Foxhound
JF-Expert Member
- Dec 15, 2013
- 28,057
- 74,465
Kuna dingi mmoja cha pombe tulikuwa tunaishi nae kota kwenye chuo kimoja. Kama kawaida ya walevi kurudi ni mida ya wanga. Sasa kuna siku kama kawaida akaenda ulevini. Sasa mida ameondoka baadae walikuja wanajeshi na mizigo yao. Walikuwa na kazi yao maalum pale ya kufanya kwa wiki moja. Kwahiyo ikabidi washike doria wenyewe hapo chuoni. Sasa kama kawaida dingi cha pombe akaamua kurudi, ila siku hiyo alirudi mapema, na alikuwa hajalewa, alionja tu! sijui kitu gani kilimgutusha! Akawa anarudi mdogo mdogo huku anasikiliza michezo(RTD enzi hizo, saa mbili kasoro). Ile anaikaribia kona ya kuingia maeneo ya kota akashtuka kusikia"hapo hapo simamaa!" We ni nani, unatoka wapi na unaenda wapi saizi?" Dingi kihoro! Pamoja na kujitambulisha ni mtumishi wa hapo chuoni, hawakumuacha! Walimrusha kichura chura, kisha wakamwambia aifiche redio yake kisha aiiibe!! Hapo kwenye kuiba redio yake ndipo alipoteseka. kila stail anayotumia, wanamkoromea, eti"mwizi gani anaiba kizembe hivyo?!" Walivyoridhika wakamwambia achukue mkulima wake atoke nduki. Mzee alifika yuko hoi na aliwatukana matusi ya kila aina. Kesho yake akaanza dozi ya metakelfin.