Waliokosa mikopo elimu juu wapewa matumaini

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
1574239590869.png

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha

Serikali imesema kuwa wanafunzi waliopunjwa na wale waliokosa mikopo inayotolewa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB), wataipata kwa sababu kilichokwamisha ni mfumo.

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha, aliyasema hayo jana, huku akiwaeleza wanafunzi hao wenye sifa ya kuipata kuwa fedha zote zilishatolewa wiki tano kabla ya wao kuripoti vyuoni.

Ole Nasha alisema halikuwa kusudio la serikali wala bodi ya mikopo kupunguza fedha hizo, kilichotokea ni mfumo ulijielekeza vibaya.

“Mnafahamu kwa sababu mfumo huu unajiendesha unaweza kuharibika lakini tayari bodi ya mikopo wameandika barua kwa vyuo vyote kuwaambia kwamba lazima kosa hilo lirekebishwe na mwanafunzi yeyote aliyepunjwa fedha zake, atapata mpaka senti ya mwisho,” alisema.

Naibu Waziri huyo aliwatangazia wanafunzi wote waliokumbwa na kadhia hiyo kwamba jitihada zinafanyika ili wapate fedha zao kwa sababu moja kubwa, waliingia mkataba.

“Ukikubali upunjwe sasa hivi bado kwenye mfumo wa kurejesha utalipa, hatutaki upate hiyo kadhia, ni mfumo ndio ulileta shida,” alisema.

Alisema wiki tano kabla ya vyuo kufunguliwa serikali ilikuwa imeshatoa Sh. bilioni 125 kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu, ikiwa ni maagizo ya Rais John Magufuli kuwa hataki wanafunzi wacheleweshewe mikopo.

“Mfahamu fedha zote zimeshatolewa kwa nusu mwaka wa kwanza, wacheleweshaji wanaanzia wanafunzi wenyewe, vyuo, taasisi zetu za udhibiti NACTE (Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi) na TCU (Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania) kama hawaendi vizuri bodi ya mikopo haitaweza kwenda mbele,” alisema.

Chanzo: Nipashe

======
Mchango wa wadau


Wengi tulifarijiwa hivi mwisho wa siku tulisoma miaka 3 bila mkopo na vigezo tulikuwa navyo.......kama mzazi anaweza kujinyima kidogo na wewe mwanafunzi ukabana matumizi basi utaishi vizuri tu

Ukiachana nawale wenye uhitaji wa kweli wa mkopo, kuna ambao wanaapply ili waishi maisha ya ndoto zao (iPhone, girlfriend mkali, kwenda shopping na supermarkets kila weekend, TV sjui fridge plus birthday parties na mambo Kama hayo) .....

Rafiki zangu wengi walipataga mkopo ila wao ndio walikuwa hawana hata 100 baada ya week 2 tu hadi week 3, pesa inakuwa imekata....

Mwisho maisha ya chuo ni mkumbo mkubwa sana, muda mwingine hata wanaotokea kwenye familia za chini wakifika chuo, utawakuta wanaenda shopping ya laki 3 hadi laki 4. wanaenda club kwa sana na kufika pesa, wanahonga mno wanawake ila ndo hivo inaumiza ila ndio lifestyle ya kichuochuo......

My take.. Mwanachuo unaweza kuishi kwa 2000 kwa siku sio lazima uishi kwa elfu 15 kwa siku..... na kwawale wadogo zetu wakiume wa chuo wajue hao kina dada ni wakawaida sana tena wengi washamba washamba tu hawana budi kutumia akili maana maisha mtaani ni magumu sana......
 
Wengi tulifarijiwa hivi mwisho wa siku tulisoma miaka 3 bila mkopo na vigezo tulikuwa navyo. Kama mzazi anaweza kujinyima kidogo na wewe mwanafunzi ukabana matumizi basi utaishi vizuri tu.

Ukiachana na wale wenye uhitaji wa kweli wa mkopo, kuna ambao wanaapply ili waishi maisha ya ndoto zao (iPhone, girlfriend mkali, kwenda shopping na supermarkets kila weekend, Tv sijui fridge plus birthday parties na mambo kama hayo)

Rafiki zangu wengi walipataga mkopo ila wao ndio walikuwa hawana hata 100 baada ya week 2 tu hadi week 3, pesa inakuwa imekata.

Mwisho maisha ya chuo ni mkumbo mkubwa sana, muda mwingine hata wanaotokea kwenye familia za chini wakifika chuo, utawakuta wanaenda shopping ya laki 3 hadi laki 4. wanaenda club kwa sana na kufika pesa, wanahonga mno wanawake ila ndo hivo inaumiza ila ndio lifestyle ya kichuo chuo.

My take: Mwanachuo unaweza kuishi kwa 2000 kwa siku sio lazima uishi kwa elfu 15 kwa siku, na kwawale wadogo zetu wa kiume wa chuo wajue hao kina dada ni wa kawaida sana tena wengi washamba washamba tu hawana budi kutumia akili maana maisha mtaani ni magumu sana.
 
Ole Nasha alisema halikuwa kusudio la serikali wala bodi ya mikopo kupunguza fedha hizo, kilichotokea ni mfumo ulijielekeza vibaya.
He must be nuts! Mfumo unajielekeza vibaya? Nuts! GIGO, halafu mtu anasema eti mfumo umejielekeza vibaya! Utawala huu kila mmoja amekengeuka! Mlaaniwe
 
Waliishiwa, hivyo walikuwa wanabuy time kuepuka migomo na manunguniko ya wanafunzi ambayo serikali ingekosa majibu.

Wamefanikisha walichokihitaji, wameshabanana kwa kodi na mengine ili kuwalipa wanafunzi. Siasa ni janja janja tu.

Vijana nafikiri sasa mmeshapata boom na mengine ya kawaida. Katimizeni wajibu wenu wa kusoma.
 
Serikali imesema kuwa wanafunzi waliopunjwa na wale waliokosa mikopo inayotolewa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB), wataipata kwa sababu kilichokwamisha ni mfumo.
Toka nilipo waona vijana wakikosa mikopo bila sababu za kueleweka huwa sipendi kukoment kuhusu HESLB na utendaji wake (leo ngoja nijaribu).

Kijana alikosa mkopo mwaka wa kwanza, kufika shuleni akakutana na kijana ambaye ndugu yake ana kaubosi huko. Yule ndugu akampeleka huyu kijana wetu kwa huyo mbaba, ndani ya wiki alipata mkopo bila ya kuongeza taarifa zozote.

Mwenzake aliyekuwa na hali mbaya zaidi, achilia mbali ku-appeal mpaka kesho hana kitu inabidi ndugu wajipige chochote kinachopatikana kimsogeze.

Hivyo waziri anajifurahisha tu kila mtu ajiandee ukiwa na bahati waweza pata lakini kwa wengi waliokosa hadi sasa sioni mkopo utatoka wapi. Inauma lakini ndio hali halisi. KUMBUKA WALITUAMBIA HAKUNA MWENYE UHITAJI ATAKAEKOSA MKOPO.
 
Duh ni noma

Toka nilipo waona vijana wakikosa mikopo bila sababu za kueleweka huwa sipendi kukoment kuhusu HESLB na utendaji wake (leo ngoja nijaribu).

Kijana alikosa mkopo mwaka wa kwanza, kufika shuleni akakutana na kijana ambaye ndugu yake ana kaubosi huko. Yule ndugu akampeleka huyu kijana wetu kwa huyo mbaba, ndani ya wiki alipata mkopo bila ya kuongeza taarifa zozote.

Mwenzake aliyekuwa na hali mbaya zaidi, achilia mbali ku-appeal mpaka kesho hana kitu inabidi ndugu wajipige chochote kinachopatikana kimsogeze.

Hivyo waziri anajifurahisha tu kila mtu ajiandee ukiwa na bahati waweza pata lakini kwa wengi waliokosa hadi sasa sioni mkopo utatoka wapi. Inauma lakini ndio hali halisi. KUMBUKA WALITUAMBIA HAKUNA MWENYE UHITAJI ATAKAEKOSA MKOPO.
Duh ni noma
 
Mie mdogo wangu alikuwa anapata kila kitu Hadi hela ya field sasa hiv hela imekuja imepunguzwa Hadi Ada kabisa.
 
Back
Top Bottom