Waliochapwa na DC Arusha na kulazimishwa kulipa fedha bila kufikishwa mahakamani waombe msaada wa kisheria kumshtaki DC

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Ni miaka karibia mitano sasa viongozi wamekuwa wakijichukulia sheria mikononi na hakuna kiongozi wa kisiasa wa juu anayekemea Jambo linaloashiria wahusika wanatekeleza msimamo wa serikali.

Wahanga wa tukio la Arusha wamelazimishwa kupigwa na kisha kulipishwa fedha zaidi ya milioni tano ambazo taarifa zinadai wamelazimishwa kuuza baadhi ya Mali zao pamoja na ndugu kuwachangia kutokana na vitisho na shinikizo lililotolewa na uongozi wa wilaya dhidi yao.

Uongozi huo ulienda mbali zaidi nakushinikiza kuwafungulia kesi zisizo na dhamana ikiwemo uhujumu uchumi wakiambiwa wamehujumu Mali ya umma na wasipotii nakulipa watawekwa ndani bila dhamana kwa kipindi kisichojulikana. Baada ya vitisho hivyo ambavyo hata vyombo vya habari vimehoji nakujiridhisha kuwepo kwa uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu hakuna chombo kiliripoti ukubwa wa kadhia hii badala yake vyombo vyote vya habari vimesimama na DC na kumfanya DC aonekane kuwa yupo sahihi.

Rai inayotolewa na familia za wahanga nikupata uwakilishi wa kisheria waweze kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya kisheria ya kile ambacho wametendewa ikiwa Ni pamoja na kuangalia njia yakupata fidia kwa madhara waliyopata.

Ikumbukwe hata watumwa baada Uhuru kwenye baadhi ya Mataifa walikuja kufungua kesi na mahakama za Dunia wakatoa maamuzi lengo likiwa nikuheshimu utu na haki za binadamu.

Kwa upande wa pili, mkuu wa wilaya kutamka adharani kuwa mchakato wa kisheria dhidi ya watuhumiwa ni kupoteza muda inaleta tafsiri kwamba serikali haiamini Kama muhimili wa mahakama una heshima yake. Kitendo Cha mahakama wakati wote kudharaulika wakakaa kimya nacho kinatia ukakasi.

Niwaombe watu wa haki za binadamu waache kukaa ofisini na kutuletea taarifa za uvunjifu wa haki za binadamu waingie kwenye vyombo vya kisheria nakuwatetea wanaoumia, atutaki takwimu za uvunjifu wa haki tunataka kusikia wamefungua kesi ngapi kutetea wananchi wanaoumizwa na ngapi wameshinda, fidia kiasi gani nk
 
Diuuu
Uhujumu uchumi na wiz
Wez wote wawe wahujumu uchumi
 
Mahakama zilipokubali kuagizwa na wanasiasa wenye viburi vya madaraka kuweka watu ndani, na kuwanyima dhamana hata kama wanastahili, dharau dhidi ya mahakama nilijua lazima ziwepo. Leo hii wananchi hatuna imani na mahakama, na wakati huohuo waliozifanya mahakama zisiaminike, nao wanazidharau!
 
Ngoja nisubir mwongozo
Mwongozo gani nilisema hii ni serikali ya kishetani.mbadala ni katiba tu watu wanadhulumiwa na kutapeliwa fedha zao na zinaporudishwa wahusika hawapewi pesa zao Kisha eti walicheza mchezo haramu.Mnakumbuka Lidesi na juzi Arusha kisa Sheria ni Sheria Hani hizo dhalimu
 
Acha kutuona wapumbavu wewe mwehu,Jana nimewasikiliza wahusika wote ,wamekiri makosa yao na kutoa faini ya tsh 5000K,halafu unakuja na stori za kwenye kahawa huku..nyambafu kabsa😡😡😵😵😵
Unajua wamwkiri katika mazingira gani?Unataka kusema sasa MaDC wageuke mahakimu wanakoongoza?Waendeshe mashtaka na watu wakikiri waadhibiwe!
 
Unajua wamwkiri katika mazingira gani?Unataka kusema sasa MaDC wageuke mahakimu wanakoongoza?Waendeshe mashtaka na watu wakikiri waadhibiwe!
who are you by the way??
Kwahiyo baada ya jana kukiri wamepita kwako wakakuambia kuwa wanaenda kushtaki?? Hizo akili mnazitoa wapi kwa mfano?? Inamaana hapo ufipa mmekuwa Duni kiasi hiki??
 
Mwongozo gani nilisema hii ni serikali ya kishetani.mbadala ni katiba tu watu wanadhulumiwa na kutapeliwa fedha zao na zinaporudishwa wahusika hawapewi pesa zao Kisha eti walicheza mchezo haramu.Mnakumbuka Lidesi na juzi Arusha kisa Sheria ni Sheria Hani hizo dhalimu
Mambo ni moto
 
Tanzania ya leo!
5532890.jpg
 
who are you by the way??
Kwahiyo baada ya jana kukiri wamepita kwako wakakuambia kuwa wanaenda kushtaki?? Hizo akili mnazitoa wapi kwa mfano?? Inamaana hapo ufipa mmekuwa Duni kiasi hiki??
Mkuu muulize tu taarifa kazitoa wapi atupe majibu,akishindwa kujibu achana naye. Unamuuliza kwa kejeli yeye ni nani akikutafuta Akijitambulisha halafu akawa ni jitu la kutisha kuliko wewe utajificha wapi? Usisahau tupo kwenye fake id na yawezakuwa Humu hadi mzee baba yupo na saa zingine anamponda aliyemteua maana hakumuagiza atende aliyotenda.
 
Back
Top Bottom