NINA kila sababu ya kumtukuza Mungu kwa uzima na afya, pia natoa pole kwa Watanzania kwa kuwapoteza ndugu na jamaa zao katika ajali iliyotokea Alhamisi wiki hii eneo la Kibamba, jijini Dar es Salaam ambapo watu wasiopungua 10 walifariki baada ya roli la mafuta kuligonga basi dogo la abiria na baadaye kulifunika.
Sina nia ya kueleza kwa undani namna ajali ilivyotokea lakini yatosha kuwapa pole na faraja wale wote waliofikwa na msiba huo huku nikiwaomba madereva kuwa makini waendeshapo vyombo vya moto ili kunusuru maisha ya abiria wanaotumia vyombo hivyo.
Leo ninataka niangazie kasoro zilizoibuliwa katika sheria ya matumizi ya fedha wakati wa uchaguzi ambayo ilisainiwa kwa mbwembwe mbele ya umati wa watu na Rais Jakaya Kikwete katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam Machi 17 mwaka huu.
Rais Kikwete, alitimiza ahadi yake aliyoitoa jijini Mwanza kuwa atasaini sheria hiyo kwa mbwembwe kwani katika hafla fupi ya kutia saini aliwaalika watu mbalimbali mashuhuri wakiwamo mawaziri, mabalozi, viongozi wa vyama vya siasa, wabunge, viongozi wa dini na wa taasisi za kijamii.
Najua Rais Kikwete aliona namna muswada wa sheria hiyo ulivyogaragazwa bungeni kiasi cha kuifanya serikali ifanye mabadiliko mengi makubwa tena kwa kutumia turufu ya wingi na nguvu ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndipo ulipopita kwa mbinde.
Takriban wiki mbili tangu kusainiwa kwa sheria hiyo, umeibuka utata wa kuingizwa kwa baadhi ya vipengele ambavyo inasemekana havikukubaliwa wala kupitishwa na wawakilishi wa wananchi (wabunge) ambao ndiyo wenye mamlaka ya kupitisha miswada ya sheria mbalimbali.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa, ndiye aliyeushtua umma kwa kuweka bayana uchomekeaji mambo huo huku baadhi ya viongozi wakionekana kutojua au kujali chochote juu ya matamshi ya kiongozi huyo wa upinzani.
Katikati ya wiki hii, Dk. Slaa alivunja ukimya kwa kuweka wazi kuwa ameshangazwa na kilichotokea Ikulu siku ya kusaini sheria hiyo ambapo amebaini kuwa kuna mtu au kikundi cha watu kimejivika ujasiri wa kuchomeka kipengele katika sheria hiyo na kikasainiwa na rais pasi idhini ya Bunge.
Je, ni kweli kuwa kuna vipengele vilivyoongezwa baada ya kupitishwa kwa muswada wa sheria hiyo na Bunge? Je, kuna kanuni inayoruhusu vipengele kuongezwa pindi Bunge likimaliza majadiliano?
Kama si ruhusa kufanya hivyo, kina nani wameshiriki kuongeza vipengele hivyo na kwa sababu zipi? Wamepanga kumdhalilisha Rais ili aonekane si msomaji wa jambo analolisaini? Kama jambo hili limetiwa mikono na watu wengine nje ya Bunge basi watendaji wanaomzunguka rais wetu hawamtakii mema yeye na nchi kwa ujumla.
Haya ni baadhi ya maswali yanayonifanya nikose majibu. Hata hivyo bado nitaendelea kujiuliza kuwa watu hao waliofikia hatua ya kuongeza kinyemela vipengele hivyo walimlenga nani zaidi na kwa faida ya nani? Je kabla ya kusaini sheria hiyo rais alikaa na kuipitia ili kuona kile kilichokubalika bungeni ndicho kilichokuwa mikononi na machoni mwake?
Najua Rais Kikwete ni miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa kukamilika kwa sheria hiyo kwa sababu alionyesha dhamira ya kukomesha matumizi makubwa ya fedha chafu katika uchaguzi, alifuatilia kwa makini mijadala ya wabunge na kile kilichokuwa mbele yake au ndiyo aliwaamini watendaji wake?
Hapa ni lazima ifahamike kama kuna kundi limejipanga kwa ajili ya kucheza rafu na kisha kumuingiza rais mkenge; ni wajibu kuwagundua na kuchukuliwa hatua madhubuti na hata ikibidi wawekwe hadharani ili jamii iweze kuwafahamu.
Hata hivyo bado tuwaulize wataalam wa masuala ya sheria ambao wakati wote pindi Bunge linapokuwa likijadili hoja nao hushiriki na kufuatilia ili pale penye tatizo waweze kulitatua au kulitolea ufafanuzi; hawa wanatumia fedha za walipakodi lakini walikuwa wapi mpaka muswada ule unatua mikononi mwa rais na kusainiwa?
Katika sheria aliyosaini rais, Dk. Slaa anasema kuna kifungu cha 7 (3), hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni. Kwa kweli nimeshangazwa sana kwa sababu rais amedanganywa katika hili.
Ni kweli Bunge halikusema ni nani anatakiwa kukagua timu ya kampeni ya nani, huku kwenye kipengele ambacho kimo kwenye sheria iliyosainiwa na rais inaonyesha kwamba timu za kampeni za mgombea urais zinatakiwa kuhakikiwa na Msajili.
Hii kweli ni sheria ya aina yake na ambayo haijawahi kutokea katika nchi yetu hata hivyo inatufanya sasa tuamini kuwa zipo sheria nyingine ambazo zimekuwa zikiongezewa vipengele lakini kutokana na kukosa watu makini wa kufuatilia basi sheria hizo ndiyo huwa vitanzi kwa jamii.
Kama kweli kuna upotoshaji umefanyika na kuongezeka kwa vipengele ipo haja ya kutafuta watu makini katika siku za usoni watakaomsaidia rais kwa kuwa hao waliokuwepo wamekuwa wakishindwa kufanya kazi ipasavyo.
Tunakumbuka tukio la rais kutoa gari la wagonjwa katika wilaya moja lakini kwa kuwa alikuwa akikumbuka wilaya aliyoiahidi alifanikiwa kuuzima mchezo ule ambao nao ulikuwa mKenge mmojawapo.
Sasa sheria hiyo ikirudishwa bungeni ili kuangaliwa upya kuna baadhi ya viongozi watakuwa wamepata ahueni kwa kuwa kwa wakati huu sheria hiyo inawabana kutokana na kushindwa kucheza rafu za kutoa rushwa kwa wazi na kutumia njia za panya ikiwemo kuitisha vikao usiku wa manane na kuongea na viongozi walio karibu na wananchi.
Je, ni wabunge wangapi ambao wameweza kugundua kuongezwa kwa vipengele hivyo na wameshindwa kutoa kauli iwapo ni kweli kuna mchezo huo? Je, wanastahili kuendelea kuwepo bungeni?
Sina nia ya kueleza kwa undani namna ajali ilivyotokea lakini yatosha kuwapa pole na faraja wale wote waliofikwa na msiba huo huku nikiwaomba madereva kuwa makini waendeshapo vyombo vya moto ili kunusuru maisha ya abiria wanaotumia vyombo hivyo.
Leo ninataka niangazie kasoro zilizoibuliwa katika sheria ya matumizi ya fedha wakati wa uchaguzi ambayo ilisainiwa kwa mbwembwe mbele ya umati wa watu na Rais Jakaya Kikwete katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam Machi 17 mwaka huu.
Rais Kikwete, alitimiza ahadi yake aliyoitoa jijini Mwanza kuwa atasaini sheria hiyo kwa mbwembwe kwani katika hafla fupi ya kutia saini aliwaalika watu mbalimbali mashuhuri wakiwamo mawaziri, mabalozi, viongozi wa vyama vya siasa, wabunge, viongozi wa dini na wa taasisi za kijamii.
Najua Rais Kikwete aliona namna muswada wa sheria hiyo ulivyogaragazwa bungeni kiasi cha kuifanya serikali ifanye mabadiliko mengi makubwa tena kwa kutumia turufu ya wingi na nguvu ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndipo ulipopita kwa mbinde.
Takriban wiki mbili tangu kusainiwa kwa sheria hiyo, umeibuka utata wa kuingizwa kwa baadhi ya vipengele ambavyo inasemekana havikukubaliwa wala kupitishwa na wawakilishi wa wananchi (wabunge) ambao ndiyo wenye mamlaka ya kupitisha miswada ya sheria mbalimbali.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa, ndiye aliyeushtua umma kwa kuweka bayana uchomekeaji mambo huo huku baadhi ya viongozi wakionekana kutojua au kujali chochote juu ya matamshi ya kiongozi huyo wa upinzani.
Katikati ya wiki hii, Dk. Slaa alivunja ukimya kwa kuweka wazi kuwa ameshangazwa na kilichotokea Ikulu siku ya kusaini sheria hiyo ambapo amebaini kuwa kuna mtu au kikundi cha watu kimejivika ujasiri wa kuchomeka kipengele katika sheria hiyo na kikasainiwa na rais pasi idhini ya Bunge.
Je, ni kweli kuwa kuna vipengele vilivyoongezwa baada ya kupitishwa kwa muswada wa sheria hiyo na Bunge? Je, kuna kanuni inayoruhusu vipengele kuongezwa pindi Bunge likimaliza majadiliano?
Kama si ruhusa kufanya hivyo, kina nani wameshiriki kuongeza vipengele hivyo na kwa sababu zipi? Wamepanga kumdhalilisha Rais ili aonekane si msomaji wa jambo analolisaini? Kama jambo hili limetiwa mikono na watu wengine nje ya Bunge basi watendaji wanaomzunguka rais wetu hawamtakii mema yeye na nchi kwa ujumla.
Haya ni baadhi ya maswali yanayonifanya nikose majibu. Hata hivyo bado nitaendelea kujiuliza kuwa watu hao waliofikia hatua ya kuongeza kinyemela vipengele hivyo walimlenga nani zaidi na kwa faida ya nani? Je kabla ya kusaini sheria hiyo rais alikaa na kuipitia ili kuona kile kilichokubalika bungeni ndicho kilichokuwa mikononi na machoni mwake?
Najua Rais Kikwete ni miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa kukamilika kwa sheria hiyo kwa sababu alionyesha dhamira ya kukomesha matumizi makubwa ya fedha chafu katika uchaguzi, alifuatilia kwa makini mijadala ya wabunge na kile kilichokuwa mbele yake au ndiyo aliwaamini watendaji wake?
Hapa ni lazima ifahamike kama kuna kundi limejipanga kwa ajili ya kucheza rafu na kisha kumuingiza rais mkenge; ni wajibu kuwagundua na kuchukuliwa hatua madhubuti na hata ikibidi wawekwe hadharani ili jamii iweze kuwafahamu.
Hata hivyo bado tuwaulize wataalam wa masuala ya sheria ambao wakati wote pindi Bunge linapokuwa likijadili hoja nao hushiriki na kufuatilia ili pale penye tatizo waweze kulitatua au kulitolea ufafanuzi; hawa wanatumia fedha za walipakodi lakini walikuwa wapi mpaka muswada ule unatua mikononi mwa rais na kusainiwa?
Katika sheria aliyosaini rais, Dk. Slaa anasema kuna kifungu cha 7 (3), hakikuwepo kabisa kwenye muswada uliojadiliwa na kupitishwa bungeni. Kwa kweli nimeshangazwa sana kwa sababu rais amedanganywa katika hili.
Ni kweli Bunge halikusema ni nani anatakiwa kukagua timu ya kampeni ya nani, huku kwenye kipengele ambacho kimo kwenye sheria iliyosainiwa na rais inaonyesha kwamba timu za kampeni za mgombea urais zinatakiwa kuhakikiwa na Msajili.
Hii kweli ni sheria ya aina yake na ambayo haijawahi kutokea katika nchi yetu hata hivyo inatufanya sasa tuamini kuwa zipo sheria nyingine ambazo zimekuwa zikiongezewa vipengele lakini kutokana na kukosa watu makini wa kufuatilia basi sheria hizo ndiyo huwa vitanzi kwa jamii.
Kama kweli kuna upotoshaji umefanyika na kuongezeka kwa vipengele ipo haja ya kutafuta watu makini katika siku za usoni watakaomsaidia rais kwa kuwa hao waliokuwepo wamekuwa wakishindwa kufanya kazi ipasavyo.
Tunakumbuka tukio la rais kutoa gari la wagonjwa katika wilaya moja lakini kwa kuwa alikuwa akikumbuka wilaya aliyoiahidi alifanikiwa kuuzima mchezo ule ambao nao ulikuwa mKenge mmojawapo.
Sasa sheria hiyo ikirudishwa bungeni ili kuangaliwa upya kuna baadhi ya viongozi watakuwa wamepata ahueni kwa kuwa kwa wakati huu sheria hiyo inawabana kutokana na kushindwa kucheza rafu za kutoa rushwa kwa wazi na kutumia njia za panya ikiwemo kuitisha vikao usiku wa manane na kuongea na viongozi walio karibu na wananchi.
Je, ni wabunge wangapi ambao wameweza kugundua kuongezwa kwa vipengele hivyo na wameshindwa kutoa kauli iwapo ni kweli kuna mchezo huo? Je, wanastahili kuendelea kuwepo bungeni?