We utakua ulikutana na afande tall,maana yeye na kihimbi ndio walikua wavuta sigara,nadhni nilikutangulia mwka
Mimi ni in-take ya O level 1996-1999 sasa kuna siku tulikuwa tunapiga sana kelele darasani, maafande 4 wakatuvamia darasani. Sasa mimi dawati langu lilikuwa la mwisho kabisa, na mlango wa darasa ulikuwa mmoja nyuma ya darasa yaani, kama milango ya magari ya zamani ya kubeba abiria, Kia. Hivyo, mara nyingi maafande wakituvamia mimi na masela wangu tunachomoka kiurahisi sana kwa kuwa dawati letu lilikuwa nyuma kabisa na karibu na mlango.
Sasa siku hiyo maafande wametuvamia wakaingia darasani 4 na mikwaju ya kutosha, sasa mimi kama kawaida yangu, nikawasubiri hile wamefika kati ya darasa mimi nikawaambia masela wangu jamani tusepe, masela wakaogopa. Basi mimi nikanyata mdogo mdogo nikachomoka class basi hile nageuka tu nakutana uso kwa uso na afande mmoja nje kumbe alikuwa anavuta sigara. Ilikuwa kama movie vile. Jamaa akanidaka akaniongiza ndani, wacha nipewe kichapo. JITE imenifunza mengi sana, I am who I am because of JITE UTE...