Walibya waliitwa Mapanya,Wanyarwanda wakaitwa Mende,TZ tunaitwa Vibaka,Maadui,Oil Chafu,Makapi, nk.

Ki Mun

JF-Expert Member
Oct 6, 2014
3,443
4,384
Historia ina mafundisho mazuri na ya wazi mno:

Jambo moja lilikuwa dhahiri mno machoni pa wananchi wengi wa Libya pale kiongozi wao alipofikia hatua ya kuhamaki na kuwaita wananchi wake MAPANYA na kwamba hatishwi na nguvu zao;Jambo moja pia lilikuwa dhahiri kwa wananchi wa Rwanda pale utawala wa Wahutu na wanamgambo wa Intarahamwe walipofikia hatua ya kuhamaki na kufikia hatua ya kuwaua wananchi wao wenyewe huku wakiwaita MENDE,

Kilichokuwa dhahiri ni kuwa saa ya ukombozi kwa wananchi wa Libya na wale wa Rwanda ilikuwa karibu mno,na kwa hakika ilifika japo kwa gharama kubwa mno.

Sasa nikiwa mzalendo ninayeipenda nchi yangu,nawaomba watanzania tuwe majasiri na tuwe wavumilivu kipindi hiki kuelekea October 25 hata tutakapoitwa VIBAKA,MAKAPI,OIL CHAFU,MAADUI na hatuwezi kujua pengine pia CCM watafikia hatua ya kutuita MAPANYA au MENDE(Inyenze).

LONG WALK TO FREEDOM...Alluta Continua!
 
CCM ya sasa kwa kuwa inakaribia 'kuaga dunia' uropokaji mwingi huo ulioutaja inaoufanya sasa hauna tofauti sana na mgonjwa anapokaribia kukata roho kwa namna anavyoropoka mambo mengi yasiyokuwa na msingi.

Hiyo tafsiri yake kwa kuwa tarehe 25/10/2015 imekaribia sana ambapo Sisiemu 'itaaga dunia' kwa hiyo hiyo hali ya hilo 'dubwasha' kuropoka ropoka haiepukiki.

Si tulishuhudia sisi wenyewe majuzi wakati Edward Lowassa alipokwenda kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa tiketi ya Chadema na Ukawa?

Eti yale mafuriko na umati wote wa watu waliomsindikiza Lowassa, gazeti la Uhuru linalomilikiwa na CCM liliripoti tukio hilo kwa kuropoka na kuweweseka kwa kuwaita waandamanaji wale maelfu kwa maelfu kuwa wote walikuwa vibaka!
 
Kuropoka mropoke nyie muisingizie CCM. Mnanchekesha!

Babu daktari wa kanoni padri Dr.W.Slaa yuko wapi?
 
Last edited by a moderator:
CCM wamebanwa pumzi,wamekosa hewa kwenye bongo zao,ndo maana wanaweweseka. Tusipoteze muda kutafuta maana mbaya ya misemo yao. Hawa ni watani kwenye siasa. Vyama vingi ni utamaduni wa nchi za magharibi, tutor mifano kutoka kwao mf siasa za USA na nchi za Ulaya. Nchi nyingi za Africa ziikuwa tawala za kifalme,ndo maana viongizi wa vyama tawala wanakuwa kama wafalme.
 
Kuropoka mropoke nyie muisingizie CCM. Mnanchekesha!

Babu daktari wa kanoni padri Dr.W.Slaa yuko wapi?

Hivi huyo babu unayemtaja kila post yako aliwahi kuku do enzi za ujana wako? Au ndiye alifungua duka nini?
Inaonyesha kama ungekuwa na mume (Nina hakika huna maana unasifa zote za kuua mume) ungemuita Dr kunako majambo na kuleta shida
 
Last edited by a moderator:
Hakuna kitu chochote kilichokuwa na mwanzo kikakosa kuwa na mwisho.

Ni dhahiri kutokana na uropokaji uliopitiliza wa maccm kwa sasa ni dalili za wazi kuwa hiko chama kikongwe kimekaribia sana 'kukata roho' na hivyo kukifanya chama hicho kifuate nyayo ya vyama vyenzake vikongwe kama vile KANU ya Kenya, UNIP ya Zambia na MCP ya Malawi vilikoenda.
 
Duh ni vibaya sana kujifananisha panya wa Libya na mende wa Rwanda ukiangalia hizo historia ni hatari kwa ustawi wa jamii
 
Acha uchochezi wa kifala wewe jaribu kuwa kimbelembele tukuzike na usauliwe baada ya October kuisha mavi kunuka wewe
 
Mwaka huu tumejiandaa kwa mabomu ya machozi na risasi za moto endapo haki yetu itaporwa hilo walitambuwe
 
Hapo hapo kwenye libya stop, niambie baada ya waasi kuchukua dola hali ya libya ilivyokuwa wakati wa gaddafi na ilivyo sasa ipi bora?

Matunda ya ukombozi wa walibya yako wapi? au ndio haya ya kuanza kuwepo kwa makundi ya kigaidi?
 
Back
Top Bottom