Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,519
Ahsante sana, ila Umesahau chumvi
Chumvi waweza kuongeza hata mezani lakini....
Ahsante sana, ila Umesahau chumvi
shortcut ANSWER.nilitegemea ungefunguka kidogo.Tumia mchele wa Jasmine...
Mcheleeee wa jasmine ukojeeee huoooooooshortcut ANSWER.nilitegemea ungefunguka kidogo.
swissme
Na maji ya moto.....Tumia mchele wa Jasmine...
mchele kutoka Tainland.Mcheleeee wa jasmine ukojeeee huooooooo
Basi mimi nimepatiaKama nimemuelewa mleta maada anaomba kufundishwa kupika wali uwe mtamu, sio mchele gani atumie. sasa mchele wa Jasmine au Thailand ukimpa kama kupika hajui utamsaidia nini.
Narudi kwenye mada.
Vifaa: Mchele nusu kilo, Nazi moja, chumvi kidogo
matayarisho: Kuna nazi, kisha chuja upate tui zito kiasi kama kidombe viwili. bandika tui lako zito jikoni, hakikisha moto si mkubwa sana
Pale linapoanza kuchemcha, linakua limeshajigawa tayari, yaani maji yanakua chini, tui juu, chota taratibu lile tui zito liweke pembeni, punguza maji yako yaliyobaki chini ambayo yanakua na weupe kiasi sababu ya Nazi. weka chumvi kisha tia mchele uliokwisha oshwa. hakikisha maji yanazidi kidogo tu kwenye mchele wako maana una tui ulilotoa mwanzo, utaliweka baadae utakapokaribia kuupalia.
Funika, moto uwe mdogo. Yale maji yakikauka, cheki kama mchele umeiva, kiasi. halafu weka lile tui ulilogawa mwanzoni, geuzi mchele wako, then palia kwa mkaa, juu na mwingine kidogo ubaki chini. Acha hivyo kwa muda wa nusu saa.
kama una oven basi washa oven, kawaida mimi natumia joto 180 deg, unakaa nusu saa. Wali tayari kwa kuliwa na mboga yoyote.
Hahahhahaa hakika huo lazima uwe wali mtamuWali mtamu unapikwa kwenye moto wa kuni na kufunikwa na mkaa juu yake ili uendelee kuiva taratibu
Wali mtamu lazima upikwe na tui la nazi halisi lililochanganywa vizuri kwa viwango sahihi kwenye maji yaliyochemka na iliki
Wali mtamu lazima mchele wake uwe ulishachambuliwa vizuri na kulowekwa kwenye maji kabla ya kupikwa
Wali mtamu lazima uwe na ukoko na matandu
Wali mtamu lazima upikwe na mwiko wa mti
Wali mtamu hupikwa na mwanamke msafi aliyeoga kabla ya mapishi na kuvaa kanga moja
Swali linalofuata utaulizwa jinsi ya kukuna nazi.Kama nimemuelewa mleta maada anaomba kufundishwa kupika wali uwe mtamu, sio mchele gani atumie. sasa mchele wa Jasmine au Thailand ukimpa kama kupika hajui utamsaidia nini.
Narudi kwenye mada.
Vifaa: Mchele nusu kilo, Nazi moja, chumvi kidogo
matayarisho: Kuna nazi, kisha chuja upate tui zito kiasi kama kidombe viwili. bandika tui lako zito jikoni, hakikisha moto si mkubwa sana
Pale linapoanza kuchemcha, linakua limeshajigawa tayari, yaani maji yanakua chini, tui juu, chota taratibu lile tui zito liweke pembeni, punguza maji yako yaliyobaki chini ambayo yanakua na weupe kiasi sababu ya Nazi. weka chumvi kisha tia mchele uliokwisha oshwa. hakikisha maji yanazidi kidogo tu kwenye mchele wako maana una tui ulilotoa mwanzo, utaliweka baadae utakapokaribia kuupalia.
Funika, moto uwe mdogo. Yale maji yakikauka, cheki kama mchele umeiva, kiasi. halafu weka lile tui ulilogawa mwanzoni, geuzi mchele wako, then palia kwa mkaa, juu na mwingine kidogo ubaki chini. Acha hivyo kwa muda wa nusu saa.
kama una oven basi washa oven, kawaida mimi natumia joto 180 deg, unakaa nusu saa. Wali tayari kwa kuliwa na mboga yoyote.
Hilo halifai kwa wanaumeSwali linalofuata utaulizwa jinsi ya kukuna nazi.
Tatizo ni kwamba aliyetoa maelezo ameweka kukuna nazi kama mojawapo ya hatua. Sasa huyo mgeni wa kupika wali kwa vyovyote hawezi kujua hilo la nazi, lazima aulize tu.Hilo halifai kwa wanaume