads zote za miji yote zinapitika kwa urahisi muda wote.
 
Back
Top Bottom