Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,305
- 12,968
Ni jambo la kushangaza. Wale wale waliolitumia jeshi pa polisi vibaya kwaajili ya manufaa yao ndio wao tena wanaolituhumu na kutaka lichunguzwe.
Ni wazi CCM ndiye mnufaika mkuu wa matumizi mabaya ya jeshi la polisi dhidi ya wapinzani. Leo anainuka katibu wa propaganda kutaka lichunguzwe.
Lakini ni jeshi hilo hilo linalozuia mikutano ya wapinzani, kuwapiga, kwafungulia mashtaka fake na hata kuuwa kwaajili ya kuilinda CCM hadi wananchi wakalibatiza jina Policcm.
Wakati wapinzani wakiugulia maumuvu ya jeshi la polisi CCM yenyewe imekuwa kama mziwanda anayedekezwa na kufanya lolote bila kuzuiwa wala kuingiliwa na mtu.
Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dsm ni miongoni mwa viongozi wa serikali waliolitumia vibaya sana jeshi la polisi kwa kuwabambikia watu kashfa za madawa ya kulevya, kukamata na kuwaweka ndani watu bila hatia, kuvamia vyombo vya habari nk lakini laajabu leo naye anasema jeshi la polisi ni baya.
Sabaya naye ni mmoja wa viongozi waliolitumia jeshi la polisi vibaya sana kwa manufaa binafsi.
Kimsingi wanaofanya jeshi la polisi lionekane la hovyo ni viongozi wa serikali na siyo polisi wenyewe kwakuwa wao kazi yao ni kutii na kutekeleza amri na ndiyo nidhamu ya jeshi.
Viongozi ndio wanaowaaambia polisi mkamateni kiongozi fulani wa upinzani kishamfungulieni mashtaka.
Hakunza zaidi
Ni wazi CCM ndiye mnufaika mkuu wa matumizi mabaya ya jeshi la polisi dhidi ya wapinzani. Leo anainuka katibu wa propaganda kutaka lichunguzwe.
Lakini ni jeshi hilo hilo linalozuia mikutano ya wapinzani, kuwapiga, kwafungulia mashtaka fake na hata kuuwa kwaajili ya kuilinda CCM hadi wananchi wakalibatiza jina Policcm.
Wakati wapinzani wakiugulia maumuvu ya jeshi la polisi CCM yenyewe imekuwa kama mziwanda anayedekezwa na kufanya lolote bila kuzuiwa wala kuingiliwa na mtu.
Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dsm ni miongoni mwa viongozi wa serikali waliolitumia vibaya sana jeshi la polisi kwa kuwabambikia watu kashfa za madawa ya kulevya, kukamata na kuwaweka ndani watu bila hatia, kuvamia vyombo vya habari nk lakini laajabu leo naye anasema jeshi la polisi ni baya.
Sabaya naye ni mmoja wa viongozi waliolitumia jeshi la polisi vibaya sana kwa manufaa binafsi.
Kimsingi wanaofanya jeshi la polisi lionekane la hovyo ni viongozi wa serikali na siyo polisi wenyewe kwakuwa wao kazi yao ni kutii na kutekeleza amri na ndiyo nidhamu ya jeshi.
Viongozi ndio wanaowaaambia polisi mkamateni kiongozi fulani wa upinzani kishamfungulieni mashtaka.
Hakunza zaidi