Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,138
Walimu wataka Waziri awajibike wizi wa malipo kwa walimu hewa
Na Gedius Rwiza
CHAMA cha Walimu Tanzania CWT, kimemtaka Waziri wa Nchi katika ofisi ya Rais (Menejimenti na Utumishi wa Umma), Hawa Ghasia, kuwajibika kwa hasara ya Sh477 milioni ambaye serikali imeingia kwa kuwalipa walimu hewa.
Naibu Katibu Mkuu, Ezekiah Oluoch aliliambia gazeti hili kuwa tamko la waziri huyo kwamba serikali imepata hasara hiyo, ni ishara ya uzembe katika ofisi yake.
Alisema CWT imeshindwa kuielewa kauli hiyo hasa ikizingatiwa kuwa Menejimenti ya Utumishi wa Umma, ndio inayoshughulikia masuala yote yanayohusu watumishi wa serikali wakiwemo walimu.
Kauli hii haiingii akilini hata kwa mtu asiyefahamu taratibu za utumishi. Ofisi Waziri Ghasia ndio inayoshughulika na kumbukumbu za wafanyakazi wote wakiwemo walimu, iweje fedha zilipwe kwa wafanyakazi hewa halafu waziri aone fahari kulitangaza hilo, alihoji Oluoch.
Alisema kwa kawaida, kila halmashauri nchini inakuwa na kumbukumbu za walimu wote wakiwemo wale waliacha kazi.
Kumbukumbu hizo ni pamoja na za walimu kuajiriwa au kuacha kazi na zinapelekwa katika wizara hiyo na Ghasia kwa wadhifa wake alipaswa kulijua hilo mapema kabla ya kuiingizia nchi hasara hiyo ya mamilioni, alisema kiongozi huyo wa CWT.
Oluoch alisema serikali inapaswa kufanya uchunguzi ili kubaini watumishi waliochota fedha hizo na kuwachukulia hatua.
Waziri Ghasia anapaswa kutoa maelezo ya jinsi fedha hizo zilivyolipwa kwa walimu hao, hili hawezi kukwepa kwa kuwa ndiye anayewajibika,alisema Oluoch.
Kauli hiyo inafuatia tangazo la hivi karibu la waziri Ghasia la kuwafukuza kazi walimu 463 waliokosa fisa na ambao wameisababishia serikali hasara ya Sh 477 milioni
Na Gedius Rwiza
CHAMA cha Walimu Tanzania CWT, kimemtaka Waziri wa Nchi katika ofisi ya Rais (Menejimenti na Utumishi wa Umma), Hawa Ghasia, kuwajibika kwa hasara ya Sh477 milioni ambaye serikali imeingia kwa kuwalipa walimu hewa.
Naibu Katibu Mkuu, Ezekiah Oluoch aliliambia gazeti hili kuwa tamko la waziri huyo kwamba serikali imepata hasara hiyo, ni ishara ya uzembe katika ofisi yake.
Alisema CWT imeshindwa kuielewa kauli hiyo hasa ikizingatiwa kuwa Menejimenti ya Utumishi wa Umma, ndio inayoshughulikia masuala yote yanayohusu watumishi wa serikali wakiwemo walimu.
Kauli hii haiingii akilini hata kwa mtu asiyefahamu taratibu za utumishi. Ofisi Waziri Ghasia ndio inayoshughulika na kumbukumbu za wafanyakazi wote wakiwemo walimu, iweje fedha zilipwe kwa wafanyakazi hewa halafu waziri aone fahari kulitangaza hilo, alihoji Oluoch.
Alisema kwa kawaida, kila halmashauri nchini inakuwa na kumbukumbu za walimu wote wakiwemo wale waliacha kazi.
Kumbukumbu hizo ni pamoja na za walimu kuajiriwa au kuacha kazi na zinapelekwa katika wizara hiyo na Ghasia kwa wadhifa wake alipaswa kulijua hilo mapema kabla ya kuiingizia nchi hasara hiyo ya mamilioni, alisema kiongozi huyo wa CWT.
Oluoch alisema serikali inapaswa kufanya uchunguzi ili kubaini watumishi waliochota fedha hizo na kuwachukulia hatua.
Waziri Ghasia anapaswa kutoa maelezo ya jinsi fedha hizo zilivyolipwa kwa walimu hao, hili hawezi kukwepa kwa kuwa ndiye anayewajibika,alisema Oluoch.
Kauli hiyo inafuatia tangazo la hivi karibu la waziri Ghasia la kuwafukuza kazi walimu 463 waliokosa fisa na ambao wameisababishia serikali hasara ya Sh 477 milioni