Davidgwakisa
Member
- Aug 29, 2011
- 8
- 0
Hizo barua za malalamiko mliziandikaje na vielelezo vipi mliambatanisha heslb?
Wakuu mi nimepata batch ya pili ingawa sijawahi kuwasilisha kitu hata kimoja kule bodi. Kwa wale wa UDSM nadhani cha muhimu ni kupeleka malalamiko kwa Daruso wako serious kweli kwenye kutetea maslahi ya mtanzania. Na pia naomba niwajulishe ambao bado hawajapata mkopo, msikate tamaa bado mapambano yanaendelea na Daruso wamesema bila kupata mikopo wanafunzi wote! Patachimbika, sio waliopata wala waliokosa wote ni kitu kimoja, tutadai haki za wanafunzi wote Tanzania.
Sio kweli kwamba zile form za mkopo ukiishajaza huwezi kubadilisha,kulikuwa na option kurekebisha sehemu ulizo jaza kimakosa ilimradi usichelewe kufanya hivyo kabla ya tarehe ya mwisho ya kutuma maombi hayo
kuna baadhi ya info ulikuwa huwez kuedit ukisha submit ikiwemo,kaz ya mzaz na swala la kifo. Mi mwenyewe hilo tatzo lilinikuta.
[h=2]UTOAJI MIKOPO KWA WANAFUNZI KATIKA MWAKA WA MASOMO 2011/2012[/h]Bodi ya Mikopo, kwa mwaka wa masomo 2011/2012, imekwishapanga kutoa mikopo kwa wanafunzi 24,628 kati ya wanafunzi 37,924wa mwaka wa kwanza waliodahiliwa katika duru ya kwanza (First selection).Hivyo, Bodi inapenda kuwataarifu wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza na Umma kwa ujumla kuwa bajeti ya ukopeshaji kwa mwaka wa masomo 2011/2012 imekatikia kwa idadi ya wanafunzi waliofanikiwa kupata mikopo kutoka kwenye kundi la "First selection" ambamo pia takriban wanafunzi 13,296 hawakuweza kupata mikopo. Hivyo, hakuna tena fedha za ukopeshaji kwa wanafunzi wengine.[h=2]3.0 HITIMISHO[/h]Waombaji hao wa mikopo na Umma kwa ujumla wanataarifiwa kuwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu katika duru ya pili au watakaochaguliwa katika duru nyingine zitakazofuatia kuwa hakuna mikopo itakayotolewa kwao kutokana na fedha za ukopeshaji kuishia kwa wale wa duru ya kwanza. Aidha, wakati wa udahili wao, wanafunzi hao wa duru ya pili na duru zilizofuatia, walielezwa bayana na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) kwamba hawatahusika na mikopo na hivyo udahili wao ni kwa njia ya kujigharamia wenyewe.Hivyo, wanafunzi husika wanashauriwa kuzingatia maelekezo hayo ya TCU na kuacha kuizonga Bodi kwa kufuatilia mikopo ambayo haitaweza kupatikana kwa mwaka huu wa fedha kutokana na bajeti ya ukopeshaji kuisha.Zimetolewa wiki 2 kuanzia tarehe 12/10/2011 kwa wale wanaoendelea na masomo ambao hawakujaza forms wafanye hivyo na kwa wale wanaotaka kujiunga upya na vyuo ambao walikosea kujaza ama forms au kushindwa kuambatanisha nyaraka hitajika wafike Bodi ya mikopo kurekebisha kasoro hizo
du haya akhsanteh kwa taarifa
wewe unasomaga tarehe hyo c ya mwaka 2011 au?
Hizo barua za malalamiko mliziandikaje na vielelezo vipi mliambatanisha heslb?