Walimu wanavyohamishwa sekondari kwenda msingi ni uonevu na ukiukwaji haki kila Mtanzania anapaswa kuulani

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Jambo hili limezua mashinikizo ya damu na hata vifo. Sababu kubwa inayotolewa na serikali katika zoezi hili ni kuwa kuna mlundamano wa walimu sekondari na uhaba wa walimu shule za msingi. Labda ni rahisi kuelewa hilo na kusema kimsingi, labda ni jambo jema kufanya namna fulani ya kusawazisha. Lakini ukweli ni kwamba kuna mambo ya kutafakari;
  • walimu wanahamishwa kwa lazima bila kuwa na uraratibu waliokubaliana na mwajiri
  • walimu wanaohamishwa wanalazimishwa kuhama bila kupewa fedha za uhamisho
  • walimu wanaohamishwa wanaenda msingi kuwa walimu wa kawaida huku wakisimamiwa na headteacher ambaye kidaraja ni mdogo kwao
Swali ambalo kila Mtanzania anajiuliza, serikali ya awamu ya tano imefikia hali ya ukatili wa namna hii na kufanya maamuzi bila kujali athari za kisaikolojia kwa watu wake? Je huu sio udikteta unaosemwa na viongozi wa upinzani na hata wananchi wengi? Inaingiaje akilini kwamba serikali yetu inaamua kwa ubabe na ulevi tu kushusa vyeo watu bila hata kufanya makubaliano ya msingi na hao watu, au angalau kuwapa fedha za uhamisho?

Na je, serikali imefikiria athari za kuwapeleka hawa walimu wa sekondari kwenye shule za msingi wakasimamiwe na wakuu wa shule ambao ni wadogo kwao ki-daraja? Mwalimu gani wa sekondari ataona ni sawa kwenda kuamriwa na mwalimu mkuu wa msingi akijua kwamba anamzidi kidaraja? Je serikali yetu katika upofu wake wa kuongoza haijaona kwamba inatatua tatizo kwa kutengeneza tatizo huko mashuleni msingi?

Tukirudi katika suala la haki za raia wa Tanzania, kinachofanywa na serikali ni uonevu uliopita mipaka. Najiuliza, chama cha walimu kiko wapi? Kwa nini hamjaenda mahakamani kupinga hili suala? Kwa nini hamjaitisha mgomo wa walimu wote wa sekondari nchini kupinga na kulaani jambo hili?

Kama serikali iliona kuna tatizo la usawaziko kati ya sekondari na msingi, basi ilipaswa ihamishe walimu kwa hiari yao, labda kwa kuwapa motisha ya fedha kwamba kutakuwa na nyongeza ya 30% kwenye mshahara wa mwalimu atakaekubali uhamisho wa namna hii, zaidi ya marupurupu ya uhamisho. Huenda tungekuwa na walimu wengi wa kujitolea kuhama kwa hiari. Lakini huwezi tu kuamua kwa ubabe kwamba kwa kuwa una madaraka nakushusha cheo, nakuhamishia msingi toka sekondari, na sikupi hela ya uhamisho.

Raisi Magufuli alikuwa mwalimu wa sekondari miaka kadhaa iliyopita. Yeye angefurahia enzi hizo kufanyiwa jambo kama hili? Kwa nini basi uwafanyie wengine jambo ambalo wewe binafsi usingekubali ufanyiwe?

Huu ubabe wa serikali unazidi sasa, na umefikia hatua ya kutovumilika.

Kama serikali inaona hili ni sawa, basi iende hata jeshini JWTZ na kuwaambia wanajeshi wenye rank za Major wanaosimamia kombania (company) na kuripoti kwa Luteni Kanali sasa wanaweza kuhamishwa, bado wakiwa Major, na kwenda kusimamia Platoon na kuripoti kwa Captain na mshahara wao hautabadilika.
 
Jambo hili limezua mashinikizo ya damu na hata vifo. Sababu kubwa inayotolewa na serikali katika zoezi hili ni kuwa kuna mlundamano wa walimu sekondari na uhaba wa walimu shule za msingi. Labda ni rahisi kuelewa hilo na kusema kimsingi, labda ni jambo jema kufanya namna fulani ya kusawazisha. Lakini ukweli ni kwamba kuna mambo ya msingi;
  • walimu wanahamishwa kwa lazima bila kuwa na uraratibu waliokubaliana na mwajiri
  • walimu wanaohamishwa wanalazimishwa kuhama bila kupewa fedha za uhamisho
  • walimu wanaohamishwa wanaenda msingi kuwa walimu wa kawaida huku wakisimamiwa na headteacher ambaye kidaraja ni mdogo kwao
Swali ambalo kila Mtanzania anajiuliza, serikali ya awamu ya tano imefikia hali ya ukatili wa namna hii na kufanya maamuzi bila kujali athari za kisaikolojia kwa watu wake? Je huu sio udikteta unaosemwa na viongozi wa upinzani na hata wananchi wengi? Inaingiaje akilini kwamba serikali yetu inaamua kwa ubabe na ulevi tu kushusa vyeo watu bila hata kufanya makubaliano ya msingi na hao watu, au angalau kuwapa fedha za uhamisho?

Na je, serikali imefikiria athari za kuwapeleka hawa walimu wa sekondari kwenye shule za msingi wakasimamiwe na wakuu wa shule ambao ni wadogo kwao ki-daraja? Mwalimu gani wa sekondari ataona ni sawa kwenda kuamriwa na mwalimu mkuu wa msingi akijua kwamba anamzidi kidaraja? Je serikali yetu katika upofu wake wa kuongoza haijaona kwamba inatatua tatizo kwa kutengeneza tatizo huko mashuleni msingi?

Tukirudi katika suala la haki za raia wa Tanzania, kinachofanywa na serikali ni uonevu uliopita mipaka. Najiuliza, chama cha walimu kiko wapi? Kwa nini hamjaenda mahakamani kupinga hili suala? Kwa nini hamjaitisha mgomo wa walimu wote wa sekondari nchini kupinga na kulaani jambo hili?

Kama serikali iliona kuna tatizo la usawaziko kati ya sekondari na msingi, basi ilipaswa ihamishe walimu kwa hiari yao, labda kwa kuwapa motisha ya fedha kwamba kutakuwa na nyongeza ya 30% kwenye mshahara wa mwalimu atakaekubali uhamisho wa namna hii, zaidi ya marupurupu ya uhamisho. Huenda tungekuwa na walimu wengi wa kujitolea kuhama kwa hiari. Lakini huwezi tu kuamua kwa ubabe kwamba kwa kuwa una madaraka nakushusha cheo, nakuhamishia msingi toka sekondari, na sikupi hela ya uhamisho.

Raisi Magufuli alikuwa mwalimu wa sekondari miaka kadhaa iliyopita. Yeye angefurahia enzi hizo kufanyiwa jambo kama hili? Kwa nini basi uwafanyie wengine jambo ambalo wewe binafsi usingekubali ufanyiwe?

Huu ubabe wa serikali unazidi sasa, na umefikia hatua ya kutovumilika.
Wewe ni mwalimu au umesimriwa?
 
Wewe ni mwalimu au umesimriwa?
Swali lako halina mchango wowote katika thread. Kama una habari zilizo relevant na thread weka hapo sio kumaliza nafasi kwenye server. Kama sielewi kinachoendela basi hilo ni kosa pia kwa serikali, haijafanya "management of change". Au tuambie ewe unaeelewa kinachoendelea, kwa nini walimu wapokee barua ya uhamisho kwenda msingi na kufa kutokana na mshituko?
 
Mwalimu ni mwalimu

Popote anaweza kufundisha

Tatizo ni mwalimu wa hisabati unataka akafundishe history

Pole walimu kwa haya ila ndo utaratibu wa kazi

Kama unaona mkataba wako umekiukwa peleka shauri mahakmani

Ila kama ulisaini uatafanya kazi popote Tanzania basi endelea kufanya kazi
 
Unaonekana umesimuliwa nenda uhulize wanalipwa hao na si kushushwa vyeo vya muundo wanabaki na vyeo vyao km ni mwl Daraja tatu c hatabaki vivo hivo
 
Mwalimu ni mwalimu Popote anaweza kufundisha
Tatizo ni mwalimu wa hisabati unataka akafundishe history

Pole walimu kwa haya ila ndo utaratibu wa kazi Kama unaona mkataba wako umekiukwa peleka shauri mahakmani

Ila kama ulisaini uatafanya kazi popote Tanzania basi endelea kufanya kazi

Hiii hali ya baadhi yetu walio na mashemeji katika uongozi wa awamu ya tano kubeza wanaoonewa ni chanzo kimojawapo cha kuendelea kufanyiwa ubabe.

Niambia, kwa kuwa Captain pilot wa wa JWTZ alisaini kufanya kazi popote Tanzania, ni sawa yeye kuondolewa JWTZ na kupelekwa kuwa Koplo pilot wa helikopta ya Polisi? Au ni sawa yeye kuondolewa kuwa Captain Airwing na kuwa Sergent kikosi cha Mizinga akaendeshe kifaru?
 
Haya mambo yanasikitisha sana na yatapelekea anguko kuu kwa elimu yetu. Wanaofanya hivyo walitakiwa na wao wapeleke watoto wao kwenye shule za umma. Siyo wasimamie kuua elimu yetu huko watoto wao wakiwapeleka Feza schools
 
Unaonekana umesimuliwa nenda uhulize wanalipwa hao na si kushushwa vyeo vya muundo wanabaki na vyeo vyao km ni mwl Daraja tatu c hatabaki vivo hivo
Nani amekuambia wanalipwa? Kawaulize wewe basi. Na wewe unaona ni sawa kuendelea kuwa Mwalimu wa daraja C ambaye ulikuwa unaripoti kwa Headmaster na sasa ukaripoti kwa Headteacher ambaye unamzidi daraja na qualifications? Na wangepokea barua za huo uhamisho wapande mashinikizo ya damu? Sidhani kama umeenda shule wewe.
 
Kumbe shida cheo
Status mkuu. Waulize wanajeshi. Akiondolewa hata tepe moja anaumia sana, japo mshahara unabaki palepale. Lakini kwa upande wa walimu kuna suala jingne la msingi. Hivi umewahi kuwa na bosi ambaye unamzidi sana ki-elimu, qualifications na mshahara? Usiombe ukakuta ana arrogance fulani. Utaona kazi chungu.
 
Status mkuu. Waulize wanajeshi. Akiondolewa hata tepe moja anaumia sana, japo mshahara unabaki palepale. Lakini kwa upande wa walimu kuna suala jingne la msingi. Hivi umewahi kuwa na bosi ambaye unamzidi sana ki-elimu, qualifications na mshahara? Usiombe ukakuta ana arrogance fulani. Utaona kazi chungu.
Aisee, pole sana mkuu!
 
mimi sioni tatizo endapo umehamishiwa jirani na eneo lako la zamani. pia sioni tatzo kuripoti kwa headteacher. Tatizo ni kama umepangwa mbali zaidi na eneo la zamani. Suala la madaraja, sioni kama ni issue so long as mshahara wako uko palepale. Msharaha unapata tatizo nini? Mambo ya madaraja wewe yanakuhusu nini? Mfano yeye ana degree wewe una masters. Tatzo liko wapi yeye kuwa headteacher? Pia hizo position ni za muda tu. anakuja mngine. tena huenda ukaja wewe mlalamikaji. Labda ungeniambia kuwa ulizoea kufundisha kiingereza na wanafunzi wakubwa so italeta shida kudeal na watoto, hapo walau ungekuwa na point kidogo. Lakini cjui madaraja hii hunishawishi kabisa
 
mimi sioni tatizo endapo umehamishiwa jirani na eneo lako la zamani. pia sioni tatzo kuripoti kwa headteacher. Tatizo ni kama umepangwa mbali zaidi na eneo la zamani. Suala la madaraja, sioni kama ni issue so long as mshahara wako uko palepale. Msharaha unapata tatizo nini? Mambo ya madaraja wewe yanakuhusu nini? Mfano yeye ana degree wewe una masters. Tatzo liko wapi yeye kuwa headteacher? Pia hizo position ni za muda tu. anakuja mngine. tena huenda ukaja wewe mlalamikaji. Labda ungeniambia kuwa ulizoea kufundisha kiingereza na wanafunzi wakubwa so italeta shida kudeal na watoto, hapo walau ungekuwa na point kidogo. Lakini cjui madaraja hii hunishawishi kabisa
Sawa Mkuu, lakini sasa hayo ndio mambo serikali ilitakiwa iwaelimishe hao waalimu. Tunaita "management of change"
 
Jambo hili limezua mashinikizo ya damu na hata vifo. Sababu kubwa inayotolewa na serikali katika zoezi hili ni kuwa kuna mlundamano wa walimu sekondari na uhaba wa walimu shule za msingi. Labda ni rahisi kuelewa hilo na kusema kimsingi, labda ni jambo jema kufanya namna fulani ya kusawazisha. Lakini ukweli ni kwamba kuna mambo ya kutafakari;
  • walimu wanahamishwa kwa lazima bila kuwa na uraratibu waliokubaliana na mwajiri
  • walimu wanaohamishwa wanalazimishwa kuhama bila kupewa fedha za uhamisho
  • walimu wanaohamishwa wanaenda msingi kuwa walimu wa kawaida huku wakisimamiwa na headteacher ambaye kidaraja ni mdogo kwao
Swali ambalo kila Mtanzania anajiuliza, serikali ya awamu ya tano imefikia hali ya ukatili wa namna hii na kufanya maamuzi bila kujali athari za kisaikolojia kwa watu wake? Je huu sio udikteta unaosemwa na viongozi wa upinzani na hata wananchi wengi? Inaingiaje akilini kwamba serikali yetu inaamua kwa ubabe na ulevi tu kushusa vyeo watu bila hata kufanya makubaliano ya msingi na hao watu, au angalau kuwapa fedha za uhamisho?

Na je, serikali imefikiria athari za kuwapeleka hawa walimu wa sekondari kwenye shule za msingi wakasimamiwe na wakuu wa shule ambao ni wadogo kwao ki-daraja? Mwalimu gani wa sekondari ataona ni sawa kwenda kuamriwa na mwalimu mkuu wa msingi akijua kwamba anamzidi kidaraja? Je serikali yetu katika upofu wake wa kuongoza haijaona kwamba inatatua tatizo kwa kutengeneza tatizo huko mashuleni msingi?

Tukirudi katika suala la haki za raia wa Tanzania, kinachofanywa na serikali ni uonevu uliopita mipaka. Najiuliza, chama cha walimu kiko wapi? Kwa nini hamjaenda mahakamani kupinga hili suala? Kwa nini hamjaitisha mgomo wa walimu wote wa sekondari nchini kupinga na kulaani jambo hili?

Kama serikali iliona kuna tatizo la usawaziko kati ya sekondari na msingi, basi ilipaswa ihamishe walimu kwa hiari yao, labda kwa kuwapa motisha ya fedha kwamba kutakuwa na nyongeza ya 30% kwenye mshahara wa mwalimu atakaekubali uhamisho wa namna hii, zaidi ya marupurupu ya uhamisho. Huenda tungekuwa na walimu wengi wa kujitolea kuhama kwa hiari. Lakini huwezi tu kuamua kwa ubabe kwamba kwa kuwa una madaraka nakushusha cheo, nakuhamishia msingi toka sekondari, na sikupi hela ya uhamisho.

Raisi Magufuli alikuwa mwalimu wa sekondari miaka kadhaa iliyopita. Yeye angefurahia enzi hizo kufanyiwa jambo kama hili? Kwa nini basi uwafanyie wengine jambo ambalo wewe binafsi usingekubali ufanyiwe?

Huu ubabe wa serikali unazidi sasa, na umefikia hatua ya kutovumilika.
Nina maswali kadhaa kwako,ukihamia shule ya msingi,mshahara wako unapunguzwa?
Saikolojia yako INA athirika vipi kwa kusimamiwa na uliye mzidi cheo,?(kuwa kiongozi sio lazima uwe na ujuzi kuliko unaowaongoza)

Kazi yenu,ni utumishi wa umma,mnastahili kulipwa kama mikataba yenu inavyosema,na kumbuka mnalipwa n kodi za wananchi,hamtufanyii hisani mnapoenda kufundisha watoto wetu,we paid for your training,we pay you to teach,go teach.
Kama mnaona malipo ni madogo,achieni ngazi,wengine waje,fanyeni kama sekta binafsi,muajiri akizingua,unaacha kazi,ukitaka mshahara zaidi,akagoma,unaacha kazi,uwezi kumlazimisha muajiri wa sekta binafsi akulipe unavyotaka,.atakubali kukulipa kama anakuhitaji sana,
Acheni kulialia,sisi mabosi wenu,wananchi,tumesema muende huko msingi,malipo mengine hakuna,ukishindwa,acha kazi
 
Nina maswali kadhaa kwako,ukihamia shule ya msingi,mshahara wako unapunguzwa?
Saikolojia yako INA athirika vipi kwa kusimamiwa na uliye mzidi cheo,?(kuwa kiongozi sio lazima uwe na ujuzi kuliko unaowaongoza)

Mkuu nitakupa mfano wa kiwango chako ili unielewe. Leo au kesho ukiwa ndani ya daladala, mwambie dereva wa daladala kwamba anaonaje akiwa mpiga debe wa hiyo daladala badala ya kuwa dereva lakini alipwe mshahara anaopata kama dereva. Akikukubalia na kutokuona mwendawazimu njoo hapa kwenye hii thread unieleze.
 
Me Nina digrii ya pili ya elimu nafundisha msingi.....kitambo acha kukariri piga kazi mkuu
 
Back
Top Bottom