Aventus
JF-Expert Member
- Mar 8, 2013
- 1,914
- 1,977
Nasema angalia ya kwako tu ...Hawa ndiyo watanzania bhana
UKIWA KIJANA.
1. Ukiwa single watakuuliza, kwanini huna Girlfriend au Boyfriend?
2. Ukiwa na mchumba, watahoji mmekaa sana mtaoana lin?
3. Ukioa utasikia, mbona hamzai nyie?sisi twataka wajomba,shangazi na wajukuu
4. Mkizaa watakuja na hii, mtoto kakua mtafutieni dada au kaka yake!
5. Ukimtafuta, utasikia mbona mnazaa haraka haraka hamuogopi maisha?maisha magumu siku hizi .....
UKIWA NA HELA
1. Ukinenepa, we unanenepa tu hivi huogopi magonjwa (presha na kisukari)
2. Ukikonda, acha ubahili, pesa zote hizo unakuwa mbahili? wengine watasema mara alitembeaga na dada/ kaka fulani mwenye ngoma ndio imekolea sasa. Hamalizi mwaka huyu, lazima tumzike tu.
3. Ukinunua gari, unanunuaje gari wakati hujajenga? huna kiwanja? Vijana wa siku hizi bure kabisa.
4. Ukijenga huna gari, yaani na usumbufu wote huu wa madaladala huna gari? tunakushangaa sana. Nunua hata pikipiki!!
UKIFANYA MAZOEZI
1. Kama ni mwembamba, wee kimbau mbau unapunguza nini kwenye ako kamwili kako, (wanajua mazoezi ni kupunguza mwili tu!)
2. Ukiwa Mnene, yaani Mungu hakupi vyote. Ona sasa amekula mikuku yake sasa ndio anateseka nayo kupungua.
JAMANI HIVI LIPI JEMA??
Credit:Nyemo
UKIWA KIJANA.
1. Ukiwa single watakuuliza, kwanini huna Girlfriend au Boyfriend?
2. Ukiwa na mchumba, watahoji mmekaa sana mtaoana lin?
3. Ukioa utasikia, mbona hamzai nyie?sisi twataka wajomba,shangazi na wajukuu
4. Mkizaa watakuja na hii, mtoto kakua mtafutieni dada au kaka yake!
5. Ukimtafuta, utasikia mbona mnazaa haraka haraka hamuogopi maisha?maisha magumu siku hizi .....
UKIWA NA HELA
1. Ukinenepa, we unanenepa tu hivi huogopi magonjwa (presha na kisukari)
2. Ukikonda, acha ubahili, pesa zote hizo unakuwa mbahili? wengine watasema mara alitembeaga na dada/ kaka fulani mwenye ngoma ndio imekolea sasa. Hamalizi mwaka huyu, lazima tumzike tu.
3. Ukinunua gari, unanunuaje gari wakati hujajenga? huna kiwanja? Vijana wa siku hizi bure kabisa.
4. Ukijenga huna gari, yaani na usumbufu wote huu wa madaladala huna gari? tunakushangaa sana. Nunua hata pikipiki!!
UKIFANYA MAZOEZI
1. Kama ni mwembamba, wee kimbau mbau unapunguza nini kwenye ako kamwili kako, (wanajua mazoezi ni kupunguza mwili tu!)
2. Ukiwa Mnene, yaani Mungu hakupi vyote. Ona sasa amekula mikuku yake sasa ndio anateseka nayo kupungua.
JAMANI HIVI LIPI JEMA??
Credit:Nyemo