Pantomath
JF-Expert Member
- Jan 4, 2019
- 781
- 3,204
Ni ngumu kuelewa/ kuamini ila kati ya watu waliojutia kusoma sana na kufaulu vizuri ni mimi.
Nilitumia nguvu nyingi kusoma O-level, na kweli nguvu zile hazikwenda bure, Nilichomoka na div 1.11, shule ya hovyo hovyo na hakuna aliyewahi pata hio tangu ianze.
Ilikua shangwe, kitu ambacho nilikuja kushukuru baadae sikuonesha masifa mtaani kipindi nilivyo faulu form 4 na hata watu wengi hawakujua.
Mzee baba nikapelekwa PCB shule kubwa ya vipaji maalum, nilifurahi sana nisijue kumbe nimejipeleka bucha na panga langu.
Sasa kule ndio Nature ika ni select, test ya kwanza nikala za uso, ndio nilifaulu lakini nahisi nilikua wa mwisho, maana kila unayemwona Kapasua si mchezo, ya pili ile nili confirm kabisa ile nimefunga kitasa.
Sikuamini macho na akili yangu, kama ni mimi wa kufunga dimba a.k.a kuzima taa? ingawa bado nipo juu ya wastani,
Sasa kuna Mwana nakaa naye karibu alikua na 66 yake akajua sijui ndio wa kwanza, bwana akaenda kwa vipanga wa darasa eti kuwachora sababu alisikia wakilalamikiana kuwa nimefeli, asijue kuwa ni kufeli katika next level ya battle lao wenyewe yeye alidhani ni wastani akajipeleka.
Anafika huko mwenye ndogo ana 93, alirudi taratibu kinyume nyume akakaa kwenye dawati akainama nikamwona anatafuna mtihani wake, Nilikua kila nikimwona nakufa kwa kicheko, Hakumaliza week akahama.
Nikajiuliza hawa watu ni wa namna gani? Ni kweli nilizembea sana katika usomaji zaidi hata ya vipanga wenyewe na mbaya zaidi kumbe wana walipiga twitions karibuni topic zote za form V kabla hata ya kuanza shule, lakini hili gap ni kubwaa, zikaja test nyingine nazo ni kukimbizwa tu.
Nikaona hapa nitaaibika mzee mzima, nikaanza kusoma upepo, uzuri Science hasa PCB tulikua wengi, nikagundua kuna mananga kama mimi na wengine ni zaidi yangu tuliofaulu kwa sifa.
Nikasema sasa hawa ndio guard yangu huku nyuma, nisije nikawa wa mwisho, pale ndio nikafufua ule msuli tena.
kwa kweli awamu hii Matokeo hayakuendana na Jitihada, Binafsi chemistry ndio ilinitesa zaidi kwenye mitihani, ila kwenye usomaji ni kawaida tofauti na physics iliyokua ngumu kwenye usomaji ila kwenye mtihani mambo kiasi yanashuka.
Zile njemba zilizo jaaliwa yaani kwao kila upande akishika kalamu ni kama inajiandika, unamwita mtu akuelekeze anakuja (uzuri sio wachoyo na uzuri zaidi mimi nilikua rafiki wa kila mtu) anakuelekeza speed anayoshuka nayo unaishia kuguna tu, kuna vitu unashindwa kuuliza maana unahisi atashangaa huyu jamaa amekujaje huku?..
Maisha yangu katika usomaji yalikua magumu sana, japo ya nje yalikua mazuri na ya furaha sana. Nilijitahidi sana kukaza, maajabu ambayo niliyafanyaga ni kuwa wa 8, baada ya hapo nikatupwa na sijawahi hata kuikaribia tena. Maana ile nafasi niliipata baada ya kujitesa sana.
Kwa kweli hapa nikakata tamaa, Tofauti na O-level masomo yalikua marahisi na unaokimbizana nao ni warahisi.
Huku masomo ni Jiwe, unaokimbizana nao ni Nondo, yaani huna pa kuchomokea. Nikaamua mimi ni kusoma tu na kufaulu hizi higher grades niwachie watabe, Ila hawa mananga wenzangu nihakikishe hawanipiti, basi...
Tatizo wengi walikua na roho nyepesi, wengi walihama, wengine walibadili Comb, kwahiyo kadiri wanavyopungua mimi nakaribiwa, maana anaacha nafasi moja nyuma, ikawa kila akiondoka mmoja naongeza kasi na wengi walikua wanatoka hizi St...... kuna jamaa mmoja yeye alizunguka round about kbsa, Hatukujua alipitia wapi na hatujawahi mwona tena. alituachia tu tranka lenye mazaga kama yote.
Mwisho wake nika ambulia 2 iliyochoka, wazee kama kawa ni div 1 na hata kwenye Top 10 walikuwepo, japo wengine walizingua pia.
Selection inatoka Natakiwa kwenda SUA tena, nikaona huu ni ujinga sasa, si ndio kule kule na watu wale wale, wengi sana naenda nao tena Course Moja, Yaani ilifika hatua nafikiria kuwakwepa sasa lakini wao walikua wanakubali sana kampani yangu.
Raha ya kusoma, ni kufaulu kadiri ya jitihada na mwishowe kupata kile unachotafuta...
kinyume na hapo ni msalaba, na mm elimu yangu ya advance ni niliiona kero...pale ndio niliamini kuna watu wamejaaliwa akili za darasani, sisi wengine tunasogeza tuu gurudumu..
Mwisho, ni matamanio makubwa sana kwa mzazi kua na mtoto mwenye jitihada darasani na baadae maisha kwa ujumla, na kwa kweli inaleta furaha sana, Pia nahisi uwezo wa mtoto kupambanua mambo umeunganika na mambo flani kutoka kwa wazazi na malezi labda.
Usione kila kijana mtaani akirudi likizo akakutajia shule nzuri na kubwa anayosoma ukasema kimoyomoyo huyu ni kichwa, Wengine ni wazunguka round about tuu, na wanachopitia huko wanakijua wenyewe.
Mwanao kama ni Nanga, usimlazimishe elimu unamtesa, ukimpatia ile basic ya kusoma, kuhesabu na kuandika ambayo ndio elimu kuu inatosha mtafutie njia nyingine, Narudia tena unamtesa mwanao, unamjengea hofu na dhana ya kushindwa kuanzia utoto matokeo yake anakua nayo na kujihisi yeye si chochote panapo wenzake.
Msikilize, msapoti kwa njia nzuri anayoihitaji, mfanye mshindi tangu utoto, Ushindi sio Darasani tu, mfanye Mshindi wa maisha.
Tusidanganyane, hakuna shule za vipaji maalum, ni shule za waliosongoka na kufaulu vizuri
Sent using Jamii Forums mobile app
Nilitumia nguvu nyingi kusoma O-level, na kweli nguvu zile hazikwenda bure, Nilichomoka na div 1.11, shule ya hovyo hovyo na hakuna aliyewahi pata hio tangu ianze.
Ilikua shangwe, kitu ambacho nilikuja kushukuru baadae sikuonesha masifa mtaani kipindi nilivyo faulu form 4 na hata watu wengi hawakujua.
Mzee baba nikapelekwa PCB shule kubwa ya vipaji maalum, nilifurahi sana nisijue kumbe nimejipeleka bucha na panga langu.
Sasa kule ndio Nature ika ni select, test ya kwanza nikala za uso, ndio nilifaulu lakini nahisi nilikua wa mwisho, maana kila unayemwona Kapasua si mchezo, ya pili ile nili confirm kabisa ile nimefunga kitasa.
Sikuamini macho na akili yangu, kama ni mimi wa kufunga dimba a.k.a kuzima taa? ingawa bado nipo juu ya wastani,
Sasa kuna Mwana nakaa naye karibu alikua na 66 yake akajua sijui ndio wa kwanza, bwana akaenda kwa vipanga wa darasa eti kuwachora sababu alisikia wakilalamikiana kuwa nimefeli, asijue kuwa ni kufeli katika next level ya battle lao wenyewe yeye alidhani ni wastani akajipeleka.
Anafika huko mwenye ndogo ana 93, alirudi taratibu kinyume nyume akakaa kwenye dawati akainama nikamwona anatafuna mtihani wake, Nilikua kila nikimwona nakufa kwa kicheko, Hakumaliza week akahama.
Nikajiuliza hawa watu ni wa namna gani? Ni kweli nilizembea sana katika usomaji zaidi hata ya vipanga wenyewe na mbaya zaidi kumbe wana walipiga twitions karibuni topic zote za form V kabla hata ya kuanza shule, lakini hili gap ni kubwaa, zikaja test nyingine nazo ni kukimbizwa tu.
Nikaona hapa nitaaibika mzee mzima, nikaanza kusoma upepo, uzuri Science hasa PCB tulikua wengi, nikagundua kuna mananga kama mimi na wengine ni zaidi yangu tuliofaulu kwa sifa.
Nikasema sasa hawa ndio guard yangu huku nyuma, nisije nikawa wa mwisho, pale ndio nikafufua ule msuli tena.
kwa kweli awamu hii Matokeo hayakuendana na Jitihada, Binafsi chemistry ndio ilinitesa zaidi kwenye mitihani, ila kwenye usomaji ni kawaida tofauti na physics iliyokua ngumu kwenye usomaji ila kwenye mtihani mambo kiasi yanashuka.
Zile njemba zilizo jaaliwa yaani kwao kila upande akishika kalamu ni kama inajiandika, unamwita mtu akuelekeze anakuja (uzuri sio wachoyo na uzuri zaidi mimi nilikua rafiki wa kila mtu) anakuelekeza speed anayoshuka nayo unaishia kuguna tu, kuna vitu unashindwa kuuliza maana unahisi atashangaa huyu jamaa amekujaje huku?..
Maisha yangu katika usomaji yalikua magumu sana, japo ya nje yalikua mazuri na ya furaha sana. Nilijitahidi sana kukaza, maajabu ambayo niliyafanyaga ni kuwa wa 8, baada ya hapo nikatupwa na sijawahi hata kuikaribia tena. Maana ile nafasi niliipata baada ya kujitesa sana.
Kwa kweli hapa nikakata tamaa, Tofauti na O-level masomo yalikua marahisi na unaokimbizana nao ni warahisi.
Huku masomo ni Jiwe, unaokimbizana nao ni Nondo, yaani huna pa kuchomokea. Nikaamua mimi ni kusoma tu na kufaulu hizi higher grades niwachie watabe, Ila hawa mananga wenzangu nihakikishe hawanipiti, basi...
Tatizo wengi walikua na roho nyepesi, wengi walihama, wengine walibadili Comb, kwahiyo kadiri wanavyopungua mimi nakaribiwa, maana anaacha nafasi moja nyuma, ikawa kila akiondoka mmoja naongeza kasi na wengi walikua wanatoka hizi St...... kuna jamaa mmoja yeye alizunguka round about kbsa, Hatukujua alipitia wapi na hatujawahi mwona tena. alituachia tu tranka lenye mazaga kama yote.
Mwisho wake nika ambulia 2 iliyochoka, wazee kama kawa ni div 1 na hata kwenye Top 10 walikuwepo, japo wengine walizingua pia.
Selection inatoka Natakiwa kwenda SUA tena, nikaona huu ni ujinga sasa, si ndio kule kule na watu wale wale, wengi sana naenda nao tena Course Moja, Yaani ilifika hatua nafikiria kuwakwepa sasa lakini wao walikua wanakubali sana kampani yangu.
Raha ya kusoma, ni kufaulu kadiri ya jitihada na mwishowe kupata kile unachotafuta...
kinyume na hapo ni msalaba, na mm elimu yangu ya advance ni niliiona kero...pale ndio niliamini kuna watu wamejaaliwa akili za darasani, sisi wengine tunasogeza tuu gurudumu..
Mwisho, ni matamanio makubwa sana kwa mzazi kua na mtoto mwenye jitihada darasani na baadae maisha kwa ujumla, na kwa kweli inaleta furaha sana, Pia nahisi uwezo wa mtoto kupambanua mambo umeunganika na mambo flani kutoka kwa wazazi na malezi labda.
Usione kila kijana mtaani akirudi likizo akakutajia shule nzuri na kubwa anayosoma ukasema kimoyomoyo huyu ni kichwa, Wengine ni wazunguka round about tuu, na wanachopitia huko wanakijua wenyewe.
Mwanao kama ni Nanga, usimlazimishe elimu unamtesa, ukimpatia ile basic ya kusoma, kuhesabu na kuandika ambayo ndio elimu kuu inatosha mtafutie njia nyingine, Narudia tena unamtesa mwanao, unamjengea hofu na dhana ya kushindwa kuanzia utoto matokeo yake anakua nayo na kujihisi yeye si chochote panapo wenzake.
Msikilize, msapoti kwa njia nzuri anayoihitaji, mfanye mshindi tangu utoto, Ushindi sio Darasani tu, mfanye Mshindi wa maisha.
Tusidanganyane, hakuna shule za vipaji maalum, ni shule za waliosongoka na kufaulu vizuri
Sent using Jamii Forums mobile app