Walimu wetu wa shule wanatufundisha kufeli kwenye maisha, hii ndio sababu (Part 1)

unafikiri kuchapwa kwa wanafunzi kuna wasaidia kwenye maisha yao ya baadae?

  • ndiyo

  • hapana


Results are only viewable after voting.
Jun 8, 2016
83
647
“mtoto usimpe confidence sana, inabidi asijiamini tutamfundisha awe vizuri”

“hivi wewe unaona ni sawa mwanafunzi kujiamini?”

Nikajaribu kuingilia kusema neno angalau moja, principle akanikatisha tena kwa kusema, “mimi nimefundisha wanafunzi wengi sana, usione kwamba mwanao ni wa tofauti, don’t think he is special hata kidogo ni kama wanafunzi wote wengine hawa”

Nikaweza kupitisha maneno machache kwa kusema “huyu mtoto mi namjua vizuri, hatokusikiliza ukimtishia, hatokusikiliza ukimpiga, hatojifunza chochote, amekuzwa tofau…..”

“ishia hapohapo sasa unanikasirisha, kama unaona sisi ku mdiscipline mtoto tumekosea wewe nenda na ada si umeshalipa, hiyo ni juu yako’ umechagua mwenyewe kulipa.” Akajibu principle

Nikasema “lakini kitu cha kwanza nakuja kuuliza kabla sijalipa hiyo ada, ni kwamba mnachapa wanafunzi?, mkaniambia hamchapi wanafunzi kabisa kuna njia za kuwarekebisha kama wamekosea, hadi ukashangaa kwamba shule zingine bado wanachapa wanafunzi, mtoto nimemleta aanze darasa la kwanza, sijalipa ada ili apigwe”

Principle akajibu “hatupigi watoto hatuanzi tu kuwachapa hovyo, ila mwanafunzi asiposikia inabidi kumrekebisha inabidi kumdiscipline”

Nikaona tupo kwenye realities mbili za tofauti sana mi na mwalimu huyu, nikatoka na mwanfunzi niliyempeleka nimefika nyumbani nikaanza kuandika post hiii…. End of story……

MADA INAANZIA HAPA SASA
SHULE ZETU NDIO SABABU NAMBA MOJA watu hawatokuja kufanikiwa kwenye maisha yao ya baadae, unaweza uka ni quote siku yoyote.
Wanafundisha watoto kutokujiamini, watoto wanaambiwa kwamba siyo special nyie ni vi wanafunzi ambao inabidi muitike mnapoambiwa mkariri kila mnachoambiwa, alafu wakija waki feli, mtoto hana akili.

ETI MTOTO HATAKIWI AJIAMINI??????
Tunasahau kwamba miaka hiyo ya 5-10 ndipo binadamu anapojengeka kiakili, personality yake yote inatokea hapa, hamna kitu cha muhimu kama kujiamini kwenye maisha, na kama kuna mzazi ambaye ana mtoto na anataka aje afanikiwe baadae mfundishe ajiamini.

Kila siku watu wanapata ideas kama mia hivi za kuweza kujikwamua kwenye maisha, kila kukicha, ukimuuliza mtu yoyote akupe idea tano ambazo anafikiri zinaweza kubadili maisha yake, atakutajia kumi, ila huyuhuyu mtu ndiye atakuja kufa bila kufanyia kazi idea hata moja kati ya hizo kumi, atabaki tu ameajiriwa mwisho wa siku ata stahafu na kuona maisha machungu, yote kwa ajili haku wekezwa kichwani mwake kuwa inabidi ajiamini. Aamini mawazo yake, ajaribu kila idea aliyonayo aanze nayo tu hata isipofanikiwa hata akifeli atajaribu tena hadi aelewe , hadi aipate. Hapa tunapata point yetu ya pili

KUCHAPWA KAMA MWANAFUNZI AKIKOSEA
Binadamu ni waajabu sana ujue, yaani mwanafunzi hujui nyumbani ana deal na nini, kichwani mwake anawaza nini, au uelewa wake ukoje, ila akikosea achapwe? Achapwe hadi aelewe siyo?

Tunafundisha wanafunzi kuwa ni vibaya kukosea, kwamba ukikosea utachapwa. My god sijui kwanini watu hawafikirii, hii inakuja kumjengea mtu kwamba inabidi asikosee, inabidi ajaribu au awekeze kwenye idea au biashara kama ana uhakika itafanikiwa tu. Wakati hakuna binadamu aliye fanikiwa bila kukosea.

Mama aliendika vitabu vya harry potter alikataliwa na publishers 12, hadi msimamizi wake akamwambia kuwa hatofanikiwa kama muandishi lakini akajiamini na hakujali kukataliwa , sahivi ana billion dollar kadhaa kwa jina lake. Bill gates tajiri wa dunia kabla ya Microsoft alifeli kwenye kampuni yake inaitwa traf-o-data kabla ya kuja kuanzisha Microsoft na kuwa tajiri number moja duniani. Kila mtu aliyefanikiwa ana historia ya kufeli.

traf-o-data-card.jpg
JKR-703051.jpg


Ukimfundisha mwanafunzi kuwa ukifeli, basi unapata adhabu, unachapwa, wenye nguvu wata kurudisha utulie hii inajengeka, we are made by our experiences, so mwanafunzi siku akikua alafu hataki kujaribu biashara, au idea yake yoyote aliyonayo ujue hii imetokea huku, njia ya elimu yetu hii ya kijinga (it is stupid).

YOU ARE NOT SPECIAL
I think watu wana hasira na maisha yao na wanakuja kuwatolea wanafunzi wachanga hizo hasira, I get it life sucks, mshahara mdogo probably, kuna mambo kama mia una deal nayo kwenye maisha yako na wewe, lakini these are kids taifa letu la kesho or whatever wanasemaga, but yeah these are the ones who are either going to build our societies ama wataharibu kila kitu. Especially wanafunzi wadogo, chekechea, darasa la kwanza hadi la tano hivi, these kids are fragile. So kama kuna mwalimu anasoma hii nakuomba ukiingia darasani acha hasira zako mlangoni.

Kila mtu is special in their own way,everyone. Na hilo ndio tatizo number moja la binadamu in general, mwanamuziki wa bongo sahivi akiona diamond kafanikiwa atataka na yeye aimbe nyimbo kama za diamond ili atoke, hajui what is special kuhusu diamond, hajui kwamba inabidi ajieangalie yeye ajue ni kitu gani special kuhusu yeye, hapana anataka afanye kama alivyo fundishwa darasani, kwamba you are not special. So ofcourse kwanini asi mgeze mwenzake alichofanya.

Kwanini sijui tunataka kuvunja watoto wadogo kwa kuwaambia wawe sawasawa wote, kila mtu afanye kitu kimoja ili kazi ya mwalimu iwe rahisi, hata kama kuna mmoja uelewa wake ni tofauti na amefundishwa na walimu tofauti alipotoka, hapana! Kila mtu awe sawa aweze kuandika sentesi kwa muda muafaka akishindwa anachapwa.

SO ANYWAY
Personally nimechapwa sanaa kipindi changu cha primary darasa la nne na kuendelea, secondary ndio usiseme. kabla ya hapo nilikuepo kwenye shule flani hivi haikusajiliwa vizuri (cough cough), ila iliendeshwa na sijui ilikua wa zambia au wa zimbabwe, walimu wangu wote siwakumbuku ila mwalimu huyu mmoja aliyenifundisha chekechea hadi darasa la pili, la tatu hivi ntamkumbuka hadi kufa, anaitwa “Mr Brown”, huyu mwalimu hadi nyumbani kwake alitualika na kutupa chakula, tulikua na connection naye nzuri sana na alitufundisha kujiamini, tulikua wachache darasani na kila mtu alipata special care kutoka kwa huyu mwalimu.

Leo wale wachache tuliofundishwa nae, nawaona walivyofika mbali. mmoja ana kampuni successful, mwingine ni mwana sayansi flani hivi ana gundua some complicated process ya kubadili uchafu wa kwenye mazingira kuwa mbolea, kwa njia rahisi, na mimi well nipo hapa najaribu kuelimisha baadhi ya watu. Sitosema huyu mwalimu ndiye alikuwa na direct cause ya mafanikio au la, ila it played a part.

Nilikutana na video hii ikanisikitisha sana, this is not right.



sasa acha hiyo, tuangalie na mwalimu wa chini hapa anaefundisha wanafunzi nchi za wenzetu, afu tujiulize tena kwanini tunabaki nyuma,



People do not think for themselves (hatutumii akili zetu tulizonazo)
labda inabidi uwe na hela za kumwaga ili mwanao apate elimu bila kuonewa na kunyanyaswa na kukuzwa vipaji vyake na kufundishwa ili kuelewa kutokana na uwezo wake, aende ma IST huko labda, bila hivyo ni kuchapwa tu kwenda mbele.

sababu kubwa huyu principle aliniambia ni kwamba “serikali inaruhusu ku discipline mwanafunzi kwahiyo hatujakosea kitu”

Kuna studies nyingi za psychology, nyingi zinazo link kuchapwa kwa wanafunzi kuwa zinawafanya wanafunzi kujenga chuki juu ya walimu na wazazi, kutojiamini, kutaka kupiga wengine, na effect zingine kibao, ila basi tu kwa kuwa haijakatazwa na hamna sheria inayowabana kuacha basi watafanya tu bila kufikiria itamu effect vipi mwanafunzi.

“it has a very bad impact on the child at the time of beating as well as in future. Sense of hatred towards parents and teacher, low self esteem, abusive relationships, getting joy from beating others and so on are some common consequences.” nime quote.

CONCLUSION
Naomba kila mtu ajiangalie kwanza, aone mapungufu yake, atafakari hao mapungufu yametokea wapi, kama una uoga wakutoongea ukipata wazo, au una sita kujaribu idea flani, au hauna confidence ya kutosha kwenye jambo lolote, au mapungufu yoyote kwenye characteristics zako zilivyo, naomba ukumbukie jinsi gani ulivyokuzwa, ulichapwa? ulikatazwa vitu gani? ulifundishwa vipi?

Mimi najijua mapungufu yangu na najua yalipotokea, bila kuyatafakari nisinge hata anza baishara zangu na venture zangu zingine, hii blog nisingeianza kwa kuhofia kama itafeli au itafikia wapi.

Kama kuna mzazi yoyote, i hope hii itakupa mwangaza kidogo. Watoto sio tu vijitu ambavyo havisikii na inabidi kuvirekebisha, hawa ni kama dumu tuseme na ukiwa jaza maji wanayohitaji watayanywa vizuri, ila ukijaza mafuta kwa kuwa kazi yako itakua rahisi, baadae usije kulalamika pale wakikuchukia, maisha yao yasipokuwa mazuri na matatizo mengine kibao.

Ningependa kujua mna mawazo gani kuhusu hili jambo.
 
Sorry, wewe si ndo yule alokataa mshahara wa zaidi ya milioni 2??
sasa mbona unahangainga kutafuta views wa blog ili uliapwe na google? Au google inalipa saana kuliko zile m2+
 
Sorry, wewe si ndo yule alokataa mshahara wa zaidi ya milioni 2??
sasa mbona unahangainga kutafuta views wa blog ili uliapwe na google? Au google inalipa saana kuliko zile m2+

naomba nipigie screenshot tangazo la goole kwenye blog unioneshe
 
Back
Top Bottom