Walimu wanawekwa ndani, wanadhalilishwa sababu ya ujenzi wa madarasa wakati si wakandarasi wala mafundi ujenzi. Nini maoni ya CWT kama chama?

polokwane

JF-Expert Member
Dec 16, 2018
3,359
5,808
Kwa hili TAMISEMI kaeni mfikiri upya mzigo mnao watwisha walimu ukiachilia mbali mzigo wa vipindi walio nao si haki na si sawa

Na CWT mpo kimya hata hamfuatilii mkaona ni madhila gani walimu walio chini ya chama chenu wana nyanyasika na kusurubishwa kwa kazi ambayo hawakuisomea na wala hawana ujuzi nayo.

Wakuu wa Wilaya wanadhalilisha walimu , wanawaweka ndani na maneno ya dhihaka sababu ya ujenzi wa madarasa? Mlifikiriaje kuwatwisha mzigo huu walimu?

Kwanini hizo pesa za ujenzi msiziingize kwenye account za vijiji au kata au hata halmashauri ili walimu waendelee na kazi yao ya kufundisha watoto? Mda mwingi walimu wanahangaika na mambo ya ujenzi hao wananchi wenyewe ushiriki wao duni sana sababu mmesha ingiza siasa huko, kwanini mnawaongezea majukumu walimu tena mazito yenye masimango na kuviziana?

Nasema kuviziana sababu vitu vingi vilivyo andikwa kwenye BOQ zenu haviakisi uhalisia wa bei zilizoko sokoni pia kuna vitu vingi sana havipo kwenye BOQ zenu wakati katika uhalisi vina gharimu pesa tena sana

Wakuu wa wilaya wana waweka ndani walimu kisa ujenzi umechelewa au upo chini ya kiwango, jaman hivi mwalimu aliye jifunza kushika chaki na kupiga kelele na wanafunz darasa la pili leo anahangaika na size za nondo ? Anahangaika na ratio za cement , ahangaike na mafundi wezi na wadokozi ambao ukipepesa macho tu wameshafichaa kilo 2 za misumari yaani siku nzima upo na ujenzi hayo kayasoma wapi kwenye cheti chake hata akastahili kusimangwa nankuwekwa mahabusu akiyakosea?

Lakini pia swala hili limeathiri sana ufundishwaji wa watoto huko madarasani maana mda mwingi ni vikao vya kamati na kuandaa mihutasari ya vikao kusimamia mafundi bado asimamie mitihani na asahihishe na kupanga matokeo ya mitihani ya wanafunzi hapo achilia mbali kuingia darasani kufundisha vipindi vyote tabu tupu huko.

Kibaya zaid TAMISEMI tarajieni kupata majengo ya hovyo kuwahi kutokea kwa sababu zifuatazo

1. Kuna baadhi majengo yamejengwa na tofali mbichi kabisa
2. Hatua za ujenzi kitaalamu hazikuzingatiwa kabisa kwenye majengo mengi kwa sababu:-
  • Mkuu wa wilaya naye ni makandarasi akienda site naye ana maelekezo yake
  • Mkurugenzi naye ni mkandarasi akienda site naye anamaelekezo yake
  • Afisa elimu naye ni mkandarasi akienda site naye ana maelekezo yake
  • Ofisa tarafa naye ni mkandarasi akienda site naye ana maelekezo yake
  • Mwenye kiti CCM wilaya naye ni mkandarasi akienda site naye ana maelekezo yake hapo bado mkuu wa mkoa, afisa tawala mkoa, Mwenyekiti wa Ccm mkoa na wengineo yaan miluzi hadi mbwa haelewi aende wapi.
  • Engineer wilaya naye ni mkandarasi akienda site naye anatoa maelekezo yake tena ya kitaalam
lakin Cha ajabu mkuu wa wilaya anaweza kupinga maelekezo ya engeneer na akataka yafuatwe yakwake sababu yeye ndiye yeye 😅😅😅.
Tofali inafyatuliwa leo kesho inajenga 😅😅😅😅 speed ya mwanga bora majengo na sio majengo bora kila mkuu wa wilaya anataka kabla tarehe 15 decemba 2021 awe wakwanza kukabidhi bora jengo sio jengo bora.

muwe na huruma nyie watu fedha hizi ni za mkopo tutalipa wakati majengo yatabomoka ndani ya miaka 5-10.

USHAURI: Kwanini TAMISEMI fedha hizi msiingize mapema sana ili kupunguza huku kufanya kazi kwa pressure kubwa na speed ambayo inachochea kabisa kupata majengo majengo yasiyo bora kabisa?

Lakini pia kwanini TAMISEMI msiingize fedha hizi kwenye account za vijiji au kata ili wao waunde kamati zao huko za vijiji na wananchi wasimamie ujenzi na walimu muwaache waendelee na wajibu wao ambao ni mzito sana kulingana na wingi wa wanafunzi? Hebu kaeni mlitafakari upya na kwa umakini swala hili hali si nzuri hata kidogo.
 
Wakati wa uchaguzi mlisaidia sana kuweka kura 10 kumi.kwenye masanduku.

Mnavuna mlichopanda.

Magu yeye kashavuna. Na wengine mtafata
Haya huwa ni mawazo ya mtu ambaye bado anawaza kizamani sana

Katika picha zote zilizo kuwa zinatumwa za wizi wa kura 2020 ulimuona mwalimu hata mmoja akifanya hilo? Mie nliwaona askari zaid , Mwalimu sikuwaona na wala sijaona picha hata moja ya mwalimu akifanya hicho unacho dai wewe sijui wewe mwenzangu kama uliona labda tuambie.
 
Haya huwa ni mawazo ya mtu ambaye bado anawaza kizamani sana

Katika picha zote zilizo kuwa zinatumwa za wizi wa kura 2020 ulimuona mwalimu hata mmoja akifanya hilo? Mie nliwaona askari zaid , Mwalimu sikuwaona na wala sijaona picha hata moja ya mwalimu akifanya hicho unacho dai wewe sijui wewe mwenzangu kama uliona labda tuambie.
Ningekutajia mmoja kwa majina yake na kituo chake cha kazi hapa sema nitafichua utambulisho wangu.
Wife ni mwalimu kuna wakati anajisahau na kuniambia kilichotokea humo kwenye kura
 
Umewasahau Maafisa manunuzi, huku Shinyanga sjui itakuwaje jmn nyie! Yaani Hela kawekewa Mkuu wa shule Maafisa manunuzi ndo wanasaka tenda ahahaha
 
Chama Cha Walimu NI taasisi ya Chama Cha Mazezeta ambayo dhamira yake si kumtetea, kumsaidia, kumkwamua Wala kutatua kero na tabu mbalimbali zinazoyakabili Walimu.

Chama Cha Walimu kipo kwa ajili ya kuwanyonya TU Walimu. Hello zinaenda kwa Chama Cha Mazezeta na viongozi wachache walioamua kusaliti Walimu wenzao
 
Haya huwa ni mawazo ya mtu ambaye bado anawaza kizamani sana

Katika picha zote zilizo kuwa zinatumwa za wizi wa kura 2020 ulimuona mwalimu hata mmoja akifanya hilo? Mie nliwaona askari zaid , Mwalimu sikuwaona na wala sijaona picha hata moja ya mwalimu akifanya hicho unacho dai wewe sijui wewe mwenzangu kama uliona labda tuambie.
Hivi huyu aliyesimama pembeni ya askali ni nani?
 

Attachments

  • 2954159_.mp4
    1.6 MB
Umewasahau Maafisa manunuzi, huku Shinyanga sjui itakuwaje jmn nyie! Yaani Hela kawekewa Mkuu wa shule Maafisa manunuzi ndo wanasaka tenda ahahaha
Ndio Kazi yao.Mimi Nina jamaa zangu wakandarasi na Wana maduka ya hardware walikataa hizo ofa za mil.20 kwa darasa full tena walipewa madarasa. 4 kila mja.

Hizo Kazi hazina faida labda uwe mjinga,walau bei zingekuwa 25-30 mil.kwa chumba kimoja full na furniture zake la sivyo waendelee kutumia wafungwa maana materials ziko juu Sana kuliko pesa ya ujenzi.
 
Ningekutajia mmoja kwa majina yake na kituo chake cha kazi hapa sema nitafichua utambulisho wangu.
Wife ni mwalimu kuna wakati anajisahau na kuniambia kilichotokea humo kwenye kura
Hahahaaaa sasa kumbe ni mkeo ndo kihiyo anza naye yeye basi,
Lakini kwa ninacho kihisi mana sijawahi kushuhudia hayo ya uchaguzin huenda hata kama mkeo kafanya hicho ulicho kisema basi muulize ni katika mazingira gani? Maana kuna wakati huenda wanashurutishwa kufanya hivyo hebu muulize uzuri huyo mkeo je? Alifanya kwa mapenzi yake kwa CCM au shuruti kwa vile ni muajiriwa wa serikali na anaogopa kufanyiwa fitna kwenye kibarua chake
 
Kwa nini walikubali kufanya Kazi ambazo sio taaluma zao? Si wanapenda udokozi acha wanyoshwe.
Uelewa wako wa mambo ni mdogo sana sana maana yaonesha hujui lolote lile siku nyingine tulia au uliza wanao jua wakuelimishe kwanza kabla ya kukoment
 
Ningekutajia mmoja kwa majina yake na kituo chake cha kazi hapa sema nitafichua utambulisho wangu.
Wife ni mwalimu kuna wakati anajisahau na kuniambia kilichotokea humo kwenye kura

Ameenda kufanya ile kazi kama mwalimu au kama kada? Unatumia nini kufikiria broo?
 
Nina kijiwe Cha welding,walikuja walimu kunipa kazi ya dawati 120 niifanye kwa siku 3 nime kataa,ni kitu kisicho wezekana.
Yaana hivyo ndivyo walivyo ambiwa na wao ndio maana hapo juu ninesema tofali linafyatuliwa leo halafu kesho linajenga ukuta
 
Back
Top Bottom