Walioiuza CHADEMA mwaka 2015 sasa hivi ndio wanachukua hatamu huku wakijinadi hawanunuliki, Watanzania hawajasahau

Tujifunze kutofautisha majungu na ukweli /uhalisia.

2015 Mbowe alifanya tukio la kipumbavu kuikabidhi chadema kwa fisadi papa.

Hasipokubali kutoka hadharani na kukiri udhaifu huo. Huo mzimu wa tamaa ya pesa utaendelea kumtafuna yeye na chama anachokiongoza.
Fisadi papa is back where he belongs, amesharudi kwa mafisadi wenzake.
 
Ndugu zangu,

Nianze tu kwa kusema Watanzania si wajinga, wanakumbuka yote yaliyotokea mwaka 2015. CHADEMA inatumia nguvu kubwa kuwanadi walioshiriki kujipatia hela kwenye siasa za mwaka 2015 huku ikiwanadi kuwa eti hao ndio ''chadema asili'' na ''hawanunuliki''. Kundi linalojinasibu kuirudisha Chadema kwenye mstari kama ile Chadema kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015 linaundwa na wafuatao, nitaweka kauli zao walizosema wakihalalisha ujasiriasiasa wao kwa kushibisha matumbo yao huku sasa wakijinasibu eti wao ndio wanataka ''chadema ya zamani''.
  1. Freeman Mbowe; huyu anarudi, huku akisema kuwa ''CCM isituchagulie Mwenyekiti, mwaka 2015 alisikika akimsifia Lowassa na Sumaye kuwa ''hatuwezi kuacha mtu anayekuja na mamilioni ya kura ili kumridhisha mtu mmoja (Dr.Slaa), alimalizia ''Chama ni watu''. Kumbuka wale wananchi wengi wa mwaka 2015 ndio watapiga kura 2020.
  2. Godbless Lema; Mwaka 2015 alitumia mistari ya Biblia akitabiri ''anguko la CCM'' kwa ujio wa EL Chadema huku akikana matamshi yake aliyowahi kumtusi EL kipindi cha kampeni za Ubunge Arumeru Mashariki. Je anaushawishi kwa watanzania?
  3. Jacob Boniface; Huyu naweza kusema ni limbukeni wa madaraka, siku hizi ukimwita jina lake ''Jacob'' haitikia anataka umwite ''Meya''. Huyu na kundi lake walikusanyika ofisini kwa Lowassa pale Mikocheni wakimshukuru kwa kuwasaidi kushinda udiwani, umeya na ubunge Dar. alisikika akisema ''Mh.Lowassa bila wewe sisi si kitu, umetubeba kwenye uchaguzi'' akikana haya maneno lazima apate laana, je anaushawishi kwa Watanzania?
  4. Peter Msingwa; Huyu kipindi cha kampeni akihojiwa Channel 10 alisema '' EL ni turufu kubwa kwani kwa utafiti waliofanya waligundua ni asilimia 5 tu ya watanzania ndio humnyima kura mtu sababu ya tuhuma za ufisadi'', hivyo wao wameamua kumpa EL kijiti cha urais ili Chadema inufake. Je Msigwa anaushawishi kwa wananchi?
  5. John Mrema; huyu ndiye alikuwa kinara akichukua nafasi ya Mnyika aliyesusa, yeye aliambatana na EL kila alipopita akiwa na kauli mbiu yake ''kama EL, Kingunge, Sumaye wametoka CCM nani atawaweza?'' kwasasa kabaki yeye na wenzake, je Watanzania watawasamehe?
  6. Halima Mdee n.k
Wapo wengi ila kwa sasa timu hii ya watu sita ndio kiini cha Chadema, wao ndio wanaona ''hawanunuliki'' japo njaa zao za mwaka 2015 bado zinawaondolea uhalali kusema ''hawanunuliki.

Nimalize tu kwa kusema kikundi hicho hapo juu hakiaminiki, kinanunulika na kwa sasa hawana uhalali kwa Watanzania.


Wakudadavuwa nini unaumia sana roho na uongozi wa Chadema usio na kitu zaidi ya mateso na karaha za polisi, rumande,mahakamani na jela?
Tumekupa vyote ambavyo kijana wa kike angetamani kuwa navyo lakini jicho kako la husuda liko Chadema na kila siku hukosi kuja na tuhuma.
Basi mama tuliza moyo wako na kibao hicho cha Lady Jide labda sumu moyoni itakuishia. Kama bado ni PM nikupatie kitu fulani lazima roho itatulia tuu
 
He is a Freeman.... Kuna majina ya kuwaita watoto aisee kumbe! Sio mtoto unamuita Jaffo, sijui Kangi ukikosea kidogo tu badala ya Jaffo unasema Jasho na huyo mwingine anaitwa Bangi!
Au unamuita sijui Boha, dengerua au kwa kiswahili chake lazima iwe balaa!
 
kama wananchi wangewasapoti wangetoka barabarani.... tatizo sasa nguvu ya umma mliiuza mwaka 2015
Hapo ndipo ulipaswa hata kumuombea kwa Mungu ampe maisha marefu Mbowe, watu wasingejengewa tabia ya ustaarabu unadhani mngekuwa salama na hizo VX kutundika bendera mabarabarani?
 
kama wananchi wangewasapoti wangetoka barabarani.... tatizo sasa nguvu ya umma mliiuza mwaka 2015
People's power haikuwa na nguvu mbele ya money power .Baada ya kupokea tu pesa ya Lowasa Chadema na akina Mbowe na akina Tundu List ghafla wakaacha kuimba people's power wakaanza kuimba wimbo mpya walioutunga ghafla baada ya kulamba pesa ule wa Lowasa mabadiliko,mabadiliko Lowasa .Chezea nguvu pesa chadema hakuna Cha people's power Wala Nini chadema Kuna wajasiliamali wa kisiasayaani political enterpreneurs akina Mbowe,Tundu Lisu ,Mdee,Mnyika,Msigwa nk Kwa political enterpreneurs Act Wazalendo Yuko Zitto Kabwe na CCM Lowasa.
 
Umewaza mbali sana mkuu,

mimi nina swali la kuongezea.

Kama chama walikiuza,tena kwa mtu mmoja tu mwenye ukwasi na kututangazia watanzania gear ya angani.
Je wakipewa IKULU itakuwaje na tamaa zao hizo?

Na tunawaona wanavyojiuza kwa mabeberu huko EU na USA.
si watatutangazia gear ya IKULU?
Hawaaminiki hawa wahuni
 
People's power haikuwa na nguvu mbele ya money power .Baada ya kupokea tu pesa ya Lowasa Chadema na akina Mbowe na akina Tundu List ghafla wakaacha kuimba people's power wakaanza kuimba wimbo mpya walioutunga ghafla baada ya kulamba pesa ule wa Lowasa mabadiliko,mabadiliko Lowasa .Chezea nguvu pesa chadema hakuna Cha people's power Wala Nini chadema Kuna wajasiliamali wa kisiasayaani political enterpreneurs akina Mbowe,Tundu Lisu ,Mdee,Mnyika,Msigwa nk Kwa political enterpreneurs Act Wazalendo Yuko Zitto Kabwe na CCM Lowasa.
Hakika
 
Watanzania na siasa za vyama,na ndiyo maana ccm itaendelea kuwepo madarakani kwa kipindi kirefu sana
Tunaambiwa ccm hawafanyi uchaguzi halali huwa miaka yote wanaiba kura sasa sijui Lowassa ndio angefanya ccm wasiibe kura au vp hata sielewi.
 
Watanzania na siasa za vyama,na ndiyo maana ccm itaendelea kuwepo madarakani kwa kipindi kirefu sana
Tunaambiwa ccm hawafanyi uchaguzi halali huwa miaka yote wanaiba kura sasa sijui Lowassa ndio angefanya ccm wasiibe kura au vp hata sielewi.
wanasema alikuwa na ''connections'' zote na alikuja na mtaalam wa kuiba kura.
 
wanasema alikuwa na ''connections'' zote na alikuja na mtaalam wa kuiba kura.
Sasa ikawaje tena hao wataalam wakaishia wapi? Sasa hivi anzungumziwa Lissu yani ndio hivyo hivyo tu hakika watanzania wanahitaji mwanasaikolojia maana hawako sawa
 
Huku siasani kuna upumbavu mwingi sana, watu wameziba masikio na pamba, wanasifu na kuabudu tu mda wote. Hawa wanaabudu CCM ya Yohana, wale wanaabudu CDM ya Freeman, hamna hata mmoja yupo constructive, hapa tunasifu na kuabudu tu...
 
Mamvi alisha wanunua DJ Mbowe na Wakili msomi uchwara Tundu Lisu kwa vipande vya fedha za kitanzania. Itakua jambo la kushangaza kuu ambia umma kua DJ na Lisu hawana bei ya kuwanunua. Lakini mimi ni nani niwa bishie Nyumbu wenye chama Chao kwa kudai DJ naLisu hawana bei?
Amakwa hakika chini ya jua vituko havitaisha.


Kwa hiyo wewe ukinunua kitu huwa huondoki nacho unaondoka na kukiacha?
 
Acha kujifanya hujui alichofanya January na Nape
Mimi ni nani nijue hadi niweze kujua walichofanya? Nachoelewa mie ni malalamiko ya wizi wa kura na vitu kama hivyo na hakujawahi kutatuliwa hayo malalamiko ila ajabu kila uchaguzi tunapewa matumaini ya kuwashinda ccm hali ya kuwa tunajua hakujatatuliwa mambo yenye kukwamisha kumtoa ccm,hivi hauoni kuwa watanzania hatupo sawa? Kuna watu ile hali ya kuilalamikiwa ccm imekuwa ni kama wanaipenda sasa wanaona raha ile kulalamika muda wote hakika kuna tatizo.
 
Nimalize tu kwa kusema kikundi hicho hapo juu hakiaminiki, kinanunulika na kwa sasa hawana uhalali kwa Watanzania.

Kwenye nchi nyingine mara tu baada ya kushindwa 2015 viongozi wote wa juu wa CDM walitakiwa kujiuzulu. Ndio demokrasia yenyewe. Sasa watu wanawaongoza kuanzia 2005, 2010, 2015 na kote wanashindwa na bado mnataka wawaongoze hadi 2060!?
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom