Walioko madarakani hawataki Katiba Mpya kwa hofu ya kuyakosa madaraka, wanaotafuta madaraka wanaitaka ili wayapate madaraka

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Jicho la tatu linaonesha kiu ya wanaodai katiba mpya ni madaraka na wanaosema iliyopo inafaa pia wanataka kubaki madarakani. Suruhisho ni nini!??

Katiba iliyopo na hata mpya inayopiganiwa haiwezekani kuwa kamilifu na timilifu kamwe hasa hasa itakayoandaliwa katika mazingira haya yenye kila aina ya mihemuko ya kisiasa

Rais aliyepo Sasa amejitahidi kwa kiasi kikubwa kuonesha kuwa katiba iliyopo ilikanyagwa kwa makusudi na mtangulizi wake. Mfano kesi za kubambikia, kuminya uhuru wa habari,nk.

Kumbe Rais anaweza kuamrisha kitu nje ya katiba na kikawa na asifanywe chochote!

Hapa Rais Samia anatupa ujumbe kuwa dawa si katiba mpya pekee! Anatueleza tuna jambo kubwa la kufanya zaidi ya kudai katiba mpya!

Nawiwa kujiuliza, hivi tunadhani hiyo katiba mpya itakuwa na uwezo kabisa wa kumfunga break Rais asiweze kutumia vyombo vya ulinzi na usalama atakavyo?

Tuna uhakika tukipata katiba mpya itakayoruhusu tume huru na kupunguza madaraka ya Rais na tukaendelea na aina ya watanzania hawa hawa, wasomi hawa hawa itamzuia huyo Rais kutumia vyombo vyake hivyo vichache atakavyopewa kikatiba kuingilia vyombo vingine au kuvunja haki za raia atakavyo?

Najua mtasema ndio atazuiwa na katiba na kutakuwa na uwezo wa kumshughulikia kwa kuvunja katiba!

Huenda mkawa sahihi, lakini tujiulize ni mara ngapi wanasiasa hawa hawa na makundi mengine yasiyo ya kisiasa yametueleza kuwa Rais aliyepita alivunja katiba na haki za raia kwa makusudi? Tulimfanya nini??

Huenda maswali yangu yanaonekana ya kizwazwa lakini yatafakari kwa kina

Mapendekezo yangu ni haya:-

1. Wanasiasa wajikite zaidi kutoa elimu ya uraia na kujitambua kwa wananchi na kuwajengea uwezo wa kujiamini na utambuzi wa haki zao. Katiba mpya bila elimu ya uraia itakuwa kazi bure!

Elimu ikitolewa na ikaeleweka, mwananchi atajua haki zake, atajua kuzidai na atajua kuzitetea na atazipigania kwa kujiamini. Halikadhalika viongozi watawaheshimu wananchi na wataongoza kwa adabu

2. Mchakato wa katiba mpya 2014 ulivurugwa na wanasiasa hawa hawa wanaoidai leo. Huu ni uthibitisho kuwa wanasiasa wanaweza wasituletee katiba nzuri kwasababu za kimaslahi.

Walioko nje watataka katiba itakayowapa fursa ya kuingia ndani na walioko ndani watapigania vipengere vitakavyowahakikishia kuendelea kubaki madarakani

Hapa mkatae mkubali lakini ukweli ndio huo! Watajificha nyuma ya kivuli Cha kuwatetea wananchi lakini mioyoni wana Jambo lao!

Kinachoweza kufanyika ni kuunda kamati maalumu ya katiba mbali na ile ya Warioba itakayowaweka pembeni wanasiasa lakini Kama itawapendeza wachukue yale maoni ya tume ya Warioba Kama Kuna cha kuboresha waboreshe Kama Kuna haja ya kuongezea watajua wenyewe

Kamati hiyo iongozwe na majaji wa mahakama kuu na wastaafu waliowahi kuwa majaji wa mahakama kuu pamoja na mawakili wabobezi

Wajumbe wengine watoke vyombo vya ulinzi na usalama wenye uzoefu wa kutosha. Hawa watasaidia kuweka vipengere vitavyodhibiti vyombo vya ulinzi na usalama.

Inaaminika taasisi uliyoitumikia Kuna mapungufu unayaona wazi lakini unashindwa kuyaziba kwasababu huna uwezo.

Wakiwepo hawa wataunda vifungu vitakavyosaidia polisi, magereza, Jwtz na TISS wasioonee watu, viongozi na watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuweka vipengere vitakavyolinda maslahi na weledi wa vyombo hivi

Wajumbe wengine watoke miongoni mwa waliowahi kuwa washauri wa Rais katika vipindi vyote.

Hawa watakuwa na nafasi nzuri ya kutoa uzoefu wao pale walipojaribu kushauri kitu either cha kuvunja katiba au kujaribu kuzuia katiba isivunjwe. Hawa watatoa uzoefu wa nini kinafanya Rais avunje katiba na nini kiwekwe kuzuia

Wajumbe wengine watoke ndani ya bunge. Hapa simaanishi wabunge. Wachukuliwe wale waliowahi kuwa makatibu wa bunge na waliowahi kuwa Maspika wa bunge au kuhudumu ndani ya ofisi ya Spika. Hawa watakuwa na nafasi nzuri ya kutoa mawazo yao wabunge wawe na sifa gani ili bunge liwe imara kusimamia serikali na vifungu gani viwekwe kulisuka bunge ki uweledi zaidi kuliko ilivyosasa ambapo limekuwa jukwaa la kuzogoana

3. Mwisho kabisa vifungu vya katiba viwe topics kwenye somo la URAIA/CIVICS/GS. Leo watu wanaambiwa katiba mpya ila ni ajabu wengi hata waliopata bahati ya kupata elimu ya darasani hawaijui hii katiba iliyopo.

Wengi wanasikia kutoka kwa wanasiasa ila wao Kama wao hawajui udhaifu au umadhubuti wa katiba iliyopo. Si ajabu leo msomi wa chuo kikuu hajui kilichomo ndani ya katiba

Ikiwa sehemu ya somo mashuleni na ikawa somo la lazima kwa ngazi fulani ya elimu itaweza kusaidia Raia wengi kutambua haki zao za kikatiba na kuzipigania kuliko ilivyosasa

Kwa Sasa wanasiasa hawana nafasi nzuri ya kuleta katiba bora Tanzania kwa maslahi mapana ya Taifa. Wengi wana focus uchaguzi wa 2025 ndiomaana agenda kuu imekuwa kutoshiriki uchaguzi bila katiba mpya

Katiba haitakiwi ku focus uchaguzi tu! Katiba ni zaidi ya uchaguzi, ni zaidi ya CCM, CHADEMA na nk. Katiba ni zaidi ya Mbowe na Samia! Katiba inatakiwa iandaliwe bila pressure na kwa focus iliyohuru itakayojali Tanzania na watanzania waliopo na wajao!
 
Ni Magufuli tu ndiyo walau alijali maendeleo ya wananchi, hawa wengine wapo busy kugombania madaraka.
 
Kwa nchi za Afrika,Katiba inaweza iwe au isiwe mwarobaini wa matatizo yetu, rushwa, ufisadi, ajira, uchumi. Mfano hebu fikiria kama South Afrika isingekuwa na Katiba imara, lile jizi Zuma lingekuwepo Madarakani likiendelea kuiba kuuza mali ya umma.

Pale Kenya Kuna Katiba mpya,Katiba imewapa uhuru wananchi na wanasiasa wanaweza kumtukana Raisi wapendavyo,lakini angalia Raisi uhuru alivyo deal na wapinzani wake ndani ya chama,wengine amewafukuza kama Aden duale,Murkomen,wabunge wa chama chake wanaompinga,wamefutwa uanachama.

Mahakama zimenyimwa pesa,Makamu wake,ametengwa kwenye dhifa zingine za kitaifa,secret service wanadiriki hata kumzuia asifike!?
Tuige China,Urusi,hawana "Katiba mpya"lakini sasa hv wanautisha ulimwengu kwa uchumi.

Korea, Japan, Philippine Wana demokrasia na Wana uchumi mkubwa na maendeleo,Katiba mpya,haileti ajira,
 
Jicho la tatu linaonesha kiu ya wanaodai katiba mpya ni madaraka na wanaosema iliyopo inafaa pia wanataka kubaki madarakani. Suruhisho ni nini!??

Katiba iliyopo na hata mpya inayopiganiwa haiwezekani kuwa kamilifu na timilifu kamwe hasa hasa itakayoandaliwa katika mazingira haya yenye kila aina ya mihemuko ya kisiasa..
Katiba bora ni lazima iweke utaratibu ni namna gani kiongozi mpumbav atawajibishwa bila kuangalia chama wala Rangi yake na hiyo ni faida kwa nchi na sio kwa atakaye poteza wala kupata madaraka.

Wananchi tumechoka kuburuzwa kama kenge.

Viongozi lazima wawaheshimu na kuwathani raia wao na sio kuwatendea kama mifugo.

Hatuwataki viongozi wapumbav

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Jicho la tatu linaonesha kiu ya wanaodai katiba mpya ni madaraka na wanaosema iliyopo inafaa pia wanataka kubaki madarakani. Suruhisho ni nini!??

Katiba iliyopo na hata mpya inayopiganiwa haiwezekani kuwa kamilifu na timilifu kamwe hasa hasa itakayoandaliwa katika mazingira haya yenye kila aina ya mihemuko ya kisiasa..
Mkuu uko sahihi kiasi fulani je Vyama vya Upinzsni vikisema vinakubali yooote kasoro Serikali 2,Vinataka Serikali 3,Na Chama tawsla kikasema serikali 2.

Na Katiba Ujue pia Ni jambo la Kisisa!

Huwezi Kuliweka Mbali na wanasiasa,

Hapa Ndipo Wnasiasa wanatukwamisha!

Ni Bora wakose mengine yooote yakwame ila la Muungano liwepo Hahaha ndio walipotukwamisha Last time wanasiasa.
 
Hapa Mpaka Wazungu/mabeberu waingilie kati kwenye kunyima misaada ndio SERIKALI itatema NDOANO kutupatia katiba Mpya.
 
Kwa nchi za Afrika,Katiba inaweza iwe au isiwe mwarobaini wa matatizo yetu, rushwa, ufisadi, ajira, uchumi. Mfano hebu fikiria kama South Afrika isingekuwa na Katiba imara, lile jizi Zuma lingekuwepo Madarakani likiendelea kuiba kuuza mali ya umma.

Pale Kenya Kuna Katiba mpya,Katiba imewapa uhuru wananchi na wanasiasa wanaweza kumtukana Raisi wapendavyo,lakini angalia Raisi uhuru alivyo deal na wapinzani wake ndani ya chama,wengine amewafukuza kama Aden duale,Murkomen,wabunge wa chama chake wanaompinga,wamefutwa uanachama.

Mahakama zimenyimwa pesa,Makamu wake,ametengwa kwenye dhifa zingine za kitaifa,secret service wanadiriki hata kumzuia asifike!?
Tuige China,Urusi,hawana "Katiba mpya"lakini sasa hv wanautisha ulimwengu kwa uchumi.

Korea, Japan, Philippine Wana demokrasia na Wana uchumi mkubwa na maendeleo,Katiba mpya,haileti ajira,
Kenya na Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi bora kabisa na zenye maendeleo barani Afrika, kwenye nchi zenye pato kubwa la taifa nadhani Kenya ipo no: 4, kuna mataifa kama Libia yaliyokuwa na mifumo ya kipuuzi hayapo hata kwenye kumi bora

Mkuu katiba mpya ni mhimu sana kwa kwa taifa letu, iweke mwelekeo wa maendeleo kwamba hata ikitokea Samia hayupo aliepo yeyote afanye kile kile, mfano Jakaya alianza kuwekeza kwenye sayansi, akajenga maabara karibu shule zote za kata (japo hakuweka vifaa) akadahili wanafunzi kuchukua diploma pale Dodoma, amekuja John akayapuuzia hajaweka vifaa pia, akawafukuza wale waliokuwa pale Dodoma tena kwa kuwaita vilaza utadhani walijipeleka wenyewe

