Waliofukuzwa Udiwani Arusha Wawa Kivutio Mkutano Wa RC

PakaJimmy

JF-Expert Member
Apr 29, 2009
16,203
8,723
Madiwani watatu kati ya wa5 waliofukuzwa uanachama kutokana na mgogoro wa uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Arusha, jana walikuwa kivutio katika mkutano wa Utambulisho wa Mkuu Mpya wa Mkoa wa Arusha Magessa Mulongo, uliofanyika katika bwalo la Polisi jijini Arusha, baada ya kujitambulisha kwa Nyadhifa zao licha ya kutoalikwa.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha Estomih Chang'a alisema ofisi yake haikuwaalika madiwani waliofukuzwa kutokana na uamuzi wa mahakama.
"Tayari nimemwagiza Mwanasheria wa Manispaa kufuatilia nakala ya hukumu hiyo ili nimwandikie Waziri husika kuomba maelekezo ya kinachofuata.
Leo sijawaalika na hata kwenye kikao cha Baraza kilichofanyika baada ya hukumu ya mahakama sikuwaruhusu kuhudhuria, labda wamekuja kama wananchi wa kawaida na wadau wa maendeleo"
alisema Chang'a.

Aisema ofisi yake haiwezi kuendelea kuwakumbatia au kuwatambua baada ya uamuzi wa mahakama iliyokataa kuwarejeshea uanachama wa Chadema.

Awali, Madiwani hao watatu walijitambulisha mkutanoni hapo bila kutarajiwa, ambapo Estomih Malla alijitambulisha kuwa ni Diwani wa kata ya Kimandolu, na Rehema Mohamed Diwani wa viti Maalum, akimalizia John Bayo ambaye alisema kuwa ni Mwenyekiti wa serikali ya mtaa kwenye kata yake.

SOURCE: Gazeti la Mwananchi Alhamisi, Sept 29, 2011.

My take:
Aibu kubwa hii!
Kwanini kujidhalilisha?...Kwa nini unaruhusu masikio yakue na kukipita kichwa, wakati unajua mbele giza?...Pole zao!
 
kwa wale wapenda coomedies kama mimi, Nafikiri mtakua mmewatch Sinema ya Mr. Bean by the tittle ''JOHN ENGLISH''

You remember what were mr. bean (John English) on agent ones' Status?

Thats tells all.
 
Hao jamaa kuna thread hapa ilisema wameamua kugombea tena kupitia nccr. Kwahiyo watakuwa wanauzauza sura maana wanaelekea kupotea kwenye ulingo wa siasa.
Othewise ni ulevi wa madaraka. Hawaamini kama walishavuliwa uongozi!

Aibu iliyowapata ni malipo ya ubaya. Siku zote mwisho wa ubaya ni aibu!
 
Tatizo la viongozi wenye IQ ndogo. Wanashindwa kufikiri kabla ya kutenda, wanatenda ndipo wanafikiri. Shame on them.
 
Nimeambiwa juzi kwamba Estomihi Mallah anataka kuhama anakoishi Kimandolu baada ya kushindwa kupita mitaani mchana.
Sisi wa kimandolu mbona huyo diwani aliyejitambusha hatambuliwi kabisa sisi tunasubiri uchaguzi wa madiwani. Ni huyu huyu kwenye sikukuu ya mashujaa alijitambulisha kama Naibu meya wa manispaa ya arusha na kupiga picha ili awepo katika kumbukumbu za historia ya manispaa ya Arusha.
 
Njaa haina adabu,kwani huko nikijidhalilisha,ni kwanini wanalazisha kuongoza?nadhani hiyo ni kushindwa kuikakbili njaa,na hii ndo imetufikisha hapa watanzania,kwani Mibunge yetu mingi huwa inapayuka ndio ili tu isije enguliwa kwa kuonekana wanakwend kinyume na matakwa ya wakubwa,hivyo utakutana na Ndioooo, nyingi kule Dodoma.na ndio hizi hata kama zinawakandamiza wapiga kura bado huwa hawaangalii,mfano huu ni dhahiri hata kwa hawa madiwani walioenguliwa,wanaendelea kujipendekeza kama waheshimiwa madiwani wakati wala watu hawana mpango nao,nadhani waliingia Chadema bila kujua uongozi uko imara kiasi gani,walidhani unafiki wa CCM uko hata Chadema,hivyo walidhani kupoteza madiwani watano itakuwa ni vigumu,kumbe kwenye ukombozi wa kweli hata kama ni wote bado wangeenguliwa.Hao ni njaa jamani kwani hawafikirii hata damu na roho za watu zilipotea Arusha,angalia leo wanabaki kujipendekeza mara kujionyesha onyesha.
Ushauri wa bure waende CCM,na wajiandae kugombea tena,si hata kilanja mkuu alikuwa anawatetea pamoja na Mkuchika?
Wanakula unafiki wao sasa wajifunze kuvumilia.
 
Kweli aisee hawa jamaa walifanya mambo mema sn mpaka wanakuwa kivutio kwa jamii.
Una mfano wa mambo hayo ututajie?

Kilichobaki kwa hawa jamaa kwa sasa ni kujichomeka mahala popote penye kusanyiko , ili watu wawaonee huruma.
Nasikia wakazi wa kata za huko watokako hata wakiwa na Ubarikio madiwani hao wanahudhuria, hata bila kualikwa...Ni kama wamepagawa, na wanatia huruma sana!
Ama kweli Majuto ni mjukuu!
 
Njia ni nyembamba wapitao ni wachache wenye nia safi na wanao ogopa Hukumu ya mwisho. Waliiona Chadema kama Daladala ya Kwenda Mbagala Siyo....????
 
Uchaguzi mdogo unakuja. Hawa walipendwa sana na ccm na serikali yake. Nadhani itakuwa busara kwa ccm na serikali yao kuwachukuwa hawa na kuwasimamisha kwenye uchaguzi kwa tiketi ya ccm ili wajipatie ushindi wa kishindo. Waziri ------------ upo hapo?
 
Back
Top Bottom