Wamachinga wafurahia uamuzi wa Rais Magufuli kutoa vitambulisho kwao. Waomba vitambulisho viongezwe tena.

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
IMG_0360.jpg


Uamuzi wa Rais Dk. John Pombe Magufuli wa kutoa vitambulisho kwa Wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) nchini, umepongezwa na kufurahiwa na Wafanyabiashara hao kwa madai kuwa, zitasaidia sana kuondokana na kero za kukimbizwa mara kwa mara na Askari wa mgambo.

Wafanyabiashara hao wamedai wanasubiri kwa hamu vitambulisho hivyo na kuipongeza sana hatua hiyo kuwa ni nzuri. "Kama biashara inafanyika bila bugudha, Sh. 20,000 ni kiwango kidogo kuchangia kwa mwaka. Wamachinga wengi hilo liko ndani ya uwezo wao."

Vitambulisho 25,000 vimetolewa kwa kila Mkoa na kitapatikana kwa gharama ya Tsh. 20,000 kila kimoja kwa lengo la kuwatambua Wafanyabiashara hao.

IMG_0362.JPG
 
Hayo ni nchi nzima
Mlipuko wa furaha nchi nzima. Kwa kweli hii ni Tz mpya. Wanyonge wanaelewa nini maana ya vitambulisho hivyo na kwanini ni muhimu kwao.

Wanaokula na kusaza hawaelewi wala hawatakaa wakaelewa. Mbaya zaidi hata waluoshauri jambo hili lifanyike wameanza kupinga.

Posho ya mabeberu haijawahi kumuacha mtu salama.

Queen Esther
 
Changamoto ya haraka inayopaswa kutatuliwa na Serikali, ni mtazamo potofu wa baadhi ya Wanachinga kudhani ukitoa hiyo 20,000 kwa ajili ya kitambulisho, basi utakuwa umemaliza. Ukweli ni kwamba, hiyo 20,000 haihusiani kabisa na ushuru unaotozwa na Halmashauri katika maeneo ya kibiashara yaliyoko kwenye Halmashauri. Mfano: ushuru wa soko, siyo kitu utakachosema kitafutwa kwani ndivyo vya so vya mapato ya Halmashauri wakati Tsh. 20,000 ni za Serikali Kuu kupitia TRA.

Ni vyema Serikali ili-address suala hili mapema.
 
Hao machinga wamekutana wap na kutoa iyo kaul moja????

Ni wafanyabiashara wa wap. Yan kauli imetolewa jna saa 7. Gazeti limechapishwa usiku. Duh

Kamachinga nliokutana nao wanadai wanshofu kubwa sana kama wakiletewa vtambulisho, wanajua kinachofata ni mfumo wa wao kulipa kodi.
 
Changamoto ya haraka inayopaswa kutatuliwa na Serikali, ni mtazamo potofu wa baadhi ya Wanachinga kudhani ukitoa hiyo 20,000 kwa ajili ya kitambulisho, basi utakuwa umemaliza. Ukweli ni kwamba, hiyo 20,000 haihusiani kabisa na ushuru unaotozwa na Halmashauri katika maeneo ya kibiashara yaliyoko kwenye Halmashauri. Mfano: ushuru wa soko, siyo kitu utakachosema kitafutwa kwani ndivyo vya so vya mapato ya Halmashauri wakati Tsh. 20,000 ni za Serikali Kuu kupitia TRA.

Ni vyema Serikali ili-address suala hili mapema.
Mkuu hilo nilakwako, raisi alisema wasisumbuliwe tena na mtu yoyote au mamlaka yoyote.
 
Sema Lumumba fc ndiyo mnaendelea kutumika kama zumali kunogesha nyimbo za watawala
 
Hao machinga wamekutana wap na kutoa iyo kaul moja????

Ni wafanyabiashara wa wap. Yan kauli imetolewa jna saa 7. Gazeti limechapishwa usiku. Duh
Lumumba wanashindwa kusema ukweli kuwa ile ni mbinu ya kujiongezea mapato maana kwa vitambulisho 670000 kwa 20000 ni bilioni 13 hizo
 
Mkuu hilo nilakwako, raisi alisema wasisumbuliwe tena na mtu yoyote au mamlaka yoyote.
Wacha kudanganyika iwe kwa bahati mbaya au makusudi hakuna cha huruma kwa machinga hapo ni kutafuta ela tu
 
Ni habari njema Tunaongeza wigo wa kodi. Changamoto nani anaratibu TRA ama wanasiasa waliokabidhiwa!? 4M ni kiwango cha juu sana kinaleta shida utambuzi.
Yaani kwa sasa watafanya kila mbinu kujikwamua kutafuta fedha
 
Hayo ni nchi nzima
Mlipuko wa furaha nchi nzima. Kwa kweli hii ni Tz mpya. Wanyonge wanaelewa nini maana ya vitambulisho hivyo na kwanini ni muhimu kwao.

