Walimu wacharazwa bakora tena, mbele ya wanafunzi wao!!

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Habari zilizorushwa na TBC1 saa 2 usiku zinaeleza kuwa baadhi ya walimu wa shule ya msingi Sakasaka iliyoko wilaya ya Meatu, Shinyanga wamechapwa viboko na Sungusungu kwa kosa la kutohudhuria mkutano wa kijiji. Pia mke wa mwalimu mkuu amechapwa viboko baada ya kuvuliwa nguo hadharani. Na kuna mmojawapo wa hao walimu alikuwa mjamzito. Walimu waliocharazwa bakora na baadhi ya wanafunzi walioshuhudia walihojiwa na mwandishi wa habari Richard Leo, kutoka Mwanza.

Hili ni tukio la pili baada ya lile lilotokea mwaka jana katika kijiji cha Katerero, Bukoba vijijini ambapo mkuu wa wilaya wa wakati huo Mnari alimwamuru askari kuwachapa viboko walimu waliokuwa wamechelewa kufika shuleni. Pamoja na Mnari kufukuzwa kazi ya ukuu wa wilaya, hakuna taarifa kama alichukuliwa hatua zaidi. Pia walimu walifungua kesi kudai fidia ingawa haijulikani hiyo kesi inaendeleaje.

Je nini kifanyike walimu waache kudhalilishwa?
 
Haya mambo bwana, lakini kisheria ukiondoa madenti si viboko kwa watu wazima hadi hakimu aruhusu? Hawa sungusungu wanao uwezo kweli kiutaratibu kuchapa viboko?
 
Haya mambo bwana, lakini kisheria ukiondoa madenti si viboko kwa watu wazima hadi hakimu aruhusu? Hawa sungusungu wanaouwezo kweli kiutaratibu kuchapa viboko?

Kwa nchi yetu kila mtu mwenye madaraka hata yakiwa madogo kiasi gani anaweza kuchapa mtu bakora. Huko vijijini hata Mjumbe wa nyumba kumi (tena akiwa wa CCM) anaweza kutembeza bakora atakavyo. Lakini walimu ndio wamejishushia dhamani yao kwa kukubali kuwa mawakala wa CCM. Kwa wingi wao na jinsi ambavyo wamesambaa kila kona ya nchi wangeamua kutotumika wangeheshimika sana.
 
Hiyoni kwa wasukuma tu. Mwalimu mzima mpaka unalazwa chini bado upo tu!!!! Ndio maana mnatishiwa amani na upendo mpaka mnakufa wakavuuu, acha wachapwe kama hata mwalimu hajui haki yake hao wanakijiji je?:angry:
 
Aisee, hii ni aibu kwa nchi inayojigamba kuwa ina utawala bora na unaofuata sheria. JK upo wapi?
 
Habari zilizorushwa na TBC1 saa 2 usiku zinaeleza kuwa baadhi ya walimu wa shule ya msingi Sakasaka iliyoko wilaya ya Meatu, Shinyanga wamechapwa viboko na Sungusungu kwa kosa la kutohudhuria mkutano wa kijiji. Pia mke wa mwalimu mkuu amechapwa viboko baada ya kuvuliwa nguo hadharani. Na kuna mmojawapo wa hao walimu alikuwa mjamzito. Walimu waliocharazwa bakora na baadhi ya wanafunzi walioshuhudia walihojiwa na mwandishi wa habari Richard Leo, kutoka Mwanza.

Hili ni tukio la pili baada ya lile lilotokea mwaka jana katika kijiji cha Katerero, Bukoba vijijini ambapo mkuu wa wilaya wa wakati huo Mnari alimwamuru askari kuwachapa viboko walimu waliokuwa wamechelewa kufika shuleni. Pamoja na Mnari kufukuzwa kazi ya ukuu wa wilaya, hakuna taarifa kama alichukuliwa hatua zaidi. Pia walimu walifungua kesi kudai fidia ingawa haijulikani hiyo kesi inaendeleaje.

Je nini kifanyike walimu waache kudhalilishwa?

Sio waalimu tu, things are now going out of proportions, jumamosi mkuu wa mkoa
( RC) katuma mapolisi na maafisa usalama kumtoa ndani ya ofisi mwenyekiti wa baraza la Ardhi na nyumba Kigoma eti kwa sababu hafuati maelekezo yake.

Inaelekea rule of law inaanza kupuuzwa, ukifanya kosa naamua adhabu ya kukupa papo hapo ndio maana yake.

Tunakwenda wapi????
 
