MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,974
Siasa za nchi hii ukizivamia bila kujua vizuri historia yake lazima zitakupeleka sehemu ambayo ulidhani haiwezekani!
Wanasiasa wanaozijua vizuri siasa za nchi hii kwa sasa wako na familia zao huku wale ambao walizivamia bila kuzijua kwa sasa wako sehemu ambayo hawakutegemea!
Anayejiita ''Mdude Chadema'' ni moja ya watu waliozivamia siasa nchini bila kuwa na ufahamu mpana!
Shangwe na sifa alizokuwa anazipata kwenye mitandao ya kijamii zilimpa sense of invincibility fable! Akadhani ni zaidi hata ya wale wanaomsifia na kumshangilia!
Anayejiita ''Mdude Chadema'' hakujua wanaomsifia na kumshangilia wanamuona kama mtoa burudani kwa sababu baadhi ya watanzania wanazichukulia siasa kama burudani!
''Sense of invincibility fable'' ilimfanya azidishe burudani zake ambazo kiuhalisia hazikuwa na mwelekeo!
Baada ya ''kuguswa'' na wenye siasa, kwa sasa waliokuwa wanampa sifa na kumshangilia hawaonekani tena! Wamehamia kwa watu wengine ambao matendo yao ya kisiasa pia ni kama watoa burudani!
Nadhani anayejiita ''Mdude Chadema'' hakuwahi kuyasoma maneno ya hekima na busara yaliyosemwa na Mwanajeshi wa Kichina, Sun Tzu yasemayo, '' If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle''.
Wazee wetu pia walituasa wakisema, ''Akili za kuambiwa, changanya na za kwako''! Hii ina maana sikiliza na uchambue kwa makini na kutafakari ulichokisikiliza kabla hujafanya maamuzi!
Kwa sasa aliyebaki anahangaika ni yeye na familia yake huku waliokuwa wanamsifia na kumshangilia wakiendelea na burudani zingine za siasa! Waliokuwa wanamsifia na kumshangilia hawaonekani hata mahakamani ili kuendeleza sifa na shangwe!
Siasa za nchi hii zina wenyewe na kama unataka kuzifanya siasa kama burudani lazima kwanza ujue kikomo chake!
Methali inayosema, '' wajinga ndio waliwao'' haikuandikwa kama burudani!
Wanasiasa wanaozijua vizuri siasa za nchi hii kwa sasa wako na familia zao huku wale ambao walizivamia bila kuzijua kwa sasa wako sehemu ambayo hawakutegemea!
Anayejiita ''Mdude Chadema'' ni moja ya watu waliozivamia siasa nchini bila kuwa na ufahamu mpana!
Shangwe na sifa alizokuwa anazipata kwenye mitandao ya kijamii zilimpa sense of invincibility fable! Akadhani ni zaidi hata ya wale wanaomsifia na kumshangilia!
Anayejiita ''Mdude Chadema'' hakujua wanaomsifia na kumshangilia wanamuona kama mtoa burudani kwa sababu baadhi ya watanzania wanazichukulia siasa kama burudani!
''Sense of invincibility fable'' ilimfanya azidishe burudani zake ambazo kiuhalisia hazikuwa na mwelekeo!
Baada ya ''kuguswa'' na wenye siasa, kwa sasa waliokuwa wanampa sifa na kumshangilia hawaonekani tena! Wamehamia kwa watu wengine ambao matendo yao ya kisiasa pia ni kama watoa burudani!
Nadhani anayejiita ''Mdude Chadema'' hakuwahi kuyasoma maneno ya hekima na busara yaliyosemwa na Mwanajeshi wa Kichina, Sun Tzu yasemayo, '' If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle''.
Wazee wetu pia walituasa wakisema, ''Akili za kuambiwa, changanya na za kwako''! Hii ina maana sikiliza na uchambue kwa makini na kutafakari ulichokisikiliza kabla hujafanya maamuzi!
Kwa sasa aliyebaki anahangaika ni yeye na familia yake huku waliokuwa wanamsifia na kumshangilia wakiendelea na burudani zingine za siasa! Waliokuwa wanamsifia na kumshangilia hawaonekani hata mahakamani ili kuendeleza sifa na shangwe!
Siasa za nchi hii zina wenyewe na kama unataka kuzifanya siasa kama burudani lazima kwanza ujue kikomo chake!
Methali inayosema, '' wajinga ndio waliwao'' haikuandikwa kama burudani!