Waliosoma miaka ya 90's-00's wamesoma kwa shida kuliko miaka iliyopita,60's-70's

Luqman mohamedy

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
892
1,226
Habari wanaJF

Nia ya kuandika uzi huu ni kuondoa fikra mgando kuwa waliosoma enzi za Mwalimu walipata shida kuliko waliosoma enzi za ruksa na kuendelea.

Hizi ndizo sababu za kubeba hoja yangu

(1) Kwa Miaka ya kuanzia 60-80 idadi ya watu ilikuwa kidogo, japo ya uchache wa taasisi za elimu ila kila mmoja mwenye nia na muamko wa kusoma aliweza kupata nafasi. Kilichokuwa kinahitajika ni juhudi binafsi tu na wachache waliokomaa walitoboa.

(2) Kwa miaka ya 60-70 elimu ya juu ilikuwa ikitolewa bure kabisa ukilinganisha na hii miaka ya karibuni elimu imegeuka pesa, kama huna pesa basi elimu utaisikia tu kwahiyo wasomi wengi wamekuwa wakipata misukosuko inayowapa msongo wa mawazo kipindi cha masomo yao na kushindwa kuzingatia masomo yao.

(3) Kwa miaka ya 60-70 ajira baada ya elimu ilikuwa ni uhakika, kwahiyo waliokuwa masomoni kwa kipindi hicho hawakuwa na wasiwasi kabisa wa ajira baada ya masomo, ukilinganisha na miaka ya sasa wasomi wengi wamekuwa wakisoma na stress za wapi wataelekea baada ya masomo yao.

(4) Kwa miaka 60-70 ubora wa elimu uliweza kudhibitiwa sababu ya uchache wa taasisi za elimu, kwahiyo wasomi wengi walitoka wakiwa na ubora mmoja.
Tofauti na sasa ubora wa elimu unategemeana na bajeti ya taasisi utayoenda na kuna taasisi ukizipita elimu yako inadharauliwa.

Hizo ndizo baadhi ya hoja zangu zikipingana na kauli ya wengi wakidai vijana wa sasa wanasoma kwa raha sababu pekee ikiwa ni teknolojia, kazi kurahisishwa na computer.

Kama utapingana nami unaruhusiwa kupinga kwa hoja sio kejeli.

Karibu na hoja yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lazima waseme kuwa wanasoma kwa raha kwakuwa kwasababu kwanza hawaumizi vichwa mitihani inavujishwa,mwanafunzi anaingia kwenye chumba Cha mtihani na maijbu mfukoni,pili hata miundo ya mitihani nayo ni rafiki kwao Kama kwa shule za msingi utakuta majibu ya kuchagua kwa kila somo yaani npaka hisabati wanajichagulia tu majibu,tatu hakuna kuloa umande ukitaka kwenda shuleni ni mwendo wa school bus,daladala na bodaboda no hayo
 
Lazima waseme kuwa wanasoma kwa raha kwakuwa kwasababu kwanza hawaumizi vichwa mitihani inavujishwa,mwanafunzi anaingia kwenye chumba Cha mtihani na maijbu mfukoni,pili hata miundo ya mitihani nayo ni rafiki kwao Kama kwa shule za msingi utakuta majibu ya kuchagua kwa kila somo yaani npaka hisabati wanajichagulia tu majibu,tatu hakuna kuloa umande ukitaka kwenda shuleni ni mwendo wa school bus,daladala na bodaboda no hayo
Nne unaenda shule ukiwa well equiped. Una kila kitu kuanzia viatu, pesa ya kula hadi simu unanunuliwa.

Enzi hizo tulikuwa tunavisikia viatu redioni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upo sahihi mkuu, baada ya kusoma boarding kwa shida pale Ifunda mwanzoni mwa miaka ya 90, nikajisemea mwanangu hata soma boarding school kutokana na risk, yaani nikitafakari sijui kwa nini sikufa, ila nilishapata shida hadi nilikoma. Labda niorodheshe kidogo hapa chini baadhi ya shida nilizopitia boarding school.
1. Shule ilikuwa na changamoto ya maji hasa madarasni na mabwenini, ukienda chooni kujisaidia unajisaidia juu ya rundo la mavi ya wenzako kama ishirini hivi wamekunya juu ya juu. Hakuna hata maji ya kutawaza, unatumia karatasi za madaftari au A4 unaisugua hadi inalainika ndo unaenda kuchambia.

2. Mabwenini vyoo ni shida, baada ya vyoo vya maji kuwa havitumiki kutokana na shida ya maji, basi tukachimba pit latrines, ambavyo navyo baada ya kujaa, vilitoa harufu kiasi kwamba ukienda kunya, ukitoka chooni kila mtu anajua umetoka kunya, yaani unanuka mwili mzima, hivyo tukawa tunaenda kunya ukiwa umevua nguo zote, la sivyo nguo ufue.

3.Vyoo vilikuwa havina staha, milango hakuna, ukiwa unakata gogo basi mnatazamana na mwenzako ambaye mmekutana chooni, basi mnakunya huku unamtazama mwenzako anavyojikamua hadi mishipa ya usoni inavimba.

4. Mabweni yalijengwa kipindi cha mkoloni, yalikuwa yamechoka, madirisha yamepasuka ya vioo, na kuingiza baridi kali, yaani kama huna blanketi huwezi ishi pale, hivyo tulikuwa tunaziba kwa vipande vya maboksi utafikiri shule haina mwenyewe.

5. Chakula tulikuwa tunajilimia wenyewe hasa mahindi, shamba lipo umbali wa kama kilometa 7 toka shule, hivyo tulikuwa tunatembea kwa miguu kwenda kulima hasa kupalilia , unapewa mraba wa kupalilia kama mita 200 hivi ndo unaruhusiwa kuondoka yaani kama magereza vile, tena unaenda kuliwa na njaa, ukimaliza ndo unarudi shule kunywa uji usio na sukari, umewekwa maziwa tu.

6. Kila siku ni kula ugali na maharagwe, ikafikia kipindi wanafunzi wengi waliishia vitamini A mwilini wakawa hawaoni usiku.

7. Ratiba ya shule haikuwa na muda wa kujifanyia usafi hadi jumapili tu, mnaamshwa saa 11 asubuhi mnakimbizwa mchaka mchaka na baridi kali hadi saa 12. Baada ya hapo na Usafi mabwenini, kufyeka nyasi, nk saa moja kamili asubuhi mnasimama assembling, kisha mnaingia darasani, saa tano uji (a.k.a tope) mnarudi tena class hadi saa tisa kasorobo, then mnakula bondo maharagwe baada ya hapo saa 10 ni assembling tena mnapangiwa kazi za jioni kulima, kufyeka, usafi vyoo, kazi za kuni, kuosha vyombo messini, hadi saa 12 jioni muda la chakula tena cha jioni, baada ya hapo ni prepo! Yaani ilikuwa chuo cha shida.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom