drmkumba
Member
- Dec 27, 2010
- 52
- 1
Katika kile kinachoonekana kutokurudi nyuma katika kupigania haki zao,walimu ambao waliitwa kusahisha mitihani ya mock kidato cha sita kanda ya mashariki ikijumuisha mikoa ya Morogoro na Pwani wiki iliyopita waligoma katakata kufanya zoezi hilo pale Ruvu sec.
Kwa mujibu wa mmoja wa walimu hao alinukuliwa akisema kwamba wamegomea kufanya kazi hiyo kwa sababu kwa kipindi kirefu wamekuwa wakinyonywa na waratibu wa mitihani hiyo ambao ni wakuu wa shule (TAHOSA EASTERN ZONE) kwa kuwalipa kila karatasi ya majibu ya mtahiniwa mmoja (script) inayosahishwa kwa Tsh 350/= tu.
Amedai kwa sasa waliwataka waandaji hao waongeze kiasi hicho kama sivyo walimu hao wangefungasha virago na kurudi waliko toka.
TAHOSA hawakuwa tayari kuongeza kiasi chochote cha senti kitu ambacho kiliwafanya walimu hao wasusie zoezi hilo nakubeba mabegi yao then kurudi walikotoka.
Kwa mujibu wa mmoja wa walimu hao alinukuliwa akisema kwamba wamegomea kufanya kazi hiyo kwa sababu kwa kipindi kirefu wamekuwa wakinyonywa na waratibu wa mitihani hiyo ambao ni wakuu wa shule (TAHOSA EASTERN ZONE) kwa kuwalipa kila karatasi ya majibu ya mtahiniwa mmoja (script) inayosahishwa kwa Tsh 350/= tu.
Amedai kwa sasa waliwataka waandaji hao waongeze kiasi hicho kama sivyo walimu hao wangefungasha virago na kurudi waliko toka.
TAHOSA hawakuwa tayari kuongeza kiasi chochote cha senti kitu ambacho kiliwafanya walimu hao wasusie zoezi hilo nakubeba mabegi yao then kurudi walikotoka.