mzalendo namba moja
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 390
- 476
Kwa namna maarifa yanavyozidi kuongezeka kuna bidhaa nyingi zinaweza tengenezwa ukiwa nyumbani tu kikubwa ujikusanyie malighafi Kwanza. Mimi binafsi nmejifunza vitu vingi na nisingependa kuwa mbinafsi, naweza kushare baadhi ya maarifa niliyonayo hapa, najua wengi wanajua pia, ukiona yafaa waweza weka maarifa yako hapa from scratch au hata video ikiwezekana.
Mfano wa maarifa hayo ni pamoja na utengenezaji wa:- sabuni zote kwa formula zote, shampoo, mishumaa, tomato soes, maji ya betri, mchanganyo wa dawa za kuprintia t-shirts, dawa za viatu, dawa za meno, mafuta ya kujipaka, lotion, spray, dawa za kusafisha malumalu, cake, pombe, wine, spirits, soda n.k, najua wengi wana wengi
Karibuni wana jukwaa
NITAANZA NA SABUNI YA MAJI
Ni sabuni nzuri kwa ajili ya matumizi ya kufulia, kudekia na kufukuzia wadudu.
Mahitaji yote yanapatikana kwenye maduka ya vjfaa vya wajasiliamali au waweza tafuta ofisi za Allied Chemicals au SIDO na kwa wale wa Mwanza tuwasiliane ili nikuelekeze..
MAHITAJI
kwa sabuni lita 25
✓chumvi yeyote kilo 1
✓ sulphonic acid ½ lita
✓Siles kilo 1
✓Rangi (uipendayo) vijiko viwili vya chakula
✓perfume (uipendayo) Mili-lita
50
✓maji lita 25
✓diaba la plastic (sio chuma)
✓mti mkavu wa kukorogea
HATUA ZA UTENGENEZAJI
Tanabahi: hii ni formula mpya, kama ipo nyingine nzuri zaidi na rahisi utaweka.
¶ baada ya kuweka maji kwenye diaba hizo lita 25 weka chumvi yote (kilo 1) kisha koroga dkk 5 na uhakikishe imeyeyuka yote
¶ Kisha tia sulphonic Acid {hakikisha umevaa gloves au kilinda mikono chochote ili tu sulphonic isikumwagikie (ni hatar ikikumwagikia)} kisha koroga kwa nusu saa nzima mpaka uone povu jeupe limeshamiri kwenye maji
¶ kisha weka Siles na koroga vizuri kwa nusu saa nyingine mpaka sabuni iwe nzito kabisa na baada ya hapo funika diaba lako na liache kwa masaa kumi na mbili kuruhusu mchanganyo ukae sawa
¶ Baada ya hapo waweza funua na kutia perfume kisha koroga dkk 5 na kisha weka rangi then koroga tena dkk 5, na sabuni itakuwa tayr kwa matumizi
tanabahi: usiache wazi muda mrefu ili kutunza perfume yako na usiiache juani, karibuni kwa maswali.
Mfano wa maarifa hayo ni pamoja na utengenezaji wa:- sabuni zote kwa formula zote, shampoo, mishumaa, tomato soes, maji ya betri, mchanganyo wa dawa za kuprintia t-shirts, dawa za viatu, dawa za meno, mafuta ya kujipaka, lotion, spray, dawa za kusafisha malumalu, cake, pombe, wine, spirits, soda n.k, najua wengi wana wengi
Karibuni wana jukwaa
NITAANZA NA SABUNI YA MAJI
Ni sabuni nzuri kwa ajili ya matumizi ya kufulia, kudekia na kufukuzia wadudu.
Mahitaji yote yanapatikana kwenye maduka ya vjfaa vya wajasiliamali au waweza tafuta ofisi za Allied Chemicals au SIDO na kwa wale wa Mwanza tuwasiliane ili nikuelekeze..
MAHITAJI
kwa sabuni lita 25
✓chumvi yeyote kilo 1
✓ sulphonic acid ½ lita
✓Siles kilo 1
✓Rangi (uipendayo) vijiko viwili vya chakula
✓perfume (uipendayo) Mili-lita
50
✓maji lita 25
✓diaba la plastic (sio chuma)
✓mti mkavu wa kukorogea
HATUA ZA UTENGENEZAJI
Tanabahi: hii ni formula mpya, kama ipo nyingine nzuri zaidi na rahisi utaweka.
¶ baada ya kuweka maji kwenye diaba hizo lita 25 weka chumvi yote (kilo 1) kisha koroga dkk 5 na uhakikishe imeyeyuka yote
¶ Kisha tia sulphonic Acid {hakikisha umevaa gloves au kilinda mikono chochote ili tu sulphonic isikumwagikie (ni hatar ikikumwagikia)} kisha koroga kwa nusu saa nzima mpaka uone povu jeupe limeshamiri kwenye maji
¶ kisha weka Siles na koroga vizuri kwa nusu saa nyingine mpaka sabuni iwe nzito kabisa na baada ya hapo funika diaba lako na liache kwa masaa kumi na mbili kuruhusu mchanganyo ukae sawa
¶ Baada ya hapo waweza funua na kutia perfume kisha koroga dkk 5 na kisha weka rangi then koroga tena dkk 5, na sabuni itakuwa tayr kwa matumizi
tanabahi: usiache wazi muda mrefu ili kutunza perfume yako na usiiache juani, karibuni kwa maswali.