JamiiForums

Official JF Response
Nov 9, 2006
6,200
4,984
Wewe ni Mwalimu (Msingi, Sekondari n,k) na unahitaji mtu wa kubadilishana naye kituo cha kazi?

Weka ombi lako hapa na wengine watawasiliana nawe.

Ni muhimu kuzingatia kuwa, ukiweka baruapepe (email), namba yako ya simu mtandaoni haishauriwi (at your own risk). Njia bora inayopendekezwa na JamiiForums ni kwa PM (Private Messages) ndani ya JF - kwa usalama wako na usiri zaidi.

MUHIMU: Ni vema kusema UPO wapi na ungependa KWENDA wapi ili wale wenye kutaka kuwasiliana nawe wapate urahisi wa kukutafuta ili kurahisisha mchakato.

Tunakutakieni utumishi mwema.

JamiiForums

Bado nazidi kuwatahadharisha wana #JF juu matapeli wana vi SMS vya mtego mfano(Mimi nimefanikiwa au Mimi Afsa TAMISEMI nitakusaidia) NA wanadai uwatumie details zako ikiwepo check No. NA atadai kiasi nusu ya PESA mchakato ukiisha ummalizie.

MWL UKIONA SMS au MTU ANAKUAMBIA UMPE PESA JUA NI TAPELI siku sio nyingi nitaanika no Zao humu Mimi washawahi hata Kunitishia amani eti nawaharibia kisa niliwafungua watu macho kama hivi.

Mwl na watumishi wengine njia sahihi NA rahisi ni kutafuta wa kubadilishana nae NA kama huwezi kuweka tangazo humu JF nitafute kwa no 0756231236 au 0689270867 nitakusaidia kuweka TANGAZO.

Nawatakieni kazi njema mungu awatangulie sana.
 
Ndg yangu, baki hukohuko Moro Town mji wenye bahari ya Mindu hewa safi kutoka milima ya Uluguru, mambo yetu pale chipkizi, mengine pale nyota4, au ze club uje huku kwenye joto, vumbi, mabomu ya Mbagala hayakuisha alafu unapajua Dondwe nayo ni Temeke nauli kama 5,000 ukija mjini.

Ushauri hamia Kinole, Matombo, ni afadhali ukawa mkulima kiliko kuja huku.
 
Unaweza kufanya kazi Moro na bado ukaenda Dar as much as u like (approx 200 kms). Unless u have a very valid reason ya kuondoka Moro au ya kuwa Dar, ungebaki tu huko.

Ndio maana usishangae wengi wanatamani kubadilishana nawe waje hapo Moro!
Ndugu yangu, natamani sana ningebaki Moro bt nalazimika kuhama ili kuungana na familia coz nimeingia ktk ulimwengu wa wawiliwawili.
 
108 Reactions
Reply
Back
Top Bottom