Wale wa madish ya ku-band na C- band pamoja na receiver pitia hapa

Dekoda zake zimandika digital video broadcasting
Decoder au receiver (king'amuzi) ni kifaa ambacho kinaconvert mawimbi kiliopokea kwenda mfumo mwingne. Niweke swali vizuri kwako, je satellite zilizopo juu zinatuma mawimbi ya analog au digital kuja duniani?
 
Decoder au receiver (king'amuzi) ni kifaa ambacho kinaconvert mawimbi kiliopokea kwenda mfumo mwingne. Niweke swali vizuri kwako, je satellite zilizopo juu zinatuma mawimbi ya analog au digital kuja duniani?
Si mtaalamu sana,nahisi ni digital kwani visimbuzi vingi vya DTT hua vimeandika hivyo
 
Hii ndio tunaita elimu mkuu, asante kwa bandiko hili. Nitakuwa nalipitia taratibu ili kuongeza maarifa zaidi kwenye ulimwengu wa satellite dish na receivers.

Kwa sasa nimenunua FTA receiver yenye uwezo wa powervu, je unaweza kuelezea hii terminology ya powervu na jinsi inavyofanya kazi?

Najaribu sana kuunganisha wifi dongle ili niweze ku-unlock baadhi ya chaneli kwa kutumia internet.
Lock mojawapo wanayotumis kufungia channel. Kuhusu internet kuna vitu vinahitajika iweze kuwa active
 
Nimeonapicha hii mtandao sasa naomba kuulizanamna ya kuipata hiyo channel ni lazima uwe na receiver y mpg4 au ht mpg2


Vp receiver y wiztech8030 ipo vzr ??
IMG-20190601-WA0005.jpeg
 
Eli
Inaendelea sehemu ya pili ya ufafanuzi
LNB ya C Band inayotoa njia mbili (2 output LNB)

Kwa kawaida mawimbi yanayotoka katika satelaiti yana masafa makubwa sana kiasi kwamba ni shida kupita katika waya ( kadri masafa yanavyoongezeka ndivyo inavyozidi kuwa rahisi kwa mawimbi kupotea katika waya) hivyo lazima masafa hayo yapunguzwe ndio yaweze kupita katika waya.

LNB ya Ku Band (10.6GHz / 10.7 hadi 12.75GHz) hufanya kazi sawa na LNB za C Band tofauti yake ni kwamba LNB za Ku Band zinafanya kazi katika masafa makubwa ukilinganisha na LNB za C Band (3.6GHz hadi 4.2GHz).


Jambo muhimu sana la kuzingatiwa.
Mawimbi yanayotumwa katika satelaiti na kupokelewa na madishi majumbani na maofisini mwetu huwa yana namna yanavyokaa. Kuna yanayokuja katika mfumo wa koili (coil) na yanayokuja katika mstari myoofu ambayo yanakuja wima (Vertically Polarized) na mengine yanakuja yakiwa yamelala (Horizontally Polarized)

Mawimbi yanayokuja mfumo wa koili:

Yanakuja katika coil za aina mbili tofauti ambazo ni:
a) Right Circular na
b) Left Circular.

Hii inamaana vituo vya televisheni /radio hutuma katika satelaiti mawimbi ambayo husafiri katika mfumo wa:
a) Left Circular Polarized
b) Right Circular Polarized
c) Horizontal
d) Vertical

Mfano:
Tuchukue mfano wa chaneli za C Band ambazo tunazipata kutoka katika satelaiti inayoitwa IS 906 iliyopo nyuzi za longitudo 64.2 Mashariki mwa mstari wa Greenwich ambayo tunaitumia sana hapa kupokea mawasiliano ya televisheni na redio ya vituo vilivyoko hapa kwetu ambavyo ni:
Chaneli 10, TBC, Startv, ITV, Capital, EATV, TVM (Mozambique), na nyinginezo.

ITV, CAPITAL na EATV mawimbi yao yanabebwa na Frequency Moja (3641MHz) na yanakuja katika mfumo wa koili (coil) katika kundi la "Right Circular - R" na TBC (3891MHz), Startv (3884MHz) mawimbi yao ni "Left Circular (L)"

LNB hupokea mawimbi yote (Left Circular Polarized, Right Circular Polarized, Vertical Polarized na Horizontal Polarized) ila hufanyia kazi mawimbi ya aina mbili tu ambayo ni Vertical Polarized na Horizontal Polarized.


Kuna kifaa (kinafanana na kipande cha sabuni) mbacho wakati wa kufunga dishi lazima ukichomeke ndani ya LNB (ndani ya feedhorn) kwa kukatiza katikakati ya antena mbili zilizoko katika LNB ya C Band au unakichomeka kilale sambamba na antena mbili zilizoko katika LNB (antena moja ni kwa vertically polarized waves na nyingine ni kwa horizontally polarized waves). Kifaa hiki kinaitwa "Teflon Slab"

"Teflon Slab" hubadilisha mawimbi yanapokatiza katika feedhorn; Right Circular polarized waves hubadilishwa kuwa "Vertical" na Left Circular polarized waves hubadilishwa kuwa "Horizontal".

Kwa mawimbi ambayo ni "linear" (Vertical na Horizontal) hakuna haja ya kuweka Teflon Slab katika LNB.
Mfano chaneli za Asia tunazozipata toka satelaiti IS 10 iliyopo nyuzi za longitudo 68.6 Mashariki mwa mstari wa Greenwich haziitaji kuweka Teflon Slab katika LNB yake.
Mawimbi ya ITV, CAPITAL, EATV ambayo ni Right Circular hubadilishwa na Teflon Slab kuwa Vertical na Mawimbi ya TBC, Startv, ambayo ni Left Circular hubadilishwa na kuwa Horizontal.

Nini sababu kubwa ya kutuma mawimbi katika njia tofauti tofauti? Namaanisha kwa nini Left Circular, Right Circular, Vertical na Horizontal?

Sababu kubwa ya kufanya hivi ni "Frequency Reuse" mawimbi ya masafa katika frequency moja mfano 3642MHz - Right Circular ni tofauti na 3642MHz - Left Circular hivyo frequency moja inaweza kutumika zaidi ya mara moja bila kuingiliana kwa kutenganishwa na "Polarity".

Vertical na Horizontal
Katika LNB kuna antena mbili; moja kwa ajili ya kuyapokea mawimbi ya vertical na nyingine kwa ajili ya mawimbi ya horizontal. Antena ya Vertical hupokea mawimbi ambayo ni Vertical na kuyapeleka katika sakiti ya Vertical na Antena ya Horizontal hupokea mawimbi ambayo ni Horizontal na kuyaeleka katika sakiti ya Horizantal.
Sakiti ya Horizontal hutumia umeme wa Voti 18V na sakiti ya Vertical hutumia Voti 13V. Umeme huu hutoka katika risiva. Kwa hiyo waya unaounganisha risiva na LNB hupeleka umeme wa voti 13V kwa sakiti ya vertical na voti 18V kwa sakiti ya Horizontal na vilevile hubeba mawimbi (Intermediate Frequency) kutoka katika LNB kwenda katika risiva.

Unapochukua rimoti ya risiva ya satelaiti na kuweka chaneli mfano; CAPITAL televisheni risiva hupeleka voti 13V katika LNB kwa sababu Capital Televisheni mawimbi yake ni Right Circular ambayo hubadilishwa na Teflon Slab kuwa Vertical. Ukichukua rimoti na kuweka chaneli ya Startv (Left Circular ambayo hubadilishwa na kuwa Horizontal) risiva hupeleka voti 18V katika LNB.

Kwa wanaounganisha risiva zaidi ya moja:
Kama tulivyoona hapo juu Vertical ni Voti 13V na Horizontal ni Voti 18V. Ukiunga risiva zaidi ya moja na kutumia LNB ambazo si "Single Solution" (LNB zenye uwezo wa kugawa mawimbi na kuyasambaza kwa risiva mbalimbali) kuna wakati baadhi ya chaneli zitagoma kuonekana.

Kwa nini baadhi ya chaneli zitagoma kuonekana?
Hii ni kwasababu katika risiva ya kwanza mtu akichagua EATV (Right Circular - Vertical = 13V) risiva yake itapeleka Voti 13V katika LNB, na mwingine akichagua TBC (Left Circular - Horizontal = 18V) risiva yake itapeleka Voti 18V katika LNB hiyohiyo. Hii huichanganya LNB na wakati mwingine risiva.
Ukitaka kuunganisha risiva zaidi ya moja hakikisha unatumia LNB ya output mbili, au zaidi ambazo output zake kila moja inajitegemea au tumia "Single Solution LNB" kwa C Band. Kwa Ku Band hutakiwa kutumia LNB ambayo ina output zaidi ya moja (kila output inajitegemea) au Quatro LNB.

Kinachofanyika katika LNB ya Ku Band.
Ndani ya LNB kuna antena mbili ndongo ambazo hupokea mawimbi ya satelaiti na kuyapeleka katika sakiti ambayo huyakuza (amplify) na kuyaelekeza katika hatua nyinginezo. Baada ya kuyakuza hupelekwa katika sakiti ambayo hutengeneza mawimbi karibia sawa na yale yaliyotoka katika satelaiti; sakiti hiyo tunaiita "local oscillator". Mawimbi yaliyotoka katika satelaiti katika Ku Band 10700MHz - 12750MHz huchanganywa na mawimbi yaliyotengenezwa na "LNB Local oscillator" ambayo ni Low Frequency 9750MHz na High Frequency 10700MHz.

Intermediate Frequency (IF):
LNB hufanya hesabu (computes) ya kuchukua mawimbi yaliyotoka katika satelaiti na kutoa yale iliyotengeneza yenyewe katika hatua tunayoiita "Heterodyning". Hata TV, Radio risiva nazo hufanya hatua hizi wakati wa kuandaa picha na sauti. Baada ya hesabu hiyo kinachopatikana ni Intermediate Frequency (IF).

Hesabu yenyewe:

Mawimbi yaliyotoka katika satelaiti katika Ku Band 10700MHz - 12750MHz.
Mawimbi yaliyotengenezwa na LNB ya Ku Band - 9750MHz - 10700MHz.
Intermediate Frequency (IF) = 950MHz - 2050MHz

Kwa baadhi ya LNB za Ku Band:
Mawimbi yaliyotoka katika satelaiti katika Ku Band 10700MHz - 12750MHz.
Mawimbi yaliyotengenezwa na LNB ya Ku Band - 9750MHz - 10600MHz.
Intermediate Frequency (IF) = 950MHz - 2150MHz



Hii inamaanisha kwamba mawimbi yanayopita katika waya kutoka kwenye LNB ya Ku Band kwenda katika risiva ni kati ya 950MHz hadi 2050MHz au 950MHz - 2150MHz. Mawimbi haya yanaweza kupita katika waya na ukitumia "spectrum analyzer" inayoweza kuona hadi 15GHz , 20GHz au 30GHz unaweza kuyaona na kuyachunguza.

ANGALIZO:
Intermediate Frequency (IF) kwa C Band inapatikana kwa hesabu ifuatayo:

C Band:
C-Band: IF frequency = local oscillator frequency - received frequency

Local Frequency ya C Band ni 5150MHz.

Mpangilio wa Masafa tunayoyatumia kupata chaneli za televisheni/ radio katika Ku Band kwa undani zaidi.


Umeme unaokwenda katika LNB toka katika Risiva
Sauti ya kuiamsha LNB (Tone)
LO (Low Frequency) Masafa ya chini katika LNB
Ukaaji wa Mawimbi (Polarization)
Masafa yanayopokelewa
IF (Intermediate Frequency)
13 V0 kHz9.75 GHzVerticalLow Band (10.70-11.70 GHz)950-1950 MHz
18 V0 kHz9.75 GHzHorizontalLow Band (10.70-11.70 GHz)950-1950 MHz
13 V22 kHz10.60 GHzVerticalHigh Band (11.70-12.75 GHz)1100-2150 MHz
18 V22 kHz10.60 GHzHorizontalHigh Band (11.70-12.75 GHz)1100-2150 MHz


Baadhi za LNB za Ku Band hufanyakazi kuanzia 10.7GHz hadi 12.75GHz na nyingine hufanya kazi kuanzia 10.6GHz hadi 12.75GHz. Katika satelaiti hii Eutelsat 36B Multichoice / DStv wapo wanatumia High Band (masafa wanayotumia yanaanzia 11.7270GHz – 12.245GHz).

Angalia jedwali hapo juu:
Vertical High Band 11.70GHz – 12.75GHz
Horizontal High Band 11.70GHz – 12.75GHz


Jambo muhimu:
Kadri masafa yanavyoongezeka ndivyo mawimbi yanavyokuwa rahisi kupotea katika waya. Katika masafa makubwa tunahitaji kutumia waya bora; vinginevyo mawimbi yanayofika katika risiva au decoder yanakuwa madogo (mawimbi hupotea njiani). Kwa lugha ya kitaalam tunasema "signal attenuation along cables". Waya tunaotumia kusafirisha mawimbi toka katika antena kwenda katika decoder za; mfano Startimes, Ting, Easy TV, au antenna zinazoungwa moja kwa moja katika televisheni zinaweza kushindwa kupitisha vizuri mawimbi kutoka katika LNB ya dishi kwenda katika risiva au decoder kama wavu wa waya unaouzunguka waya wa katikati wa"COAXIAL CABLE" hauna waya nyingi (if the coaxial cable shielding is not well brided).


Ku Band ipo ndani ya "Electromagnetic Spectrum - 3GHz hadi 30GHz" katika masafa ya 10.7GHz (10700MHz) hadi 12.75GHz (12750MHz) kutoka katika satelaiti (Ku band Television downlink frequencies).

Au setup mwenyewe kwa kubadilisha (edit katika risiva); LNB Frequencies za C Band ambazo ni 5150MHz na kuweka za Ku Band kama inavyoonekana hapa chini.

Satellite setup (katika risiva):
LNB Frequency
Low Frequency: 9750MHz
High Frequency: 10700MHz

Katika channel search (kila risiva ina MENU yake tofauti na nyingine):
Ingiza masafa (frequency), Symbol Rate na polarization (polarization weka Auto) katika jedwali ifuatayo (chagua mojawapo). Anza kutafuta signal. Ukishapata unganisha kila kitu sawa (weka waya vizuri) alafu unganisha decoder ya Multichoice/Dstv; utapata picha.

Mfano:

Ingiza katika risiva au decoder:

Frequency : 11785
Symbol Rate: 27500
Polarization: Horizontal
FEC (Forward Error Correction): ¾ au Auto
Mambo ya kuzingatia wakati wa kutafuta chaneli za Multichoice / DStv yanayotoka katika satelaiti Eutelsat 36B.

Baada ya kutafiti sana mawimbi ya satelaiti hii yanaonekana kuwa imara (stable) kwa frequency zote ila kuna tatizo linalojitokeza ni upande wa dishi.

Tatizo lenyewe:
Kutokana na sababu za kijiografia sisi (Tanzania) tupo jirani na satelaiti hii (inakuwa kama ipo utosini). Madishi yanayotumika kwa wingi kupokea chaneli za Multichoice/ DStv ni ya kipenyo cha sentimita 90(cm). Mara nyingi wakati wa mvua kwa wanaotumia madishi ya ukubwa huu lazima mawimbi yakatikekatike. Kwa sababu kadri masafa yanavyozidi kuongezeka katika "electromagnetic spectrum" unavyozidi kwenda juu; ("SOMA ELECTROMAGNETIC SPECTRUM") ndivyo yanavyozidi kuathiriwa na mvua. Ili kupata mawimbi ambayo hayakatiki hata wakati wa mvua tunahitaji kutumia madishi ya ukubwa wa sentimita 120(cm) ambayo ni sawa na mita 1.2(m).
Madishi mengi ya Ku Band yaliyopo sokoni (satellite dishes on the market) yanasumbua wakati wa kutafuta satelaiti hiyo kwasababu hayazunguki sana (vertical movement). Yanaishia pale satelaiti ilipo hivyo inakuwa vigumu kurekebisha vizuri ilikupata mawimbi vizuri. Pia stand zake (dish bases) zinazokuja na madishi hayo ni fupi kiasi kwamba ukizifunga ukutani madishi yanagusa ukutani. Hili ni tatizo lililopo katika utengenezaji wa madishi ya Ku Band na Multichoice/ Dstv inabidi tatizo hili walitazame kwasababu linawahusu.

Uwekaji wa LNB.
Kitu muhimu cha kuangalia wakati wa kufunga dishi ni namna ya kuweka LNB (Ulalo wa LNB) ukiiweka vibaya inaweza ikakataa kutoa signal hata kama dishi limekaa vizuri (hii ni kwa dishi la Ku Band na C Band), kwa sababu katika LNB kuna antenna (probe) mbili ambazo moja kwa ajili ya chaneli ambazo ni “vertical” na nyingine kwa ajili ya chaneli ambazo ni “horizontal”. Katika kanuni za kurusha mawimbi lazima antenna inayorusha iwe imekaa sawa na antenna inayopokea.
Hii inamaanisha kwamba kama antenna iliyopo katika “transponder” ya satelaiti imesimama (vertical) na LNB ya dishi linalopokea mawasiliano hayo lazima antenna yake nayo iwe vertical. Vilevile kwa chaneli za Horizontal. Hatua ya kurekebisha LNB ili antenna yake ikae sawa na mawimbi inayoyapokea huitwa “LNB Skew Adjustment”.

Kufunga LNB ya Ku Band katika dish la C Band.
LNB ya Ku Band ukiifunga katika dishi la C Band inaweza kufanya kazi ikiwa dishi hilolinaelekea katika satelaiti yenye chaneli unazozitafuta. Katika hili ni muhimu kuangalia unapofunga LNB ya Ku Band katika dishi la C Band. Mawimbi yakiwa na nguvu sanayanaweza kuiharibu LNB.

Jedwali lililoko hapo chini linaonesha Masafa na Channel za Multichoice/ Dstv tunazozipokea nchini Tanzania na nchi nyingine ambazo Eutelsat 36B inafikisha mawimbi yake.
Haya masafa huwasaidia mafundi wakati wa kufunga madishi (kutafuta signal za Dstv).

Masafa ya chaneli za Multichoice /DStv toka katika satelaiti Eutelsat 36B.
Masafa katika Megahertz (MHz)
Symbol Rate
Polarization
FEC (Forward Error Correction)
1172727500Vertical (V)¾ (au Auto)
1174727500Horizontal¾ (au Auto)
1176627500Vertical¾ (au Auto)
1178527500Horizontal¾ (au Auto)
1180427500Vertical¾ (au Auto)
1182327500Horizontal¾ (au Auto)
1184327500Vertical¾ (au Auto)
1186227500Horizontal¾ (au Auto)
1188127500Vertical¾ (au Auto)
1190026480Horizontal¾ (au Auto)
1191927500Vertical¾ (au Auto)
1194027500Horizontal¾ (au Auto)
1195827500Vertical¾ (au Auto)
1197727500Horizontal¾ (au Auto)
1199627500Vertical¾ (au Auto)
1201527500Horizontal¾ (au Auto)
1203427500Vertical¾ (au Auto)
1205427500Horizontal¾ (au Auto)
1207327500Vertical¾ (au Auto)
1224527500Horizontal¾ (au Auto)

ANGALIZO:
Masafa katika jedwali yapo katika Megahertz na Megahertz 1000MHz (Megahertz elfu moja) ni sawa na Gigahertz moja (1GHz).

b) CHANELI ZA C BAND TOKA KATIKA SATELAITI MBALIMBALI.

Kuna aina ngapi za madishi ya C Band:
Kuna aina tatu za madishi ya C Band kutokana na utengenezaji.

1. Madishi ya Bati (Aluminium alloyed satellite dishes)
2. Madishi ya Wavu (Mesh Satellite dishes).
3. Madishi yanayotengenezwa kwa vioo (enforced glass fibre satellite dishes).

Madishi ya bati na madishi ya wave (Mesh) hayana tofauti sana katika utendaji (upokeaji wa mawimbi kutoka katika satelaiti).

Matatizo yanayoyakumba Madishi katika ukanda wetu:
Tatizo kubwa katika ukanda wetu hasa maeneo ya mwambao mwa Bahari ya Hindi (Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Tanga, Mtwara, Mogadishu, Mombasa, na maeneo mengine kusini, kaskazini, Mashariki na Magharibi mwa Afrika na Mabara mengine ni mvuke wenye chumvi kutoka baharini ambao husababisha madishi ya bati yapate kutu na kuharibika haraka.

Madishi ya Bati.
Madishi mengi ya bati yanayoletwa nchini Tanzania ni mchanganyiko aluminium, chuma na madini mengine na hivyo kusababisha yapate kutu kiurahisi. Ukifunga dishi kuelekea satelaiti 906, IS 10 katika maeneo ya mwambao wa Bahari ya Hindi na baadhi ya sehemu za Tanzania Bara lazima maji yatuame (kwa madishi ya bati) baada ya mvua kunyesha kwa sababu ziilipo satelaite hizi nyuzi 64.2 na 68.6 Mashariki na sisi hapa kwetu mfano Dar es Salaam tunapofunga dishi halilali sana na kumwaga maji badala yake maji hutuama na kuliharibu dishi baada ya muda mfupi.Jaribu kuangalia madishi yenu baada ya mvua kunyesha mtaona hili. Tatizo la kutuamisha maji huzidi kupungua kadri tunavyozidi kuingia ndani (Magharibi ) mwa Bara la Afrika; mfano mtu aliyeko Kigoma, Ngara au Kagera dishi lake linaweza lisituamishe maji kwasababu tunavyozidi kwenda mbali na satelaiti ndivyo dishi inabidi lilale sana kuipata satelaiti hiyo
View attachment 1084393

Picha hapo juu niliipiga jijini Dar es Salaam. Inaonesha Satellite dish la upana wa futi 8 lililofungwa kuelekea satelaiti Intelsat 906, Intelsat 10 na Intelsat 20 likiwa limetuamisha maji baada ya mvua. Kwa kuwa madishi haya hayatengenezwi kwa kutumia aluminium peke yake (aluminium huwa haipati kutu) huwa yanapata kutu haraka na kutoboka.

View attachment 1084394



View attachment 1084395
Picha hapo juu inaonesha dishi madishi mawili ya bati kwa ajili ya kupokea masafa ya C Band au Ku Band



Madishi ya Wavu.
Madishi mengi ya Wavu yametengenezwa kwa aluminium (pure aluminium) hivyo si rahisi kupata kutu. Pia kwa kuwa madishi ya wavu (Mesh dishes) yana Matundu; huwa hayaruhusu maji ya mvua kutuama na hivyo kuyanusuru yasipate kutu kwa urahisi. Sehemu za dishi la wavu zinazopata kutu kiurahisi ni bolts na nut zake, na mihimili ambapo madishi yanafungwa (dish bases, dish poles). Ni muhimu kuyapaka Grease ili kuzuia kutu

View attachment 1084396

Picha hapo juu inaonesha Dishi la Wavu la linalozunguka (moving Mesh dish) kwa ajili ya C Band na Madogo kwa ajili ya Ku Band
View attachment 1084397
Picha hapo juu inaonesha Dish la Wavu linalozuzunguka (moving mesh dish) kwa ajili ya C Band na Madishi modogo Mawili ya Ku Band

Ufungaji wa dish la C Band hauna tofauti kubwa na Dish la Ku Band. Dish la C Band ni kubwa kuliko la Ku Band. Madishi ya C Band huanzia futi 6ft, 8ft, 10ft, 12ft na kuendelea.

Satelaiti tunazopata chaneli za C Band katika ukanda wetu.
Katika ukanda wetu tunaweza kuona chaneli nyingi toka katika satelaiti kwa kufunga madishi ya C Band. Baadhi ya satelaiti tunazoweza kupata katika eneo letu kwa kufunga madishi kuanzia futi nane (8ft) na kuendelea ni NSS 12, NSS7, IS901, IS902, IS904, IS905, IS906, IS 17, IS907, NSS806, IS10, Apstar 7, Thaicom 5 na nyinginezo.

Matatizo katika mawasiliano.
Matatizo yanayosumbua wakati wa kutafuta satelaiti hizo ni mwingiliano wa mawasiliano kati ya Masafa ya satelaiti katika C Band 3.6GHz - 4.2GHz na mawasiliano ya kawaida (terrestrial transmissions) katika baadhi ya sehemu na baadhi ya miji.
Mfano maeneo ya katikati ya Jiji la Dar es Salaam tatizo hili ni sugu kutokana na kuwa na vifaa vingi vinavyofanya kazi katika C Band 3.6GHz - 4.2GHz (there are many devices transmitting within the Frequency Range 3.6GHz - 4.2GHz).

Tatizo jingine ni baadhi ya chaneli kuwa na mawimbi ambayo hayana nguvu na hivyo kuyafanya yasipatikane katika madishi. Kwa sasa kuna tatizo la mawimbi yanayobeba chaneli:
TBC (Tanzania) Transponder No. 93, Masafa 3.891GHz - Left Circular
Startv (Tanzania) Transponder No. 93, Masafa 3.884GHz - Left Circular
UBC (Uganda
) Transponder No. 11, Masafa 3.721GHz - Right Circular
Channel Ten (Tanzania) Transponder No. 93 Masafa 3.905GHz - Left Circular
Agape TV Network (Tanzania) Transponder No. 93, Masafa 3.900GHz - Right Circular

kutoka katika satelaiti inayoitwa Intelsat (IS906 iliyopo nyuzi za longitudo 64.2 Mashariki mwa Mstari wa Greenwich) kutokuwa na nguvu nahivyo kushindwa kupatikana katika madishi ya yenye kipenyo (diameter) cha futi sita (6ft) na kupatikana kwa tabu katika madishi ya futi nane (8ft).

Nini kinaweza kuwa chanzo cha kutopatikana kwa chaneli hizo hapo juu?
Kutokupatikana kwa chaneli hizo hapo juu kunaweza kusababishwa na:

Sababu ya kwanza:
Nguvu ya mawimbi yanayopelekwa katika satelaiti kuwa ndogo (low satellite uplink power).
Kwa kawaida huwa kuna makubaliano (mikataba) kati ya wamiliki wa vituo vya redio na televisheni vinavyotumia satelaiti na wamiliki wa satelaiti. Mikataba hiyo huonesha nguvu ya mawimbi yanayopelekwa katika satelaiti. Mamlaka zinazodhibiti mawasiliano katika nchi mbalimbali hupewa nakala za mikataba hiyo. Nguvu ya mawimbi (uplink power) yanayokwenda katika satelaiti inaweza kuongezwa au kupunguzwa katika vituo vya redio/ televisheni vinavyotumia satelaiti ila haitakiwi kuzidi kiwango walichokubaliana.
Ukiongeza nguvu ya mawimbi yanayokwenda katika satelaiti yakazidi kiwango cha makubaliano na mmiliki wa satelaiti (above contract power) unaweza kusababisha mwingiliano na chaneli nyingine katika satelaiti; chaneli ambazo masafa yake yanakaribiana na chaneli yako. Wakati wa kuongeza nguvu ya mawimbi yanayokwenda katika satelaiti katika vituo vya televisheni/ radio lazima yawepo mawasiliano kati ya pande mbili ili nguvu isizidi kiwango au isipungue kiwango.
Vituo vingi husaini mikataba ambayo power level ni ndogo kwa sababu ya gharama (kadri unavyopeleka nguvu kubwa katika satelaiti ndivyo unavyolipa zaidi). Kumbuka kulipia Transponders gharama yake si mchezo.
Wengine husaini mikataba ambayo nguvu ya mawimbi yake ni ndogo kwa kukosa wataalam wa kuwashauri vizuri juu ya hilo.

Sababu ya pili:
Katika satelaiti kuna kifaa kinachoitwa "Transponder".

Transponder ni nini?

Transonder ambayo kwa mara nyingi huitwa kwa kifupi XPDR, XPNDR, TPDR or TP maana yake kwa jina la kitaalam ni "Transmitter - Responder".
Ni kifaa ambacho kipo ndani ya satelaiti ambacho kazi yake ni kupokea mawimbi katika masafa makubwa toka ardhini (mfano katika vituo vya redio na televisheni katika C Band 5.850GHz - 6.425GHz, katika Ku Band 14.0GHz - 14.5GHz kuyakuza (amplification) na kuyapunguza masafa (downconvert) kwa C Band 3.6 - 4.2GHz na kwa Ku Band 10.7GHz - 12.75GHz na kuyarusha tena ardhini katika uso wa dunia ambapo tunayapokea majumbani mwetu na maofisini mwetu kwa kutumia madishi. Satelaiti moja inaweza kuwa na idadi ya transponder hadi 70.
Satelaiti huwa zina muda wa kukaa angani. Zikianza kuchoka Transponder zilizoko katika satelaiti hushindwa kufanya kazi vizuri na wakati mwingine kusababisha matatizo kama haya.

Anayeweza kutoa jibu kamili juu ya kupotea kwa mawimbi au mawimbi kuwa madogo katika satelaiti husika ni vituo vya televisheni / radio husika, mmiliki/operator wa satelaiti husika na Mamlaka zinazotumika kudhibiti Mawasiliano katika nchi husika. Mfano IS 906 inamilikiwa na kampuni inayoitwa Intelsat iliyoko na makao yake makuu Atlanta, Marekani.
Ni wajibu wa Mamlaka zinazosimamia Mawasiliano katika nchi zao kuhakikisha hayo mawasiliano ambayo wanatoa leseni kwa waendeshaji wa vituo vya Televisheni na Radio kupitia satelaiti yanapatikana. Katika Tanzania anayetakiwa kusimamia hili ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Kenya Tume yao ya Mawasiliano inaitwa CCK, Uganda - inaitwa UCC, Rwanda - inaitwa RURA, Burundi - inaitwa ARCT, Zimbabwe - inaitwa POTRAZ na nchi nyingine (kila nchi ina Mamlaka/Tume yake ya udhibiti wa Mawasiliano.
Tatizo tulilonalo katika nchi nyingi juu ya kubaini matatizo haya ni kutokuwa na vifaa vya kutosha hasa katika upande wa kudhibiti mawasiliano yanayokwenda au yanayotoka katika satelaiti.

Tatizo la Tatu:
Ukifunga dishi sehemu ambayo ina mitambo inayorusha mawimbi sawa na unayoyapokea toka katika satelaiti dishi linaweza lisifanye kazi au nguvu ya mawimbi unayoyapokea itakuwa ndogo kwa sababu kunakuwa na mwingiliano wa mawasiliano. Kiwango cha madhara ya mwingiliano wa mawasiliano ya satelaiti toka mitambo iliyopo jirani (nearby terestrial transmissions) hutegemea nguvu ya mawimbi yanayotoka katika mitambo hiyo. Ila ukifuatilia ukaona tatizo la kutopatikana kwa mawasiliano lipo sehemu nyingi; mikoa mingi au nchi nyingi ujue tatizo hilo linatokana na sababu nilizozitaja hapo juu.

Mwingiliano wa Mawasiliano katika jiji la Dar es Salaam.
Kumewahi kuwepo kwa matatizo makubwa ya mwingiliano wa mawasiliano katika C Band kati ya mwaka 2007 hadi 2008 katika jiji la Dar es Salaam matatizo yaliyofanya baadhi ya chaneli za televisheni/radio toka katika satelaiti zisipatikane kabisa. Tatizo hili lilisumbua sana.
Tatizo la mwingiliano wa mawasiliano hukumba zaidi madishi yanayofungwa juu ya maghorofa kuliko madishi yanayofungwa chini kwa sababu mawasiliano kutoka mitambo ya jirani huwa yapo katika mstari mmoja (line of site) na madishi yanayofungwa juu ya maghorofa.

View attachment 1084398

Picha/ grafu hapo juu imetokana na kipimo nilichofanya kwa kutumia Spectrum Analyzer tarehe 24 Februari, 2008 katika jiji la Dar es Salaam katikati ya Kijitonyama na Mikocheni. Kipimo hiki nilikichukua nikiwa chini tu. Kama ingekuwa juu ya maghorofa ambapo mawasiliano yanakatiza kiwango cha mawimbi yanayoingilia mawasiliano kingekuwa juu sana. Wakati huo kulikuwa na mwingiliano mkubwa wa mawasiliano kutoka katika satelaiti na kusababisha baadhi ya mawasiliano kutoka katika satelaiti mbalimbali kuwa magumu sana. Nilianza kulifuatilia suala hili kwa karibu na kugundua kulikuwa na vifaa/ transmitter (vifaa vingi vilikuwa vinatumika kwa mawasiliano ya data) zilizokuwa zikifanya kazi katika masafa ambayo yametengwa kupokea mawasiliano kutoka katika satelaiti. Hili tatizo lilikuwa kubwa na liliharibu mawasiliano ya data na chaneli za televisheni/ redio (mfano ITV, CAPITAL, EATV, CHANNEL TEN na nyinginezo) kutoka katika satelaiti mbalimbali.

Maelezo ya Picha / Graph:
Katika grafu kuna X na Y Axis.
X Axis: Katika grafu kutoka kushoto kwenda kulia ( masafa), kati ya mstari na mstari ni Megahertz 100MHz. Kutoka Mwanzo wa grafu hadi mwisho (Span) ni 1GHz.Maana yake kutoka 3.5GHz - 4.5GHz. Katikati ya grafu ni 4GHz.

Y Axis: Katika grafu kuanzia chini hadi juu huu inaonesha nguvu ya mawimbi (power levels).

Picha ilipigwa (scanning) kutoka 3.5GHz - 4.5GHz.
Kutoka 3.5GHz hadi 3.6GHz kuna mawasiliano ya internet/data.
Masafa 3.6GHz - 4.2GHz yametengwa kwa ajili ya kupokea mawasiliano kutoka katika satelaiti katika C Band mfano ITV, EATV, CAPITAL (3.641GHz), TBC 3.891, Startv 3.884GHz, Channel Ten 3.905GHz)
Matuta yanayoonekana katika grafu ni mawasiliano yaliyokuwa yakifanyika katika masafa hayo.

Katikati ya 3.6GHz - 4.2GHz hakukutakiwa kuwa na Matuta (transmissions):
Katika Grafu:
Mark 1: 3.764GHz
Mark 2: 3.817GHz
Mark 3: 4.025GHz
Mark 4: 4055GHz

Ukiangalia katika grafu kuanzia 3.6GHz hadi 4.2GHz kuna matuta ambayo ni mawasiliano (local terrestrial transmissions) zilizosababisha kukoseka/ kupotea baadhi ya mawasiliano.

Nini kinachotakiwa kufanyika endapo mawasiliano yanaingiliwa.
Ni wajibu wa Mamlaka/Tume zinazosimamia na kudhibiti Mawasiliano katika nchi husika kuhakikisha masafa yanatumika kama yalivyopangwa.
Na ikitokea hivyo hao watu wanaofanya hivyo lazima wanyanganganywe masafa hayo kwa sababu wanakuwa wanayatumia kinyume na utaratibu. Kwa kufanya hivyo husababisha mwingiliano au kupotea kwa mawasiliano ya watu wengine.

Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kurusha mawasiliano kati ya 3.7GHz hadi 4.2GHz katika Afrika, Ulaya na Urusi (Region 1) kwa sababu masafa hayo yametengwa na ITU (International Telecommunications Union) kwa ajili ya kupokea mawasiliano ya televisheni/ redio na data kutoka katika satelaiti.
Tazama ukurasa wa ITU katika blog hii.


Masafa ya C Band kwa Undani:

Masafa ya C Band Duniani​
Band
Masafa ya Kupeleka mawimbi katika satelaiti Masafa ya Kupokea Mawimbi kutoka katika satelaiti
Standrd C - Band5.850–6.4253.625–4.200
Extended C - Band6.425–6.7253.400–3.625
INSAT / Super – Extended C - Band6.725–7.0254.500–4.800
Urusi C - Band5.975–6.4753.650–4.150
LM C - Band5.7250–6.0253.700–4.000


Ufungaji wa LNB zaidi ya Moja katika Madishi ya C Band.
Inawezekana kufunga LNB za C Band katika dishi la futi 6 (6ft), 8ft, 10ft na kuendelea.

Madishi yote ya C Band (kuanzia kipenyo cha futi 6ft, 8ft, 10ft na kuendelea) yametengenezwa kwa ajili ya kupata chaneli kutoka katika satelaiti moja ila kuna utundu/ubunifu wa kuliwezesha dishi moja lipokee chaneli toka satelaiti zaidi ya moja ambazo zipo karibu karibu. Hii inawezekana kufanya hivyo kwa kufunga LNB zaidi ya moja (mara nyingi LNB 2, 3 na wengine hata LNB 4). Kufanya hivi kuna faida na hasara zake:

Faida zake:
Mfumo huu hutuwezesha kupata chaneli nyingi kutoka katika satelaiti tofauti tofauti. Mfumo ulioenea hapa mjini ni ufungaji LNB mbili, tatu au nne katika madishi ya futi 6ft na futi 8ft.
LNB ya 1 ni ya C Band na hupokea chaneli kutoka satelaiti IS 906 (Intelsat 906).
LNB ya 2 ni ya C Band na hupokea chaneli kutoka satelaiti IS 10 (Intelsat 10) na Intelsat 7 @ 68.6E
LNB ya 3 ni ya Ku Band na hupokea chaneli kutoka satelaiti NSS12 (ili kupata chaneli za Zuku, KBC (Kenya) n.k.
LNB ya 4 ni ya Ku Band na hufungwa juu ya LNB ya C Band ili iweze kupokea chaneli zinazotumwa katika masafa ya Ku Band kutoka katika satelaiti IS 10 @ 68.5 Mashariki mwa Greenwich. LNB ya Ku Band hufungwa hapo kwa kuitoboa LNB ya C Band (inayopokea chaneli kutoka IS 10) au hufungwa pembeni kidogo (kwenye mkono wa dishi).

Wengine hufunga hadi LNB 4 au 5 katika dishi la futi 6ft au 8ft kupata chaneli kutoka satelaiti nyinginezo kama IS902 na satelaiti nyinginezo.

Jambo muhimu la kuzingatia:
Kuna baadhi ya satelaiti ambazo hufanya kazi katika masafa ya C Band tu, nyingine masafa ya Ku Band tu na nyingine hufanya kazi katika masafa ya C Band na Ku Band.

Hasara zake:
Kufunga LNB nyingi katika dishi moja ni kulilazimisha dishi lifanye kazi ya ziada (kulitumia kikamilifu). Faida zake nimezitaja hapo juu (kupata chaneli nyingi toka satelaiti tofauti tofauti).
Kwa kuwa dishi linakuwa limelazimishwa ; baadhi ya chaneli hasa ambazo mawimbi yake kutoka katika satelaiti hayana nguvu huwa zinakatika katika na wakati mwingine huwa hazipatikani kabisa kwa sababu dishi linakuwa halijalenga katika satelaiti moja (linakuwa katikati).

Mfumo mzuri wa kupata chaneli mbalimbali toka katika satelaiti tofauti tofauti ni kufunga madishi zaidi ya moja kila dishi likilenga satelaiti yake au dishi moja lilenge satelaiti mbili (kwa ambazo zipo karibu karibu na ambazo mawimbi yake yana nguvu sana).

JAMBO LA MUHIMU KUZINGATIWA:
Hakuna madhara yoyote ukisimama mbele ya dishi linalopokea mawasiliano kutoka katika satelaiti (downlink satellite dish) kwasababu mawimbi yanayotoka katika satelaiti yanakuwa yamesafiri umbali mrefu na hivyo nguvu yake inakuwa ndogo.

Unaweza kupata madhara ukisimama kwa muda mrefu mbele ya satelaiti dishi (parabolic reflectors) za VSAT hasa zinazofungwa chini na antena bapa (flat antenna) mfano antena zinazotumika kwa ajili ya mawasiliano kama INMARSAT, antena za RADAR, antena za SNG (Satellite News Gathering) ambazo hupeleka mawasiliano katika satelaiti. Pia ukisimama karibu na antena za GSM/CDMA, antena za microwave links kwa muda mrefu unaweza kupata madhara (hasa mafundi wanaozifunga).

Minara ya kurusha matangazo ya redio na televisheni hurusha mawimbi yenye nguvu zaidi hewani kuliko ya mitambo ya simu ingawa masafa yake yanakuwa madogo kuliko ya mawasiliano ya simu. Hata ukifungua muziki kwa sauti ya juu unapata madhara (hasa kwa watoto wadogo ambao ngoma ya masikio - "diaphram" ni rahisi kutoboka). Madhara mengine yanatokea baada ya muda mfupi na mengine baada ya muda mrefu.
Kila kitu duniani kina athari zake kwa viumbe hai; hata mimea, miti, majani ya miti hutoa mionzi ingawa kwa kiwango kidogo (chukua dishi lizungushe kama unatafuta mawimbi ya televisheni fulani kutoka katika satelaiti mfano katika C Band badala ya kulielekeza dishi juu katika satelaiti lielekeze katika miti utaona mawimbi (signal) ikiongezeka. Kama hutumii Spectrum Analyzer unaweza kutumia hata risiva ya satelaiti.

Si rahisi kukwepa athari zinazotokana na mionzi iliyopo katika mawimbi hapa duniani kwa sababu duniani tumezungukwa na mawimbi ambayo mengine yanatokana na ulimwengu huu (natural radiations) na mengine yanatokana na vifaa / mitambo ya kutengenezwa na binadamu (manmade radiations). Tunachoweza kufanya ni kujitahidi kujiepusha kuishi karibu na sehemu au na vifaa/mitambo inayotoa mionzi yenye nguvu sana. (Mitambo isifungwe karibu sana na makazi ya watu: kuna antena za minara ya simu zinafungwa katika maghorofa jirani kabisa na madirisha ya nyumba).
Mionzi mbalimbali iliyopo hapa duniani (mionzi ya asili) na ya kutengenezwa na binadamu (man made) hupunguza muda wa binadamu kuishi hapa duniani

Shukrani sana kwa hii elimu ndogo niliyo nayo naamini wapo wengi wanao fahamu zaidi na ukitembelea mitandao mbalimbali wameeleza kwa undani zaidi
Elimu safi nimepata kitu cha kujifunza hapa
 
king'amuz cha Ting(Dish) kinaandka “Descrambled rejected” chaneli nying hazionyesh adi hiz za nyumban..Apa tatzo ni nn mkuu Eli79 na wajuvi wengne
 
Back
Top Bottom