Hiyoni kwa wasukuma tu. Mwalimu mzima mpaka unalazwa chini bado upo tu!!!! Ndio maana mnatishiwa amani na upendo mpaka mnakufa wakavuuu, acha wachapwe kama hata mwalimu hajui haki yake hao wanakijiji je?:angry:

Hapana mkuu. Siyo tatizo la wasukuma tu. Albert Mnari alichapa walimu wa Bukoba. Na hao walikuwa wasukuma? Kuna tatizo kubwa zaidi ya Wasukuma au Wahaya.
 
Kutojua haki yako ni tatizo kwa Watanzaniawengi.
kule kanda ya ziwa sungusungu ndiye askari wa usalama barabarani, kutuliza gasia, na pia ndiyo jeshi la ulinzi, kwa hiyo pale kilichotokea ni ugaidi tu wa kuwavamia walimu na kuwapiga, sidhani kama kulikuwa na jinsi ya wanawake hao kujikinga (angalau wanaume) hasa kwa vile walichukuliwa kama wahalifu kwa kutohudhuria vikao vya serikali ya kijiji (sungusungu). Zamani ilikuwepo tabia ya kuwatenga watu wanaohisiwa kuwa wahalifu, pamoja na wale wasioshiriki shughuli za kijamii, ukikutwa hata unamsalimia mtu aliyetengwa na wewe pia unatengwa!
Tusiwalaumu walimu hawa, kwani mambo haya yapo kila sehemu, hata askari wetu wanawakwida watu na kuwapiga bila hatia. sioni tofauti kati ya sungusungu na wanausalama wetu.
 
Habari zilizorushwa na TBC1 saa 2 usiku zinaeleza kuwa baadhi ya walimu wa shule ya msingi Sakasaka iliyoko wilaya ya Meatu, Shinyanga wamechapwa viboko na Sungusungu kwa kosa la kutohudhuria mkutano wa kijiji. Pia mke wa mwalimu mkuu amechapwa viboko baada ya kuvuliwa nguo hadharani. Na kuna mmojawapo wa hao walimu alikuwa mjamzito. Walimu waliocharazwa bakora na baadhi ya wanafunzi walioshuhudia walihojiwa na mwandishi wa habari Richard Leo, kutoka Mwanza.

Hili ni tukio la pili baada ya lile lilotokea mwaka jana katika kijiji cha Katerero, Bukoba vijijini ambapo mkuu wa wilaya wa wakati huo Mnari alimwamuru askari kuwachapa viboko walimu waliokuwa wamechelewa kufika shuleni. Pamoja na Mnari kufukuzwa kazi ya ukuu wa wilaya, hakuna taarifa kama alichukuliwa hatua zaidi. Pia walimu walifungua kesi kudai fidia ingawa haijulikani hiyo kesi inaendeleaje.

Je nini kifanyike walimu waache kudhalilishwa?

Walimu wakilipwa mshahara mzuri na kuwekewa mazingira mazuri ya kufanyia kazi, uzalilishwaji na upuuzi wote huu utakwisha.
 
Hapana mkuu. Siyo tatizo la wasukuma tu. Albert Mnari alichapa walimu wa Bukoba. Na hao walikuwa wasukuma? Kuna tatizo kubwa zaidi ya Wasukuma au Wahaya.[/QUOTE]

Umesema kweli , watu tunalifungia macho na kuona ni kitu kidigo, hatuwezi kujua kusho na keshokutwa itakuwaje na nani atafanya nini kwenye magnitude gani, wahenga walisema mdharaumwiba mguu huota tende!!!!!
 
Hili jambo lilikuwepo vijijini siku nyingi ambapo mtendaji wa kijiji anatoa adhabu kwa kuwacharaza bakora wananchi. Tatizo huko vyombo vya habari hakuna ndo maana taarifa hazijulikani. Kipindi kile nikiwa kijijini, nilishuhudia hiyo hali, na watu waliikubali kwasababu ya uelewa wao, kipato chao na mazingira. Ndo maana hii inaipa CCM company ya kupeta, maana licha ya kuchapwa wale watu hawaelewi zaidi ya thi-thi-e-mu. WACHA WAPATE BAKORA NDO ZITAWAZINDUA.
 
Nchi inapokosa utawala wa sheria matokeo yake ni hayo...Kila mtu anajiona ana uwezo wa kuamua chochote!...Adhabu ya mtu aliyekosa kuhudhuria kikaon ni kiboko?...Idont think so!...huu ni udhalilishaji!
 
Watoto siku zote huiga toka kwa wakubwa zao, walichofanya sungusungu wa shinyanga ni zao tu la wanachofanya wakubwa wengine, na hii ni wazi kuwa hapa TZ hakuna kitu kama utawala wa sheria. lakini mimi niwakumbushe tu hapa"wakubwa" wao wako ndani ya nyumba za vioo na wanawaudhi waponda kokoto, usiku utakokucha waponda kokoto wakagundua kuwa hao wanaowaudhi wanaishi kwenye nyumba za vioo.....
 
