Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
DK. KABOUROU AJITOSA UENYEKITI KIGOMA
Makada saba wa CCM wamerejesha fomu kuchuana kugombea nafasi ya uenyekiti wa Mkoa wa Kigoma, akiwemo Dk. Aman Walid Kabourou.
Katibu wa CCM Mkoa wa Kigoma, Mohamed Nyawenga, alisema kuwa waliorejesha fomu hizo ni Azim Seleman Premji, ambaye anatetea kiti chake, Nashoni William Bidyangunze, William Ntahindala Ruturi, Nunu Mrisho Mwamba, Dk. Aman Walidi Kabourou, Michael Mbwano Ndereka na Edgar Mkosamali.
Alisema wagombea wote kwa pamoja walichukua fomu na kuzirudisha na kwamba hakuna tatizo lolote lililojitokeza katika uchukuaji fomu na urudishaji.