A
Anonymous
Guest
Wazazi na wanafunzi tunalalamikia tabia ya baadhi ya walimu wa Shule za Msingi Gmhasa iliyopo Ilala, Dar es Salaam kuwashinikiza watoto kuhudhuria shule siku za mwisho wa wiki (Jumamosi), pamoja na kuchangishwa fedha za mitihani.
Inadaiwa kuwa baadhi ya mitihani hulipiwa, jambo ambalo linaibua maswali kwa wazazi kuhusu matumizi ya ruzuku ya serikali inayotolewa kwa ajili ya uendeshaji wa shule.
Pia, watoto ambao hawahudhurii masomo ya Jumamosi au kushiriki michango hiyo ya fedha, wanasemekana kuadhibiwa siku ya Jumatatu wanaporejea shule. Hali hii imekuwa ikiwatia wasiwasi wanafunzi na wazazi kwa ujumla.
Wazazi wanaiomba mamlaka husika kulifuatilia suala hili ili kuhakikisha sheria na taratibu za elimu zinazingatiwa, na haki za watoto zinalindwa.
Inadaiwa kuwa baadhi ya mitihani hulipiwa, jambo ambalo linaibua maswali kwa wazazi kuhusu matumizi ya ruzuku ya serikali inayotolewa kwa ajili ya uendeshaji wa shule.
Pia, watoto ambao hawahudhurii masomo ya Jumamosi au kushiriki michango hiyo ya fedha, wanasemekana kuadhibiwa siku ya Jumatatu wanaporejea shule. Hali hii imekuwa ikiwatia wasiwasi wanafunzi na wazazi kwa ujumla.
Wazazi wanaiomba mamlaka husika kulifuatilia suala hili ili kuhakikisha sheria na taratibu za elimu zinazingatiwa, na haki za watoto zinalindwa.