Mujumba
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 853
- 306
WAFANYABIASHARA katika jengo la Machinga Complex, Dar es Salaaa, wamefichua mpango wa baadhi ya wanasiasa kuwashawishi ili washiriki maandamano. Mbali ya hilo, wamewaomba Watanzania wakubali kwamba serikali ya awamu ya nne imefanya na inaendelea kufanya mambo makubwa na mazuri yenye lengo la kuboresha biashara zao, hivyo wasibezwe na kukatishwa tamaa.
Abubakary Rakesh alisema hayo jana wakati akisoma risala ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyabiashara Ndogo Ndogo Machinga katika mkutano maalumu uliofanyika kwenye ukumbi wa Korea. Rakesh alisema kutokutekelezwa na kuzipatia ufumbuzi kero zinazowakabili kunatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa vikundi vya wafanyabiasahara kutaka kushiriki maandamano na kuleta vurugu.
Aliwaomba machinga watulie kwani utulivu huo ndiyo utakuwa nyenzo za kumwezesha Rais Jakaya Kikwete kufanya juhudi za utekelezaji wa ahadi yake ya ujenzi wa machinga sita zikiwemo mbili za jijini Dar es Salaam.
Tunaomba na kuwasihi baadhi ya viongozi wa vyama vya wafanyabiashara ndogo ndogo na wafanyabiashara wenyewe kuacha kutumiwa na kutumika isivyo halali na wanasiasa kwa ajili ya manufaa ya watu wachache kisiasa, alisema.
Rakesh aliwashauri wanasiasa kuacha kuwatumia vibaya baadhi ya viongozi wa wafanyabiashara hao kwa manufaa yao binafsi.
Alisema wafanyabiashara hao ni moja ya makundi ya wananchi ambao wameathirika na kukosekana kwa umeme na kwamba hawapendezewi na hali hiyo.
Pia, wameomba wapunguziwe kodi katika jengo la Machinga Complex kutoka sh. 60,000 kwa mwezi hadi sh. 20,000 na wamelaani kitendo kilichofanywa na Manispaa ya Kinondoni, kuwavunjia vibanda wafanyabiashara wa eneo la Big Brother, Urafiki.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema Dar es Salaam ipo imara na inaendelea, hivyo wasiwadanganye kwa kutumia udhaifu wao. Alisema majina ya wanasiasa wanaotaka maandamano hayo wanayo.
Abubakary Rakesh alisema hayo jana wakati akisoma risala ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyabiashara Ndogo Ndogo Machinga katika mkutano maalumu uliofanyika kwenye ukumbi wa Korea. Rakesh alisema kutokutekelezwa na kuzipatia ufumbuzi kero zinazowakabili kunatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa vikundi vya wafanyabiasahara kutaka kushiriki maandamano na kuleta vurugu.
Aliwaomba machinga watulie kwani utulivu huo ndiyo utakuwa nyenzo za kumwezesha Rais Jakaya Kikwete kufanya juhudi za utekelezaji wa ahadi yake ya ujenzi wa machinga sita zikiwemo mbili za jijini Dar es Salaam.
Tunaomba na kuwasihi baadhi ya viongozi wa vyama vya wafanyabiashara ndogo ndogo na wafanyabiashara wenyewe kuacha kutumiwa na kutumika isivyo halali na wanasiasa kwa ajili ya manufaa ya watu wachache kisiasa, alisema.
Rakesh aliwashauri wanasiasa kuacha kuwatumia vibaya baadhi ya viongozi wa wafanyabiashara hao kwa manufaa yao binafsi.
Alisema wafanyabiashara hao ni moja ya makundi ya wananchi ambao wameathirika na kukosekana kwa umeme na kwamba hawapendezewi na hali hiyo.
Pia, wameomba wapunguziwe kodi katika jengo la Machinga Complex kutoka sh. 60,000 kwa mwezi hadi sh. 20,000 na wamelaani kitendo kilichofanywa na Manispaa ya Kinondoni, kuwavunjia vibanda wafanyabiashara wa eneo la Big Brother, Urafiki.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema Dar es Salaam ipo imara na inaendelea, hivyo wasiwadanganye kwa kutumia udhaifu wao. Alisema majina ya wanasiasa wanaotaka maandamano hayo wanayo.