Kuna mambo John kayafanya, mfano wale askari waliokuwa wanakusanya kodi (task force) mama Samia kawatoa, kuna watu walitiwa hatiani na serikali ya John lakini leo wapo mtaani

Harafu John kujenga uwanja wa ndege Chato alishauriana na nani? Bunge lilipitia? Ununuzi wa ndege je? maanake ni kwamba katiba hii imempa madaraka ya kufanya chochote Rais akitaka, au unataka mpaka siku Rais aje aamulishe ukatwe miguu ndo ujue katiba ni mbovu?

Ngoja nikueleweshe kidogo kama ni mtu wa kuelewa utaelewa mkuu, mfano sisi kama taifa tumepitia mifumo mingi sana kielimu (mitaala) hii imetokea kutokana na mahitaji ya wakati huo, mimi ukiniuliza kuhusu maili, futi na yadi sijui kitu mkuu kwa sababu sikuzisoma
mimi nilisoma kuanzia milimita mpaka kilomita, lakini pia waulize wazee wa kipindi hicho kama walisoma TEHAMA

Katiba hii imekuwa kuukuu tunahitaji katiba mpya mkuu, harafu miaka 44 iliyopita wazee wetu waliandika historia kutupatia katiba hii, wewe hutaki kuwa sehemu ya historia kwa vizazi vijavyo kama na wewe ulikuwa sehemu ya mabadiliko ya katiba?
 
Umeandika vyema sana. Hili liko wazi wanataka kuifanya katiba ipatikane ndani ya miezi mitatu. Ajabu sana. Chadema ni wahuni. Katiba inatakiwa ipatikane hata ndani ya miaka 10 au hata 20. Iandikwe vema, ijadiliwe na iwekewe ulinzidhidi ya mtu yyte atakae taka kuibadili au kuivunja na mchakatao wa kubadili kipengele flani Yaan kipengele ili kibadilishwe inatakiwa kijadiliwe baada ya rais flani kutoka madarakani wa wakati huo kuepusha favour kwake esp kipengele ycha mihimili ya dola.
 
Katiba siyo takwa la waliopo madarakani wala siyo takwa la ambao hawapo madarakani bali ni takwa la wananchi.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Wanaoitaka Katiba mpya hawaitaki ili wapate madaraka bali kuleta Demokrasi ya kweli nchini. Nchi iwe na HAKI na UHURU kwa raia wote bila kujali itikadi zao. Chaguzi ziwe za HAKI na HURU, vyombo vya habari viwe huru kutenda kazi zao bila woga wa kufungiwa, kutekwa, kubambikiwa kesi na hata kuuawa.

Jicho la tatu linaonesha kiu ya wanaodai katiba mpya ni madaraka na wanaosema iliyopo inafaa pia wanataka kubaki madarakani. Suruhisho ni nini!??

Katiba iliyopo na hata mpya inayopiganiwa haiwezekani kuwa kamilifu na timilifu kamwe hasa hasa itakayoandaliwa katika mazingira haya yenye kila aina ya mihemuko ya kisiasa

Rais aliyepo Sasa amejitahidi kwa kiasi kikubwa kuonesha kuwa katiba iliyopo ilikanyagwa kwa makusudi na mtangulizi wake. Mfano kesi za kubambikia, kuminya uhuru wa habari,nk.

Kumbe Rais anaweza kuamrisha kitu nje ya katiba na kikawa na asifanywe chochote!

Hapa Rais Samia anatupa ujumbe kuwa dawa si katiba mpya pekee! Anatueleza tuna jambo kubwa la kufanya zaidi ya kudai katiba mpya!

Nawiwa kujiuliza, hivi tunadhani hiyo katiba mpya itakuwa na uwezo kabisa wa kumfunga break Rais asiweze kutumia vyombo vya ulinzi na usalama atakavyo?

