Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Majuzi Alhamisi nilikuwa sehemu nyakati za jioni hivi, nikasikia kwenye taarifa ya habari ya Redio Uhuru ikisema kwamba Mwenyekiti wa WAMA (ile Taasisi ya Fisti Ledi wa inji hii ya Bongo) amewaambia wananchi kwamba wakichagua CCM Taasisi ya WAMA itachukua watoto wawili kutoka kila wilaya na kuwagharamia masomo. Sasa mimi nikajiuliza WAMA ni chama cha siasa mpaka kishiriki kwenye kampeni za uchaguzi moja kwa moja bila kificho?. Nakumbuka wakati fulani Prof. Anna Tibaijuka alikuwa anaongoza NGO ya wanawake (jina limenitoka), lakini NGO ile ilipigwa stop kufanya shughuli zake kwa tuhuma za kujishughulisha na shughuli za kisiasa ikiegemea Upinzani. Vipi leo WAMA wanafanya hayo tena kwa uwazi halafu wahusika wanakaa kimya?