Waliotandikwa viboko Ikulu hawa hapa

Kuhusu kuua huyu mzee hakuwa muuaji hata kidogo. Hapa tumpe haki yake kabisa. Hata wale waliostahili kuuawa yeye hakusaini wauawe. Katika uongozi wake wa zaidi ya miaka 20 nasikia alisaini wauawe watu wawili tu ( ambao hata wewe ungesahini). Ina semekana mmoja alimuua binti yake ili apate malipo ya bima.

Vile vile nakumbuka Marehemu Mohamed Babu (RIP) kusema kuwa Nyerere alimwokoa asiuawe, hivyo alikuwa anawajali hata watu wengine mzee wa watu.

Kwa upande wa kuwatandika Bakora kama ilivyoanishwa na TBC katika kipindi chake Mimi siungi mkono kabisa, nafikiri hapa alipotoka. Mwanzoni nilifikiri ni porojo kumbe wapi.Hii inaonyesha ni jinsi gani akishaona jambo lina manufaa,.alikuwa anajituma kupita kiasi kuhakikisha jambo hilo linatekelezwa.

Kwa ujumla mzee huyu alikuwa na nia nzuri kabisa karibu katika kila “move” aliyoianzisha mfano JKT, vijiji vya Ujamaa n.k. Lakini katika kila jambo kuna uzuri na ubaya wake. Kwa vijiji vya ujamaa ukitembelea vijiji vya nchi nyingine kama Kenya na Uganda ndipo utajua uzuri wa wazo lile. Huku kwetu kuna mpango angalau lkn kwa wenzetu ni tofauti kabisa.

Tukirudi nyuma kuna mtu kaongelea porojo juu ya viongozi wetu wakuu, hasa Mwl. Na mzee Kawawa kweli kwa watanzania “Documentation” ni sifuri. Mambo mengi ya uongo yanasemwa, kwa kuwa hakuna anaye yakanusha yanaonekana ya kweli wakati sivyo.

Mwisho mjadala huu ulianzishwa kwa nia ya kupata mawazo ya watu juu ya mambo yaliyojiri siku za nyuma, Hii itatusaidia wakati mwingine tukipewa nafasi tujue jinsi ya kukabiliana na changamoto mbali mbali katika utendaji kazi.

Majina yaliyotumika mwanzoni BMW na JKN ni ya kusadikika tu kwa nia ya kuanzisha mjadala na kichwa cha habari kwa nia hiyo hiyo pia.

Tatizo standards zetu lax za kiafrika tunataka kuua rais mpaka aamrishe majeshi kama alivyoamrisha Ben Mkapa Jan 17 visiwani, au achinje kinyama kama Iddi Amin.

The "Great Leap Forward" na "Cultural Revolution" (tulipokopi Siasa ni Kilimo na mambo mengi ya Azimio la Arusha) the two Maoist initiatives killed millions in China, and Mao is held responsible even though he may not have ordered soldiers to kill people directly. Ukiendesha villagization bila ya kufanya a small pilot na kuona effects vizuri halafu watu wakafa kutokana na bad policy and implementation hujaua?

Tuache kuwa na lax standards, hizi ndizo zinatusababisha tubaki kwenye umaskini day in day out.
 
Mkitaka kufahamu mazuri ya Mwalimu angalieni yanayotuandama sasa hasa baada ya yeye kuwa ameondoka hapa DUNIANI. Angalau nimemsikia Msekwa jana akikiri hadharani kuwa walikosea kuiacha MIIKO na MAADILI ya UONGOZI alioiacha Mwalimu.

I can equally say ukitaka kufahamu jinsi Mwalimu alivyokuwa dikteta wa one man show aliyeshindwa kuandaa leadership ya kuja kuchukua uongozi baada yake angalia uongozi wote baada yake.
 
Bluray,
Kama kuna kosa ambalo naweza kusema Nyerere alifanya ni hili la Urithi ktk UONGOZI..
Kifupi navyomjua mimi Nyerere hakuwa mjanja katika hilo, hata wanawe mwenyewe aliwapenda zaidi waliopwaya kiakili..Sielewi kama ilikuwa ugonjwa au alitaka zaidi control..
Pengine ni jadi yetu maanake sisi Miafrika, mtoto juha juha na mpole sana ndiye tunampa sifa za mtoto mzuri! Yule makeke na anapenda kum challenge mzee huyo ni mhuni na hasara atapigwa laana.
 
