Travelogue_tz
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 848
- 1,212
Habari wadau. Yajayo yanafurahisha.
Waliokuwa Wabunge wa Viti Maalum 19 wakiongozwa na Halima Mdee wameanza kutofautiana hasa baada ya kufutwa Uanachama, na mapokeo ya maamuzi hayo kwa BAWACHA wenzao na Wanachama kwa ujumla.
Kwa taarifa zilizopo ni kwamba Dada mmoja kutoka Mbeya ameungana na wenzake na wameanza kushinikiza ili waende kuonana na mwenyekiti ili kuomba msamaha.
Jambo hili limeathiri mpango wa pamoja wa kutoa tamko kulaani kuvuliwa uanachama, kutokana na baadhi kutokubaliana na matamshi yanayokinzana na misimamo yao.
Muda unakwenda kasi, muda si mrefu tutasikia mapya juu ya mchongo mzima wa jinsi suala hili lilivyokuwa, watasema wenyewe na tutaelewa vizuri.
Waliokuwa Wabunge wa Viti Maalum 19 wakiongozwa na Halima Mdee wameanza kutofautiana hasa baada ya kufutwa Uanachama, na mapokeo ya maamuzi hayo kwa BAWACHA wenzao na Wanachama kwa ujumla.
Kwa taarifa zilizopo ni kwamba Dada mmoja kutoka Mbeya ameungana na wenzake na wameanza kushinikiza ili waende kuonana na mwenyekiti ili kuomba msamaha.
Jambo hili limeathiri mpango wa pamoja wa kutoa tamko kulaani kuvuliwa uanachama, kutokana na baadhi kutokubaliana na matamshi yanayokinzana na misimamo yao.
Muda unakwenda kasi, muda si mrefu tutasikia mapya juu ya mchongo mzima wa jinsi suala hili lilivyokuwa, watasema wenyewe na tutaelewa vizuri.