Wanaokula na kusaza hawaelewi wala hawatakaa wakaelewa. Mbaya zaidi hata waluoshauri jambo hili lifanyike wameanza kupinga.

Posho ya mabeberu haijawahi kumuacha mtu salama.

Queen Esther

Hivi unaweza kusoma.tena wewe mwenyewe ukaelewa?
 
Lumumba wanashindwa kusema ukweli kuwa ile ni mbinu ya kujiongezea mapato maana kwa vitambulisho 670000 kwa 20000 ni bilioni 13 hizo
Haujui unataka nini ndugu yangu. Ulishaona wapi mtu akapewa haki lakini bila kuambiwa wajibu wake?
 
Changamoto ya haraka inayopaswa kutatuliwa na Serikali, ni mtazamo potofu wa baadhi ya Wanachinga kudhani ukitoa hiyo 20,000 kwa ajili ya kitambulisho, basi utakuwa umemaliza. Ukweli ni kwamba, hiyo 20,000 haihusiani kabisa na ushuru unaotozwa na Halmashauri katika maeneo ya kibiashara yaliyoko kwenye Halmashauri. Mfano: ushuru wa soko, siyo kitu utakachosema kitafutwa kwani ndivyo vya so vya mapato ya Halmashauri wakati Tsh. 20,000 ni za Serikali Kuu kupitia TRA.

Ni vyema Serikali ili-address suala hili mapema.
Yaani naiona kodi ya kichwa inarudi kwa speed ya bomberdier
 
View attachment 963920

Uamuzi wa Rais Dk. John Pombe Magufuli wa kutoa vitambulisho kwa Wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) nchini, umepongezwa na kufurahiwa na Wafanyabiashara hao kwa madai kuwa, zitasaidia sana kuondokana na kero za kukimbizwa mara kwa mara na Askari wa mgambo.

Wafanyabiashara hao wamedai wanasubiri kwa hamu vitambulisho hivyo na kuipongeza sana hatua hiyo kuwa ni nzuri. "Kama biashara inafanyika bila bugudha, Sh. 20,000 ni kiwango kidogo kuchangia kwa mwaka. Wamachinga wengi hilo liko ndani ya uwezo wao."

Vitambulisho 25,000 vimetolewa kwa kila Mkoa na kitapatikana kwa gharama ya Tsh. 20,000 kila kimoja kwa lengo la kuwatambua Wafanyabiashara hao.

View attachment 963918
Hilo gazeti ni uhuru au tanzanite
 
Changamoto ya haraka inayopaswa kutatuliwa na Serikali, ni mtazamo potofu wa baadhi ya Wanachinga kudhani ukitoa hiyo 20,000 kwa ajili ya kitambulisho, basi utakuwa umemaliza. Ukweli ni kwamba, hiyo 20,000 haihusiani kabisa na ushuru unaotozwa na Halmashauri katika maeneo ya kibiashara yaliyoko kwenye Halmashauri. Mfano: ushuru wa soko, siyo kitu utakachosema kitafutwa kwani ndivyo vya so vya mapato ya Halmashauri wakati Tsh. 20,000 ni za Serikali Kuu kupitia TRA.

Ni vyema Serikali ili-address suala hili mapema.
kwani wao wanaelewa hayo??badaye watakuja kulia na kuanza kuwaona TRA,wanawaonea na jiwe kama kawaida yake anakaa pembeni ili asionekane mbaya kumbe ndio maelekezo yake!!hiyo 20,000 ni ya kitambulisho ili uingizwe kwenye system hapo sasa ndio uanze kukamuliwa!!
 
Kama mungekuwa na nia ya dhati ya kuwasaidia machinga hakukuwa na haja yakuwatoza hiyo sh 20000 maana hao machinga pia ni watanzania ambao wanalipishwa ushuru mbali mbali kupitia kwenye shughuli zao.muwaache kuwadanganya watu hatudanganyiki
Haujui unataka nini ndugu yangu. Ulishaona wapi mtu akapewa haki lakini bila kuambiwa wajibu wake?
 
kwani wao wanaelewa hayo??badaye watakuja kulia na kuanza kuwaona TRA,wanawaonea na jiwe kama kawaida yake anakaa pembeni ili asionekane mbaya kumbe ndio maelekezo yake!!hiyo 20,000 ni ya kitambulisho ili uingizwe kwenye system hapo sasa ndio uanze kukamuliwa!!
Hawampati mtu
 
Back
Top Bottom