Bluray,
Kama kuna kosa ambalo naweza kusema Nyerere alifanya ni hili la Urithi ktk UONGOZI..
Kifupi navyomjua mimi Nyerere hakuwa mjanja katika hilo, hata wanawe mwenyewe aliwapenda zaidi waliopwaya kiakili..Sielewi kama ilikuwa ugonjwa au alitaka zaidi control..
Pengine ni jadi yetu maanake sisi Miafrika, mtoto juha juha na mpole sana ndiye tunampa sifa za mtoto mzuri! Yule makeke na anapenda kum challenge mzee huyo ni mhuni na hasara atapigwa laana.

Right,

Kwa mfano,

Ile account ya Warioba kuhusu constitutional crisis aliyotaka kuleta Nyerere kwa ku force appointment ya Mgonja ina reveal mengi sana, ina confirm mpaka alichotaka ku debunk Warioba.

Nyerere alipenda kuwa one man show mwenye control zote, ndiyo maana alimpenda Karume pamoja na mapepe yake yote kwa sababu ilipofika kwa Nyerere Karume alifunga breki.Ndiyo maana alikorofishana na kina Kambona, Bibi Titi na Aboud Jumbe Mwinyi kwa sababu walikuwa wana m challenge.Kambona hakutaka upuuzi wa chama kimoja back in the sixties, unaona kabisa Nyerere is hardly the saint he is made out to be.

Ganesh yuko wapi aje amtetee mzee wake hapa na personal anecdotes.
 
Blueray,
Uongozi hauandaliwi na mtu mwingine. Uongozi ni hulka. Mwulize Mkapa alijifunza nini kutoka kwa Nyerere. Mwulize Obama aliandaliwa na nani?
 
Blueray,
Uongozi hauandaliwi na mtu mwingine. Uongozi ni hulka. Mwulize Mkapa alijifunza nini kutoka kwa Nyerere. Mwulize Obama aliandaliwa na nani?

Hata mimi nilitaka kumjibu hivyo hivyo. You either have it or you don't!
 
Blueray,
Uongozi hauandaliwi na mtu mwingine. Uongozi ni hulka. Mwulize Mkapa alijifunza nini kutoka kwa Nyerere. Mwulize Obama aliandaliwa na nani?

ndiyo nyie nyie mnaoacha watoto bila ya kuwaandaa kwa maisha.

Uongozi ni hulka na si kila mtu ana hulka ya uongozi.Tukishajua hilo, rais, kwa sababu the buck stops at his desk, anatakiwa kuchagua watu wenye hulka ya uongozi na kuwaweka kwenye team yake, aka wa groom kiasi kwamba akiondoka yeye wawe na uwezo wa kuongoza.

Sasa obviously Nyerere alikuwa failure, kitu pekee chenye jina lake kilicho survive mpaka sasa ni muungano, ambao unakufa soon anyway.Kwa hiyo sitegemei failure huyu awe na uwezo wa ku groom watu waende kuongoza nchi.
 
ndiyo nyie nyie mnaoacha watoto bila ya kuwaandaa kwa maisha.

Uongozi ni hulka na si kila mtu ana hulka ya uongozi.Tukishajua hilo, rais, kwa sababu the buck stops at his desk, anatakiwa kuchagua watu wenye hulka ya uongozi na kuwaweka kwenye team yake, aka wa groom kiasi kwamba akiondoka yeye wawe na uwezo wa kuongoza.

Mkapa alikuwa groomed. Hilo halina ubishi. Lakini mtu huwezi kutabiri tabia ya mtu baadae itakuwaje. Sasa kwa hilo nalo umlaumu Nyerere? Puliiiiiiz
 
Ukweli wa mambo naanza kuona kwanini MIAFLIKA HIPO ILIVYO. Mawazo ni kitu muhimu sana. Kushabikia kupiga viboko ndio kumejenga nidhamu ya woga. Na sishangahi kwanini mijitu kama JK iliyoenda shule kwa nidhamu ya woga kushindwa kuongoza.
 
ndiyo nyie nyie mnaoacha watoto bila ya kuwaandaa kwa maisha.

Uongozi ni hulka na si kila mtu ana hulka ya uongozi.Tukishajua hilo, rais, kwa sababu the buck stops at his desk, anatakiwa kuchagua watu wenye hulka ya uongozi na kuwaweka kwenye team yake, aka wa groom kiasi kwamba akiondoka yeye wawe na uwezo wa kuongoza.

Sasa obviously Nyerere alikuwa failure, kitu pekee chenye jina lake kilicho survive mpaka sasa ni muungano, ambao unakufa soon anyway.Kwa hiyo sitegemei failure huyu awe na uwezo wa ku groom watu waende kuongoza nchi.
Julius,
Nilitaka kukupa Thanks lakini leo computer yangu imegoma.
Blueray,
Wala hunifahamu na huwezi kunifahamu nyuma ya keyboard. For yr information mwanangu wa kwanza amegraduate he is working for the State Department. My second child is graduating in May 2010. Na by the way huwezi kuchagua mtu kuwa anafaa kuongoza, especially among Watanzania ambao sasa imedhihirika wote walikuwa wanafiki mbele ya Mwalimu. Na labda hilo ndilo kosa alilofanya Mwalimu. He was wrong on Mkapa, he was wrong on Salim just as he was wrong on Kenyatta. Obama alichaguliwa na nani vile kuwa kiongozi wa Marekani? Uongozi ni hulka!
 
