Walimu Shule ya Sekondari Butimba na kashfa ya kujihusisha kimapenzi na Wanafunzi

ALT

Member
Oct 6, 2021
78
90
HABARI YA WANABODI?

Kuna huu upumbavu, umenikera. Hebu tusaidiane kuutatua.

NI JUU YA WAALIMU MALAYA WA BUTIMBA SEKONDARI-MWANZA


....Mwalimu mwanzalima na mwalimu paul....(JELA INAWAITA)

Mwalimu wa Butimba sekondari wiki hii alitaka kumbaka mwanafunzi ila Mungu saidia aliweza kumponyoka na kukimbia.

Mwanafunzi huyo wa kike sketi yake ilichanika, ilikuwa masomo ya saa tisa hivi.

Mwanafunzi alienda moja kwa moja kwa mama yake na kumjuza juu ya tukio hili. Mzazi alitoa taarifa kwa kiongozi mmoja wa chama na kiongozi wa chama akaijuza serikali na serikali ikamtuma afisa elimu wa wilaya ya Nyamagana kutatua mgogoro huo.

Mwalimu aliohijwa ila alikana kabisa kuhusika na tukio hilo.

Kikao cha mkuu wa shule na walimu pia hakikuzaa matunda, mwalimu bado alikana kata kata kuhusika na tukio hilo.

Mkuu mpya wa shule alimuita mzazi wa binti huyo wakaongea nae kwa kumpoza ili suala liishe, na hakika kwa mzazi na mwanafunzi ni kama limeisha.

Timu ya afisa elimu wamesema watapeleleza zaidi kuufahamu ukweli.

HALI YA SASA YA MWALIMU ALIYETAKA KUBAKA

Tangu timu ya afisa elimu kusema watalifanyia uchunguzi, mwalimu ameonekana akiongea na baadhi ya wanafunzi wa kike akiwa na sura ya hofu kana kwamba kuna kitu anataka kuficha.

TUKIO HILI LILITOKEAJE?

Kwa ufupi walimu hao wawili ofisi yao ni maabara ambayo ina magrill na mapaazia mazito.

Mwanafunzi huyu aliitwa na mwalimu huyo kuchukua mtihani wake.

Mwanafunzi huyo alienda, mashuhuda wawili wanazidi kusimlia.

Mwanafunzi alipoingia, pazia lilishushwa. Gafla wakaskia kelele kama ugomvi, niache, niache. Dakika sio nyingi, vitu kama vinadondoka ndani, ndipo mwanafunzi akatoka akikimbia huku kashikilia sketi imechanika. Moja kwa moja akaenda nyumbani

Binti huyu anasema mwalimu huyu amekuwa akimtongoza tangu kidato cha kwanza.

MWALIMU MWINGINE

Mwalimu mwingine huyu, anaekaa maabara. Mwenye sifa kama mwalimu wa kwanza. Huwaita wanafunzi na kuwawekea mziki kwenye smart phone na wanafunzi kuanza kucheza.

Mara kadhaa huwashika makalio na matiti na baadhi yao huwapa miadi wakutane siku za Jumamosi au Jumapili.

MHANGA MMOJA ANASIMULIA

Mwanafunzi mmoja wa kike, form one alichukizwa na kitendo cha mwalimu huyu, alimshika matiti na makalio. Alienda na kusema kwa mzazi.

Mzazi alilipeleka kwa mkuu wa shule, kikao kiliwekwa na mwalimu alionywa ingawaje hakukubali kosa.

Mwanafunzi huyu kaandamwa sana na walimu hawa wawili kwa manyanyaso ya kijinsia hadi anaomba ahamishwe shule. Ni matusi kwake na kejeli . Kwamba, umeshtaki imesaidia nini? Kwani hujawai kufanya?

Inauma sana.

YUPO MWALIMU ALIWAHI KUOA MWANAFUNZI BUTIMBA

Yupo mwalimu, alimpiga mimba mwanafunzi akiwa form 3, wazazi walimlazimisha amuoe na mpaka sasa alimuoa na hakuna hatua ya kisheria iliyochukuliwa kwa mwalimu huyo.


MKUU WA SHULE ALIYEAMIA MKOLANI SEKONDARI ANAJUA HAYA.

Aliwahi kumshuhudia mwalimu wa kiume amemkumbatia mwanafunzi maabara kimapenzi ila hakufanya lolote.

KIKAO CHA WAZAZI JANUARI
Mkuu wa shule mpya aliitisha kikao januari, suala la uzinzi wa walimu lilisemwa, ila hakuna hatua stahiki zilizo chukuliwa.

Wenye mamlaka nendeni karejee minutes za kikao cha Januari cha wazazi mtajua.

WAZIRI WA ELIMU NA TAASISI HUSIKA

Hili limezidi, linawakwaza waalimu, sana sana wa kike. Kwasababu hakuna hatua stahiki zinazo chukuliwa.

Mkishindwa kazi zenu, tutawasaidia. Haiwezekani mabinti wanyanyaswe kingono wapumbavu nyie mpo.

Imagine anafanyiwa mwanao, utajisikiaje?