Tuna uhakika tukipata katiba mpya itakayoruhusu tume huru na kupunguza madaraka ya Rais na tukaendelea na aina ya watanzania hawa hawa, wasomi hawa hawa itamzuia huyo Rais kutumia vyombo vyake hivyo vichache atakavyopewa kikatiba kuingilia vyombo vingine au kuvunja haki za raia atakavyo?

Najua mtasema ndio atazuiwa na katiba na kutakuwa na uwezo wa kumshughulikia kwa kuvunja katiba!

Huenda mkawa sahihi, lakini tujiulize ni mara ngapi wanasiasa hawa hawa na makundi mengine yasiyo ya kisiasa yametueleza kuwa Rais aliyepita alivunja katiba na haki za raia kwa makusudi? Tulimfanya nini??

Huenda maswali yangu yanaonekana ya kizwazwa lakini yatafakari kwa kina

Mapendekezo yangu ni haya:-

1. Wanasiasa wajikite zaidi kutoa elimu ya uraia na kujitambua kwa wananchi na kuwajengea uwezo wa kujiamini na utambuzi wa haki zao. Katiba mpya bila elimu ya uraia itakuwa kazi bure!

Elimu ikitolewa na ikaeleweka, mwananchi atajua haki zake, atajua kuzidai na atajua kuzitetea na atazipigania kwa kujiamini. Halikadhalika viongozi watawaheshimu wananchi na wataongoza kwa adabu

2. Mchakato wa katiba mpya 2014 ulivurugwa na wanasiasa hawa hawa wanaoidai leo. Huu ni uthibitisho kuwa wanasiasa wanaweza wasituletee katiba nzuri kwasababu za kimaslahi.

Walioko nje watataka katiba itakayowapa fursa ya kuingia ndani na walioko ndani watapigania vipengere vitakavyowahakikishia kuendelea kubaki madarakani

Hapa mkatae mkubali lakini ukweli ndio huo! Watajificha nyuma ya kivuli Cha kuwatetea wananchi lakini mioyoni wana Jambo lao!

Kinachoweza kufanyika ni kuunda kamati maalumu ya katiba mbali na ile ya Warioba itakayowaweka pembeni wanasiasa lakini Kama itawapendeza wachukue yale maoni ya tume ya Warioba Kama Kuna cha kuboresha waboreshe Kama Kuna haja ya kuongezea watajua wenyewe

Kamati hiyo iongozwe na majaji wa mahakama kuu na wastaafu waliowahi kuwa majaji wa mahakama kuu pamoja na mawakili wabobezi

Wajumbe wengine watoke vyombo vya ulinzi na usalama wenye uzoefu wa kutosha. Hawa watasaidia kuweka vipengere vitavyodhibiti vyombo vya ulinzi na usalama.

Inaaminika taasisi uliyoitumikia Kuna mapungufu unayaona wazi lakini unashindwa kuyaziba kwasababu huna uwezo.

Wakiwepo hawa wataunda vifungu vitakavyosaidia polisi, magereza, Jwtz na TISS wasioonee watu, viongozi na watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuweka vipengere vitakavyolinda maslahi na weledi wa vyombo hivi

Wajumbe wengine watoke miongoni mwa waliowahi kuwa washauri wa Rais katika vipindi vyote.

Hawa watakuwa na nafasi nzuri ya kutoa uzoefu wao pale walipojaribu kushauri kitu either cha kuvunja katiba au kujaribu kuzuia katiba isivunjwe. Hawa watatoa uzoefu wa nini kinafanya Rais avunje katiba na nini kiwekwe kuzuia

Wajumbe wengine watoke ndani ya bunge. Hapa simaanishi wabunge. Wachukuliwe wale waliowahi kuwa makatibu wa bunge na waliowahi kuwa Maspika wa bunge au kuhudumu ndani ya ofisi ya Spika. Hawa watakuwa na nafasi nzuri ya kutoa mawazo yao wabunge wawe na sifa gani ili bunge liwe imara kusimamia serikali na vifungu gani viwekwe kulisuka bunge ki uweledi zaidi kuliko ilivyosasa ambapo limekuwa jukwaa la kuzogoana

3. Mwisho kabisa vifungu vya katiba viwe topics kwenye somo la URAIA/CIVICS/GS. Leo watu wanaambiwa katiba mpya ila ni ajabu wengi hata waliopata bahati ya kupata elimu ya darasani hawaijui hii katiba iliyopo.

Wengi wanasikia kutoka kwa wanasiasa ila wao Kama wao hawajui udhaifu au umadhubuti wa katiba iliyopo. Si ajabu leo msomi wa chuo kikuu hajui kilichomo ndani ya katiba

Ikiwa sehemu ya somo mashuleni na ikawa somo la lazima kwa ngazi fulani ya elimu itaweza kusaidia Raia wengi kutambua haki zao za kikatiba na kuzipigania kuliko ilivyosasa

Kwa Sasa wanasiasa hawana nafasi nzuri ya kuleta katiba bora Tanzania kwa maslahi mapana ya Taifa. Wengi wana focus uchaguzi wa 2025 ndiomaana agenda kuu imekuwa kutoshiriki uchaguzi bila katiba mpya

Katiba haitakiwi ku focus uchaguzi tu! Katiba ni zaidi ya uchaguzi, ni zaidi ya CCM, CHADEMA na nk. Katiba ni zaidi ya Mbowe na Samia! Katiba inatakiwa iandaliwe bila pressure na kwa focus iliyohuru itakayojali Tanzania na watanzania waliopo na wajao!
 
Jicho la tatu linaonesha kiu ya wanaodai katiba mpya ni madaraka na wanaosema iliyopo inafaa pia wanataka kubaki madarakani. Suruhisho ni nini!??

Katiba iliyopo na hata mpya inayopiganiwa haiwezekani kuwa kamilifu na timilifu kamwe hasa hasa itakayoandaliwa katika mazingira haya yenye kila aina ya mihemuko ya kisiasa

Rais aliyepo Sasa amejitahidi kwa kiasi kikubwa kuonesha kuwa katiba iliyopo ilikanyagwa kwa makusudi na mtangulizi wake. Mfano kesi za kubambikia, kuminya uhuru wa habari,nk.

Kumbe Rais anaweza kuamrisha kitu nje ya katiba na kikawa na asifanywe chochote!

Hapa Rais Samia anatupa ujumbe kuwa dawa si katiba mpya pekee! Anatueleza tuna jambo kubwa la kufanya zaidi ya kudai katiba mpya!

Nawiwa kujiuliza, hivi tunadhani hiyo katiba mpya itakuwa na uwezo kabisa wa kumfunga break Rais asiweze kutumia vyombo vya ulinzi na usalama atakavyo?

Tuna uhakika tukipata katiba mpya itakayoruhusu tume huru na kupunguza madaraka ya Rais na tukaendelea na aina ya watanzania hawa hawa, wasomi hawa hawa itamzuia huyo Rais kutumia vyombo vyake hivyo vichache atakavyopewa kikatiba kuingilia vyombo vingine au kuvunja haki za raia atakavyo?

Najua mtasema ndio atazuiwa na katiba na kutakuwa na uwezo wa kumshughulikia kwa kuvunja katiba!

Huenda mkawa sahihi, lakini tujiulize ni mara ngapi wanasiasa hawa hawa na makundi mengine yasiyo ya kisiasa yametueleza kuwa Rais aliyepita alivunja katiba na haki za raia kwa makusudi? Tulimfanya nini??

Huenda maswali yangu yanaonekana ya kizwazwa lakini yatafakari kwa kina

Mapendekezo yangu ni haya:-

1. Wanasiasa wajikite zaidi kutoa elimu ya uraia na kujitambua kwa wananchi na kuwajengea uwezo wa kujiamini na utambuzi wa haki zao. Katiba mpya bila elimu ya uraia itakuwa kazi bure!

Elimu ikitolewa na ikaeleweka, mwananchi atajua haki zake, atajua kuzidai na atajua kuzitetea na atazipigania kwa kujiamini. Halikadhalika viongozi watawaheshimu wananchi na wataongoza kwa adabu

2. Mchakato wa katiba mpya 2014 ulivurugwa na wanasiasa hawa hawa wanaoidai leo. Huu ni uthibitisho kuwa wanasiasa wanaweza wasituletee katiba nzuri kwasababu za kimaslahi.

Walioko nje watataka katiba itakayowapa fursa ya kuingia ndani na walioko ndani watapigania vipengere vitakavyowahakikishia kuendelea kubaki madarakani

Hapa mkatae mkubali lakini ukweli ndio huo! Watajificha nyuma ya kivuli Cha kuwatetea wananchi lakini mioyoni wana Jambo lao!

Kinachoweza kufanyika ni kuunda kamati maalumu ya katiba mbali na ile ya Warioba itakayowaweka pembeni wanasiasa lakini Kama itawapendeza wachukue yale maoni ya tume ya Warioba Kama Kuna cha kuboresha waboreshe Kama Kuna haja ya kuongezea watajua wenyewe

Kamati hiyo iongozwe na majaji wa mahakama kuu na wastaafu waliowahi kuwa majaji wa mahakama kuu pamoja na mawakili wabobezi

Wajumbe wengine watoke vyombo vya ulinzi na usalama wenye uzoefu wa kutosha. Hawa watasaidia kuweka vipengere vitavyodhibiti vyombo vya ulinzi na usalama.

Inaaminika taasisi uliyoitumikia Kuna mapungufu unayaona wazi lakini unashindwa kuyaziba kwasababu huna uwezo.

Wakiwepo hawa wataunda vifungu vitakavyosaidia polisi, magereza, Jwtz na TISS wasioonee watu, viongozi na watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuweka vipengere vitakavyolinda maslahi na weledi wa vyombo hivi

Wajumbe wengine watoke miongoni mwa waliowahi kuwa washauri wa Rais katika vipindi vyote.

Hawa watakuwa na nafasi nzuri ya kutoa uzoefu wao pale walipojaribu kushauri kitu either cha kuvunja katiba au kujaribu kuzuia katiba isivunjwe. Hawa watatoa uzoefu wa nini kinafanya Rais avunje katiba na nini kiwekwe kuzuia

Wajumbe wengine watoke ndani ya bunge. Hapa simaanishi wabunge. Wachukuliwe wale waliowahi kuwa makatibu wa bunge na waliowahi kuwa Maspika wa bunge au kuhudumu ndani ya ofisi ya Spika. Hawa watakuwa na nafasi nzuri ya kutoa mawazo yao wabunge wawe na sifa gani ili bunge liwe imara kusimamia serikali na vifungu gani viwekwe kulisuka bunge ki uweledi zaidi kuliko ilivyosasa ambapo limekuwa jukwaa la kuzogoana

3. Mwisho kabisa vifungu vya katiba viwe topics kwenye somo la URAIA/CIVICS/GS. Leo watu wanaambiwa katiba mpya ila ni ajabu wengi hata waliopata bahati ya kupata elimu ya darasani hawaijui hii katiba iliyopo.

Wengi wanasikia kutoka kwa wanasiasa ila wao Kama wao hawajui udhaifu au umadhubuti wa katiba iliyopo. Si ajabu leo msomi wa chuo kikuu hajui kilichomo ndani ya katiba

Ikiwa sehemu ya somo mashuleni na ikawa somo la lazima kwa ngazi fulani ya elimu itaweza kusaidia Raia wengi kutambua haki zao za kikatiba na kuzipigania kuliko ilivyosasa

Kwa Sasa wanasiasa hawana nafasi nzuri ya kuleta katiba bora Tanzania kwa maslahi mapana ya Taifa. Wengi wana focus uchaguzi wa 2025 ndiomaana agenda kuu imekuwa kutoshiriki uchaguzi bila katiba mpya

Katiba haitakiwi ku focus uchaguzi tu! Katiba ni zaidi ya uchaguzi, ni zaidi ya CCM, CHADEMA na nk. Katiba ni zaidi ya Mbowe na Samia! Katiba inatakiwa iandaliwe bila pressure na kwa focus iliyohuru itakayojali Tanzania na watanzania waliopo na wajao!
Ni moja ya Uzi Bora kabisa
 
Back
Top Bottom