Jamani wana JF naomba kupewa ufafanuzi juu ya hawa mawaziri 4, kuna baadhi ya vyombo vya habari waliandika na kutangaza kuwa mawaziri 3 walifukuzwa ila mmoja alijiuzuru, vingine vingine vilitangaza wamejiuzulu na vingine wakatangaza Rais katangaza kutengua uteuzi wao huku mwingine akitangaza kujiuzulu, PM alitangaza kuwa Rais anaweza kuwateua tena maeneo mengine, Je, aliyejiuzulu naye anawezateuliwa tena? je, waliofukuzwa watawezaje kuteuliwa tena? kama walijiuzulu kuna barua waliandika kuthibitisha kuwa wamejiuzulu? karibu kwa ufafanuzi