Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,701
- 36,120
Mimi ninafanya kazi taasisi moja iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, wizara ambayo Magufuli kahudumu kwa muda mwingi.
Hapa watu kuhamishiwa wizarani au mtu wa wizarani kuja hapa ni jambo la kawaida tu.
Ngoja nikupe kisa kimoja tu cha huyu aliyekuwa msaidizi wa Magufuli. Kuna kipindi alitaka kujenga sasa alipoona ukaribu wake na mh. Magufuli (kipindi akiwa waziri) alimshirikisha dhamira yake. Alimwita baba naomba unikopeshe milioni 5 niongezee na kiasi nilichonacho nijenge. Nitakurudishia baba. Jamaa aliambulia majibu ya kukaripiwa kama mtoto.
Huyu mtu mpaka Magufuli anafariki akiwa Rais bado alikuwa mmoja wa wafanyakazi wake.
Hapo point si kumsaidia kila mtu anayehitaji msaada kwake maana hata yeye mwenyewe alikuwa na mahitaji yake binafsi. Point iliyonifanya nilete uzi ni majibu ya ukali aliyompa kana kwamba hamfahamu kabisa.
Hapa watu kuhamishiwa wizarani au mtu wa wizarani kuja hapa ni jambo la kawaida tu.
Ngoja nikupe kisa kimoja tu cha huyu aliyekuwa msaidizi wa Magufuli. Kuna kipindi alitaka kujenga sasa alipoona ukaribu wake na mh. Magufuli (kipindi akiwa waziri) alimshirikisha dhamira yake. Alimwita baba naomba unikopeshe milioni 5 niongezee na kiasi nilichonacho nijenge. Nitakurudishia baba. Jamaa aliambulia majibu ya kukaripiwa kama mtoto.
Huyu mtu mpaka Magufuli anafariki akiwa Rais bado alikuwa mmoja wa wafanyakazi wake.
Hapo point si kumsaidia kila mtu anayehitaji msaada kwake maana hata yeye mwenyewe alikuwa na mahitaji yake binafsi. Point iliyonifanya nilete uzi ni majibu ya ukali aliyompa kana kwamba hamfahamu kabisa.