USHAURI
Ni kazi rahisi, TAKUKURU, wekeni mtego, mtawashika hawa wapumbavu wote asubuhi na mapema. Kuanzia mkuu wa shule anayelea mpaka hao walimu wanaoacha wake zao na kutafuna watoto.

Nawasilisha.


MREJESHO MUDA HUU( SAA 2 KAMILI)

Tumbo ni joto kwa mukulu wa kaya hapa kituoni(skuli butimba).

Naona mkulu anaita vitoto vyote vya kike shule kuviambia vifunguke. Viseme changamoto vinazopitia na ikiwezekana viwataje waalimu tunaokula wanafunzi.

Usijikoshe kijinga mkulu. Huo muda mbona unao siku nyingi sana?

Subiri rungu zito kabla ya jua leo kuzama.


Ushauri ninaoweza kukupa, wape karatasi wanafunzi waandike majina ya sisi waalimu tunaowakula, tofauti na hapo, najiandaa kuchukua kiti chako.

Kituo kimekushinda. Maana, rafiki yako mkubwa ndie anakuzunguka kwa ushauri wa kijinga.

Ona unavyohaha sasa.

Mshkuru mkuru wa kituo cha dodoma kukutonya. Ira ariyesanua hili usihangaike kumtafuta. Tupo kituo kimoja, hapa hapa.

Ukiweza, chukua simu ya kila mmoja utamjua mbaya wako.



YALIYOJIRI KWA UFUPI SIKU NZIMA SKULI


1. Wanafunzi wa kike andikeni majina ya walimu wenye tabia hizo mbovu. Usiandike jina ili tuwabaini.
Kuna matcha wametisha wametajwa na jinsia kee kama wote.( shoo ilismamiwa na mkulu wa skuli).

2. Afisa mwajiri mida mida akatimba.

Maelezo yakachkuliwa kwa mhanga. Nao mashahidi wakanyoosha maelezo. Mwishowe bhana, sket iliyochanika si ilishonwa nyumbani?

Kwaiyo ushahidi hakuna, ivyo kesi hakuna. Hahaha......

Hebu kwasasa niishie hapa. Ila waalimu wengi tumo humu wa butimba hadi twafahamiana kwa miandiko.

Acha nishibe nianze mtaja mmoja mmoja kwa id zenu. Maana akat mkuu katueka kikaangoni tulikana kutohusika.

Mungu anatuona. Tutalipwa ujira wetu.


YAANI MWANAFUNZI KUSHONA SKETI ILIYOCHANWA KATIKA TUKIO LA KUJARIBU KUBAKWA KAFUTA USHAHIDI?

NANI ATAMFUNGA PAKA KENGELE?


MREJESHO.....
Wapenz.....nawashwa kutoa list ya makx ambzo walim wenxang wamepat baad ya wanafnx wa kke kpewa kratas na kuandka majna yao....max ya juu ni (....) na ya xchn ni (mja).....

Niiek list .....nawash...nawashw...nawashaaaa mieeee.....fupa.....fupa.....buyu moto hliiiii.....kna xcheupe daw anaumia kuntafta mie nan.....nyoooo....mie nko naw ktuo kmoj....na kesh ntaknnlia xchai.....


CC::

KATIBU MWAJIRI WILAYA NY'GANA
AFISA ELIMU
 
Mwalimu acha roho mbaya,wewe unalalama humu jukwaani Kama Nani?!!
Hao mashuhuda walishuhudia DYUDYU ikizama?!au walimshikia miguu?

Epuka kuwa chanzo Cha kumfanya binadamu mwenzio aishi kwa tabu hapa Duniani,mwache avune alichokipanda bila wewe KUHUSIKA Ila kwa hapa nawewe unaonekana una kawivu ka kike.
 
hao waalimu wanaotaka kubaka ni wapumbavu, hv hyo shule inauongozi kweli mpaka mwalimu anataka kubakia maabara, Af wazazi nao wamekua wajing mwanao anaraka kubakwa we unapeleka kesi kwa kiongozi wa chama?

i wish mwanangu afanyiwe hvo akianani nazaa na walimu wote hapo shule
 
Mwalimu acha roho mbaya,wewe unalalama humu jukwaani Kama Nani?!!
Hao mashuhuda walishuhudia DYUDYU ikizama?!au walimshikia miguu?

Epuka kuwa chanzo Cha kumfanya binadamu mwenzio aishi kwa tabu hapa Duniani,mwache avune alichokipanda bila wewe KUHUSIKA Ila kwa hapa nawewe unaonekana una kawivu ka kike.
aishi kwa taabu kivipi, upumbavu wake wa kutaka kubaka ndani ya maabara ndo akaliwe kimya?
 
Ndugu Mwalimu Asante kwa Taarifa ila ilitakiwa ukatoe ushirikiano kwa vyombo husika kulileta huku inaweza kutafsiriwa kama majungu au kashfa kwaajili ya kuwachafua waalimu wenzako ukizingatia hadi sasa hakuna ushahidi wowote unaowaweka hatiani.

Au mnabifu binafsi? Maana waalimu mnachekeana usoni ila mnazomeana moyoni
 
Back
Top Bottom