Wamachinga Kahama waonja "Joto ya jiwe" ya Polisi na Mgambo sambamba na Mkurugenzi wa Halmashauri

Idea nzuri hii mkuu, kwasababu inaonakana si rahisi kuwalazimisha waende kwenye hayo masoko yalijengwa kwa sababu mbali mbali. Basi ni bora njia hiyo itumike itakua poa sana.
Nimeona Waafuganistan wanagawana duka moja watatu na wanachangia kodi pamoja. Kama halmashauri ikiweka kodi laki moja kwa mwezi wanaweza kugawana mwenye leseni akatoa 30 na wenzake kutoa 35x2
 
Kuna Mama mmoja alisikika akinena baada ya kushiba urojo, viazi mbatata na juisi ya miwa "Mimi na mwendazake ni wale wale, tofauti yetu ni jinsia tu, msini dharau kisa mimi ni mwanamke, zege hailali, kazi iendelee, na nawaahidi mimi ni muendelezo wake mwendazake".

Jopo la wateja waliokua pale kilingeni walicheka sana kana kwamba ni kichekesho.

#Ama kweli Kazi Inaendelea.
Wewe acha upunguani

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Kuna Mama mmoja alisikika akinena baada ya kushiba urojo, viazi mbatata na juisi ya miwa "Mimi na mwendazake ni wale wale, tofauti yetu ni jinsia tu, msini dharau kisa mimi ni mwanamke, zege hailali, kazi iendelee, na nawaahidi mimi ni muendelezo wake mwendazake".

Jopo la wateja waliokua pale kilingeni walicheka sana kana kwamba ni kichekesho.

#Ama kweli Kazi Inaendelea.
Mwendazake hakuwanyanyasa machinga
 
Hatujawahi kuwa na upungufu wa wabaunifu wa majengo. Tatizo la umachinga ni uchumi unaoshindwa kutoa ajira nzuri na rasmi katika sekta muhimu.Ufunguzi wake hauwezi kuwa kujaza majengo barabarani.
Wanafunzi wa chuo cha Ardhi wanaweza kupewa project ya kubuni majengo kando ya barabara kuu. Halmashauri ziyajenge na kupangisha Wamachinga.

Mji utakua msafi, watauza bidhaa kwa heshima na hawataki na adha za mvua na jua.
 
Toka lini cdm mmeanza kutetea wamachinga? Nyie tunajua ni watetezi wa mabeberu!

Kwa unafiki mumo sana. Hilo kama limetokea litamalizwa tu lakini sio kete ya cdm kujipenyeza.

Cdm mmeshatuonyesha rangi zenu halisi endeleeni kuvuna mlichopanga. Juzi juzi tu hapa kutwa kumchamba aliyekua mtetezi wa wanyonge na kuwakebehi hao hao wamachinga waliokuwa wanamlilia! Mlifika mbali mpaka mkafikia kutukana kabila la wasukuma, haya cdm ngoja tuone.
Huna akili.
 
Kama unafanya biashara maeneo yasiyo rasim na ukaambiwa utoke hutoki utapigwa tu (in Pinda’s voice )
 
Kama wanafanya umachinga ili kujikimu kimaisha hakuna tatizo. Hawa ni watanzania wenzetu ambao wanatafuta chochote ili waweze kuishi.

Kama mimi na wewe tumefanikiwa kuishi maisha ambayo hayahusiani na umachinga, basi tushukuru sana. Tusitumie shibe yetu kutaka kuharibu shibe za wengine ambazo hata kuzipata kwake ni mbinde
 
"Wakati mnaendelea na mijadala mingine nawafahamisha kwamba Mkurugenzi wa Kahama Anderson Msumba akiwa na Polisi & Mgambo wamewavamia wafanyabiasha wa Kahama na kuwapiga virungu kisha wameiba bidhaa za Wafanyabiasha hao kwa madai kuwa wanafanya biashara maeneo ambayo sio sahihi."- Hilda Newton

View attachment 1857843

E0NhMwdXIAAW0HL (1).jpeg
 
Hii Nchi tuibadili jina iwe The United Republic of Umachingania and Zanzibar UMAZANIA.
 
Nimeona Waafuganistan wanagawana duka moja watatu na wanachangia kodi pamoja. Kama halmashauri ikiweka kodi laki moja kwa mwezi wanaweza kugawana mwenye leseni akatoa 30 na wenzake kutoa 35x2
Wale jamaa hata wanawake wanashea hawanaga shida,Vita vya muda mrefu vimeaathiri sana

USSR
 
"Wakati mnaendelea na mijadala mingine nawafahamisha kwamba Mkurugenzi wa Kahama Anderson Msumba akiwa na Polisi & Mgambo wamewavamia wafanyabiasha wa Kahama na kuwapiga virungu kisha wameiba bidhaa za Wafanyabiasha hao kwa madai kuwa wanafanya biashara maeneo ambayo sio sahihi."- Hilda Newton

View attachment 1857843
Kwanini hao machinga wanadekezwa sana? yaani wao kila mahali ni mabiashara yao tu. Hata kwenye choo wanaweka biashara.
 
Toka lini cdm mmeanza kutetea wamachinga? Nyie tunajua ni watetezi wa mabeberu!

Kwa unafiki mumo sana. Hilo kama limetokea litamalizwa tu lakini sio kete ya cdm kujipenyeza.

Cdm mmeshatuonyesha rangi zenu halisi endeleeni kuvuna mlichopanga. Juzi juzi tu hapa kutwa kumchamba aliyekua mtetezi wa wanyonge na kuwakebehi hao hao wamachinga waliokuwa wanamlilia! Mlifika mbali mpaka mkafikia kutukana kabila la wasukuma, haya cdm ngoja tuone.
Kwa taarifa yako Magufuli aliamua kuwaachia hao wamachinga wafanye biashara holela ili kuwawin, baada ya kugundua wamachinga wengi wana mapenzi na Cdm. Hivyo kwa sasa ccm imebidi ifanye penzi la shuruti na wamachinga ili kuhakikisha cdm hawawasogelei, na kutengeneza ushawishi zaidi kwao. Ila tatizo ni moja, penzi la lazima halidumu hata mtumie njia gani.
 
Kama wanafanya umachinga ili kujikimu kimaisha hakuna tatizo. Hawa ni watanzania wenzetu ambao wanatafuta chochote ili waweze kuishi.

Kama mimi na wewe tumefanikiwa kuishi maisha ambayo hayahusiani na umachinga, basi tushukuru sana. Tusitumie shibe yetu kutaka kuharibu shibe za wengine ambazo hata kuzipata kwake ni mbinde
Ndugu uko sahihi laini hii haimanishi wazibe njia za waenda kwa miguu,ngazi za kupandia zimejaa wao,barabara(ndani ya barabara),kwani uko mkoa gani mwenzetu inawezekana huko kero za hawa hazipo?
Hizo fujo ndizo zinamfanya kila mmoja akimbilie jijini kwani anaweza fanya biashara popote,kuna watu nilikuwa nawaambia kama umeshindwa kufanya bishara hizi ndogo ndogo kipindi cha JPM basi hutaweza.Ni ruksa,ukienda posta mbele ya ofisi za watu mama ntilie kibao,pale Mwanza maeneo ya miti mirefu kuna sehemu fence za watu zimezibwa na vibanda wameachiwa gate tu la kuingilia na kutoka hata hiyo fence haina maana.
 
Kwa taarifa yako Magufuli aliamua kuwaachia hao wamachinga wafanye biashara holela ili kuwawin, baada ya kugundua wamachinga wengi wana mapenzi na Cdm. Hivyo kwa sasa ccm imebidi ifanye penzi la shuruti na wamachinga ili kuhakikisha cdm hawawasogelei, na kutengeneza ushawishi zaidi kwao. Ila tatizo ni moja, penzi la lazima halidumu hata mtumie njia gani.
Ndugu hii signature yako "'Ukitaka kuwa masikini nchi hii, danganywa kwenda kulima. Utalima kwa gharama zako lakini wakati wa kuuza utapangiwa bei na anayeishi mjini"
Wenye mamlaka wameiona kweli?Mbona unatuvunja moyo sisi wakulima? 🤣 🤣 🤣
 
"Wakati mnaendelea na mijadala mingine nawafahamisha kwamba Mkurugenzi wa Kahama Anderson Msumba akiwa na Polisi & Mgambo wamewavamia wafanyabiasha wa Kahama na kuwapiga virungu kisha wameiba bidhaa za Wafanyabiasha hao kwa madai kuwa wanafanya biashara maeneo ambayo sio sahihi."- Hilda Newton

View attachment 1857843
Huyu Hilda Newton ni binti mzushi na muongomuongo sana....

Sijui hizo siasa zake za kizushi zitamfikisha wapi.......

Hao wamachinga wameambiwa wahamie maeneo yaliyopangwa kiutaratibu sasa kosa la DED ni nini?!!! Khaaa 😲😲😲
 
Back
Top Bottom