Bluray,

Mkuu katika hilo mimi nipo na Nyerere.. Tanzania inahitaji Dikteta huu mpango wa Ubia umetufikisha hapa tulipo. JK anashindwa kufanya maamuzi muhimu kwa sababu nyuma yake kuna wajanja kupindukia...

Yaani ni jadi ya Miafrika mkuu wangu. Kumsaidia ndugu yako ni jambo zuri sana lakini ukituma fedha kwa nduguyo zitaliwa. Ukituma ki mini bus utakikuta juu ya mawe na hakuna akiba bank, haya usiposaidia nduguzo wewe ni mgumu, mshenzi na Mbinafsi. Lipi bora! wakati mwingine kuwa Mbinafsi inasaidia sana maanake tunatuma fedha Bongo kwa maelfu hakuna kinachoendelea..Kuwa kiongozi wa familia ya Kiafrika ni jukumu kubwa na gumu kuliko kitu chochoite, isipokuwa kumchagua mbora kati ya nduiguzo ndio muhimu, wachache wameweza kufanikiwa.

Nyerere kama sisi wengine hakuwa na ujanja huo, urithi ni tatizo la Kiafrika ndio maana Wazee wetu wanapokufa na mali zao huenda kaburini..mifano ni mingi sana (i.s Mzee marehemu Lubama)yaani taifa letu linakufa kiuongozi kama familia zetu..
 
Bluray,

Mkuu katika hilo mimi nipo na Nyerere.. Tanzania inahitaji Dikteta huu mpango wa Ubia umetufikisha hapa tulipo. JK anashindwa kufanya maamuzi muhimu kwa sababu nyuma yake kuna wajanja kupindukia...
Unahitaji dikteta. Nionyeshe dikteta mmoja wa Afrika aliyefanya vizuri?
 
Ukweli wa mambo naanza kuona kwanini MIAFLIKA HIPO ILIVYO. Mawazo ni kitu muhimu sana. Kushabikia kupiga viboko ndio kumejenga nidhamu ya woga. Na sishangahi kwanini mijitu kama JK iliyoenda shule kwa nidhamu ya woga kushindwa kuongoza.

JK Kaenda shule wapi? Hiyo degree ya siasa za DARUSO?

Hivi ushawahi kumsikia JK anaongea kama mchumi? Hata Zitto anaweka analysis za uchumi zilizokuwa mara 10 zaidi ya utumbo wa JK.
 
Unahitaji dikteta. Nionyeshe dikteta mmoja wa Afrika aliyefanya vizuri?

Acha Afrika..kwani Afrika ni nchi gani inayofanya vizuri ukiondoa Afrika Kusini. Wapi duniani dikteta aliyefanya vizuri?

Hapa watu wasichanganye kati ya rule of law na dictatorship? Vitu viwili tofauti kabisa
 
Zakumi,
Muamar Ghadafi na Hussein Mubarak hawa wamefanya vizuri kuliko marais wote wa demokrasia combined...

Hapa tunaona kabisa kwamba approaches zetu ziko so different hatuwezi kukubaliana chochote cha msingi.

Gaddafi amefanya kizuri gani ambacho mtu yeyote mwenye mafuta na uroho uliodhibitiwa angeshindwa? Mubarak amefanya kizuri gani watu wanagombania mikate huko Misri mpaka mwaka huu?
 
Acha Afrika..kwani Afrika ni nchi gani inayofanya vizuri ukiondoa Afrika Kusini. Wapi duniani dikteta aliyefanya vizuri?

Hapa watu wasichanganye kati ya rule of law na dictatorship? Vitu viwili tofauti kabisa

Tuko pamoja. Rule of law na udikteta ni vitu viwili tofauti. Lakini wajomba kwa kuona hawaendelei wanataka kukimbilia udikteta. Mchukueni Mugabe.
 
Tuko pamoja. Rule of law na udikteta ni vitu viwili tofauti. Lakini wajomba kwa kuona hawaendelei wanataka kukimbilia udikteta. Mchukueni Mugabe.

Sisi hatuna rule of law! Hata semblance ya rule of law hatuna. Tungekuwa na rule of law kusingekuwa na huu ufisadi uliopo sasa.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom