Walionunua nyumba zetu wazirudishe

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
JK; nyumba zetu!
Tanzania Daima

LEO tunaandika suala hili kwa mara ya 12. Kwa mara nyingine tena, tunawakumbusha Watanzania wenzetu na viongozi wetu kuwa msimamo wetu katika suala linalohusu uuzwaji wa nyumba za serikali kwa viongozi wetu wakati wa serikali iliyopita uko wazi.
Imani yetu katika maamuzi haya ni kwamba, Watanzania tumeibiwa mali na viongozi wetu walioamua kuitumia vibaya dhamana ya madaraka tuliyowapa.

Bunge letu limekaa vikao vingi Dodoma tangu suala hilo lilipozuka na kulalamikiwa, na dalili zinaendelea kuonyesha wazi kuwa hakuna mwenye dhamira ya kuzikomboa nyumba zetu ambazo tunaamini tumeporwa.

Pamoja na kukiri kuwa Bunge limeendelea kuweka rekodi mpya kila wakati, hasa wakati huu lilipounda kamati teule ya kuchunguza mkataba wa Richmond, bado tunaendelea kulalamika kuwa limeacha suala jingine muhimu la kulitolea maamuzi ya kibunge.

Kama lilivyoshindwa kufikia maamuzi mazito ya pamoja katika masuala ya mgogoro wa Reginald Mengi na Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima, mikataba ya madini na mengine mengi, bado limeendelea kukwama kutumalizia suala la uuzwaji wa nyumba za serikali kwa baadhi ya watumishi wa umma.

Kimsingi, Bunge hilo pia limeshindwa kujadili au japo kudodosa kuhusu ulipofikia uamuzi wa serikali wa kuzirejesha baadhi ya nyumba hizo ambazo ziliuzwa kwa viongozi wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa.

Kwetu sisi wa Tanzania Daima, kama tulivyopata kusema huko nyuma, ukimya huu wa wabunge wetu, waliokuwa na fursa nyingi za kulivalia njuga suala hili, hata kama ikibidi kuandaa hoja binafsi, ni wa kukatisha tamaa.

Tunasema ni wa kukatisha tamaa kwa sababu suala hili ni moja ya mambo ambayo kwa kiwango kikubwa yalipingwa na watu wengi wakati wa utekelezwaji wake, hata kufikia hatua ya malalamiko haya kumfikia Rais Kikwete.

Mbele ya waandishi wa habari, Kikwete alilitangazia taifa hili mwanzoni mwa Oktoba mwaka jana kuwa, tayari serikali ilikuwa imeshaanza kuchukua hatua ambazo zitawezesha kurejeshwa kwa baadhi ya nyumba hizo ambazo alisema ziliuzwa kwa makosa.

Ingawa tulikuwa miongoni mwa Watanzania walioipokea kauli hiyo ya Kikwete kwa mikono miwili, msimamo wetu tangu wakati huo umekuwa wazi kabisa kwamba msamiati wa ‘baadhi ya nyumba’ unapaswa kuondolewa na badala yake urejeshwaji unapaswa kuwa wa ‘nyumba zote’ zilizouzwa.

Tunasema hivyo tukiamini kwa dhati kabisa kuwa, uamuzi mzima wa kuziuza nyumba hizo ulifanywa pasipo kuweka mbele masilahi ya taifa, na hivyo unapaswa kufutwa ili kumaliza fedheha hiyo ya kihistoria ambayo tutaendelea kuilalamikia siku nenda - rudi.

Tunaamini unyeti wa maeneo zilikojengwa nyumba hizo, umuhimu wa nyumba zenyewe na ukweli kwamba, uongozi ni dhana ya kupokezana vijiti kama alivyopata kusema Rais Kikwete, uamuzi wowote wa kuipokonya serikali rasilimali yake muhimu unapaswa kufutwa pasipo kuangalia matokeo ya kufanya hivyo. Tulitegemea wabunge wangeliona hili.

Tunahitimisha maoni yetu tukilikumbusha taifa kuachana na usahaulifu, hasa ule unaohusu masuala ya msingi.

Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa, ukimya wetu unatoa mianya ya nyumba zetu kuendelea kuuzwa kwa siri, huku zile tulizoahidiwa kurudishwa zikiendelea kubakia mikononi mwa watu. Hali hii lazima tukabiliane nayo.
 
Mie naomba na nyumba alizodhulumu nyerere zirudishwe kwa waliodhulumiwa kama wapo hai na kwa warithi wao kama wenyewe walisha fariki.
 
Zomba we are talking about nyumba za serikali ambazo JK naye alinunua ama aligawiwa maana alikiri kuwa nayo moja .Sasa aanze yeye kurudisha wengine wafuate
 
Zomba we are talking about nyumba za serikali ambazo JK naye alinunua ama aligawiwa maana alikiri kuwa nayo moja .Sasa aanze yeye kurudisha wengine wafuate
I know, but remember kuna raia walidhulumiwa majumba yao na nyerere, I think tungeanziya hapo kwenye kudhulumiwa raia.
 
Zomba nakujua kwa kusimamia hoja sometimes lakini wacha kuchanganya madawa . Tunataka nyumba za serikali ambazo Taifa lilipata hasara na si ajabu bado linapata kwa mawaziri na Majaji kukaa mahotelini kaka .
 
...nyumba zenyewe ni migofu tuu imebaki bora waliuza kupunguza gharama za kutunza nyumba hizo maana mpaka mleo tungeendelea kuhudumia mafisadi tuu,cha maana watupimie viwanja vizuri na barabara zionekane,maji na miundo mbinu na tutajenga za kwetu nzuri zaidi ya hizo za Oysterbay...ila zile zilizotaifishwa na serikali 1967 zirudishwe kwa wenyewe au warithi wao maana ile ni dhuluma mbaya sana
 
Zomba nakujua kwa kusimamia hoja sometimes lakini wacha kuchanganya madawa . Tunataka nyumba za serikali ambazo Taifa lilipata hasara na si ajabu bado linapata kwa mawaziri na Majaji kukaa mahotelini kaka .
Aaahh, jamani nimeona mada ni majumba nami nikakumbuka nyerere alivyo dhulumu watu nyumba zao, kama nimekosea kwa kuutaja ufisadi wa nyerere kwa kudhulumu, basi nisamehe.
 
Ni Vyema Angeanza Kurudisha Yake Kwanza Huyu Mtu Nyie Mwacheni Tu Anajua Anchofanya Na Mungua Anakwenda Tenda Mambo Ya Ajbu Mpaka Watu Washangae Hakuna Linaloshindikana Kwa Mola,,,,na Hata Hiyo Moja Labda Ilikuwa Inajulikana Vipi Hizo Zisojulikana????kulikuwa Na Watu Wanatumia Magari Ya Su Mapka Kubebea Nyasi Za Ngambo Hilo Ni Gari Maalam((typ..water))??nk...wakarudisha Sembuse Hizo Nyumba...ushindi Lazima
 
Zomba nakujua kwa kusimamia hoja sometimes lakini wacha kuchanganya madawa . Tunataka nyumba za serikali ambazo Taifa lilipata hasara na si ajabu bado linapata kwa mawaziri na Majaji kukaa mahotelini kaka .

... hao mawaziri na majaji si wanunue nyumba zao kwani lazima serikali iwanunulie nyumba,wape posho kidogo ambazo zipo kisheria,hii tabia ya kuwaweka mawaziri kwenye nyumba za bure na magari matatu au manne ndio ufisadi wenyewe,wanapata mishahara mikubwa sana na posho kibao waende bank wakakope wajenge za kwao...angalieni kagame alichofanya Rwanda maana hicho ndicho tunachohitaji hakuna fleet ya magari ya serikali na amekomesha kabisa kila mtu anajinunulia la kwake na kama unataka mkopo kachukue bank
 
Mwalimu wakati anachukua alitoa sababu gani ? Aliziuza ama aliwapa ndugu zake wakakaa ? Alienda nazo Butiama ?Hebu Zomba sema ufisadi wa Mwalimu kwenye majumba haya . Wataje wanao dai hizo nyumba na tueleze kama Taifa lilipata hasara kwa nyumba zile kuchukuliwa na Mwalimu .
 
Mwalimu alitaifisha nyumba za watu 1967 na moja ya nyumba hizo ilikuwa ya babu yangu lakini tumesharudishiwa ila kuna wengi hazijarudi,najua hakufanya binafsi ila ni policy zake za kidikteta
 
Mwalimu wakati anachukua alitoa sababu gani ? Aliziuza ama aliwapa ndugu zake wakakaa ? Alienda nazo Butiama ?Hebu Zomba sema ufisadi wa Mwalimu kwenye majumba haya . Wataje wanao dai hizo nyumba na tueleze kama Taifa lilipata hasara kwa nyumba zile kuchukuliwa na Mwalimu .
vyovyote alivyozifanyia si point, point is alidhulumu na dhulma yoyote ni ufisadi.
 
... hao mawaziri na majaji si wanunue nyumba zao kwani lazima serikali iwanunulie nyumba,wape posho kidogo ambazo zipo kisheria,hii tabia ya kuwaweka mawaziri kwenye nyumba za bure na magari matatu au manne ndio ufisadi wenyewe,wanapata mishahara mikubwa sana na posho kibao waende bank wakakope wajenge za kwao...angalieni kagame alichofanya Rwanda maana hicho ndicho tunachohitaji hakuna fleet ya magari ya serikali na amekomesha kabisa kila mtu anajinunulia la kwake na kama unataka mkopo kachukue bank
Nadhani hilo la Kagame ni zuri na la kujifunza, nyie watu sirikali mnaopitia hapa JF, si mjifunze hayo na muyatekeleze nahapa kwetu.
 
Back
Top Bottom