Waliohusika tukio la askari kumuua raia Kigoma kwa risasi wachukuliwe hatua, Serikali yaombwa Jeshi la Polisi lichunguzwe

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimelaani tukio la mauaji ya Juma Ramadhan (35) kupigwa risasi na askari wakati Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma likidhibiti vurugu, Machi 14, 2022 katika Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

LHRC imetoa wito hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya afisa wa Polisi waliohusika katika tukio hilo, iundwe Tume Huru ya kijaji kufanya uchunguzi wa kifo hicho na kuanzisha chombo huru kwa ajili ya kupokea na kuchunguza matukio dhidi ya Jeshi la Polisi.

Wamesema Jeshi la Polisi linatakiwa kuzingatia mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Matumizi ya Nguvu na Silaha wa Mwaka 1990 pamoja na Mwongozo wa Utendaji kazi wa Jeshi la Polisi (PGO marejeo ya mwaka 2021).
FN9qylTXoAEhbTz.jpg

FN9q6RNXMAESx6f.jpg
 
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimelaani tukio la mauaji ya Juma Ramadhan (35) kupigwa risasi kisha kufariki dunia wakati Jeshi la Polisi mkoani Kigoma likijaribu kudhibiti vurugu, Machi 14, 2022 katika Uwanja wa Lake Tanganyika- Kigoma.

LHRC imesema licha ya Polisi kuwa na mamlaka ya kuzuia ghasia bado linawajibika kuzingatia, kuheshimu na kulinda misingi, kanuni, taratibu namiongozi mbalimbali ya utendaji kazi wa jeshi hilo.
View attachment 2152912
View attachment 2152913
Wao wanalaani sisi watanzania tunaona poa tu.
 
Watalaani na itaishia hapo.

Polisi hawatajali juu ya familia yake, Mke wake mjane, watoto wake na ndugu wanaomtegemea

Pia sidhani kama watagharamia mazishi yake. Hii nchi hii
 
Katiba mpya ndio mwarobaini wa hii issue ya hawa majambazi in uniforms, katiba mpya itatupatia IPID, hawa watakua wana deals na matukio yote ya kisheria ambao jeshi la polisi nao ni suspects, hawa watakua na uwezo to open the docket, investigate ,arresting (suspects kama ni polisi)na kuwafikisha mahakamani, hawa watakua na ofisi within vituo vya polisi, but watanzania tutapiga demo humu kama ilivyokua mtwara, tunasahau na maisha yanaendelea,igp leo alikua anatoa gari somewhere na nimemwona Kingai akitoka nyumba ya ibada, sijui alikua anasali nini mle wakati mikono yake imejaa damu za binadamu wenzake.
 
Back
Top Bottom