Wale wa madish ya ku-band na C- band pamoja na receiver pitia hapa

Mkuu naomba frqnce za hii kitu,nina kisimbuzi cha zuku hope itafanya kazi
Kumbuka Zuku Decoder ipo katika Pay Tv Subscription nadhani kisheria ni makosa kutumia decoder hiyo ikiwemo Azam, Ting, Startimes, n.k. Hivyo kama unapenda fta channels tatuta receiver ya FTA na dish kubwa upate kilicho cha halali!
 
Habari wajuvi mm niko dar nina receiver yng ya qsat q11g nmei update software sasa ina support powerVu, biss nk. Sasa nauliza kama ntanunua dish kubwa la FTA hata la ft6 naweza kufaidi hzo channels za moviez km HBO,Sony px nk
 
Habari wajuvi mm niko dar nina receiver yng ya qsat q11g nmei update software sasa ina support powerVu, biss nk. Sasa nauliza kama ntanunua dish kubwa la FTA hata la ft6 naweza kufaidi hzo channels za moviez km HBO,Sony px nk
Mi nilikuwa na qsat 11 na 13 ziliharibika mpaka mwisho nilipata CNN HBO SKYNEWS ALJAZEERA BBC

SONY HAZIFUNGUKI SASA HIVI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafuta modem ya huwaei pia iseti risiver yako ipokee donge. Au Kuna ka wife fulani ambayo ukiwa nayo unatumia hotsport ya simu
Mkuu nina swal msaada iv risiva kama gtmedia v7 8 na 9 naona zina support iptv youtube na cccam na pia zina wifi ndan yake kwa hapa tz inaweza kutumika kwa kutumia dish lip la cband au haya kama ya dstv ya ku band na channel zinaweza kuwa unlocked kama ukilipia cccam account maana naona weng wameconnect tu na internet wanachek epl na uefa champions league msaada wako mkuu nipate mwanga kabla cjainunua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zinauzwa sh ngapi hapa Tz na zinapatikana wapi??
Mkuu nina swal msaada iv risiva kama gtmedia v7 8 na 9 naona zina support iptv youtube na cccam na pia zina wifi ndan yake kwa hapa tz inaweza kutumika kwa kutumia dish lip la cband au haya kama ya dstv ya ku band na channel zinaweza kuwa unlocked kama ukilipia cccam account maana naona weng wameconnect tu na internet wanachek epl na uefa champions league msaada wako mkuu nipate mwanga kabla cjainunua

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahitaji kuweka lnb mbili ili nipate satelite mbili kutoka katika dish la sm 40 ,

Satelite nayotumia kwa sasa ni azer space 2, 45' je niunganishe na satelite ipi ili nipate FTA CHANNEL

sent from toyota Allex
 
Nahitaji kuweka lnb mbili ili nipate satelite mbili kutoka katika dish la sm 40 ,

Satelite nayotumia kwa sasa ni azer space 2, 45' je niunganishe na satelite ipi ili nipate FTA CHANNEL

sent from toyota Allex
...
Unaweza kupata fta 52°e ila utapata kikwazo cha size yako ya dishi na mahala ulipo ...
...
 
Naomba mnisaidie FTA freauency za azer space 2 tofauti na 11637v 300000



sent from toyota Allex
 
Mkuu nina swal msaada iv risiva kama gtmedia v7 8 na 9 naona zina support iptv youtube na cccam na pia zina wifi ndan yake kwa hapa tz inaweza kutumika kwa kutumia dish lip la cband au haya kama ya dstv ya ku band na channel zinaweza kuwa unlocked kama ukilipia cccam account maana naona weng wameconnect tu na internet wanachek epl na uefa champions league msaada wako mkuu nipate mwanga kabla cjainunua

Sent using Jamii Forums mobile app
Dish la futi nane au zaidi la bati hasa liwe la Prime

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MAWASILIANO YA SATELAITI
Satelaiti ni nini?
Ni mwezi (moon), sayari (planet) au mashine inayozunguka sayari au nyota.

Satelaiti ya kwanza kutengenezwa na binadamu, kupelekwa angani na kuwekwa katika obiti kuzunguka dunia iliitwa SPUTNIK 1.

Ilitengenezwa na Urusi na kupelekwa angani tarehe 4 Octoba, 1957. Satelaiti hii ilisafiri kwa mwendo wa kilomita 29,000(km) kwa saa ikitumia dakika 96.2 kukamilisha mzunguko wa dunia. Ikiwa angani ilituma mawimbi ya mawasiliano katika masafa ya 20.002MHz na 40.002MHz ambayo yalipokelewa na mitambo ya redio za amateur “amateur radio” duniani kote. Iliendelea kutuma mawimbi kwa siku 22 baadaye nguvu ya betri za transmita hizo ziliisha nguvu tarehe 26 Octoba, 1957.

Satelaiti hiyo ilianza kudondoka toka katika obiti angani na kuungua tarehe 4 Januari, 1958 baada ya kuingia kwenye anga ya dunia (atmosphere). Ilikaa angani kwa muda wa miezi mitatu.

Kuna satelaiti za aina ngapi?
Kuna satelaiti za aina mbili:

· Satelaiti za asili (Natural satellites) mfano; Dunia (Dunia huzunguka Jua) na Mwezi (mwezi huzunguka Dunia).

· Satelaiti za kutengenezwa na Binadamu (Artificial satellites).
View attachment 1084346

SATELAITI
Kuna aina ngapi za Satelaiti za kutengenezwa na binadamu?
Zipo satelaiti za aina nyingi na zimetengwa kwa matumizi mbalimbali.

· Satelaiti kwa ajili ya utafiti na uchunguzi sayari za mbali, galaxies na vitu vingine vinavyoelea angani (Astronomical satellites).
· Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kufanya mawasiliano (Communications Satellites).
· Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kuangalia hali ya hewa (Weather Satellites).
· Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya matumizi ya Ki-intelijensia na Kijeshi (Intelligence and Military Operations Satellites).

· Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kufanya utafiti wa dunia na vitu vingine vilivyoko angani mfano (Biosatellites ambazo hubeba viumbe hai kwenda angani kwa ajili ya utafiti).
· Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kufuatilia mabadiliko ya dunia na mazingira (Earth Observational Satellites).

· Ofisi za uchunguzi wa anga zinazoelea angani (Space Stations).
· Vifaa (mitambo) vyote vinavyokuwa angani katika obiti (Manned Spacecrafts / Spaceships).
· Satelaiti ndogo zinazounganishwa katika satelaiti nyingine kwa waya mwembamba unaoitwa tether (Tether Satellites)

· Satelaiti kwa ajili ya kutambua (mahali/ sehemu) katika uso wa dunia (positioning satellites) mfano GLONASS ni mfumo wa Urusi, GPS(Global Positioning System) ni mfumo wa Marekani, GALILEO ni mfumo wa Ulaya (European Union), China mfumo wao COMPASS kwa sasa unaitwa BeiDou, IRNSS ni mfumo wa India. Mfumo wa GNSS (Global Navigation Satellite System) huunganisha mifumo niliyoitaja hapo juu.

Satelaiti zote hapo juu zipo katika obiti (orbit) zilizopo katika umbali tofauti kutoka katika uso wa dunia. Obiti hizo ni:
LEO (Low Earth Orbit) umbali kuanzia kilomita 0 hadi 2000km juu ya uso wa dunia; baadhi ya satelaiti zilizopo katika ukanda huu ni Kituo cha Kimataifa cha Satelaiti kilichopo umbali wa kilomita mia nne (400km) kutoka katika uso wa dunia kinachoitwa ISS (International Space Station), satelaiti za uchunguzi wa dunia (earth observation satellites), satelaiti za upelelezi, Satelaiti zinazotumika katika "Remote Sensing"

KITUO CHA KIMATAIFA CHA SATELAITI (INTERNATIONAL SPACE STATION - ISS)KINACHOZUNGUKA DUNIA KATIKA UMBALI WA KILOMITA 400km (umbali kati ya 330km na 435km kutoka ardhini) KUTOKA ARDHINI.

Taarifa nyingine:
Kilirushwa angani tarehe 20 Novemba, 1998
Kinazunguka dunia. Spidi yake inafika hadi 28,800km/saa. (Leo tarehe 30 Desemba, 2017, kati ya saa 1:00 hadi saa 1:10) usiku (Muda wa Afrika Mashariki); ((19:00 to 19:10) PM GMT + 3) kimesafiri kwa spidi kati ya 27,613km/saa hadi 27,617km/saa) katika umbali wa kati ya kilomita (400)km na (406)km juu ya uso wa dunia).

DOKEZO:
Kilomita 400km na 406km ni umbali kutoka ardhini hadi kilipopita kituo hicho (Altitude). Maana yake kituo hicho kilipanda kwenda juu katika muda huo kutoka kilomita 400km hadi kilomita 406km.
Kiligharimu dola za Kimarekani Bilioni 150 (150 Billion Us Dollar).
Kilitengenezwa kwa ushirikiano wa Marekani, Urusi, Japan, Canada na baadhi ya nchi za Ulaya.
.
MEO/ICO (Medium Earth Orbit/Intermediate Circular Orbit) umbali kati ya kilomita 2000km na 35786km juu ya uso wa dunia; baadhi ya satelaiti zilizopo katika ukanda huu ni satelaiti za utambuzi wa mahali katika uso wa dunia namaanisha za GPS (kilomita 20,200km), GLONAS (19,100km), GALILEO (23,222km), satelaiti zinazotumika kutuma na kupokea mawasiliano kaskazini mwa dunia (northern pole) na kusini mwa dunia (southern pole).




View attachment 1084352


MIFUMO MBALIMBALI YA SATELAITI
GEO (Geostationary Earth Orbit): Umbali wa kilomita 35,786km juu ya uso wa dunia katika Ikweta. Satelaiti zilizopo katika umbali huu huzunguka kwa kasi sawa na kasi ya dunia.

Mfano wa satelaiti zilizopo katika umbali huu ni zile za mawasiliano ya Televisheni, Data (intaneti), redio, mawasiliano ya simu (mfano Thuraya ambayo hutumia satelaiti mbili ambazo ni Thuraya 2 na Thuraya 3 ambazo hutumika kutoa huduma za mawasiliano ya simu za satelaiti "satellite phones" katika bara la Asia, Afrika, Ulaya na Australia ), mawasiliano ya kiintelijensia, mawasiliano ya kijeshi, satelaiti za uchunguzi wa hali ya hewa, satelaiti za kurekebisha data katika uso wa dunia (mfano OmniSTAR).

Dokezo: Satelaiti zote zilizopo katika umbali wa kilomita 35,786km juu ya uso wa dunia katika Ikweta (latitudo 0) huzunguka sawa na kasi ya dunia. Satelaiti zilizopo katika umbali huo juu ya uso wa dunia nje ya mstari wa Ikweta haziwezi kuzunguka kwa kasi sawa na kasi ya dunia.

HEO (High Earth Orbit): umbali zaidi ya kilomita 35,786km. Satelaiti zilizopo katika umbali huu huzunguka kwa kasi ndogo kuliko kasi ya dunia. Mfano wa satelaiti iliyoko katika ukanda huu ni VELA 1A.

Satelaiti tunazozitumia kupokea mawimbi ya televisheni / redio zipo katika kundi la Satelaiti za Mawasiliano (Communication Satellites). Satelaiti hizi za mawasiliano tunazozitumia kupitisha mawasiliano ya televisheni na redio (zipo katika Geosynchronous Orbit) umbali wa kilomita 35,786km kutoka ardhini katika Ikweta na husafiri kwa kasi sawa na kasi ya dunia.

Mawasiliano kutoka katika satelaiti za mawasiliano zilizopo katika "Geosynchronous Orbit"(GSO).
KUTAFUTA CHANELI MBALIMBALI ZA TELEVISHENI / REDIO KUTOKA KATIKA SATELAITI MBALIMBALI ZA MAWASILIANO ZILIZOPO KATIKA GEOSYNCHRONOUS ORBIT (GSO); OBITI AMBAYO KWA MAJINA MENGINE HUITWA (PARKING ORBIT au CLARKE BELT au GEOSYNCHRONOUS ARCH).

Kwa kuwa dunia ina umbo la duara si rahisi watu wote tulioopo katika uso wa dunia (namaanisha mabara yote) tukatumia satelaiti moja kupokea mawasiliano toka katika satelaiti. Kusema hivi namaanisha mfano satelaiti tunayoitumia sana (IS 906 @ 64.2E (nyuzi za longitudo 64.2 Mashariki mwa Greenwich) katika ukanda wetu Tanzania ikiwemo haiwezi kufikisha mawimbi yake Marekani kwa sababu Marekani wanakuwa upande mwingine wa uso wa dunia (they are below the horizon of the reach of this satellite) hii ni vile vile kwa satelaiti zinazoimulika Marekani hata sisi hatuwezi kupata mawimbi yake.

Mfano baadhi ya satelaiti za Intelsat (IS 902, IS 906, IS 904, IS 10, IS 17, IS 907 na nyinginezo zilizoko juu ya usawa wa Afrika na bahari ya Hindi na wao wakitaka kupokea mawasiliano yake wanatumia kituo chao kilichopo Afrika Kusini au vituo vingine.

Baadhi ya satelaiti ambazo nilishazifanyia utafiti na mawimbi yake yanafika hapa Tanzania zipo kati ya nyuzi za longitudo 27 Magharibi mwa Mstari wa Greenwich na nyuzi za longitudo 85 Mashariki mwa Mstari wa Greenwich. Dishi linalozunguka (horizon to horizon) linaweza kupata chaneli mbalimbali kutoka satelaiti hizi kwa kuzunguka kupitia satelaiti moja baada ya nyingine (from 27 West to 85 East). Kadri unavyoelekea Magharibi ya dunia ndivyo utakavyozidi kupata satelaiti zilizopo Magharibi ya dunia huku ukipoteza za Mashariki ya dunia; na kinyume chake (and vice versa).

Baadhi ya satelaiti ambazo zinazunguka kwa kasi sawa na kasi ya dunia; ambazo zipo katika "Geosynchronous Orbit or Parking Orbit" zinazopatikana katika eneo letu (Tanzania na nchi za jirani zimeorodheshwa chini. Satelaiti hizi hutumika kwa mawasiliano mbalimbali mfano Data /Internet, Televisheni, Radio, Mawasiliano ya Ki-intelijensia, kijeshi na mawasiliano mengine.

Intelsat 907 @ 27.5W: VoA TV, Alhurra TV Iraq, Alhurra TV Europe, RTG (Guinea),
Intelsat 905 @ 24.5W: Nile Drama, Syria 1,
SES 4 @ 22W: Bolivia Mux, Truth TV, TV Universal,
NSS7 @ 20W: CNN, TBN, Emmanuel TV, MBC (Malawi), Lesotho TV, TPA, Trinity Broadcasting
Intelsat 901 @ 18W: Ethiopia Educational Media Agency
Telstar 12 @ 15W:

Nilesat 201 @ 7W: DW Arabia, BBC Arabic, Abu Dhabi, Abu Dhabi Sport 1, Dubai Sport 2, DM, TV, National Geographic Channel,
Intelsat 10 - 10W @ 1W: BBC World Service, RTS1 (Senegal)
Rascom QAF 1R @ 2.8E: Libya Satellite TV, Libyan Mux, RTNC, Digital Congo (Congo)
SES 5 @ 5E: ZUKU, SABC 1, SABC 2, SABC 3, ETV, STARTIMES

Eutelsat 7A @ 7E: Record Mozambique, MBC 1, MBC 2, CRTV, RTS 1 (Senegal), BBC Persian, ORTM, Raha Tv, TPA Internacional, VoA TV Persian, Azam TV,
Eutelsat 10A @ 10E: Startimes, Agape TV Network,
Amos 5 @ 17E: Zambia Mux, Reuters Live, Doordarshan, Kingdom Africa TV, Bible Exploration TV, Fashion TV Europe, TING (Tanzania), Continental, (Amos 5@ 17E ilipoteza mawasiliano na ardhini (duniani) tarehe 22/11/2015).

Eutelsat 36A @ 36E: TING Channels (Tanzania), NTV Plus, Afrique TV,
Eutelsat 36B @ 36E: CCTV News, CCTV 4 Europe, Multichoice DStv channels
NSS 12 @ 57E: ZUKU, KBC- Kenya, Family TV - Kenya, ETV (Ethiopia), VoA TV Africa, American Embassy tv Network etc.),

Intelsat 904 @ 60E: Uganda Mux, Kenya Mux, NTV (Kenya), KBC Channel 1 (Kenya), TBC 1, NTV, Uganda (Kenya), Swazi TV, ZNBC,
Intelsat 902 @ 62E: NTV (Kenya), Citizen TV (Kenya), SABC 1 - 3 (South Africa), Sky International,
Intelsat 906 @ 64.2E: ITV, EATV, CAPITAL, TBC, STARTV, TVM (Mozambique), UBC (Uganda), Chanel 10,

View attachment 1084353

Picha hapo juu ni Intelsat 906 @ 64.2E inakofikisha Mawimbi yake katika masafa ya C Band (Hemi, Zonal & Global Beams)
Intelsat 17 @ 66E: HMTV, Captain TV, ABN (India), V6 News, DStv, Bunge la Jamhuri ya Tanzania

Picha chini ni sehemu duniani ambapo mawasiliano ya satelaiti hii (IS 17) yanafika.

View attachment 1084356
Picha hapo juu ni sehemu mawasiliano ya satelaiti hiyo yanapofika katika masafa ya C Band (C Band Landmass Coverage)
View attachment 1084357
Picha hapo juu ni sehemu mawasiliano ya satelaiti hiyo yanapofika katika masafa ya Ku Band (African Ku Band Beam); (Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mawasiliano yao yapo katika "beam" hii).
View attachment 1084359

Picha hapo juu ni sehemu mawasiliano ya satelaiti hiyo yanapofika katika masafa ya C Band (C Band Western Hemisphere Coverage).
View attachment 1084360

Picha hapo juu ni sehemu mawasiliano ya satelaiti hiyo yanapofika katika masafa ya C Band (Global C Band Coverage).

View attachment 1084368

Picha hapo juu ni sehemu mawasiliano ya satelaiti hiyo yanapofika katika masafa ya Ku Band (Europe and Middle East Ku Band Coverage)

View attachment 1084371


Picha hapo juu ni sehemu mawasiliano ya satelaiti hiyo yanapofika katika masafa ya Ku Band (Russian Ku Band Coverage).

Intelsat 20 @ 68.5E: Indiasign, NHK World TV (Japan), Peace TV Bangla, India TV, South Korea Mux, CTS (South Korea), Hope TV India, YTN World, VTV (India), Peace TV, God TV Africa, Africa Unite TV, ABN (Nigeria), Messiah TV, Citizen TV (Kenya), UB (South Africa), Emmanuel TV, CTV, 3ABN International, Press TV, CCTV, EWTN, DStv South Africa,

Eutelsat 70B: Canadian Forces Radio & TV,

Intelsat 22@72.1: Family TV (Kenya), KBC Channel 1, Citzen TV, GBS

ABS 2 @ 75E:

Apstar 7 @ 76.5E: ERT World, Channel 9 (Bangladesh), God Asia,

Thaicom 5 @ 78.5E: Somalia National TV, TV5 Cambodia, T Sports Channel, Shop Thailand, Spring TV News, MRTV, na nyinginezo.

Thaicom 6@78.5E:

Express MD1 @ 80E:

Dishi linaloweza kufanya kazi hii vizuri katika C Band ni la kipenyo kuanzia futi sita 6ft, 8ft, 10ft, 12ft na kuendelea (hasa kuanzia futi kumi 10ft na kuendelea kutegemea na nguvu ya mawimbi unayoyapokea.).
Kwa madishi ambayo hayazunguki (fixed satellite dishes) inabidi ufunge madishi mengi kila dishi liwasiliane na satelaiti yake. Ndio maana ukienda katika vituo vya televisheni/ redio mfano ITV, Startimes na vingine unakuta madishi mengi ya kupokea mawasiliano (chaneli) mbalimbail kutoka katika satelaiti tofauti tofauti.

Masafa ya Mawimbi ya Televisheni / Redio kwenda (uplink frequencies) katika satelaiti katika eneo letu ITU Region 1 (Afrika, Ulaya, Uarabuni na Urusi).

Masafa yanayotumika kupeleka mawimbi katika satelaiti toka vituo vya Televisheni/Redio vinavyotumia Ku Band katika ukanda wetu (ITU Region 1) ni kati ya 14.0GHz - 14.5GHz.

Masafa yanayotumika kupeleka mawimbi katika satelaiti toka vituo vya Televisheni/Redio vinavyotumia C Band katika ukanda wetu (ITU Region 1) ni kati ya 5.850GHz - 6.425GHz.

Masafa ya Mawimbi ya Televisheni / Redio toka katika satelaiti (downlink frequencies) katika eneo letu ITU Region 1 (Afrika, Ulaya, Uarabuni na Urusi)

Mawasiliano ya Televisheni na Redio tunazozipokea toka katika satelaiti yapo katika "Electromagnetic Spectrum" kati ya 3GHz - 30GHz.

Kwa C Band masafa yanayotumika kutuma mawasiliano toka katika satelaiti hadi kwenye madishi tunayoyatumia ni 3.7GHz - 4.2GHz.

Kwa Ku Band masafa yanayotumika kutuma mawasiliano toka katika satelaiti hadi kwenye madishi tunayoyatumia ni 10.7GHz hadi 12.75GHz.

a) CHANELI ZA MULTICHOICE/ DSTV
Kutafuta chaneli za Multichoice/ Dstv kutoka katika satelaiti Eutelsat 36B iliyopo nyuzi za longitudo 35.9 (Mashariki mwa Mstari wa Greenwich) wanayoitumia kutupatia chaneli zao. Hii ni kwa sehemu ambazo satelaiti hii inafikisha mawimbi yake Tanzaniaikiwa mojawapo.

Eutelsat 36B iliyopo nyuzi za longitudo 35.9 Mashariki mwa mstari wa Greenwich.

Satelaiti hii iko wapi?

Satelaiti hii ipo katika nyuzi za longitudo 35.9°E Mashariki mwa Mstari wa Greenwich.

Ni satelaiti inayomilikiwa na kampuni ya Eutelsat; ilitengenezwa na Kampuni inayoitwa Thales Alenia Space iliyopo katika bara la Ulaya (ina ofisi Ufaransa, Italia, Ubelgiji, Hispania na Califonia - Marekani). Ilipelekwa angani na kuwekwa katika obiti 36,485.7km toka ardhini (ipo katika nyuzi za longitudo 35.9°E) juu ya Ikweta tarehe 24/11/2009 na kifaa kinachoitwa Proton Rocket. Muda wake wa kutumika ikiwa angani ni miaka kumi na tano (miaka 15) maana yake mwaka 2009 + miaka 15 = mwaka 2024.

Kwa hiyo muda wa kuitumia satelaiti hii ni hadi mwaka 2024. Eutelsat 36B imeambatanishwa na Eutelsat 36A ambayo ipo katika nyuzi za longitudo 36 Mashariki mwa mstari wa Greenwich (zilivyowekwa ni kama satelaiti moja.). Ikiwa katika obiti yake inafikisha mawimbi yake Afrika, Ulaya, Urusi, Maeneo ya Uarabuni na katikati ya bara la Asia.

Eneo katika bara la Afrika ambalo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake "Eutelsat 36 B Footprints on Sub Saharan Beam"


View attachment 1084372

Picha hapo juu inaonesha maeneo ambayo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake; pembeni ni kiwango cha mawimbi "signal power" toka katika satelaiti (nguvu ya mawimbi haiko sawa kwa maeneo yote ambayo satelaiti hii inafikisha mawimbi yake. Sehemu nyingine mawimbi yana nguvu sana na sehemu nyingine nguvu ya mawimbi ni ya kawaida.

Eneo katika bara la Ulaya ambalo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake "Eutelsat 36 B Footprints on Central European Beam"

View attachment 1084373

Eutelsat 36B Central European Beam
Eneo katika bara la Asia na Ulaya ambalo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake "Eutelsat 36 B Footprints on Eutelsat 36B Eurasia beam"


View attachment 1084377

Eutelsat 36B Eurasia beam

Eneo katika Urusi ambalo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake "Eutelsat 36 B Footprints on Eutelsat 36B Russia beam"

View attachment 1084378

Eutelsat 36B Russia beam

Eneo katika bara la Afrika ambalo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake "Eutelsat 36 B Footprints on Eutelsat 36B Southern Africa beam"


View attachment 1084379

Eutelsat 36B Southern Africa beam

Vifaa muhimu vinavyohitajika wakati wa kutafuta chaneli kutoka katika satelaiti yoyote:

Spectrum Analyzer inayoweza kuonyesha mawimbi (electromagnetic radiations) hadi 15GHz, 20GHz au 30GHz (IF Range 950MHz to 2150MHz). Spectrum analyzer huonesha picha ya mawimbi, masafa yake, nguvu iliyoko katika mawimbi na hata kama mawimbi yanaingiliana yanaonekana. Kwa ufupi Spectrum Analyzer huonesha kila kitu (picha kamili ya mawimbi katika masafa mbalimbali).

Mitambo hapo juu inaitwa Spectrum Analyzer. Vifaa hivi hutusaidia kuona, kusikia, kupima na kuchunguza tabia za mawimbi katika "Electromagnetic Spectrum". Zipo Spectrum Analyzer za uwezo tofauti wa kuona mawimbi tokea 20Hz hadi 3GHz, 10GHz, 26GHz, 67GHz na kuendelea.

Field Strength meter (huonesha nguvu ya mawimbi husika).

Satellite Finder (zipo za digitali na analojia) baadhi ya mita za analojia hutoa mlio fulani ambao wakati unatafuta signal mlio huo huongezeka kadri mawimbi ya masafa unayoyatafuta yanavyoongezeka. Satellite Finder za digitali baadhi huonesha mawimbi kidijitali na nyingine huonesha mawimbi na picha. Satellite Finder za analojia hufungwa kati ya (LNB/ LNC (Low Noise Block) / Low Noise Converter respectively) na risiva/king'amuzi na za dijitali hufungwa moja kwa moja katika LNB/LNC.

Compass kwa ajili ya kuonesha uelekeo wa dishi (kuzungusha dishi kuelekea magharibi, kaskazini mashariki, kaskazini magharibi, mashariki, kusini mashariki, kaskazini mashariki, kusini, kaskazini, kutegemea sehemu ulipo duniani kutoka satelaiti unayoitafuta. Kwa lugha ya kitaalamu "Azimuth Angle". Dishi lazima lielekezwe satelaiti ilipo.

Mfano kama satelaiti ni Intelsat 906 (nyuzi 64) dishi linaelekea Kaskazini Mashariki (tukiwa Dar es Salaam) kwa sababu satelaiti hiyo ipo juu ya bahari ya Hindi jirani na maeneo ya India. Kwa maeneo mengine dishi linaweza kuelekea uelekeo tofauti kwa sababu inategemea anayefunga dishi alipo katika uso wa dunia kutoka katika satelaiti hiyo.

Inclinometer kwa ajili ya kupima ulalo au mwinuko wa dishi "elevation angle" (mzunguko wa dishi juu na chini).

Pimamaji (Spirit Level): Pimamaji ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba dishi linakaa katika msawazo; na kama unafunga katika bomba hakikisha bomba linasimama wima (upright) nyuzi 90).

TV ndogo kwa ajili ya kuonesha picha (kama unatumia Satellite Finder, King'amuzi au Risiva ya kawaida).

Vifaa vinginevyo (toolbox).

Angalizo:
Kama huna Spectrum Analyzer unaweza kutumia Field Strength Meter (Signal Strength Meter) kama huna vyote hapo unaweza kutumia Satellite Finder pamoja na King'amuzi au satelaiti risiva ya aina yoyote.

Kutafuta chaneli za Multichoice/Dstv.
Wakati wa kutafuta chaneli (signal) za Multichoice/ Dstv mafundi wengi hutumia ving'amuzi vya Multichoice/Dstv.

Ukifika site bila King'amuzi cha Dstv ufanyeje?

Wazo mbadala:
Unaweza kutumia satelaiti risiva yoyote; wakati wa kutafuta chaneli chagua satelaiti yoyote ambayo imesetiwa (satelite setup) katika Masafa ya LNB: Low Frequency 9750MHz na High Frequency 10700MHz. Haya ni masafa yanayotengenezwa na sakiti inayoitwa "local oscillator" iliyopo katika king'amuzi au risiva.

Kabla ya yote tuone hatua muhimu ambayo hufanyika katika LNB:

LNB ni nini?
Kirefu cha LNB ni "Low Noise Block".
Ni kifaa kinachofungwa katikati ya dishi (at the focus of the dish) kwa madishi yanayoitwa Prime Focus Dishes (Madishi ya C Band; madishi ya futi sita na kuendelea) na pembeni mwa dishi kwa madishi ya Ku Band (Offset dishes; madishi ya sentimita 60 na kuendelea). Kazi yake kubwa ni kupokea mawimbi kutoka katika satelaiti, kuyaongeza nguvu, kuyapunguza masafa (downconvert), na kisha kuyapeleka katika king'amuzi au risiva ambayo huyatengeza na kutoa RF (Radio Frequency), Video Baseband (Video Signal) na Sauti (Audio). Mawimbi yaliyopatikana katika king'amuzi au risiva yakiunganishwa katika televisheni tunapata picha na sauti.

Katika Ku Band masafa televisheni na redio yanayofika katika dishi ni kuanzia 10.6GHz au 10.7GHz hadi 12.75GHz.

Aina za LNB.
Zipo LNB za aina nyingi. Baadhi ya LNB zinazotumika katika mawasiliano ya televisheni kwa kuzitofautisha kutokana na Masafa.
1. LNB za Ku Band na
2. LNB za C Band.
3. LNB za Ka Band

a) LNB za Ku Band (LNB zilizoandikwa 10.7GHz hadi 12.75GHz); baadhi ya LNB za Ku Band
zimeandikwa 10.6GHz hadi 12.75GHz. Ni LNB zinazofanya kazi ya kupokea mawimbi ya
Televisheni / Redio kutoka katika satelaiti kuanzia 10.6GHz /10.7GHz hadi 12.75GHz.
Kuna aina mbalimbali za LNB za Ku Band baadhi yake ni LNB zinazotoa "output moja",
"output mbili", "output nne", "output nane", Quatro na nyinginezo. LNB za Quatro haziwezi kuunganishwa
moja kwa moja katika king'amuzi au risiva; inabidi ziunganishwe katika vifaa hivyo kupitia vifaa
vinavyoitwa "multiswitch"

Madishi yanayotumika kupokea masafa katika Ku Band (kwa madishi makubwa zaidi ya aina hii (offset ku band) mfano kuanzia 180cm unaweza kufunga LNB ya C Band





View attachment 1084385

Picha hapo juu inaonesha dishi la kupokea mawasiliano ya televisheni katika Ku Band. Yapo madishi ya ukubwa tofauti kuanzia kipenyo cha sentimita 30, 45, 60, 90, 120,180 na kuendelea. Katika ukanda wetu (Tanzania na nchi za jirani) tunatumia zaidi madishi ya sentimita 90cm.

Ni vizuri zaidi kutumia Madishi ya kipenyo cha sentimita 120cm kwa sababu mawimbi katika masafa ya Ku Band huathiriwa sana na mvua (hunyonywa na matone ya mvua) na kusababisha picha kukatikakatika wakati na wakati mwingine picha kupotea kabisa wakati mvua zinaponyesha.
LNB za Ku Band

View attachment 1084389
LNB ya Ku Band ya njia moja (Single output Ku Band LNB)

View attachment 1084392
LNB ya Ku Band ya njia nane (Eight output octo LNB). Kila njia "Output" inajitegemea.

b) LNB za C Band:
Ni LNB zinazofanya kazi ya kupokea mawimbi ya Televisheni / Redio kutoka katika
satelaiti kuanzia 3.6GHz hadi 4.2GHz. Zipo za aina nyingi mfano
1. Single Solution C Band LNB. Hii ni LNB yenye output moja lakini inauwezo wa kugawa
mawimbi (satellite signal kwa zaidi ya risiva moja).
2. LNB za output moja, output mbili, output nne na kuendelea.
ITAENDELEA.....................................


Quatro
Hii ipoje?
 
Kwema wadau, pale soko la AliExpress vinauzwa ving'amuzi kibao. Inawezekana kununua hivyo ukafunga hapa Tanzania na vikafanya kazi?
Asante
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom