PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,723
Madiwani watatu kati ya wa5 waliofukuzwa uanachama kutokana na mgogoro wa uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Arusha, jana walikuwa kivutio katika mkutano wa Utambulisho wa Mkuu Mpya wa Mkoa wa Arusha Magessa Mulongo, uliofanyika katika bwalo la Polisi jijini Arusha, baada ya kujitambulisha kwa Nyadhifa zao licha ya kutoalikwa.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha Estomih Chang'a alisema ofisi yake haikuwaalika madiwani waliofukuzwa kutokana na uamuzi wa mahakama.
"Tayari nimemwagiza Mwanasheria wa Manispaa kufuatilia nakala ya hukumu hiyo ili nimwandikie Waziri husika kuomba maelekezo ya kinachofuata.
Leo sijawaalika na hata kwenye kikao cha Baraza kilichofanyika baada ya hukumu ya mahakama sikuwaruhusu kuhudhuria, labda wamekuja kama wananchi wa kawaida na wadau wa maendeleo" alisema Chang'a.
Aisema ofisi yake haiwezi kuendelea kuwakumbatia au kuwatambua baada ya uamuzi wa mahakama iliyokataa kuwarejeshea uanachama wa Chadema.
Awali, Madiwani hao watatu walijitambulisha mkutanoni hapo bila kutarajiwa, ambapo Estomih Malla alijitambulisha kuwa ni Diwani wa kata ya Kimandolu, na Rehema Mohamed Diwani wa viti Maalum, akimalizia John Bayo ambaye alisema kuwa ni Mwenyekiti wa serikali ya mtaa kwenye kata yake.
SOURCE: Gazeti la Mwananchi Alhamisi, Sept 29, 2011.
My take:
Aibu kubwa hii!
Kwanini kujidhalilisha?...Kwa nini unaruhusu masikio yakue na kukipita kichwa, wakati unajua mbele giza?...Pole zao!
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha Estomih Chang'a alisema ofisi yake haikuwaalika madiwani waliofukuzwa kutokana na uamuzi wa mahakama.
"Tayari nimemwagiza Mwanasheria wa Manispaa kufuatilia nakala ya hukumu hiyo ili nimwandikie Waziri husika kuomba maelekezo ya kinachofuata.
Leo sijawaalika na hata kwenye kikao cha Baraza kilichofanyika baada ya hukumu ya mahakama sikuwaruhusu kuhudhuria, labda wamekuja kama wananchi wa kawaida na wadau wa maendeleo" alisema Chang'a.
Aisema ofisi yake haiwezi kuendelea kuwakumbatia au kuwatambua baada ya uamuzi wa mahakama iliyokataa kuwarejeshea uanachama wa Chadema.
Awali, Madiwani hao watatu walijitambulisha mkutanoni hapo bila kutarajiwa, ambapo Estomih Malla alijitambulisha kuwa ni Diwani wa kata ya Kimandolu, na Rehema Mohamed Diwani wa viti Maalum, akimalizia John Bayo ambaye alisema kuwa ni Mwenyekiti wa serikali ya mtaa kwenye kata yake.
SOURCE: Gazeti la Mwananchi Alhamisi, Sept 29, 2011.
My take:
Aibu kubwa hii!
Kwanini kujidhalilisha?...Kwa nini unaruhusu masikio yakue na kukipita kichwa, wakati unajua mbele giza?...Pole zao!