Walioiongezea IPTL mkataba ni wahujumu uchumi wachukuliwe hatua!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
IPTL imekuwa na mkataba wa kifisadi na Tanesco kwa kuiuzia Tanesco umeme kwa bei ya juu zaidi ya soko na kuifanya Tanesco iendeshwe kwa hasara kwa sababu tozo zake ziko chini ya bei ya umeme Tanesco walizozinunulia!

Tusiukwepe ukweli ya kuwa waliowaongezea IPTL mkataba kwa masharti yale yale ya kifisadi na la ajabu hadi leo waliowaongezea mkataba IPTL hawajachukuliwa hatua kwa makosa ya jinai ya kuuhujumu uchumi.

Baada ya kuwaongezea IPTL mkataba wa kuendelea kuifilisi Tanesco bila kuishirikisha EWURA na kuigeuza EWURA rubber stamp ni wazi waliingilia majukumu ya kisheria ya EWURA.

Bila kuwachukulia hatua wahusika hawa na EWURA kugoma kuwaongezea muda wa leseni IPTL hadi watakapokubali kuwauzia Tanesco umeme bei chini ya bei Tanesco inawauzia wateja wake na kufuta capacity charges ambazo sisi ni kati ya nchi chache sana zina mikataba na wawekezaji ya kipumbavu kama hii.

Tumbua tumbua majipu hewa huku tunalinda saratani ni utapeli wa kutisha wa kisiasa ambao wakati tu ndiyo utawaumbua wasanii hawa.

Waliowaongezea mkataba IPTL ni baraza la mawaziri la JK ambalo mtumbua majipu ni Mjumbe sasa ni nani wa kumfunga paka kengele?
 
IPTL imekuwa na mkataba wa kifisadi na Tanesco kwa kuiuzia Tanesco umeme kwa bei ya juu zaidi ya soko na kuifanya Tanesco iendeshwe kwa hasara kwa sababu tozo zake ziko chini ya bei ya umeme Tanesco walizozinunulia!

Tusiukwepe ukweli ya kuwa waliowaongezea IPTL mkataba kwa masharti yale yale ya kifisadi na la ajabu hadi leo waliowaongezea mkataba IPTL hawajachukuliwa hatua kwa makosa ya jinai ya kuuhujumu uchumi.

Baada ya kuwaongezea IPTL mkataba wa kuendelea kuifilisi Tanesco bila kuishirikisha EWURA na kuigeuza EWURA rubber stamp ni wazi waliingilia majukumu ya kisheria ya EWURA.

Bila kuwachukulia hatua wahusika hawa na EWURA kugoma kuwaongezea muda wa leseni IPTL hadi watakapokubali kuwauzia Tanesco umeme bei chini ya bei Tanesco inawauzia wateja wake na kufuta capacity charges ambazo sisi ni kati ya nchi chache sana zina mikataba na wawekezaji ya kipumbavu kama hii.

Tumbua tumbua majipu hewa huku tunalinda saratani ni utapeli wa kutisha wa kisiasa ambao wakati tu ndiyo utawaumbua wasanii hawa.


Lowasa huyo lazima ashitakiwe!
 
TUMECHOKA NA FUKUZA FUKUZA YA WATUMISHI WA SERIKALI AFU TUNAWAONA WANADUNDA MITAANI NA PESA WALIZOIBIA SERIKALI.WASHITAKIWE KWANZA NA KUFILISIWA PIA
 
ss unaleta mada baada ya mtu kutumbuliwa? au hujui kama kashatumbuliwa?

zile mvi mpaka ziishe kbs ndo atabaki salama
 
TUMECHOKA NA FUKUZA FUKUZA YA WATUMISHI WA SERIKALI AFU TUNAWAONA WANADUNDA MITAANI NA PESA WALIZOIBIA SERIKALI.WASHITAKIWE KWANZA NA KUFILISIWA PIA
Hao waliowaongezea mkataba IPTL ni akina nani kama siyo baraza la mawaziri la JK na walifanya hivyo kwa manufaa ya nani?

Unapomtumbua kibosile wa Tanesco kwa kuongeza bei ili amudu gharama za kifisadi zilizopitishwa na vikao vya baraza la mawaziri ambavyo ulishiriki sasa wakuwajibika ni yupi hasa?
 
ss unaleta mada baada ya mtu kutumbuliwa? au hujui kama kashatumbuliwa?

zile mvi mpaka ziishe kbs ndo atabaki salama
Baraza la mawaziri lote la JK watujuze ni kwa masilahi gani walimuongezea IPTL mkataba?
 
Lakini ni kiini macho kwani watumbua majipu hawataki kufukua makaburi kuona kilichozikwa ni nini hasa!
Ambalo sielewi ni kama wana mkataba ni lazima wana haki ya kupewa leseni? Na kama wameshindwa kupata leseni wanaweza kushitaki kwa kunyimwa? Naomba nijue kama IPTL kupata mkataba automatically wanakuwa na guaratee ya kupata leseni ya usalishaji umeme. Na mkatabq utakuwa ni kati ya TANESCO na IPTL na siyo kati ya serikali na IPTL. Naomba kufafanuliwa hapa.
 
Nyinyi si mnaogopa tutashitakiwa?
Aloahidi kutofukua makaburi ni JPM hapo upinzani unaingiaje?? Waloasisi hii mikataba wanajulikana na CCM msituone hatuna akili.

Pia ujinga wa kutengeneza kadi za chadema na kuwapa watu wenu ati waact km wanazirudisha ni upumbafu wa zaidi ya kujitekenya kisha kujichekelesha
 
Ah ah Leo upinzani wamekuwa kikwazo mbona wakati mkiingia iyo mikataba bungeni kwa hati za dharula uku mkijivunia uwingi wenu upinzani hamkuwashirikisha???

Ilo lenu CCM jipangeni nalo. Msisingizie upinzani
Ni maswali ambayo kamwe hawezi kuyajibu hata umpe karne nzima
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom