Walioshindikiza Katiba ni hawa

Mashujaa Ndio Hawa. Nchi Ingekuwa Mbali Bila JK Kuiba Kura. Huu Ndio Utanzania Sio Kukaa Kimya Kila Siku na Kutegemea Wachache Waamue.
 
Mkuu,

Ni hao tu? au kuna watangulizi wao?
Unajua kuwa madai ya katiba hayakuanza jana? au October 2010?
Sina nia ya kutokuwapa Credit kwa kazi yao nzuri katika hili la kudai katiba na kushinikiza pia....
Lakini pia tusiwasahau akina Mtikila na wengineo.
 
Watanzania tunaanza kuvuna matunda ya shinikizo lililoanzishwa na chadema baada kubaini kuwa kulikuwa na wizi mkubwa wa kura katika uchaguzi mkuu uliopita, na kwamba kutokana na katiba iliyopo, wahusika wakuu wa wizi huo wasingeliweza kufikishwa mahakamani. Kutokana na upeo mkubwa ulionao uongozi wa juu wa chadema, uliweza kubaini kwa usahihi kabisa, ya kwamba kwasababu ccm kama wafaidika wakubwa wa wizi huo, nafsi zao zitakuwa zinawasuta, na hivyo kwa wakati huu hawatakuwa na jeuri ya kuwekea kizingiti madai ya katiba mpya. Na hadi sasa mambo yamekwenda kama yalivyo tabiriwa. Hata hivyo zinahitajika juhudi zaidi; hivi sasa ccm imebuni huu mradi wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru kwa madhumuni ya kupoteza lengo. Bila ya kuwa waangalifu utakuta mawazo ya watu wengi yanaelekezwa katika matayarisho ya sherehe hizo.
 
Umesahau kuwa vuguvugu la Katiba halikuanza leo?! umemsahau Mtikila? umesahau tume mbalimbali kama vile Nyarali na Kisanga? unafikiri vuguvugu lake lilitokana na nini? HIVYO WATANZANIA NDIO WANAOSHINIKIZA KATIBA!
 
Hivi celinba kombani na werema wanamtetea nani?...................sisi tunaotaka namna ya kutawaliwa tunataka mabadiliko ya katiba wao wanatuletea upuuzi je ni kwa maslahi ya nani.................
Kuna sababu ya wao kuendelea kutuongoza?,,,nadhani tukifanya maandamanoi tushinikize wjiuzuru kwani ni waropokaji tu
 
..uongozi ni sawa na mbio za kupokezana kijiti.

..off course kilio cha katiba kilianzishwa na wakongwe kama Chifu Fundikira, Balozi Kasanga Tumbo,Mzee Kasela-Bantu, Mzee Mloo, Mzee Mapalala, Mabere Marando, Christopher Mtikila, Maalim Seif,na hata wabunge wa CCM "G-55."

..lakini hapa katikati harakati hizo zilianza kufifia.

..Chadema, kupitia mgombea wao, Dr.Slaa, ndiyo walioibua upya harakati za kudai katiba wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu.

..zaidi kile kitendo cha wabunge wa Chadema kususia hotuba ya JK bungeni kili-raise awareness kuhusu umuhimu wa katiba mpya nchi hii.
 
Chadema ni wadandiaji wa Kudai katiba kila mtu anajua hili Chadema nguvu mpya ya 2010 sio wao kama watasema wamepewa vijiti kutoka kwa wenzao kusogeza mbele harakati tutawaheshimu hao Kina Tindu Lissu kama ni wanaharakati wa Kweli wasingekimbia nchi kudai katiba mpya na kuja kujificha MAREKANI wakati kina Mtikila , Lipumba na Maalim Seif , MApalala ,Almarhum Mloo , Mabere Marando wengineo Njelu Kasaka Mwanzilishi wa G55 hawa ndio Wapigania Katiba Tanzania Nyerere aliowaita wasaliti na Hata Mzee Cwigemisi Malecela ana nafasi yake kupigania haki za Watanganyika , Fundikira , Ksanga Tumbo na wengieno ila Slaa na kudi lao hawakuamo kupigania Katiba Mpya huu ndio ukweli tunajua mara ngapi Mtikila ametiwa ndani kwa kesi za ajabu ajabu kunyanganywa nyumba yake kwa kupambana na serikali kupiganai haki za Watanzania kuna kundi la Wazawa Iddi Simba pia waliataka kuwapigania wazawa huko ni kupigania katiba.
 
Mlekwa,

..hakuna kilichoharibika hapa.

..tutaendelea kuwaenzi na kuwaheshimu waanzilishi wa harakati za kudai katiba mpya.

..wakati huohuo tunawaunga mkono vijana wapya wanaojitokeza kuendeleza harakati hizo.
 
Tunawapa hongera sana, bahati mbaya hawakushinda uRais?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom