Walimu wapya waliokosa mishahara mwezi aprili kupewa dabo mwezi huu

V2C

Member
Feb 17, 2014
21
2
Nimepata habari za kuaminika toka kwa DEO mmoja mkoani RUVUMA kwamba Walimu wapya wote waliokosa Mshahara mwezi Aprili, watapewa Dabo mwezi huu yaani Mshahara wa mwezi Aprili na Mei. Vipi walimu wenzangu wa Halmashauri nyingine mnataharifa zozote juu ya hili?
 
DEO katuambia, pia Katibu wa TSD kasema kwani Fedha zote zimetumwa kwa kila Halmashauri.
 
Hakuna hiyo kitu mnajidanganya mtapewa wa mwezi huu then wa april mtaudai .ukisikia malimbikizo ya mshahara ndio hayo
 
Huku wilaya moja ya mbuge Baduweli-Dodoma, wamepewa hela yao jana. So msikalili eti haitotokea. Kuna wengine huku hawakuamin na kubeza eti hadi nauli hatutapewa. Nauli tumepewa na mshahara wa mwezi wa 4 tumepata. Shahidi mimi mwenyewe. Wilaya ya BAHI
 
Hela ipo kaka. Halafu walimu wazoefu wanapinga sana mapinduzi ya kimfumo mpya wa malipo, na muda wote wao ni kukatisha tamaa. Mara watakwambia sisi zamani tulikaa miezi 6 bila mshahara, mara hiki na kile. Sasa hata waziri Kawambwa kwamba hadi 31/6/2014 serikali haitakuwa na deni toka kwa walimu. Hivyo wamerekebisha kila kitu.
 
Jana nilikuwa h/mashauri ya KILINDI~Tanga. pia wamesema hela zimeletwa zote za miezi miwili DEO aliniambia tutapewa utaratibu wake namna ya kupewa. Pengine ni kweli WALIMU WA ZAMANI ACHENI KUISHI KWA KUKARIRI kama wewe ulikaa miezi 10 bila mshahara haimaanishi mwenzako nae afanyiwe the same
 
Huku wilaya moja ya mbuge Baduweli-Dodoma, wamepewa hela yao jana. So msikalili eti haitotokea. Kuna wengine huku hawakuamin na kubeza eti hadi nauli hatutapewa. Nauli tumepewa na mshahara wa mwezi wa 4 tumepata. Shahidi mimi mwenyewe. Wilaya ya BAHI

wameingiza zote kwenye akaunti AU wametumia njia gani
 
ndio wapewe si haki yao, mbona mimi walinipa kwaiyo na wenzangu wana haki ya kupata pesa zao bana.
 
Kuna jamaa yangu yupo dsm hakupata mwezi ulioisha lkn pia hata mwezi huu kaambiwa hatapata kuna tatizo lilifanyika.Ni balaa hata yakukopeshwa hakuna
 
Nashukuru kwa kupata sitahiki zetu walimu bila bughuza. Mishahara yote tumepewa. JAMANI TUSIKARIRI, Eti government works on papers, kwani Haijui kama kuwa kundi fulani linadai au litadai. Kwanin kuna local government?.
 
Back
Top Bottom