Wale ombaomba wa kusukumwa kwenye wheelchair wamepotelea wapi?

maroon7

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
11,144
15,143
Aisee kweli hapa mjini kila kitu ni dili la mtu. Mtakumbuka wale walemavu ombaomba waliokua wanasukumwa kwenye wheelchair walisambaa kila kona ya Dar kuanzia asubuhi hadi usiku,wanaingia kwenye bar,migahawa,madukani na kwinginek.

Mpaka tukawa tunajiuliza mbona wanaowasukuma ni mabaunsa kwanini wasipige vibarua wasaidie hao walemavu kumbe baadae ikaja gundulika kuna mtu mmoja ambae alikuwa anawatoa mikoani kawalundika kwenye nyumba yake kila siku wanaleta hesabu.

Baada ya dili kuvumbuluka yule mzee alikamatwa na cha kushangaza toka kipindi hicho hadi leo sijaona hata mmoja anaetembezwa kwenye wheelchair kwa style ile. Hii inaashiria kuwa hata mkuu wa mkoa wetu Makala akiamua kuwarudisha na kuwaaondoa mitaani kwa kiasi kikubwa itafanikiwa ila pia wafanye uchunguzi kuwabaini wenye mtandao huo wa ombaomba asichukulie tu poa eti ni ombaomba mmojammoja.

Sasa imagine kama mtu mmoja aliweza kuwamwaga ombaomba jiji zima na akawapa wheelchair na kuwahost unadhani haiwezekani kuwadhibiti hawa wengine kwa style hiyo?

Uchunguzi ukifanyika amini nawaambia asilimia 90 hatutawaona mtaani.
 
Daaah huyo mwamba nimemkubali sema alikuwa na wazo zuri kibiashara make naye aliinvest pesa nyingi sana!Unadhani wheelchair moja bei gani na wametapakaa jiji zima.
Kweli wachaga wanaakili mingi ya biashara aisee
 
Wengi wao wamehamia ZANZIBAR na ni shida kupita kiasi kwani kuomba yenyewe wanalazimisha. Kuna kipindi fulani waliletwa vipofu wengi sana ikawa wanasambazwa mitaani kwa magari na jioni wanakuja kuchukuliwa. Lakini hawa vipofu hawapo tena wameletwa wenye kuona.

Huu ni mtandao mkubwa sana lakini serikali yetu smz haina hata habari za kero za hawa ombaomba.
 
Wapo waombaji wenye uhitaji.
TOA utabarikiwa na MUNGU
Wengi wao wamehamia ZANZIBAR na ni shida kupita kiasi kwani kuomba yenyewe wanalazimisha. Kuna kipindi fulani waliletwa vipofu wengi sana ikawa wanasambazwa mitaani kwa magari na jioni wanakuja kuchukuliwa. Lakini hawa vipofu hawapo tena wameletwa wenye kuona.

Huu ni mtandao mkubwa sana lakini serikali yetu smz haina hata habari za kero za hawa ombaomba.
 
Wapo waombaji wenye uhitaji.
TOA utabarikiwa na MUNGU

Sio kwa hawa wanaoletwa kutoka mikoani kuja kufanya kazi ya omba omba. Kwa taarifa yako mapato ya kutwa huchukuliwa na hao wanaowaleta. Hawa hawafai kuwapa kitu chochote.
 
ukiona bado wapo.ujue kuna watoaji hyo misaada.
Usipotoa wewe.watatoa wengine.
wewe ungeendelea Tu na maisha yako
Sio kwa hawa wanaoletwa kutoka mikoani kuja kufanya kazi ya omba omba. Kwa taarifa yako mapato ya kutwa huchukuliwa na hao wanaowaleta. Hawa hawafai kuwapa kitu chochote.
 
Waliyokuwa wanawatuma walikamatwa
Ile ilikuwa michongo ya watu,mtu anapeleka hesabu kwa tajiri ama eicher vile

Ova
 
Kuna mmoja alikua analalamika makusanyo ya siku yameshuka kutoka elf 40 had elf 20 kwa siku unaweza ukatamani kuwa ombaomba
 
Back
Top Bottom