KERO Responded Walimu wenye umri mkubwa wanapoomba Ajira Portal alama zao za ufaulu ziwe tofauti na waliohitimu hivi karibuni

KERO Responded Walimu wenye umri mkubwa wanapoomba Ajira Portal alama zao za ufaulu ziwe tofauti na waliohitimu hivi karibuni

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi kwa taaluma yangu ni mwalimu. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikihangaika kutafuta ajira serikalini kupitia Ajira Portal. Nimekuwa nikifanya usaili mara kwa mara, napita hatua ya maandishi hadi kufika hatua ya mahojiano ya ana kwa ana (oral), lakini mwisho wa siku sipati nafasi.

Kinachoniumiza zaidi ni kwamba umri wangu umeenda—nina miaka 35 na zaidi—lakini hali yangu inalinganishwa moja kwa moja na wahitimu waliomaliza vyuo juzi tu. Ukweli ni kwamba, nimekaa mtaani kwa zaidi ya miaka 10 nikijaribu kila njia, lakini bado ninapewa nafasi sawa ya ushindani bila kuzingatia uzoefu na muda niliopambana.

Inakatisha tamaa sana. Unajituma hadi kufika hatua ya mwisho ya usaili, lakini hakuna kinachobadilika.

Vilevile, ninaona changamoto kwa waombaji wenye ulemavu. Wapo wanaofika hadi hatua ya mwisho ya mahojiano na wana vigezo vyote, lakini bado hawapati nafasi. Hii inaumiza zaidi, kwa sababu wanapaswa kupewa kipaumbele au angalau kuangaliwa kwa jicho la ziada kutokana na hali zao.

Kwa kweli hali hii inahitaji kuangaliwa upya.

Mapendekezo yangu:
Kuwe na utaratibu wa kuzingatia umri na muda tangu mhitimu amalize chuo katika mchakato wa ajira.
Mfano, kwa waombaji wenye miaka 35 na zaidi na waliomaliza muda mrefu, vigezo vya ufaulu viwe na mlinganisho tofauti na wahitimu wapya.
  • Endapo msahiliwa mwenye umri mkubwa atafikisha angalau alama 50 au zaidi katika usaili, apewe kipaumbele, kwa kuzingatia jitihada na muda aliopambana.
  • Kwa waombaji wenye mahitaji maalum (ulemavu), endapo wamekidhi vigezo na kupata alama za kutosha (mfano 50 na kuendelea), wasaidiwe kupata nafasi za ajira kama sehemu ya kuwajali na kuwapa usawa wa fursa.
Naamini kabisa kuna watu wengi kama mimi wanaopitia hali hii. Tunaomba huruma na haki vitumike katika mifumo ya ajira.

Pia soma ~ Sekretarieti ya Ajira: Kuna muda umri unazingatiwa kwenye usaili wa ajira lakini kwanza unatakiwa kufaulu
 
kwa umri huo ulipaswa uwaongoze ndugu usitafute kichaka mchujo ni muhimu
 
Usahili wa PSRS unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni sio utashi wa mtu.
 
Mimi kwa taaluma yangu ni mwalimu. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikihangaika kutafuta ajira serikalini kupitia Ajira Portal. Nimekuwa nikifanya usaili mara kwa mara, napita hatua ya maandishi hadi kufika hatua ya mahojiano ya ana kwa ana (oral), lakini mwisho wa siku sipati nafasi.

Kinachoniumiza zaidi ni kwamba umri wangu umeenda—nina miaka 35 na zaidi—lakini hali yangu inalinganishwa moja kwa moja na wahitimu waliomaliza vyuo juzi tu. Ukweli ni kwamba, nimekaa mtaani kwa zaidi ya miaka 10 nikijaribu kila njia, lakini bado ninapewa nafasi sawa ya ushindani bila kuzingatia uzoefu na muda niliopambana.

Inakatisha tamaa sana. Unajituma hadi kufika hatua ya mwisho ya usaili, lakini hakuna kinachobadilika.

Vilevile, ninaona changamoto kwa waombaji wenye ulemavu. Wapo wanaofika hadi hatua ya mwisho ya mahojiano na wana vigezo vyote, lakini bado hawapati nafasi. Hii inaumiza zaidi, kwa sababu wanapaswa kupewa kipaumbele au angalau kuangaliwa kwa jicho la ziada kutokana na hali zao.

Kwa kweli hali hii inahitaji kuangaliwa upya.

Mapendekezo yangu:
  • Kuwe na utaratibu wa kuzingatia umri na muda tangu mhitimu amalize chuo katika mchakato wa ajira.
    Mfano, kwa waombaji wenye miaka 35 na zaidi na waliomaliza muda mrefu, vigezo vya ufaulu viwe na mlinganisho tofauti na wahitimu wapya.
  • Endapo msahiliwa mwenye umri mkubwa atafikisha angalau alama 50 au zaidi katika usaili, apewe kipaumbele, kwa kuzingatia jitihada na muda aliopambana.
  • Kwa waombaji wenye mahitaji maalum (ulemavu), endapo wamekidhi vigezo na kupata alama za kutosha (mfano 50 na kuendelea), wasaidiwe kupata nafasi za ajira kama sehemu ya kuwajali na kuwapa usawa wa fursa.
Naamini kabisa kuna watu wengi kama mimi wanaopitia hali hii. Tunaomba huruma na haki vitumike katika mifumo ya ajira.
Mkuu hongera kwa kufika oral, ila pambana tu ,ipo siku utatoboa.

Juz juzi tulikua tunajaza mikataba ya kazi, mimi wa 2019 ila nimeajiriwa 2026 pembeni yangu alikua dogo kahitimu 2025 kaajiriwa 2026 tareh 1 na mimi na masomo sawa namimi, hapo ndipo nikaamini maisha hayapo fair na wakati wa mungu ni wakati sahihi, stay strong keep moving boss.
 
Mimi kwa taaluma yangu ni mwalimu. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikihangaika kutafuta ajira serikalini kupitia Ajira Portal. Nimekuwa nikifanya usaili mara kwa mara, napita hatua ya maandishi hadi kufika hatua ya mahojiano ya ana kwa ana (oral), lakini mwisho wa siku sipati nafasi.

Kinachoniumiza zaidi ni kwamba umri wangu umeenda—nina miaka 35 na zaidi—lakini hali yangu inalinganishwa moja kwa moja na wahitimu waliomaliza vyuo juzi tu. Ukweli ni kwamba, nimekaa mtaani kwa zaidi ya miaka 10 nikijaribu kila njia, lakini bado ninapewa nafasi sawa ya ushindani bila kuzingatia uzoefu na muda niliopambana.

Inakatisha tamaa sana. Unajituma hadi kufika hatua ya mwisho ya usaili, lakini hakuna kinachobadilika.

Vilevile, ninaona changamoto kwa waombaji wenye ulemavu. Wapo wanaofika hadi hatua ya mwisho ya mahojiano na wana vigezo vyote, lakini bado hawapati nafasi. Hii inaumiza zaidi, kwa sababu wanapaswa kupewa kipaumbele au angalau kuangaliwa kwa jicho la ziada kutokana na hali zao.

Kwa kweli hali hii inahitaji kuangaliwa upya.

Mapendekezo yangu:
  • Kuwe na utaratibu wa kuzingatia umri na muda tangu mhitimu amalize chuo katika mchakato wa ajira.
    Mfano, kwa waombaji wenye miaka 35 na zaidi na waliomaliza muda mrefu, vigezo vya ufaulu viwe na mlinganisho tofauti na wahitimu wapya.
  • Endapo msahiliwa mwenye umri mkubwa atafikisha angalau alama 50 au zaidi katika usaili, apewe kipaumbele, kwa kuzingatia jitihada na muda aliopambana.
  • Kwa waombaji wenye mahitaji maalum (ulemavu), endapo wamekidhi vigezo na kupata alama za kutosha (mfano 50 na kuendelea), wasaidiwe kupata nafasi za ajira kama sehemu ya kuwajali na kuwapa usawa wa fursa.
Naamini kabisa kuna watu wengi kama mimi wanaopitia hali hii. Tunaomba huruma na haki vitumike katika mifumo ya ajira.
laiti kama ungekuwa unafahamu kinachoendelea wala usingeandika
 
Upuuzi huu, unashindwa kupambana mwnyw unakimbilia mambo ya umri.

Kama umri unaenda bc tupa taulo waachie Gen Z


Kwahy nawe unawataka na hao madogo wasote mtaani miaka 10 kama ww 😂 acheni roho mbaya nyie vizee
Hivi unafahamu kama Psrs huwa wana consider umri wanapopangia watu vituo vya kazi? ?
 
Lengo la interview ni kubalance ajira kwa umri au kupata watu mahili.
 
Back
Top Bottom