Kutojua haki yako ni tatizo kwa Watanzaniawengi.
kule kanda ya ziwa sungusungu ndiye askari wa usalama barabarani, kutuliza gasia, na pia ndiyo jeshi la ulinzi, kwa hiyo pale kilichotokea ni ugaidi tu wa kuwavamia walimu na kuwapiga, sidhani kama kulikuwa na jinsi ya wanawake hao kujikinga (angalau wanaume) hasa kwa vile walichukuliwa kama wahalifu kwa kutohudhuria vikao vya serikali ya kijiji (sungusungu). Zamani ilikuwepo tabia ya kuwatenga watu wanaohisiwa kuwa wahalifu, pamoja na wale wasioshiriki shughuli za kijamii, ukikutwa hata unamsalimia mtu aliyetengwa na wewe pia unatengwa!
Tusiwalaumu walimu hawa, kwani mambo haya yapo kila sehemu, hata askari wetu wanawakwida watu na kuwapiga bila hatia. sioni tofauti kati ya sungusungu na wanausalama wetu.

Hiyo ni kwa upande mmoja kwa upande wa pili ni kudharau utawala wa sheria, mtu unapata wapi haki ya kumhukumu mwenzio na kumchapa viboko? Mijini ndio zaidi haki zetu zinapokwa sie tunacheka tu eti maborn town. Amoeba, Umeunderestimate hawawakwidi bali wanawapiga risasi na kuwauwa watu eti majambazi na sisi badala ya kusimama na kulaani tunaunga mkono tuu. Tangu polisi wameanza hakuna inquiry hata moja ilitumwa kuangalia kama ni kweli au la.
.
 
Hiyo ni kwa upande mmoja kwa upande wa pili ni kudharau utawala wa sheria, mtu unapata wapi haki ya kumhukumu mwenzio na kumchapa viboko? Mijini ndio zaidi haki zetu zinapokwa sie tunacheka tu eti maborn town. Amoeba, Umeunderestimate hawawakwidi bali wanawapiga risasi na kuwauwa watu eti majambazi na sisi badala ya kusimama na kulaani tunaunga mkono tuu. Tangu polisi wameanza hakuna inquiry hata moja ilitumwa kuangalia kama ni kweli au la.
.

naagree mkuu,
hata huo utawala wa sheria wenyewe hupo hapa Tanzania. ni wanausalama na vigogo wangapi walio na kesi mahakamani?....kati ya hao ni asilimia finyu sana wanaohukumiwa kwa kuvunja haki za raia, wengi wanapiga risasi raia, kuwacharaza bakora, na kuwatukana matusi ya kuwadharirisha hadharani (unakumbuka waalimu wanafunzi wa chuo kimoja walivyoitwa WAPUMBAVU na kigogo wa kike?). Hao ndiyo wenye dhamana ya kusimamia utawala wa sheria, hebu nambie watawezaje wakati wenyeewe ndy wako mstari wa mbele katika kuzibaka hizo sheria?!

Signature yako inaongea jambo la msingi kabisa mkuu.
 
Nimeshangazwa na kusikitishwa sana na kitendo hiki pale nilipokuwa naangalia habari jana ..na hii si mara ya kwanza kutokea
Kuna mtu mwenye mamlaka ya kwachapa walimu viboko??
 
Jamani hiki kitendo ni cha kulaaniwa kwa nguvu zote, na hao sungusungu pamoja na mwenyekiti wao wawekwe ndani na wao wacharazwe viboko.

Leo imeanza kwa walimu tunachekelea kesho itakuwa wafanyakazi wa maofisini wanatolewa nje na kuchapwa na sisi tunaendelea kuchekelea.

Masikini walimu wamekosa nini? Ndio waliotutoa kwenye ujinga leo hii ndio fadhila yao! POLENI SANA WALIMU KWA UDHALILISHAJI HUO
 
Kwa mwendendo huu, itafika mahali waalimu washinde kuwafundisha wanafunzi, kwani wanafunzi watajichukulia hatua na kuwachraza viboko waalimu.
Hivi viongozi wa juu serikalini wanaliona hili? na kama wanaliona, wanasemaje?

Ningewashauri hao waalimu wawachukulie hatua za kishari ahao watu waliowacharaza viboko, ikiwa ni pamoja na waalimu wote kugoma kufunfudisha katika shule hiyo.
 
Dah hii kali tena, richad leo wa TBC anabahati sana ya kupata habari za kuchekesha flani hivi na oia kuripot kwake ndo huwa nacheka zaidi.
 
Back
Top Bottom