Walitaka Bunge Live ili watie aibu Bunge

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,556
29,642
Nimekuwa naangalia mfululizo clip ya video ambayo inaonyesha namna Mnyika alivyoamua kwa dhati kuchafua hali ya hewa Bungeni...

Alikuwa na nafasi ya kusikilizwa lakini aliamua kudhalilisha kiti cha Spika huku akijua bunge lipo Live. Hiki ndicho wapinzani wanachokitaka yaani kutengeneza motions ndani ya Bunge ili waonekane wanaonewa.

Najua wapo Watanzania wanaoamini mhalifu yeyote ni shujaa. Ni wazi Mnyika amefanya uhalifu dhidi ya kiti cha Spika. Kama alikuwa na malalamiko angetumia utaratibu wa kukaa na kuinuka tena kuhoji mbunge aliyemuita yeye ni MWIZI. Lakini najiuliza kama yeye siyo mwizi kweli ya nini kuhamaki? Angetumia busara.

Kwa namna alivyokuwa anaongea alionekana kama amepiga balimi kadhaa. Hata maiki ilipokuwa imezimwa lakini bado alikuwa anaporomoka maneno yasiyofaa.

Halafun najiuliza wanaharakati wa Tanzania ambapo uhuni unaofanywa na wanasiasa uchwara wa upinzani wanaufumbia macho, lakini wakichukuliwa hatua wanahaha kwenye media kuwa nchi haina Demokrasia.

Jamani hii Golden Fleet ni ya nani kule ACACIA?
 
JPM amewachanganya wajomba zetuu. yaanii
Wamevulugwa. kwa saasa hawana cha kuwambia wanainchiii.

JPM. MUngu akubariki kwani raisi kama wewe ndo tulikusubiria miaka mingi.
 
Hayo ni matokoe ya upendeleo,angesema maneno hayo mbunge wa upinzani akimtaja mwenzake mwizi ndio mngejua spika ana masikio 100!
Kutetea mwizi kwa style ile kunamsababisha naye awemo kwenye kundi hilo
 
Nimekuwa naangalia mfululizo clip ya video ambayo inaonyesha namna Mnyika alivyoamua kwa dhati kuchafua hali ya hewa Bungeni...

Alikuwa na nafasi ya kusikilizwa lakini aliamua kudhalilisha kiti cha Spika huku akijua bunge lipo Live. Hiki ndicho wapinzani wanachokitaka yaani kutengeneza motions ndani ya Bunge ili waonekane wanaonewa.

Najua wapo Watanzania wanaoamini mhalifu yeyote ni shujaa. Ni wazi Mnyika amefanya uhalifu dhidi ya kiti cha Spika. Kama alikuwa na malalamiko angetumia utaratibu wa kukaa na kuinuka tena kuhoji mbunge aliyemuita yeye ni MWIZI. Lakini najiuliza kama yeye siyo mwizi kweli ya nini kuhamaki? Angetumia busara.

Kwa namna alivyokuwa anaongea alionekana kama amepiga balimi kadhaa. Hata maiki ilipokuwa imezimwa lakini bado alikuwa anaporomoka maneno yasiyofaa.

Halafun najiuliza wanaharakati wa Tanzania ambapo uhuni unaofanywa na wanasiasa uchwara wa upinzani wanaufumbia macho, lakini wakichukuliwa hatua wanahaha kwenye media kuwa nchi haina Demokrasia.

Jamani hii Golden Fleet ni ya nani kule ACACIA?

Hizi akili za kibashite hizi taabu tupu! Hivi kwa "scenario" ya jana aliyetia aibu ni Mnyika au ni Ndungai?
 
Back
Top Bottom