Walinzi wa Museveni & Gaddafi watwangana vikali- Karume Asukumwa!!!

Mkuu Mkandara.
Naomba nikuweke sawa, Makubaliano yanakuwa kila kitu na walinzi pia inakubalika kutegemea pia na makubaliano, Gadaffi ndio alifika na msafara wake masaa mawili na nusu kabla.

Utaratibu mwingine ni wa kawaida na kama umesoma ile habari uzuri kwa ile fujo ya Uwanjani Nakivubo ni kwamba walinzi wa Uganda waliona kuwa kuna watu wengi ambao walitaka kufika mahala pa VIP especially Arabs walipowazuia ndipo fujo ilianza.

2. kwa suala la Msikitini wale walinzi kilichowapa kiburi ni ile kuwa huu Msikiti tumeujenga sisi ni wetu hakukuwa na jingine kwani pale walitaka waachiwe suala zima la ulinzi wao, ikumbukwe kuwa Mh. Karume alipokuwa akijaribu kuinama avue viatu alisukumwa na hao walinzi kwa kudhani kuwa anataka kufanya kitu mbaya.

Suala la matamshi ya kebehi kwa Biblia hakuna haja ya kumzushi hata ukiingia kwenye archive ya Monotor utaiona na hata wakuu wa dini wa Uganda wame condemn hiyo statement ya Gadaffi.

Ninachotaka kusema ni nini Gadaffi ni Arrogant sana, si muhukumu ila hilo liko wazi kwa vituko vyake tuu.

Kumbuka mengi ya mambo aliyokuwa akifanya alifanya wakati wa Kampeni zake za kuutaka Urais wa Africa.

Uswahiba wa Gadaffi na M-7 haukuanza jana Bwana Mkandara. Gadaffi alijua kuwa haungwi mkono hasa Kusini mwa jangwa la Sahara na alitaka sana kupata ushawishi toka kipande hii, na alimtumia M-7 kwani M-7 naye alitaka kumtumia Gadaffi kwa kampeni yake ya Urais wa Jumuiya ya Africa ya Mashariki (na bado dhamira anayo).

na ndio maana alianza kujenga misikiti na hata Dodoma na Mombasa iko mbioni kwenye mpango huo pia.

Kumbuka ziara yake ya Nchi za Kusini mwa Africa mika michache ilopita ambapo alitumia magari na mbwembwe nyingi ni katika kampeni hiyo.

Binafsi suala hili siliangalii kwenye angle ya kidini zaidi lakini naangalia dhamira yake na hali halisi ya sasa

3.
 
Karl Peters alitumia shanga za rangi mbali mbali na vitambaa aina ya madulufu; vyeupe bluu na kijani kurubuni babu zetu hadi wakaingia gauge na kugawanyika na kuruhusu Mjerumani kututawala.

Leo Viongozi wasomi wajionao wana vision na uwezo mkubwa kuliko akina Kimweri wanarubuniwa kwa mtindo ule ule wa Karl Peters isipokuwa safari hii wanapewa $100,000.00 ili uruhusu wizi wa $Trillion. Au zawadi nyingine yeyote ile kisha kumruhusu mtoaji zawadi kugani majigambo yake mbele za wake zao na wakwe zao.

Sisi Watu wa Dunia ya 3 tunapenda mno kila kilichokuwa labeled BURE, au Kwa Gharama ya mtu mwingine.

Hakuna Bure kwa sababu Bure haijawahi Ku Exist na wala haita.

Hata Remmy aliimba ukikopa kwa Mpemba na huna cha kulipa Utadondoka naye kama malipo.( Kukatwa Mjengo)

Ona viongozi wa SISIEMU na wenzao wa nchi nyingine za Afrika wanvyolazimika kudondoka na Mashirika ya Kigeni tena mbele za watu wote wanaowaheshimu ili kulipia the so called BURE!!!!

Uwezo wa kuleta Mageuzi ya kiuchumi hauanzi na fedha, unaanza na Vision. Ukivisualize developement crystal clear na kuiweka kwenye Draft fedha siku zote si tatizo.
Ukitanguliza fedha katika mipango yako ya maendeleo ni wazi kwamba fedha yako itatumika bila kuleta mageuzi yeyote kwa sababu dira ya maendeleo ni maono siyo fedha.
Ndiyo maana Dubai inasonga mbele katika viwanja vya uchumi na Biashara kuliko Saudia wenye utajiri mkubwa wa Mafuta mara 1000 ya Dubai.
Fedha bila Vision nifedheha kama hiyo ya Viongozi wa nchi 11 kwenda kudharirishwa kwa kupigwa vikumbo na malofa wa kilibya kisa Per DM ya Gadaffi.

Sisi kule kwetu Malinyi tuna msemo uwezao kutafsiriiwa kwa kiswahili chepesi kama.

UMASIKINI NI UCHI WA MBWA no body wants it.
 
Malinyi, Ngoelanga au Mtimbira?
Sema kwa Kimalinyi sijui kindamba au Kipogoro niusikie kaka!
nasikia kila Rais aliyekwenda pale alilamba mshiko!!

Kama ni kweli shame on Us!!!
 
Malinyi, Ngoelanga au Mtimbira?
Sema kwa Kimalinyi sijui kindamba au Kipogoro niusikie kaka!
nasikia kila Rais aliyekwenda pale alilamba mshiko!!

Kama ni kweli shame on Us!!!

Tatizo la kuzaliwa Malinyi na kukulia Manzese ndo hilo kuongea hakipandi.

Mimi nemezaliwa Malinyi lakini Baba alizaliwa Madilu huko Njombe, akiwa kijana mdogo babu alizamia Malinyi.


We subiri kama hujasikia kwamba Gaddafi alilipia kila kitu kwenye huo Mnuso.
Viongozi wetu ikifika saa ya mlo midomo mikubwa kuliko Chewa
 
Ukweli unabaki siku zote walinzi wa Gaddafi wanapenda kuleta fujo na dharau kwa wenzao wa nchi nyingine, ukiangalia kulikuwa na umuhumi wowote wa kumsukuma Karume au Museveni mwenyewe? Inamaana wakati wanajadiliana hawakuwa na picha za viongozi watakaoudhuria?

Ukisoma hiyo article hapo juu utaona kuwa walikuwa na beef tangu jamaa wameingia Uganda jumapili iliyopita.
 
Lakini kwa madudu yaliyotokea lilikuwa jambo la busara kwa Kikwete kutokwenda!!!
 
aliendika anastahiki kusamehewa kikwete kawakilishwa na karume kwa maana hio karume yupo pale kuiwakilisha tanzania na sio zanzibar.

hata yeye kikwete angelienda huenda kulikuwa na shughuli nyengine anataka kuzifanya au aliamua amuwakilishe.

lkn wengine waosha vinywa waache wastarehe

;;;;;;;;;;;;mtu wa pwani rais wetu hakwenda alikuwa na shughuli muhimu ya kupumzika MIKUMI....

........TANZANIA si nchi ya kiislamu...uganda si nchi ya kiislamu pia but they are known to do anything kama wanafaidika ..ndio maana wao wapo IOC pamoja na kuwa waislamu si wengi kuzidi wakristu huko...na sisi sio tu hatupo bali haitatokea tukajiunga..........nafikiri gadafi angweza kufikisha ujumbe kwa lugha nyepesi,,,mara nyingine mtu anaweza kukupa kitu bure lakini kwa lugha ya aina ile akaondoka akakuachia vita au manunguniko ya kidini..kutoka kwenye dini iliyokashifiwa....ndio maana nasema watu kama hao hatutafurahi kuwapokea hapa kwetu!!!....

tunajua alijenga msikiti wa butiama akishirikiana na mwalimu nyerere ..hakuja kuufungua na anajenga msikiti dodoma ...sio lazima ukiisha sharti lake liwe aje kuufungua yeye...kama atautumia kama jukwaa la kukebehi sehemu kubwa ya jamii ya tanzania....kama ulivyo uislamu ....hata tripoli hawawezi kukubali hilo....
 
Bastola zilikuwa "nje nje" na baadhi ya walinzi wamejeruhiwa vikali kwa "compound fractures" (madaktari tusaidieni, "compound fracture" ndio kitu gani? Mie naelewa kidogo kuwa "fracture" ni kuvunjika mfupa kama wa mkono au mguu, sasa walipoandika hiyo "compound" sijaelewa, sijui ni kuvunjika labda pamoja na jeraha jingine au ni kitu gani?)[/SIZE]


Ndugu yangu..tunaposema "compound Fractures" ina maana kwamba mbali na fracture kunakuwepo pia na kidonda...kama kwenye ngozi ambapo ni rahisi kama bakteria nk kupita hapo. Ili ni somo refu lakini kwa ufupi ndo hivyo...
 
Inasemekana kuwa ameondoka Uganda bila kuaga kwani alikuwa akisubiriwa mahali kwa ajili ya kwenda kuweka jiwe la msingi lakini mwenyeji wake akasikia kuwa jamaa yuko Airport anatambaa zake!!

Huyu mtu mwehu!!
 
Inasemekana kuwa ameondoka Uganda bila kuaga kwani alikuwa akisubiriwa mahali kwa ajili ya kwenda kuweka jiwe la msingi lakini mwenyeji wake akasikia kuwa jamaa yuko Airport anatambaa zake!!

Huyu mtu mwehu!!

Haha nimejikuta nacheka mwenyewe, ebanae rockstar wetu Gaddafi naona kiburi kimemzidi sasa duh!!
 
Nilitaka kuhoji hiloi gathering lakini nikasema wacha mie ni Myahudi si Mkristo si nisije itwa mdini bure lakini inalate maswali mengi sana.Viongozi 11 for what ? Yaani gaddafi amekuwa ka Bush kadogo Africa ?
NI vurumai za wazungu na waarabu kuendelea kuigawa Afrika pamoja na watumwa wake!Nafikiri hawakufurahishwa na mapokezi ya bwana mkubwa mwingine(Bush/USA) ambaye/ambao ni mahasimu kihistoria!Anyways walishangazwa sana kuona walinzi wa Uganda wanawabana na kutokuwanyenyekea na kuwauzia uhuru mithili ya ziara ya Bush Afirka..Nafikiri walijisikia kutaka kuwatwanga masumbwi weusi hao ambao sasa wanaelekea kutaka kumtumikia mzungu!sasa waganda wakahisi hilo na ndio maana wakablame racism na superiority!wazungu na waarabu wote mabaguzi tu!Hii ni the new era of scrambling and new pertition of our beloved continent of AFRIKA!
 
Ndugu yangu..tunaposema "compound Fractures" ina maana kwamba mbali na fracture kunakuwepo pia na kidonda...kama kwenye ngozi ambapo ni rahisi kama bakteria nk kupita hapo. Ili ni somo refu lakini kwa ufupi ndo hivyo...

Aisee, Dr. Kishaju, wacha bwana! Ni medical school gani wanaotoa maelezo hayo ya 'ompound fracture?' Si lazima uelezee jambo kwa hisia tu bila ya kuwa na ujuzi nalo!
 
Pope,

Mkuu utanisamehe kwani maelezo yako bado kabisa hayajagonga mfupa!... bado haiingii akilini hata kidogo mnachojaribu kusema hapa.
Sioni tofauti ya viongozi toka Ulaya, Asia na Marekani wakifanya tofauti na Gadaffi..
Bush kaahidi ujenzi wa vitu kibao na vyandarua juu lakini haonekani kwa dini yake isipokuwa rais wa Marekani. Makanisa yanajengwa hakuna anayeulizia kanisa kubwa na Uganda, Kenya wala Tanzania lakini inapofikia swala la misikiti inakuwa issue kwenu na hata hesabu zake mnazijua zaidi kuliko hata waislaam wenyewe. (sikujua kama Gadaffi anajenga msikiti Dodoma).
Tazama picha zote mkuu wangu zinaonyesha mapambano ya walinzi ktk gate la kuingilia ndani hata kama hawa walinzi hawakutakiwa kuwepo ktk jukwaa basi watu wa kulaumiwa ni serikali ya Uganda kwa kutokuwa na mpango mzuri wa kina nani wanaruhusiwa kuwepo jukwaa la VIP. mahala popote uendapo shughuli kubwa kama hii watu hupewa vitambulisho vya vibanio ambavyo vinaonyesha wazi ruksa ya kuingia ama kwa rangi zake ruksa ya kwenda backstage, front ama VIP.
Nachojaribu kusema hapa waliopigana ni walinzi wake ambao kisheria na kutokana na kazi zao walikuwa na kila haki ya kuhakikisha wapo karibu na rais wao kumlinda kama walivyoteuliwa na kukubaliwa kuingia nchini kwa visa kama walinzi.
Uganda walikuwa na kila haki ya kukataa lundo la walinzi hao toka walipopokea maombi ya visa, pili haiwezekani ugonvi wa bodyguards lawama apewe Gadaffi sioni uhusiano inaonyesha kama vile mnataka kusema waliyafanya haya kwa amri ya Gadaffi...

Kisha mada hii yote imejaa Udini zaidi ya kile kilichotokea. Nimeomba hiyo hotuba uiweke hapa hakuna haja yangu kutafuta sehemu hali wewe unafahamu inapatikana wapi.. imwage hapa watu tusome kisha tutaamua uzito ya hiyo hotuba kwani kama nilivyosema namfahamu Gadaffi ktk maswala haya ya dini ni mjanja sana na nadhani ndiye pekee ktk viongozi waarabu wanaoruhusu Ukristu na madhehebu mengine ku Practice freely ndani ya nchi yake yenye waislaam zaidi ya asilimia 97. Huwezi kupata kiongozi MWARABU muislaam mwenye msimamo kama wa huyu jamaa.

What's wrong kwa Gadaffi kujaribu kuwa rais wa Afrika?.. kiburi chake ama uwezo wake kuongoza.. Gadaffi ni kiongozi bora Afrika na amedhihirisha nchini mwake. Hakuna M Libya anayekimbia nchi yake kwa Umaskini wala kulilia misaada na Libya ni cnhi pekee ktk Afrika yenye kulipa mishahara mikubwa wananchi wake kuliko hata nchi za Ulaya. Sasa ikiwa hawa ni matajiri na wanataka kutusaidia kipi kibaya haswa ikiwa tupo radhi kupokea misaada kama hiyo hiyo toka nchi nyinginezo?..
Je, kwa sababu wao ni taifa la Kiafrika. waarabu, waislaam ama ni kipi haswa?

Yote anayoyafanya ni kwa interest ya Afrika kuliko Jumuiya ya waarabu ambao hawampendi kwa commitment yake kwa Afrika.
 
Jamani tunasahau kuwa wakati Kikwete yuko MoFA Gaddafi aliwapa yale mabenz meusi, so hawa wawili wanajuana at least back then. Anyways I think ilikuwa good move kwa muungwana kutokuudhuria again kudos!!!
MUUNGWANA AMEKWEPA MASWALI MAZITO KUTOKA KWA GHADAFI!UNAJUA HUYU JAMAA HUWA HAKAWIZI!SASA ANGEULIZWA INAKUWA VIPI UMYENYEKEE KAFIRI KIASI HICHO?ANYWAYS HII NI COUNTERBALANCE KATI YA WAARABU NA WAZUNGU!HUYU ANFUNGUA MSIKITI..YULE ANAFUNGUA KANISA,KWANINI WASIJE KUFUNGUA VITU KAMA HOSPITALS ETC? HAYA MAMBO YA KUJA KUTUBAGUA HUKU AFRIKA KWA MISINGI YA DINI WALIZOTULETEA!SCRAMBLING AND MORE SCRAMBLING!
 
.....kuna utoto wa kijinga sana umeiingia ktk hii forum!! kishaju yupo sahihi kabisa, kwa maelezo mafupi kwa layman asiyejua cpd fx......wewe KALAMU na mwenzako MTU MZIMA mna ishu zenu na naomba mwache utoto!! kama nyie mnajua sana basi wekeni maelezo yenu...........watu wengine bwana, criticism zenu zimekaa kimajungu na zinajitosheleza kujua ninyi ni watu wa namna gani!! very -ve personalities.

Hapana, mimi nasema 'hayupo sahihi kabisa.' Kuwepo na kidonda kwenye ngozi hakuifanyi 'definition' ya 'compound fracture' kuwa sahihi, hasa kwa mtu asiyekuwa na ufahamu na jambo hilo.
Ni mhimu pawepo na kuvunjika mfupa, na matokeo ya mfupa huo kujitokeza kwenye ngozi ndio kunaifanya hiyo 'fracture' kuwa 'compound.'

More negative personality is vivid in your statement.
 
kitu kile kile, kishaju alizungumzia kuvunjika na kuwepo kwa kidonda!! utawezaje kuzungumzia fx bila kuwepo kwa fx???.....ndio maana nasema criticism yako ya kijinga!!! na kwa taarifa yako sio lazima mfupa utokeza, ila ile access tu na chances kubwa za infection(s) kwenye fractured area inawezatosha kusema ni cpd fx............unaweza kuendelea kubisha, kwasababu upo negative sana!! rudia kusoma nini kishaju aliandika. watu wengine bwana, kuna kilaza mwenzako(mtu mzima) huko juu alibisha kwamba cpd fracture kwa jina lingine sio open fracture...mnatia aibu!!!.

We umesomea unesi nini?
 
Back
Top Bottom