Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Habari zilizorushwa na TBC1 saa 2 usiku zinaeleza kuwa baadhi ya walimu wa shule ya msingi Sakasaka iliyoko wilaya ya Meatu, Shinyanga wamechapwa viboko na Sungusungu kwa kosa la kutohudhuria mkutano wa kijiji. Pia mke wa mwalimu mkuu amechapwa viboko baada ya kuvuliwa nguo hadharani. Na kuna mmojawapo wa hao walimu alikuwa mjamzito. Walimu waliocharazwa bakora na baadhi ya wanafunzi walioshuhudia walihojiwa na mwandishi wa habari Richard Leo, kutoka Mwanza.
Hili ni tukio la pili baada ya lile lilotokea mwaka jana katika kijiji cha Katerero, Bukoba vijijini ambapo mkuu wa wilaya wa wakati huo Mnari alimwamuru askari kuwachapa viboko walimu waliokuwa wamechelewa kufika shuleni. Pamoja na Mnari kufukuzwa kazi ya ukuu wa wilaya, hakuna taarifa kama alichukuliwa hatua zaidi. Pia walimu walifungua kesi kudai fidia ingawa haijulikani hiyo kesi inaendeleaje.
Je nini kifanyike walimu waache kudhalilishwa?
Hili ni tukio la pili baada ya lile lilotokea mwaka jana katika kijiji cha Katerero, Bukoba vijijini ambapo mkuu wa wilaya wa wakati huo Mnari alimwamuru askari kuwachapa viboko walimu waliokuwa wamechelewa kufika shuleni. Pamoja na Mnari kufukuzwa kazi ya ukuu wa wilaya, hakuna taarifa kama alichukuliwa hatua zaidi. Pia walimu walifungua kesi kudai fidia ingawa haijulikani hiyo kesi inaendeleaje.
Je nini kifanyike walimu waache kudhalilishwa?